Namna ya kujitwaharisha mkojo wa Mtoto mdogo Najisi Hafifu
(c) Najisi Hafifu:
Najisi hafifu ni mkojo wa mtoto mdogo wa kiume chini ya miaka miwili ambaye hajaanza kula chakula ila maziwa tu. Uhafifu wa najisi hii hupatikana katika kutwaharisha. Tofauti na najisi ndogo, najisi hafifu hutwaharishwa kwa kumwagia maji tu ile sehemu iliyonajisika bila ya kusugua. Hivi ndivyo alivyofanya Mtume (s.a.w) kama tunavyojifunza katika hadith ifuatayo:
Aysha (r.a) amesimulia kuw a mtoto mchanga wa kiume aliyekuwa angali ananyonya aliletwa kwa Mtume (s.a.w) aliagiza maji na kuyamiminia juu ya pale palipo kojolewa ”. (Muslim)
Hadathi Ndogo
Kuwa katika hadathi ndogo ni kuwa katika hali ya kutokuwa na udhu na huondolewa hadathi hiyo kwa kutia udhu baada ya kuzingatia na kutekeleza kwa ukamilifu masharti na nguzo za udhu.
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 Kitabu cha Afya 👉2 Simulizi za Hadithi Audio 👉3 Dua za Mitume na Manabii 👉4 web hosting 👉5 kitabu cha Simulizi 👉6 Madrasa kiganjani
Post zinazofanana:
Makosa Yanayofanywa Wakati wa Swala
Swala ni nguzo ya pili ya Uislamu baada ya Shahada na ni ibada ya kwanza ambayo mja atahisabiwa nayo Siku ya Kiyama. Kwa sababu ya umuhimu wake mkubwa, Muislamu anatakiwa kuiswali kwa usahihi kulingana na mafundisho ya Mtume Muhammad (Swalla Allahu Alayhi Wasallam). Hata hivyo, watu wengi hufanya makosa mbalimbali wakati wa swala, mengine kwa kutokujua na mengine kutokana na uzembe. Makosa haya yanaweza kupunguza thawabu za swala au hata kuifanya swala kuwa batili. Katika makala hii tutajifunza makosa ya kawaida yanayofanywa wakati wa swala, madhara yake, na namna ya kuyarekebisha.
Soma Zaidi...