picha

Sababu za maumivu ya tumbo kitovuni na dalili zake

Somo Hili linakwenda kukueleza kuhusu sababu za maumivu ya tumbo kitovuni na dalili zake

SABABU ZA MAUMIVU YA TUMBO KITOMVUNI NA DALILI ZAKE

 

1.Kuwepo na uvimbe kwenye njia ya chakula (digestive track) kitaalamu hufahamika kama gastroenteritis. Hali hii inaweza kusababishwa na virusi, bakteria ama parasite. Mgonjwa anaweza kusikia maumivu na yanaweza kuwa ni makali sana. Mara nyingi maumivu haya yanapoa yenyyewe bila hata kuhitaji matibabau ha huondoka ndani ya siku chache. Ila ni vyema kumuona daktari kwa uchunguzi zaidi.

 

Dalili zakeTofauti na kuwa mgonjwa atakuwa anaumwa na tumbo kwenye kitomvu, lakini tumbo hili litafungamana na dalili zifuatazo:-1.Kuharisha2.Kichefuchefu3.Kutapika4.Homa5.Kutokwa na jasho sana

 

2.Kuvimba kwa appendix. Maumivu ya tumbo kwenye kitomfu yanaweza kuashiria ugonjwa wa appendix, kitaalamu hufahamika kama appendicitis. Kama utahisi maumivu makali ya tumo kitomvuni kisha ghafla yanahamia upande wa kulia wa tumbo kwa chini, huashiria tatizo hili. Tofauti na kuwepo kwa maumivu haya pia mgonjwa ataona dalili flani.

 

Dalili za ugonjwa wa appendix1.Kujaa kwa tumbo na kukaza kama mtu aliye vimbiwa2.Kichefuchefu3.Kutapika4.Kuhisi maumivu ambayo huwa yakiongezeka kila unapokohoa ama unapojongea.5.Mvurugiko wa tumbo kama kukosa choo au kuharisha6.Homa7.Kukosa hamu ya kula.

 

Ugonjwa huu ni katika magonjwa ambayo yanahitajika kutibiwa mapema na haraka sana. Endapo mgo jwa atachelewa kutibiwa appendix inaweza kupasuka, na endapo itapasuka inaweza kuhatarisha maisha.

 

3.Vidonda vya tumboYes maumivu ya tumbo kitomvuni yanaweza kuwa yamesababishwa na vidonda vya tumbo, huwenda vipo kwenye tumbo la chakula ama sehemu ya juu ya utumbo mdogo inayotambulika kama duodenum. Tofauti na maumivu ya tumbo kwenye kitomvu pia mgonjwa ataona dalili zifuatazo

 

Dalili za vidonda vya tumbo:1.mvurugiko wa tumbo2.Kuhisi tumbo kujaa na kucheua3.Kichefuchefu4.Kutapika5.Kukosa hamu ya kula6.Kutoa hewa kwa mdomoni kwa sauti

 

4.Matatizo kwenye kongoshoHuu ni ugonjwa unaosababisha kuvimba kwa kongosho kitaalamu huitwa Pancreatitis. Maradhi haya yanaweza kuja ghafla sana bila ya kuonyesha ishara za awali. Pia zinapoonyesha dalili zake huwa ni kama:-

 

Dalili za maradhi ya kongosho1.Kichefuchefu2.Kutapika3.Homa4.Mapigo ya moyo kuongezeka

 

5.Kuwa na ngriri ya heniaUgonjwa huu huwapata wanaume, na hutokea pale ambapo baadhi ya tishu za tumboni zinapoingia kwenye misuli ya tumboni karibu na kitomvu. Kwa watu wazima upasuaji hufanyika ili kutibu tatizo.

 

6.Kama kuna kizuizi katika utumbo kinachozuia chakula kutembea. Tatizo hili likichelewa kutibiwalinaweza kuwa hatari zaidi. Tatizo hili huweza kusababishwa na:-1.Mashambulizi ya bakteria2.Henia3.Uvimbe4.Kama kulitokea shida wakati wa kufanyiwa upasuaji.

 

Dalili1.Kichefuchefu2.Kutapika3.Tumbo kujaa4.Kupunguwa maji5.Kukosa hamu ya kula6.Kukoa choo7.Homa8.Kuongezeka kwa mapigo ya moyo

 

7.Matatizo katika mishipa mikuu ya damu kwenye tumbo (aortic aneurysm). hili ni tatizo la kiafya linalosababishwa na kudhoofu na kutanuka kwa kuta za mishipa mikuu ya damu. Hali hii inaweza kuhatarisha maisha ya mtu kama mishipa ya damu itapasuka na kupelekea damu kuingia tumboni, hii inaweza kupelekea maumivu makli. Maumivu haya yanaweza kuathiri na viungo vingine.

 

Dalili nyingine:-1.Kupata pumzi kwa tabu2.Kushuka kwa presha ya damu3.Kuongezeka kwa mapigo ya moyo4.Kuzimia5.Udhoifu wa ghafla upande mmoja wa mwili

 

8.Kama kutakuwa na shida wakati wa mzunguko wa damu katika tumbo (mesenteric ischemia). hii hutokea endapodamu inayotembea kwenye utumbo mdogo itapata usumbufu, kwa mfano ikiganda. Mgonjwa anaweza kusikia maumivu makali ya tumbo. Maumivu haya huandamana na dalili kama:-1.Kuongezeka kwa mapigo ya moyo2.Kuona damu kwenye choo

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 2021/11/10/Wednesday - 09:45:38 pm Topic: magonjwa Main: Afya File: Download PDF Views 2015

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
๐Ÿ‘‰1 Tafasiri ya Riyadh Swalihina    ๐Ÿ‘‰2 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    ๐Ÿ‘‰3 Kitabu cha Afya    ๐Ÿ‘‰4 Simulizi za Hadithi Audio    ๐Ÿ‘‰5 kitabu cha Simulizi    ๐Ÿ‘‰6 Bongolite - Game zone - Play free game   

Post zinazofanana:

Magonjwa ya moyo

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu magonjwa ya moyo

Soma Zaidi...
Ugonjwa wa kisukari

Ugonjwa wa kisukari hurejelea kundi la magonjwa yanayoathiri jinsi mwili wako unavyotumia sukari kwenye damu (glucose). Glucose ni muhimu kwa afya yako kwa sababu ni chanzo muhimu cha nishati kwa seli zinazounda misuli na tishu zako. Pia ndio chanzo ki

Soma Zaidi...
Dalili za ugonjwa wa kichaa cha mbwa

Posti hii inahusu zaidi dalili za ugonjwa wa kichaa cha mbwa ,kwa kawaida Ugonjwa huu utokea kuanzia kwenye wiki ya pili mpaka mwaka mmoja na hapo Ugonjwa unakuwa bado haujaonesha Dalili na Dalili zikishaonekana ni vigumu kutibika.

Soma Zaidi...
Madhara ya kuwepo Kwa usaha kwenye mapafu

Post hii inahusu Zaidi madhara ambayo yanaweza kutokea Kwa mgonjwa mweye usaha kwenye mapafu.

Soma Zaidi...
Dalili za UTI kwa wanaume

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu dalili za UTI upande wa wanaume

Soma Zaidi...
Dalili za Ugonjwa wa mapigo ya moyo

Mapigo ya moyo ni hisia za kuwa na moyo wa haraka, Kupepesuka au kudunda. Mapigo ya moyo yanaweza kuchochewa na mafadhaiko, mazoezi, dawa au, mara chache, hali ya kiafya. Ingawa mapigo ya moyo yanaweza kuwa ya kutisha, kwa kawaida hayana madhara. Katik

Soma Zaidi...
Dalili za upungufu wa maji mwilini.

Upungufu wa maji mwilini hutokea unapotumia au kupoteza Majimaji mengi zaidi ya unayonywa, na mwili wako hauna maji ya kutosha na Majimaji mengine ya kufanya kazi zake za kawaida. Usipochukua nafasi ya Vimiminika vilivyopotea, utapungukiwa na maji.

Soma Zaidi...
Maambukizi ya magonjwa ya ngono

Posti hii inahusu athari za maambukizi ya magonjwa ya ngonoย  ambapo magonjwa ya ngono isipokuwa UKIMWIย  yanatibika .mgonjwa anashauriwa kuwahi hospitali au kituo chochote cha afya kupata matibabu mara anapoona dalili za magonjwa haya.

Soma Zaidi...
Madhara ya maambukizi kwenye tumbo

Posti hii inahusu zaidi madhara ya maambukizi kwenye tumbo,hasa pale ambapo mgonjwa hakutibiwa

Soma Zaidi...
WAJUE FANGASI, AINA ZAKE, DALILI ZAKE NA MATIBABU YAKE

Fangasi huweza kuishi na kuathiri maeneo mbalimbali ndani ya mwili.

Soma Zaidi...