picha

mimi mara ya mwisho kubleed ilikuwa tareh 3/9 nilisex tarehe 4 je ni kwel nna mimba maana hadi sasa sijableed au ni kawaida tu

Je unaijuwa siku yako hatari ya kupata mimba. Na itakuwaje kama tayari umebeba mimba changa. Nakala hii inakwenda kukushauri machache kuhusu maswali haya.

Swali: 

mimi mara ya mwisho kubleed ilikuwa tareh 3/9 nilisex tarehe 4 je ni kwel nna mimba maana hadi sasa sijableed au ni kawaida tu

 

Jibu: -

Kwanza ilitakiwa kujuwa mzunguruko wako una siku ngapi?  Hii itatusaidia kujuwa kama eidha unaweza pata ujauzito ama huwezi. 

 

Tafiti zinaonyesha kuwa yai huweza kuanza kukomaa kuanzia siku ya 10 toka kupata hedhi mpaka siku ya 14. hii ni kwa wanawake wengi. Ila si wote. Kikawaida yai hutolewa (ovulation) kwa makadiria ya siku 12 mpaka 16 kabla ya kupata hedhi nyingine. Yaani unaweza kuhesabu kabla ya kuingia hedhi siku 12 nyuma, kisha toa siku 4 mnyuma ndani ya siku nne zizi ndizo yai hutolewa. siku hizi ndizo moja wapo yai hutolewa. Kwa mfano:--


 

👉 1.Mwanamke mwenye mzunguko wa siku 21, sasa tunatoa siku 12 nyuma kabla ya kuingia hedhi (21 - 12 = 9) kisha toa nne nyuma (9-4=5) basi mwanamke huyu anaweza kutoa yai kati ya siku ya 5 na 9 katika siku zake.


 

👉 2.Mwanamke mwenye mzunguruko wa siku 32: tunaanza kutoa siku 12 nyuma kabla ya kupata hedhi yake (32-12=20) tonatoa siku nne tena nyuma (20-4=16) kwa hiyo mwanamke huyu anaweza kutoa yai kati ya siku ya 16 mpaka 20.


 

👉 4.Mwanamke mwenye siku 28: 28-12 = 16 kisha toa siku 4 nyuma 16 - 4 = 12. hivyo siiku ambazo yai hukomaa kwa mwenye siku 28 ni kati ya 12 mpaka 16.

 

Kwa kutumianjia hii unaweza kujuwa kama ulishiriki siku hatari ama laa. 

 

✍️ Kuhusu kutopata hedhi

Itambulike kuwa unaweza usipate hedhi kwa sababu nyingi.  Ujauzito sio pekee sababu ya kukosa hedhi.  Sababu nyingine ni: -

👉 1. Maradhi

👉 2. Shida katika homoni

👉 3. Mazingira

👉 4. Matumizi ya madawa

👉 5. Hali ya hewa

 

Zipo sababu nyingine zaidi.  Hivyo huwezi kusema una ujauzito kisa tuvhujapata siku zako. 

 

NINI UFANYE;:

🚑 1. Fika kituo cha afya upate vipimo 

🏥 2. Tumia kilimo chanyumbani kupima

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu
Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: Uzazi Main: Post File: Download PDF Views 3539

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 kitabu cha Simulizi     👉2 Kitau cha Fiqh     👉3 Tafasiri ya Riyadh Swalihina     👉4 Kitabu cha Afya     👉5 Bongolite - Game zone - Play free game     👉6 Simulizi za Hadithi Audio    

Post zinazofanana:

Dalili za Maambukizi na Uvimbe katika mirija ya uzazi

Posti hii inazungumzia kuhusiana na maambukizi na uvimbe katika  mirija ya uzazi. Mara nyingi hutumiwa sawa na ugonjwa wa uvimbe kwenye fupa nyonga (PID), ingawa PID haina ufafanuzi sahihi na inaweza kurejelea magonjwa kadhaa ya njia ya juu ya uzazi

Soma Zaidi...
Nini kinasababisha uume kutoa maji meupe bila muwasho,na tiba yake ni ipi

Je unasumbuliwa na Majimaji kwenye uume. Je unapata miwasho, ama maumivu wakati wakukojoa.

Soma Zaidi...
Njia za kugundua kama mtoto amevunjika baada ya kuzaliwa

Post hii inahusu zaidi njia mbalimbali ambazo mtoa huduma anaweza kuzitumia kuangalia kama mtoto amevunjika baada ya kuzaliwa.

Soma Zaidi...
Habar doctor mm nahc kuwa ni mjamzito tumbo la chin ya kitovu linaniuma muda mwingine linaacha chuchu zinawasha na cku niliyokutana na mume wangu ni cku 11

Kuna uwezekano una ujauzito ila hujajijuwa, huwenda hujapata dalili zozote. Unataka kujuwa kama una ujauzito baada ya tendo la ndoa.

Soma Zaidi...
Mwanaune anapataje fangasi kwenye uume

Post hii itakujulishs kwa namna gani mwanaune anaweza kupata fangasi kwenye uume wake

Soma Zaidi...
Faida na hasara za kutumia uzazi wa mpango

Tunaposema uzazi wa mpango, tunamaanisha ile hali ya kuachanisha muda kutoka mtoto hadi mwingine. Inatakiwa angalau mtoto na mtoto wapishane miaka miwili. Uzazi wa mpango ni maamuzi kati ya mama na baba.

Soma Zaidi...