picha

Saumu (funga)

Nguzo za uislamu (EDK form 3:dhana ya elimu ya uislamu)

Saumu (Funga).
Umuhimu wa swaumu (Funga) katika Uislamu.

Funga ya mwezi wa Ramadhani ni nguzo ya nne katika Uislamu.
Funga ya mwezi wa Ramadhani ni faradhi kwa waislamu wote na ni miongoni mwa nguzo za Uislamu baada ya shahada, swala na zakat.
Rejea Quran (2:183).

Kufunga mwezi wa Ramadhani ni utambulisho wa Uislamu wa mtu.
Mtu akiacha nguzo hii kwa makusudi ni sababu na ishara tosha ya kutoka katika Uislamu.

Kufunga mwezi wa Ramadhani ni utambulisho wa Ucha-Mungu wa mtu.
Funga ya Ramadhani na sunnah zingine ni kielelezo cha Ucha-Mungu wa muislamu zikitekelezwa vilivyo.
Rejea Quran (2:183).

Kutofunga mwezi wa Ramadhani makusudi hupelekea kukosa msamaha.
Muislamu asipofunga mwezi wa Ramadhani makusudi basi, hukosa msamaha, na rehma na hustahiki adhabu za Mwenyezi Mungu (s.w).  

Kufunga mwezi wa Ramadhani ni amri ya Mwenyezi Mungu (s.w).
Kufunga mwezi wa Ramadhani ni faradhi (amri) kwa waislamu wote isipokuwa wenye udhuru.
Rejea Quran (2:183). 

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 2022/01/18/Tuesday - 07:11:13 pm Topic: Fiqh Main: Dini File: Download PDF Views 2098

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Simulizi za Hadithi Audio    👉2 Bongolite - Game zone - Play free game    👉3 Dua za Mitume na Manabii    👉4 Tafasiri ya Riyadh Swalihina    👉5 Madrasa kiganjani    👉6 kitabu cha Simulizi   

Post zinazofanana: