picha

Sababu za kushuka surat Ikhlas

Surat Ikhlas ni katika sura za kitawhid ambazo zilishuka miaka siku za mwanzoni mwa utume. Sura hii imekuja kujibu maswali mengi kuhusu Allah ikiwemo, Allah ni nani?

Sababu za kushuka surat al-Ikhlas

SURATUL-IKHLAS.
Inaelezwa kuwa walimfuata Mayahudu kumfata mtume (s.a.w) na kumwambia awasifie namna ambavyo Mola wake alivyo ndipo Allah akaishusha sura hii. Pia katika kauli nyingine ni kuwa Makafiri waliokuwa wakiabudia masanamu walimwendea Mtume (s.a.w) na kumwambia awaeleze sifa na namana Mola wake alivyo ndipo Allah akateremsha sura hii. Sura hii ni katika sura za mwanzo kabisa kushuka Makka na mafundisho yake yanavunja kabisa ibada ya masanamu na Ukristo na kila mafundisho ya miungu wengi.


 

Mama Aisha anasimulia ya kwamba Mtume s.a.w. alipokuwa akienda kitandani kwake kila usiku, aliunganisha vitanga vya mikono yake, kisha anavisomea Qul huwallaahu na Qul a'uudhu birabbil falaq na Qul a'uudhu birabbinnaas, na anavipulizia, kisha anavipaka mwili wake wote kila anapoweza kupagusa toka kichwani; na akifanya hivyo mara tatu (Bukhari jalada la 3).


 

FADHILA ZA SURAT AL-IKHLAS

Amesimulia ‘Abdallah Ibnhabib kuwa Mtume amesema “QUL HUWA LLAHU AHADU na mu’awadhatayn (qul a’udhu birabin-nasi na qul a’udhu birabil-falaq) (mwenye kuzisoma ) asubuhi na jioni zinatosheleza kwa kila kitu.(amepokea ahmad, Tirmidh na Nisai).

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: Quran Main: Post File: Download PDF Views 3841

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 ai web app     👉2 Dua za Mitume na Manabii     👉3 Bongolite - Game zone - Play free game     👉4 Simulizi za Hadithi Audio     👉5 Kitau cha Fiqh     👉6 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    

Post zinazofanana:

HUKUMU ZA TAFKHIIM NA TARQIQ

Jifunze namna ya kusoma quran, pata mafunzo ya tajwid hapa

Soma Zaidi...
Tofauti kati ya sura za makkah na madinah

Quran (EDK form 3:dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Makundi ya Id-ghamu katika usomaji wa Quran Tajwid

Kama tulivyoona kuwa id-ghamu ipo katika aina kuu mbili ambazo ni id-ghamu bighunnah na id-ghamu bighair ghumnah. Sasa hapa tutajifunza makundi mengine ya idhgamu.

Soma Zaidi...
Adabu za kusikiliza quran

ADABU ZA KUSIKILIZA QURANI 1.

Soma Zaidi...