Sababu za Kushuka Surat Al-Masad (tabat yadaa) na fadhila zake

Sababu za Kushuka Surat Al-Masad (tabat yadaa) na fadhila zake

4.

Download Post hii hapa

Sababu za Kushuka Surat Al-Masad (tabat yadaa) na fadhila zake

4.SURATUL-MASAD
Sura hii pia ni katika sura za kushuka Maka. Wanaeleza Maulamaa kuwa sababu ya kushuka sura hii ni kuwa mtume (s.a.w) alipopewa amri ya kulingania bila ya siri aliwaita watu wa Maka ili awalinganie na hapo baba yake mdogo Mtume (s.a.w) aitwaye Abdul a€?Uzza ambaye Qurani imemuita Abuu Lahabi yaani baba wa moto alitowa maneno ya upumbavyu na upuuzi juu ya ujumbe wa Allah na hapo Allah akateremksha sura hii.



Huyu Abu Lahab jina lake hasa ni Abdul Uzza, naye alikuwa baba mdogo wa Mtume s.a.w. Neno Abuu Lahab - baba wa miali ya moto - ni jina ambalo hutumika kwa ajili ya mtu ambaye hali yake n nya asili ni ya moto na ya uasi, na pia hutumika kwa ajili ya mtu ambaye anawachochea wengine. Hivyo bwana huyu amepangwa jina hili na Qur'an kwa sababu ya uadui wake kwa Mtume s.a.w.



Siku ya kwanza Mtume alipowaita Wakureishi ili kuwaeleza habari za ujumbe wake, huyu Abu Lahab, alimkaripia akasema, "Uangamizwe, je umetuitia maneno haya!" (Bukhari). Na ilikuwa desturi yake kila mara kumfuata Mtume aendako na kuwaambia watu wasimsikilize, akisema, Mtume ni jamaa yake na ni mwehu. Kadhalika mkewe Abu Lahab aliyeitwa Ummi Jamil bint Harb, dada wa Abu Sufiyan, alikuwa mwanamke mbaya sana aliyekuwa anamwudhi sana Mtume na kumsumbua na hata kumsingizia-singizia mambo ya upuuzi. Na kwa sababu ya masingizio yake ameitwa mchukuzi wa kuni (Bukhari), ambazo kwazo amejikokea moto wa Jahanamu, (Razi).



FADHILA ZA SURAT HII

fadhila za sura hii ni kama za sura nyingine kuwa utapata thawabu. Hakuna hadithi sahihi iliyonukuliwa kueleza fadhila za surahii kama zinavyotajwa sura nyingine. zipo baadhi ya nukuu zinanukuliwa kuwa Mtume (s.a.w) amesema "mwenye kusoma sura hii, hatakuwa makazi sawa na Abuu lahab". Haikunukuliwa hadithi hii katika vitabu vikuu va hadith, na sikuweza kupata ushahidi juu ya usahihi wa hadithi hii.



                   

Download Post hii hapa

Jiunge nasi WhatsApp
Upate Update zetu

Download App Yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.

Download Now Bongoclass Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Quran Main: Dini File: Download PDF Views 1754

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
πŸ‘‰1 Simulizi za Hadithi Audio    πŸ‘‰2 kitabu cha Simulizi    πŸ‘‰3 Madrasa kiganjani    πŸ‘‰4 Bongolite - Game zone - Play free game    πŸ‘‰5 Kitau cha Fiqh    πŸ‘‰6 Kitabu cha Afya   

Post zinazofanana:

Ni nini maana ya Idh-har katika usomaji wa Quran
Ni nini maana ya Idh-har katika usomaji wa Quran

Hapa utajifunza kuhusu hukumu ya Idh-har katika usomaji wa Quran.

Soma Zaidi...
quran na sayansi
quran na sayansi

QURANI KATIKA ZAMA ZA SAYANSI NA TEKNOLOJIAAsalaalaamu alykum warahmatullah wabarakaatuh.

Soma Zaidi...
Sababu za kushuka Surat al Kafirun
Sababu za kushuka Surat al Kafirun

Sura hii imekuja kukata rai ya Makafiri wa Makka kuhusu ibada ya ushirika. Hivi leo tungesema kuhusu dini mseto.

Soma Zaidi...
Sababu za kushuka surat al qadir
Sababu za kushuka surat al qadir

Asbab nuzul surat al qadi. Hii ni sura ya 97 katika mpangilio wa mashaf. Surat al qadir imeteremshwa Madina na ina aya 5.

Soma Zaidi...
Hukumu ya Ikhfau katika tajwid
Hukumu ya Ikhfau katika tajwid

Ikh-fau ni moja ya hukumu za nun sakina na tanwin kwenye hukumu za Quran tajwid

Soma Zaidi...
Sababu za kushuka surat al-Fiyl
Sababu za kushuka surat al-Fiyl

Al fiyl ni neno la Kiarabu lenye maana ya tembo. Sura hii inazungumziakisa cha jeshi lenye tembo. Jeshi hili lilikuwa na nia ya kuvunja al qaaba

Soma Zaidi...
Hukumu za Idh-har na id-gham katika laam al-maarifa
Hukumu za Idh-har na id-gham katika laam al-maarifa

Laam al- maarifa inaweza kusomwa kwa idgham au idh-har pindibitakapokutana na herufi za shamsiya au qamariya.

Soma Zaidi...
Je, mtu anaweza kusoma quran akiwa amelala?
Je, mtu anaweza kusoma quran akiwa amelala?

Kusoma Qur'an kuna faida kubwa kwa Muislamu, kwanza kunampatia thawabu, kunatoa nuru maisha yake, mwili wake na kumlinda na mashetani na watu wabaya. Quran ni dawa na pozo kwa magonjwa. Thawabu za Qur-an hulipwa kwa kila herufi. Quran pia huja kutet

Soma Zaidi...
Amri ya Kuchinja Ng'ombe
Amri ya Kuchinja Ng'ombe

Kutokana na kuishi kwao Misr kwa muda mrefu, Mayahudi waliathiriwa na ibada za kishirikina za Wamisr.

Soma Zaidi...
HUKUMU ZA MIIM YENYE SAKINA
HUKUMU ZA MIIM YENYE SAKINA

SURA YA NNE HUKUMU ZA MIYM YENYE SAKNA HUKUMU ZA MIYM SAKINA: Mym sakina ni miym ambayo haina i’rab ( Ω…Ω’).

Soma Zaidi...