image

Wanaoongozwa na wasioongozwa na quran

Wanaoongozwa na wasioongozwa na quran

Wanaoongozwa na Qur-an:



Lengo la kushushwa Qur-an kama ilivyobainishwa katika Qur-an yenyewe ni kuwaongoza binaadamu wote katika njia iliyonyooka. Njia iliyonyooka ni njia sahihi ya maisha itakayomuwezesha binaadamu kufikia lengo la kuumbwa kwake. Pamoja na Qur-an kuwa muongozo kwa watu wote, haiwaburuzi kwa nguvu kwenye uongofu bila ya wao wenyewe kudhamiria kuongoka.Qur-an huongoza wacha-Mungu tu kama tunavyojifunza katika aya zifuatazo:


"Hiki ni kitabu kisichokuwa na shaka ndani yake, ni uwongozi kwa wamchao Mwenyezi Mungu.Ambao huyaamini yasiyoonekana (maadam yamesemwa na Mwenyezi Mungu na Mtume wake) na husimamisha Swala na hutoa katika yale Tuliyowapa.Na ambao wanaamini yaliyoteremshwa kwako na yaliyoteremshwa kabla yako na wanaamini (kuwa iko) Akhera. Hao wako juu ya uongozi utokao kwa Mola wao, na hao ndio wenye kufaulu." (2:2-5)



Kwa mujibu wa aya hizi wanaongozwa na Qur-an ni wacha-Mungu wenye sifa zifuatazo:
- Waumini wa kweli wa vipengele vyote vya nguzo za Imani. - Wasimamishaji Swala. (Rejea juzuu ya pili).
- Wanaotoa yale aliyowaruzuku Allah (s.w) kwa ajili ya kuwahurumia wanaadamu wenye kuhitajia msaada na katika kusimamisha Dini ya Allah(s.w). Aliyoturuzuku Allah (s.w)ni kila tulichonacho ikiwa ni pamoja na mali, elimu, afya, nguvu,vipaji na kadhalika.


Wasioongozwa na Qur-an:
Tunajifunza katika Qur-an kuwa makundi mawili ya watu Makafiri (na washirikina) na Wanafiki hawataongozwa na Qur-an. Kuhusu makafiri na washirikina tunafahamishwa:


Hakika wale waliokufuru ni sawa kwao ukiwaonya (kwa hii Qur-an) au usiwaonye; hawataamini. (Kama kwamba) Mwenyezi Mungu amepiga muhuri juu ya nyoyo zao na juu ya masikio yao; na juu ya macho yao pana vifuniko; basi watakuwa na adhabu kubwa. (2:6-7)



Pamoja na Qur-an kuwa na sifa ya ukweli na uwazi kama majina yake yanavyodhihirisha, haiwezi kuwaongoza wapinzani (makafiri) wa wazi wa Mwenyezi Mungu(sw) na ujumbe wake. Haiwezi kwa sababu binaadamu amepewa uhuru na Mola wake wa kuamua na kufanya atakavyo. Akiamua kutii anaweza na akiamua kuasi anaweza. Hivyo mtu aliyeamua kuukataa mwongozo huu kwa makusudi huna namna ya kumuongoza.



Kuhusu wanafiki tunafahamishwa:


"Na katika watu, wako (wanafiki) wasemao "Tumemuamini Mwenyezi Mungu na siku ya mwisho" na hali ya kuwa si wenye kuamini. Wanataka kumdanganya Mwenyezi Mungu na wale walioamini, lakini hawadanganyi ila nafsi zao, nao hawatambui. Nyoyoni mwao mna maradhi, na Mwenyezi Mungu amewazidishia maradhi. Basi watakuwa na adhabu iumizayo kwa sababu ya kule kusema kwao uongo.(2:8-10)


Na wanapoambiwa msifanye uharibifu ulimwenguni Husema "Sisi ni watengenezaji." Hakika wao ndio waharibuji, lakini hawatambui. Na wanapoambiwa: "Aminini kama walivyoamini watu, "husema "Oh! Tuamini kama walivyoamini wapumbavu?" Hakika wao ndio wapumbavu lakini hawajui. (2:11-13)


Na wanapokutana na walioamini husema, "Tumeamini," na wanapokuwa peke yao kwa mashetani wao husema: "Hakika sisi tu pamoja nanyi, tunawacheza shere tu." Na Mwenyezi Mungu atalipa shere yao na kuwawacha katika upotofu wao wakitangatanga ovyo. Hao ndio waliokhiari upotofu kuliko uongofu, lakini biashara yao haikupata faida wala hawakuwa wenye kuongoka." (2:14-16)



Wanafiki pamoja na kujiita Waislamu na pengine wakawa ni wanachuoni wa Qur-an walio mahiri katika kuifasiri Qur-an kwa kutumia balagha, mantiq, sarfu, n.k; hawataongozwa na Qur-an maadamu wamekhiari maslahi ya dunia kinyume na mwongozo wa Mwenyezi Mungu(sw). Si tu hawa wasomi wa Qur-an wenye sifa hizo zilizoainishwa katika aya hizi hawataongozwa na Qur-an bali pia Allah (s.w) amewafananisha na mbwa katika aya zifuatazo:


"Na wasomee (Ewe Muhammad) habari za wale tuliowapa Aya zetu (kuzijua), kisha wakajivua nazo (wasizifuate). Na shetani akawaandama na, wakawa miongoni mwa waliopotea.Na kama tungelitaka tungeliwanyanyua kwazo, lakini wao waligandamana na ardhi (kutaka maslahi ya kidunia wakayapuuza ya Akhera) na wakayafuata matamanio yao. Basi hali yao ni kama hali ya mbwa; ukimpigia kelele (hukimbia na huku) anahema, na ukimwacha pia huhema.Hiyo ndio hali ya watu waliokadhibisha Aya zetu. Basi simulia hadithi, huenda wakatafakari. "(7:1 75-176)



Hivyo, kwa mujibu wa Aya hizi, mnafiki hata akiwa ni A’alim (Sheikh) wa Qur-an na Hadith, kamwe hawezi kuongozwa na Qur-an.




                   






           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 384


Sponsored links
πŸ‘‰1 kitabu cha Simulizi     πŸ‘‰2 Kitau cha Fiqh     πŸ‘‰3 Madrasa kiganjani     πŸ‘‰4 Kitabu cha Afya    

Post zifazofanana:-

Hukumu za mim sakina na tanwinkwenye hukumu za tajwid
Hukumu za kim sakina na tanwin ni idgham shafawiy, idh-har shafawiy, na Ikhfau shafawiy Soma Zaidi...

Dai kuwa Muhammad (s.a.w) aliitunga Qur-an ili Kuwania Madaraka na Ukubwa
(x) Dai kuwa Muhammad (s. Soma Zaidi...

quran na sayansi
YALIYOMONENO LA AWALI1. Soma Zaidi...

Haikufundisha Mtume Muhammad quran kwa lengo la kurekebisha tabia za waarabu
Soma Zaidi...

Tafsiri na mafunzo ya sura zilizochaguliwa - Saratul-fiyl
Quran (EDK form 3:dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

Sifa za wanafiki katika quran
Soma Zaidi...

Maana ya qalqala na aina zake katika usomaji wa Quran tajwid
Qalqala imegawanyika katika makundi mawili ambayo ni Qalqalatul qubra yaani qalqala kubwa na qalqalat as shughura yaani qalqala ndogo. Soma Zaidi...

Makundi ya Id-ghamu katika usomaji wa Quran Tajwid
Kama tulivyoona kuwa id-ghamu ipo katika aina kuu mbili ambazo ni id-ghamu bighunnah na id-ghamu bighair ghumnah. Sasa hapa tutajifunza makundi mengine ya idhgamu. Soma Zaidi...

quran na sayansi
Soma Zaidi...

yaliyomo: HUKUMU YA MIM SAKINA, NUN SAKINA, MADA, WAQFU, QALAQALA, TAFKHIM NA TARQIQ, USOMAJI WA QURAN
DARSA ZA TAJWID YALIYOMOSURA YA 01 . Soma Zaidi...

Sababu za kushuka surat al-Falaq na surat an-Nas na fadhila za kusoma sura hizi
SURAT AL-MUAWIDHATAYN (SURAT AL-FALAQ NA SURATUN-NAS) Inaelezwa kuwa sura mbili hizi zilishuka pamoja, na maulamaa wanaelezea kuwa Mtume (s. Soma Zaidi...

Sababu za kushuka surat al Zilzalah
surat Zalzalah ni sura ya 99 katika mpangilio wa Quran, na ina aya 8. Sura hii imeteremshwa Madina ila pia kuna kauli zinathibitisha kuwa ni ya Makkah. Katika hadithi iliyopewa daraja la hassan na Imam Tirmidh Mtume S.A.W amesema kuwa kusoa surat Zilzalah Soma Zaidi...