Ni mali ipi inatakiwa kutolewa zaka?
Mali inayojuzu kutolewa Zakat, Nisaab na kiwango cha Zakat
Aina ya mali inayojuzu kutolewa Zakat imeelezwa kwa wazi katika
Qur-an na Hadith sahihi. Mali inayojuzu kutolewa Zakat ni ile iliyofikia au kuzidi kima maalum kiitwacho Nisaab na kubakia katika milki ya mwenye hiyo mali kwa kipindi chote cha mwaka mmoja. Kila aina ya mali ina nisaab yake, Nisaab ni kiwango cha mali kinachostahiki kitolewe Zakat. Aina ya mali inayojuzu kutolewa Zakat ni:
(i)Mazao yote ya shambani
(ii)Wanyama wafugwao kwa ajili ya chakula
(iii)Dhahabu (gold), fedha (silver), au fedha taslim (cash)
(iv)Vito (mapambo ya dhahabu na fedha)
(v)Madini na mali ya kuchimbuliwa chini ya ardhi au mali ya kuokota
(vi)Mali ya biashara
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 Madrasa kiganjani 👉2 Kitau cha Fiqh 👉3 Bongolite - Game zone - Play free game 👉4 Tafasiri ya Riyadh Swalihina 👉5 Simulizi za Hadithi Audio 👉6 web hosting
Post zinazofanana:
Haki za viumbe na mazingira
Haki na uadilifu katika uislamu (EDK form 3: Dhana ya elimu ya uislamu)
Soma Zaidi...Jinsi ya kusherehekea siku ya idi katika uislamu
Uislamu umeweka taratibu maalumu za kuzifata katika kusherehekea siku ya idi.
Soma Zaidi...