fadhila za kusoma quran

Fadhila na umuhimu wa kusoma quran 1.

fadhila za kusoma quran

Fadhila na umuhimu wa kusoma quran
1.quran ni kamba,ponyo,kinga,nuru na ni kitu chenye kuokoa.
Kwa ufupi unaweza kusema qurani ina kila kitu ambacho tunakihitajia katika maisha yetu. Qurani inaweza kutumika kama tiba ya kuondoa maradhi ana kinga dhidi ya maradhi, uadui na husda. Pia ni nuru inayoweza kumuongoza mtu wapi apite. Qurani humkinga mtu na maadui, maradhi, husda na kila kitu kubada. Maneno haya unaweza kuyakuta katika hadithi ndeefu aliyoipokea al-haakim katika mapokeza ya ‘Ablahhah Ibn Mas’ud kuwa Mtume amesema “……hakika hii qurani ni kamba ya Allah, na ni nuru iliyo wazi, na ni pozo lenye kunufaisha, na ni ngome (ya kujikinga) kwa mwenye kushikamana nayo na ni kitu chenye kuokoa kwa mwenye kuifuata.…..”

2.Qurani ni yenye kuombea shifaa siku ya qiyama.
Watu watakuwa katika hali na wakati mgumu siku ya qiyama. Katika tabu za namna hiyo qurani itakuwa ni yenye kuwaombea watu wake wapate shifaa mbele ya Allah. Amasimulia Abuu Umamah kuwa “nimemsikia Mtume akisema ‘isomeni qurani, kwani hakika itakuja siku ya kiyama hali yakuwa ni yenye kuwaombea watu wake’” (amepokea Muslin)

3.Ukisoma herufi moja unaandikiwa mema (thawabu) 10.
Amesimulia Ibn msud kuwa mtume amesema “mwenye kusoma herufi moja katika kitabu cha Allah atapata jema moja, na jema moja hulipwa kwa mara kumi kwa mfano wake.…”(amepokea Tirmidh). Katika muendelezo wa hadithi Mtume anasema ukisema ALM hizi ni herufi tatu, hivyo kila moja hulipwa kwa kumi.

4.Wenye kusoma qurani ndio watu bora.
Mtume amewapa nafasi kubwa sana watu ambao wanaisoma qurani. Katika masimulizi ya ‘Uthman Ibn ;Afan mtume amesema “mbora wenu ni yule mwenye kujifundisha qurani kisha akaifundisha.” (amepokea Bukhari, Abuu Dauw na Tirmidh).

5.Mtu atapandishwa darsa kwa kiasi alichohifadhi qurani peponi.
Watu watakapoingia peponi watapandishwa madaraja ya peponi kulingana na kiasi cha mtu anachoweza kusoma katika qurani. Amesimulia Abdallah Ibn Umar kuwa Mtume amesema ataambiwa mtu aliyeisoma qurani (akiwa peponi) soma na upande darja na uisome kama ulivyokuwa ukiisoma ulivyokuwa dunianai. Kwa hakika makazi yako yataishia pale itakapoishia aya ya mwisho utakayoisoma”. (amepokea Abuu Dawd na tirmidh).

6.Mwenye kusoma vizuri qurani atakuwa na malaika.
Amesimulia Aisha kuwa mtume amasema mwenye kusoma qurani na akawa mahiri nayo (anaisoma vizuri) atakuwa pamoja na malaika wema wenye kutii. Na yule mwenye kuisoma na akawa anakwamakwama (hajaiweza vizuri na anajitahidi aiweze) na huku anashaka atapata malipo mara mbili” (amepokea bukhari, Muslim na wengine).


                   

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Download App yetu
Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Sira Main: Dini File: Download PDF Views 2388

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 kitabu cha Simulizi    👉2 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉3 Tafasiri ya Riyadh Swalihina    👉4 Bongolite - Game zone - Play free game    👉5 Dua za Mitume na Manabii    👉6 Simulizi za Hadithi Audio   

Post zinazofanana:

Uasi katika dola ya kiislamu na matokeo yake

Uasi katika dola ya kiislamu na matokeo yake.

Soma Zaidi...
Makubaliano ya Mkataba wa Al Fudhul

Sara na historia ya Mtume Muhammad s.a.w, sehemu ya 13. Hapa utajifunza historia ya Mkataba wa al fudhul na makubaliano yake.

Soma Zaidi...
HISTORIA YA MTUME DHUL-KIFL(A.S)

Mtume Dhul-kifl ananasibishwa na Ezekiel anayetajwa ndani ya Biblia.

Soma Zaidi...
KIKAO CHA KUMFUKUZA MTUME MUHAMMAD KUTOKA MAKKAH (MAKA), KIKAO ALICHOHUDHURIA IBLISI

KIKAO CHAKALIWA KUJADILI HATMA YA MUHAMMAD KATIKA MJI WA MAKAHiki ni kikao kizito hakijapata kutokea toka muhammad katika ji wa maka.

Soma Zaidi...
Mtume Muhammad s.a. w akutana na Bahira

Sura na historia ya Mtume Muhammad s.a. w sehemu ya 11

Soma Zaidi...