picha

Nia za kupima ujauzito ukiwa nyumbani, Njia kuu 10 za kiasili za kupima mimba changa

Kuna njia nyingi zinatajwa zinapima mimba kama chumvi, sukari, mafuta na sabuni. Hata hivyo zipo njia zaidi ya 10 za kiasili za kupima ujauzito. Utajifunza hapa zote

Nia za kupima ujauzito ukiwa nyumbani, Njia kuu 10 za kiasili za kupima mimba changa



JE NAWEZA UPIMA UJAUZITO KWA KUTUMIA CHUMVI NA SUKARI?




Haswa hili ni swali zuri, wanawake wengi wamekuwa wakitafuta makala hizi na wanazipata. Namna ya kupima ujauzito kwa kutumia sukari ama chumvi. Ila nikwambie kitu si sukari na chumvi tu balli zipo njia nyingine kama:-



Njia nyingine za kupima ujauzito ukiwa nymbani:-
1.Sukari
2.Chumvi
3.Sabuni
4.Mafuta
5.Delto
6.Shampoo
7.Dawa ya mswaki na yingine.



Nini kinafanyika. Unachanganya kiasi cha mkojo vyema ukawa wa asubuhi. Unaandaa chombo na kuweka moja kati ya hizo zilizotajwa juu. Unaweza kutumia kijiko kimoja kcha mkojo ama kikombe. Uwiyano wa vilivyotaja juu uwe zawa na mkojo, ama mkojo uziti kidogo. Kisha subiria kwa dakika 5 hadi 10. kama utaona mabadiliko yeyote ya rangi yametokea ama utaona kuna mapovu yanachemka basi takuwa ni mjamzito.



Je nji hizi ni sahihi?
Kwa ufupi njia hizi si sahihi kabisa. Haziwezi kukupa majibu ya kweli. Waandishi wengi wameandika lakini ukweli ni kuwa huu ni uwongo. Njia sahihi ni kwenda kupima kwa kipimo maalumu, vinginevyo utapoteza muda bure. Yes wakati mwingine unaweza kupima ukaona mabadiliko na ukawa ni mjamzito kweli. Lakini mabadiliko hayohayo utakayoyaona anaweza kuyaona hata asiye mjamzito.



Je watu wa zamani walikuwa wanapimaje ujauzito?





NJIA ZA KIASILI WALIZOTUMIA ZAMANI KUPIMA UJAUZITO:



1.Kukojoa kwenye nafaka (mbegu za ngano na shayiri)
Tafiti zilizofnywa na wavumbuzi wa mabo ya kale (archeologist) wamegunduwa kuwa yapata miaka 1350 KK kabla ya kuzaliwa Yesu kuwa wanawake wa Misri (Egypt) walikuwa wanapotaka kujuwa kama wamebeba ujauzito walikuwa wakichukuwa viroba vya ngano na shayiri (barley) kisha wanakojolea kiroba chote. Kama ngano itaota basi mwanamke ana ujauziti tena wa mtoto wa kike. Na kama shayiri itaota atakuwa na ujauzito wa mtoto wa kiume. Na kama nafaka hizi hazitaota basi mwanamke hana ujauzito.



Ni kuwa katika mwanamke mjamzito kwenye mojo wake kuna homoni ambazo zinachochea ukuwaji wa mbegu. Baada ya kukojolea pishori lile mbegu hazifukiwi, hivyo ztaota mulemule kwenye kiroba kile bila ya kufukiwa kwenye udogo. Miaka ya 1960 wanasayanzi wa leo walifanya tafiti wakagunduwa kuwa njia hii ni sahihi ya asilimoa 70%.



2.Kitunguu.
Njia hii ilifanywa na wagiriki mikaa ya zamani sana. Matabibu wa kigiriki walikuwa wanapotaka kujuwa kama mwanmke ana ujauzito walikuwa wakiinguiza kwenye uke wa mwanamke kitunguu na kukiacha humo kwa usiku mzima. Na kama ikifika asubuhi mwanamke akawa anatowa harufu ya kitunguu kwenye mdomo wake basi ana ujauzito. Wagiriki waliamini kuwa mwanamke akiwa na ujauzito uke wake unauwezo mkubwa wa kufyonza vitu. Tafiti hii haikuweza kuthibitishwa na sayansi hili leo.



3.Kwa kutumia funguo ama kitasa.
Njia hii ilifanya kwa namna hii, endapo mwanamke anajihisi ni mjamzito alikuwa anachukuwa fnguo ama kitasa kisha anaweka kwenye bakuli kisha anakojowa kiasi cha mkojo kuzamisha funguo ama kitasa kisha anaacha hivyo kwa muda wa masaa matatu. Kama akitowa hakuna mabadiliko ya michubuko ama rangi ana chochote basi mwanamke ni mjamzito. Njia hii [ia haikuweza kuthibitishwa hivi leo.



4.Kwa kuangalia rangi ya macho.
Moja katika matabibu wa zamani sana wa kifaransa aliyetambulika kama Jacques Guillemeau yeye aliamini kuwa macho ndio kioo cha mwili, hivyo unaweza kujuwa maradhi na hali ya mwili wa kutumia macho. Aliamini kuwa mwanamke mjamzito macho yake yameingia ndani kidogo, mboni ya macho yake imesinyaa kidogo na mishipa ya neva ilajitokeza pembezoni mwa macho. Wanasayansi wa leo pia wameshindwa kuthibitisha usahihi wa njia hii, ijapokuwa ni kweli mabadiliko yanaweza kutokea kwenye macho ila si kwa kipindi cha mwanzo.



5.Njia uliyojulikana kama Piss Prophets
Njia hii ilitumiaka miaka ya 1600, matabibu hawa walikuwa wakipima ujauzito kwa kutumia kuangalia mkojo. Hawa waliamini kuwa mkojo wa mjamzito unakuwa ni msafi naani hauna uchafu, una rangi ya limao bivu lililopauka lakini unakuwa na ukungu kwa mbali juu yake. Pia matabibu hawa hawakuishia hapa walikuwa wakiangalia uwepo wa maradhi engine kwa kuangalia mkojo. Wanasayansi wa leo pia wameshindwa kuthibitisha usahihi wa njia hii.



6.Kwa kutumia riboni:
Njia hii ilikuwa na mzunguruko kidogo, nikuwa mwanamke anapojihisi ni mjamzito anakwenda kwa tabibu. Tabibu atamwambia akojoe kwenye beseni, kisha tabibu atachukuwa riboni na kuitia kwenye beseni lenye mkojo. Baada ya muda ataitoa na kuikausha, kisha ataichoma mbele karibu na mwanamke. Kama harufu ya riboni itamfanya mwanamke ahisi kichefuchefu basi atakuwa ana ujauzito. Wanasayansi waleo pia hawakuweza kuthibitisha njia hii.



7.Kwa kutimia Sungura ama wanyama wadogo wadogo kama panya.
Njia hii iligunduliwa miaka ya 1900 na matabibu waliojulikana kwa majina ya Bernhard Zondek na Selmar Aschheim. Hawa miaka ya 1940 waliamini kuwa mkojo wa mjamzito ukiingizwa kwenye mwili wa vijinyama vidogo basi ovari zao huwa kubwa. Baadaye jaribio hili lilijikita sana kwa kutumia sungura. Wanasayansi wa leo walionyesha kuwa njia hii ilikuwa na ukweli kiasi japo sio njia nzuri maana ilihitajika kumuuwa sungura ili kuchunguza kama ovari zimekuwa kubwa.



8.Kwa kutumia chura.
Njia hii ilianza kutumika Afrika ya Kusini. Wao walikuwa wakutumia chura wa kike. Waliamini kuwa endapo chura wa kieke akichomwa sindano yenye mkojo wa mwanamke mjamzito, basi chura huyo atataga mayai ndani ya masaa 12.



Njia nyingine:
9.Kuangalia mwendo, yaani jinsi anavyotembea mjamzito ni tofauti na mwanamke asiye mjamzito.
10.Kwa kuaangalia ongezeko la mapigo ya moyo. Kama mapigo ya moyo yameongezeka basi mwanamke ana ujauzito.



Njia zilizotajwa hapo juu zilikuwa zukitumika katika nyakati zake na zilionekana kusaidia kwa wakati ule. Ni kweli njia hizo zina madhaifu makubwa lakini si kila wakati zilikuwa zikikosea. Wakati mwingine zilikuwa zikipatia, ni kwa sababu mwanamke alikuwa ni mjamzito kweli. Hata hivyo ilibidi pia kuangalia dalili nyingine za ujauziti ndipo tabubu alikuwa akitoa jibu.



Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Jiunge nasi WhatsApp
Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Uzazi Main: Afya File: Download PDF Views 20354

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Tafasiri ya Riyadh Swalihina    👉2 Madrasa kiganjani    👉3 Dua za Mitume na Manabii    👉4 Kitabu cha Afya    👉5 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉6 Kitau cha Fiqh   

Post zinazofanana:

mim ninaujauzito wa mwezi mmoja lakini naona kama hali fulani ya damu inanitoka sehemu ya Siri inafanana na damu ya wakati wa period

Kutokuwa na damu wakati wa ujauzito ni hali uliyo ya kawida lakini inapaswa kujuwa sifa za damu hiyo nabje unatoka kwa namna gani. Kama unasumbuliwa na tatizo hili makala hii ni kwa ajili yako.

Soma Zaidi...
Siku za kupata ujauzito

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu siku za kupata ujauzito

Soma Zaidi...
Njia za kuzuia mimba zisiharibike.

Posti hii inahusu zaidi njia mbalimbali ambazo zinaweza kutumika ili kuweza kuzuia mimba zisiharibike, kwa sababu kila mama anayebeba mimba anategemea kupata mtoto kwa hiyo na sisi hamu yetu ni kuhakikisha kwamba mtoto anazaliwa kwa kuzuia mimba kuharibik

Soma Zaidi...
Uchafu unaotoka ukeni na rangi zake.

Posti hii inahusu zaidi uchafu unaotoka ukeni na rangi zake, kwa kawaida ukeni utolewa uchafu, uchafu huo unaweza kuwa kawaida na unaweza kuwa na rangi mbalimbali kutokana na kuwepo kwa Maambukizi.

Soma Zaidi...
Dalili za PID

Posti hii inahusu zaidi dalili za PID maana yake ni maambukizi kwenye pelvic kwa kitaalamu huitwa pelvic infection disease, ni ugonjwa unaoshambulia sana wanawake na wasichana

Soma Zaidi...
Chanzo cha tezidume, dalili zake na tiba zake.

Post hii inakwenda kukufunza mambo mengi kuhusu tezi dume kama chanzo, dalili, matibabu, njia za kujikinga na mambo hatari yanayoweza kukusababishia kupata tezi dume.

Soma Zaidi...
Mwanamke anatema mate mara kwa mara je inaweza kuwa ni ujauzito?

Ni kweli kuwa kutema mate mara kwa mara inaweza kuwa ni dlili za ujauzito. Lakini itambulije kuwa pekee sio kithibitishi cha ujauzito.

Soma Zaidi...
Uchungu usio wa kawaida kwa akina Mama.

Posti hii inahusu zaidi uchungu usio wa kawaida kwa akina Mama, kwa kawaida uchungu unapaswa kuwa ndani ya masaa Kumi na mawili ila Kuna wakati mwingine uchungu unaweza kuwa zaidi ya masaa Kumi na mawili na kusababisha madhara yasiyo ya kawaida kwa Mama n

Soma Zaidi...
Mm tumbo linaniuma mara kwa mara na linakua kama linages alaf kichwa kinauma mara kwa mara na nakosa choo wakati mwingine na kiuno kinauma je?inawezakua n ujauzito? Maana nilshirki tendo la ndoa siku ya tano baada ya kutoka hedhi

Dalili za mwanzo za ujauzito zinaweza kuwa ni changamoto kwamwanamke hasa ikiwa ndio mimba yake ya kwanza. Maumivu ya tumbo, kujaa kwa tumbo gesi, kukosa choo ama hamu ya kula na kadhalika huweza pia kuambatana na ujauzito.

Soma Zaidi...