Somo Hili linakwenda kukueleza kuhusu sababu za maumivu ya tumbo kitovuni na dalili zake
SABABU ZA MAUMIVU YA TUMBO KITOMVUNI NA DALILI ZAKE
1.Kuwepo na uvimbe kwenye njia ya chakula (digestive track) kitaalamu hufahamika kama gastroenteritis. Hali hii inaweza kusababishwa na virusi, bakteria ama parasite. Mgonjwa anaweza kusikia maumivu na yanaweza kuwa ni makali sana. Mara nyingi maumivu haya yanapoa yenyyewe bila hata kuhitaji matibabau ha huondoka ndani ya siku chache. Ila ni vyema kumuona daktari kwa uchunguzi zaidi.
Dalili zakeTofauti na kuwa mgonjwa atakuwa anaumwa na tumbo kwenye kitomvu, lakini tumbo hili litafungamana na dalili zifuatazo:-1.Kuharisha2.Kichefuchefu3.Kutapika4.Homa5.Kutokwa na jasho sana
2.Kuvimba kwa appendix. Maumivu ya tumbo kwenye kitomfu yanaweza kuashiria ugonjwa wa appendix, kitaalamu hufahamika kama appendicitis. Kama utahisi maumivu makali ya tumo kitomvuni kisha ghafla yanahamia upande wa kulia wa tumbo kwa chini, huashiria tatizo hili. Tofauti na kuwepo kwa maumivu haya pia mgonjwa ataona dalili flani.
Dalili za ugonjwa wa appendix1.Kujaa kwa tumbo na kukaza kama mtu aliye vimbiwa2.Kichefuchefu3.Kutapika4.Kuhisi maumivu ambayo huwa yakiongezeka kila unapokohoa ama unapojongea.5.Mvurugiko wa tumbo kama kukosa choo au kuharisha6.Homa7.Kukosa hamu ya kula.
Ugonjwa huu ni katika magonjwa ambayo yanahitajika kutibiwa mapema na haraka sana. Endapo mgo jwa atachelewa kutibiwa appendix inaweza kupasuka, na endapo itapasuka inaweza kuhatarisha maisha.
3.Vidonda vya tumboYes maumivu ya tumbo kitomvuni yanaweza kuwa yamesababishwa na vidonda vya tumbo, huwenda vipo kwenye tumbo la chakula ama sehemu ya juu ya utumbo mdogo inayotambulika kama duodenum. Tofauti na maumivu ya tumbo kwenye kitomvu pia mgonjwa ataona dalili zifuatazo
Dalili za vidonda vya tumbo:1.mvurugiko wa tumbo2.Kuhisi tumbo kujaa na kucheua3.Kichefuchefu4.Kutapika5.Kukosa hamu ya kula6.Kutoa hewa kwa mdomoni kwa sauti
4.Matatizo kwenye kongoshoHuu ni ugonjwa unaosababisha kuvimba kwa kongosho kitaalamu huitwa Pancreatitis. Maradhi haya yanaweza kuja ghafla sana bila ya kuonyesha ishara za awali. Pia zinapoonyesha dalili zake huwa ni kama:-
Dalili za maradhi ya kongosho1.Kichefuchefu2.Kutapika3.Homa4.Mapigo ya moyo kuongezeka
5.Kuwa na ngriri ya heniaUgonjwa huu huwapata wanaume, na hutokea pale ambapo baadhi ya tishu za tumboni zinapoingia kwenye misuli ya tumboni karibu na kitomvu. Kwa watu wazima upasuaji hufanyika ili kutibu tatizo.
6.Kama kuna kizuizi katika utumbo kinachozuia chakula kutembea. Tatizo hili likichelewa kutibiwalinaweza kuwa hatari zaidi. Tatizo hili huweza kusababishwa na:-1.Mashambulizi ya bakteria2.Henia3.Uvimbe4.Kama kulitokea shida wakati wa kufanyiwa upasuaji.
Dalili1.Kichefuchefu2.Kutapika3.Tumbo kujaa4.Kupunguwa maji5.Kukosa hamu ya kula6.Kukoa choo7.Homa8.Kuongezeka kwa mapigo ya moyo
7.Matatizo katika mishipa mikuu ya damu kwenye tumbo (aortic aneurysm). hili ni tatizo la kiafya linalosababishwa na kudhoofu na kutanuka kwa kuta za mishipa mikuu ya damu. Hali hii inaweza kuhatarisha maisha ya mtu kama mishipa ya damu itapasuka na kupelekea damu kuingia tumboni, hii inaweza kupelekea maumivu makli. Maumivu haya yanaweza kuathiri na viungo vingine.
Dalili nyingine:-1.Kupata pumzi kwa tabu2.Kushuka kwa presha ya damu3.Kuongezeka kwa mapigo ya moyo4.Kuzimia5.Udhoifu wa ghafla upande mmoja wa mwili
8.Kama kutakuwa na shida wakati wa mzunguko wa damu katika tumbo (mesenteric ischemia). hii hutokea endapodamu inayotembea kwenye utumbo mdogo itapata usumbufu, kwa mfano ikiganda. Mgonjwa anaweza kusikia maumivu makali ya tumbo. Maumivu haya huandamana na dalili kama:-1.Kuongezeka kwa mapigo ya moyo2.Kuona damu kwenye choo
Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.
Download NowUmeionaje Makala hii.. ?
Posti hii inahusu zaidi njia zinazotumika ili kuangalia Maambukizi kwenye mifupa.
Soma Zaidi...Fangasi huweza kuishi na kuathiri maeneo mbalimbali ndani ya mwili.
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi hatua au mbinu za kupambana na ugonjwa wa UTI kwa sababu ugonjwa huu umekuwa tishio kubwa kwa sasa kwa hiyo tunapaswa kutumia njia mbalimbali ili kuweza kupambana na Ugonjwa huu.
Soma Zaidi...Hepatitis A ni ugonjwa wa kuambukiza wa ini unaosababishwa na virusi vya Hepatitis A. Virusi ni mojawapo ya aina kadhaa za virusi vya Hepatitis vinavyosababisha kuvimba na kuathiri uwezo wa ini wako kufanya kazi.
Soma Zaidi...Post hii inahusu Zaidi dalili za kuwepo Kwa usaha kwenye mapafu, ni dalili ambazo zinaweza kujitokeza Kwa mgonjwa,Kwa hiyo baada ya kuona dalili hizi mgonjwa anapaswa kuwahi hospital mara moja Kwa ajili ya matibabu.
Soma Zaidi...Posti hii inahusu namna madonda koo yanavyotokea, ni jinsi na namna Magonjwa haya au Maambukizi yanavyotokea na kuweza kusababisha madhara kwa watu.
Soma Zaidi...ugonjwa wa kiseyeye, chanzo chake vipi unatokea na ni zipi dalili zake. Yote haya utayapata hapa
Soma Zaidi...Saratani inahusu ugonjwa wowote kati ya idadi kubwa ya magonjwa ambayo yanaonyeshwa na ukuaji wa seli zisizo za kawaida ambazo hugawanyika bila kudhibitiwa na kuwa na uwezo wa kupenya na kuharibu tishu za kawaida za mwili. Saratani mara nyingi ina uwezo
Soma Zaidi...Kama una tatizo la midomo kuchubuka na kuwa myeupe ama kuwa na vidonda. Post hii inakwenda kuangalia swala hili.
Soma Zaidi...Posti hii inaelezea kuhusiana na hatua za kufata ili kujikinga au kuepuka maradhi ya tumbo.kuna vitu vikikosekana husababisha maumivu ya tumbo.
Soma Zaidi...