image

Mtume amezaliwa mwaka gani?

Na tumemuusia mwanaadamu afanye wema kwa wazazi wake.

v

Maadili katika surat Al-Ahqaf


Na tumemuusia mwanaadamu afanye wema kwa wazazi wake. Mama yake amechukua mimba yake kwa taabu na akamza kwa taabu. Na kubeba mimba yake hata kumwachisha ziwa; (uchache wake) ni miezi thelathini. Hata anapofikia baleghe yake na akawa mwenye umri wa miaka arubaini, (mtoto mwema) husema: "Ee Mola wangu! Niwezeshe nishukuru neema zako ulizonineemesha mimi na wazazi wangu, na niwezeshe nifanye vitendo vizuri unavyovipenda, na unitengenezee watoto wangu; kwa yakini ninatubu kwako; na hakika mimi ni miongoni mwa waliosilimu (walionyenyekea)." (46:15).


Hao ndio tunaowakubalia vitendo vyao vyema walivyovifanya, na tunayapita kando makosa yao, (tunayasamehe); (watakuwa) miongoni mwa watu wa Peponi: miadi ya kweli waliyoahidiwa. (4 6:16).



Na ambaye anawaambia wazazi wake: "Kefule nyi! Oh! Mnanitishia kuwa nitafufuliwa; na hali karne nyingi, (watu wengi) zimekwisha pita kabla yangu (wala hazikufufuliwa)?" Na hao (wazee wake) wawili huomba msaada wa Mwenyezi Mungu; (na humwambia mtoto wao:) "Ole wako! Amin (haya unayoambiwa). Hakika ahadi ya Mwenyezi Mungu ni kweli." Lakini yeye husema: "Hayakuwa haya (mnayoyasema) ila ni visa vya watu wa kale (tu si maneno ya kweli)."



Hao ndio ambao imelazimika hukumu juu yao (ya kutiwa Motoni, pamoja na mataifa yaliyopita kabla yao ya majini na watu, hakika hao ndio waliojitia khasarani. (46:17-18)
Kutokana na aya hizi tunajifunza kuwa:



(a)Hatunabudi kuwafanyia wema wazazi wawili na hasa mama ambaye anapata dhiki kubwa katika kutuzaa na kutunyonyesha mpaka kufikia umri wa miaka miwili.



(b)Hatunabudi kumshukuru Allah (s.w) kwa kutuneemesha kwa neema mbali mbali ikiwa ni pamoja na kuwapa wazazi wetu moyo wa huruma na mapenzi ya kutulea mpaka kufikia utu uzima.



(c)Pamoja na kumshukuru Allah (s.w), hatubabudi kuwashukuru wazazi wetu kwa kutulea kwa huruma na mapenzi. Shukrani zetu kwao tutazidhihirisha kwa kuwatii, kuwafanyia ihsani na kuwaombea dua na maghfira kwa Allah (s.w).


(d)Hatuna budi kujiepusha mbali na kuwafanyia wazazi wetu ufedhuli na jeuri. Tusisubutu hata kuwagunia.



(e)Hatunabudi kuomba kizazi chema na kumuomba Allah (s.w) atuwezeshe kukilea vyema kizazi chetu.



(f)Hatunabudi kufuatilia kwa makini usia mwema wanaotupa wazazi wetu.



(g)Hatunabudi kuleta toba na kuomba maghfira mara kwa mara (angalau kila siku mara mia moja).




                   






           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 396


Sponsored links
👉1 kitabu cha Simulizi     👉2 Kitau cha Fiqh     👉3 Madrasa kiganjani     👉4 Kitabu cha Afya    

Post zifazofanana:-

tarekh 09
KULELEWA NA BABU YAKE:Mzee ‘Abdul Al-Muttalib alimchukuwa mjukuu wake na wakarejea Makkah na aliendelea kuishinae na kumlea kwa mapenzi makubwa sana. Soma Zaidi...

Maandalizi ya hijrah ya mtume na waislamu kuhamia madinah
Bara arabu zama za jahiliyyah (EDK form 2 dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

Mafunzo kutokana na vita vya badri
Dola ya uislamu madinah (EDK form 3: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

Mafunzo Yatokanayo na Historia ya Nabii Daud(a.s)
Kutokana historia ya Nabii Daud (a. Soma Zaidi...

Mateso waliyoyapata waislamu wa mwanzo Maka, na orodha ya waislamu walioteswa vikali
Pili, Maquraish walimuendea Mtume(s. Soma Zaidi...

MTUME MUHAMMAD (S.A.W)ANAKUTANA NA BAHIRA (MTAWA WA KIYAHUDI)
KUKUTANA NA BAHIRA (MTAWA) WA KIYAHUDIMzee Abu talib alikuwa ni mfanya biashara, hivyoslikuwa akimchukuwa kijana wake kwenda kwenye biashara. Soma Zaidi...

Historia ya bi Khadija na familia yake na chanzo cha utajiri wake.
Sira na historia ya Mtume Muhammad s.a.w, sehemu ya 17. Historia ya Bi Khadija na familia yake. Soma Zaidi...

Vita vya wenyewe kwa wenyewe baada ya kif cha khalifa Uthman
Soma Zaidi...

Utekwaji wa Misri na Gavana Muawiya
Soma Zaidi...

Maswali kuhusu Quran
Quran (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

KIKAO CHA KUMFUKUZA MTUME MUHAMMAD KUTOKA MAKKAH (MAKA), KIKAO ALICHOHUDHURIA IBLISI
KIKAO CHAKALIWA KUJADILI HATMA YA MUHAMMAD KATIKA MJI WA MAKAHiki ni kikao kizito hakijapata kutokea toka muhammad katika ji wa maka. Soma Zaidi...

Wapinzani wa Ujumbe wa Nabii Salih(a.s)
Baada ya Nabii Salih(a. Soma Zaidi...