dalili za mimba changa na siku ya kupata mimba

Jifunze namna ya kuthibitisha dalili za ujauzito kuwa ni za kweli. Tambuwa namna ya kupima mimba na muda mujarabu wa kupima

dalili za mimba changa na siku ya kupata mimba



JE NITAHAKIKISHA VIPI KAMA NINA UJAUZITO?




Hili ni swali la msingi kabisa, maana unaweza kuwa na dalii za ujauzitio lakini si ujauzito, ama unaweza kuwa ujauzito lakini ukipima huoni kitu. Sasa nini tufanye. Njia pekee ya kuhakiki kama ni ujauzito ama sio ni kupima. Unaweza kutumia kipimo cha mkojo ukiwa nyumbani ama kwenda kupima hospitali.



Kama utatumia kipimo cha mkojo fika duka la dawa na hakikisha unapewa kipimo kilichokuwa hakiku expire. Pata maelekezo kutoka kwa uuzaji kama ni mara yako ya kwanza. Pia maelekezo utaweza kuyakuta kwenye hiko kipimo ila lugha inaweza usielewe. Kipimo hili kinafanya kazi kwa kuangalia uwepo wa kemikali ambazo huzaliwa wakati wa ujauzito. Endapo zitakuwepo kipimo kitaonyesha kuwa ni mjamzito.



Sasa ni muda gani unafaha kupima?
Ni vyema kupia wiki mbili baada ya kukosa hedhi. Endapo utapima wiki moja baada ya kukosa hedhi ama utapima mapema zaidi kuna uwezekano kuwa hutapata majibu kama ni mjamzito. Hivyo inashauriwa sana kusubiri baada ya wiki mbili toka kukosa hedhi ndipo upime. Kama utakwenda kupima hospitali haina shida hata ukiwahi maana zipo njia nyingi wanaweza kutumia.



Nina dalili za uajauzito lakini nikipima sina?
Hili ni katika maswali ambayo wanawake wengi wamekuwa wakiuliza. Inatokea anazo dalili zote za ujauzito lakini akipima hakuna kitu. Kuna sababu nyingi juu ya swala hili. Kabla ya kuendelea na somo hili zaidi, wacha nikufahamishe kuwa, yafuatayo yanaweza kusababisha usione ujauzito kwenye kipimo:-



1.Kama umepima mapema kabisa
2.Kama kipimo ni kibovu
3.Kama umekosea namna ya kupima
4.Kama huna ujauzito
5.Homoni za ujauzito hazipo za kutosha kwenye mkojo.



Hizi ni katika sababu tu zinazotokea hasa wakati wa kupima. Sasa wacha tuingie katika somo hili kitaalamu zaidi. Ni kwa nini unaweza kupata dalili za uajauzitio zilizotaja hapo juu lakini ukipima huna hata ujauzito?. nitaangalia hoja kuu tano za kutokea kwa hali hizi kama ifuatavyo:-



1.Kukosa Hedhi
Kukosa hedhi ni dalili ya ujauzito, lakini haimaanishi kuwa ni lazima utakuwa mjamzito. Kwani mwanamke anaweza kukosa hedhi kwa moja ya sababu zifuatazo:-
A.Uwiyano usiosawa wa homoni (hormene imbalance)
B.Madawa
C.Maradhi katika ovari
D.Magonjwa kama ya PID
E.Misongo ya mawazo
F.Vyakula
G.Njia za uzazi wa mpango



2.Kuuma kujaa na kuvimba kwa matiti. Hii inaweza kuwa ni dalili ya ujauzito.akini pia hali hii inaweza kusababishwa na mambo kadhaa ambayo yanaweza yakakufanya uhisi ni mjamzito.kwa mfano:-
A.Kuwepo kwa uvimbe kwa ndani (breast sore)
B.Kuwepo kwa shida katika tishu za matiti (fibrocystic breast tissue)
C.Kwa wakati mwingine mazoezi makali yanaweza kusababisha hali hii.
D.Uvutaji wa sigara
E.Pia uwiyano mbaya wa homoni (hormone imbalany)



3.Maumivu ya kichwa na kichefuchefu yanaweza kusababishwa pia na sababu nyingine. Ijapokuwa inakadiriwa kuwa asilimia 70 ya kichefuchefu ni ujauzito. Mengine yanayoweza kusababisha ni misongo ya mawazo, vyakula, maradhi na vidonda vya tumbo, sumu katika vyakula na mengineyo.



4.Maumivu ya tumbo na kutokwa na damu kidongo (cramping and spotting). dalili hizi zinawezakufana na sana na mwanzoni mwa hedhi, dalili hizi hazimaanishi moja kwa moja utakuwa na ujauzito. Kwani huwenda pia zikasababishwa na uwiyano mbaya wa homoni (hormone imbalance), matumizi ya baathi ya njia za uzazi wa mpango, matumizi ya madawa, misongo ya mawzo, mashambulizi ya bakteria mwilini (PID) na maradhi yanayojulikana kama uterine fibrinoid.



5.Uchovu, nadhani hapa sina haja ya kuzungumza sana maana kila mtu anafahamu kuwa uchovu unaweza kusbabishwa na mambo mengi sana kama mazoezi, kazi, maradhi mengine.



Hivyo kama unapata dalili za ujauzito na kila ukipima hakuna kitu vyema kufika kituo cha afya kwenda kucheki vyema huwenda kuna kitu haki[o sawa.



Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Download App yetu
Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Uzazi Main: Afya File: Download PDF Views 3622

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Kitau cha Fiqh    👉2 Madrasa kiganjani    👉3 Kitabu cha Afya    👉4 kitabu cha Simulizi    👉5 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉6 Simulizi za Hadithi Audio   

Post zinazofanana:

Ay ni iv kipimo cha mimb uanz kutoa majb ndan ya mda gan wik mwez au iko vipi?

Kipimo cha Mlimba huweza kuonyesha mimba changa mapema sana. Pia ni rahisi kutumia na kinapatikana kwa bei nafuu. Je ungeoendavkujuwa ni muda gani kinatoa majibu sahihi?

Soma Zaidi...
Kazi ya homoni ya testosterone

Posti hii inahusu zaidi kazi ya homoni ya testosterone, hii homoni kwa kiwango kikubwa ukutwa kwa wanaume ndiyo homoni ambayo umfanya mwanaume aonekane jinsi alivyokuwa na sifa zake zote.

Soma Zaidi...
mambo HATARI KWA UJAUZITO (MIMBA) mambo yanayopelekea kujauzito kuwa hatarini kutoka

Tofauti na mambo matano yaliyotajwa hapo juu kuwa yanapelekea ujauzito kutoka, kuna mambo mengine ambayo yanaweza kuuweka ujauzito kuwa hatarini.

Soma Zaidi...
Mimi naumwa na tumbo chini ya kitovu upande wa kulia, ninapotok kushiriki tendo la ndoa ndonapata maumivu zaid pia nawashwa sehemu za siri itakuwa shida ni nin?

Maumivu ya tumbo baada ya tendo la ndoa yanaweza kuwa ni dalili ya maradhi fulani, ama shida kwenye mfumo w uzazi. PID na UTI hutuhumiwa kuwa ni katika sababu hizo. Ila zipo nyingine nyingi tu. Kama ina hali hii vyema ukafika kituo cha afya

Soma Zaidi...
Mda wa kufanya tendo la ndoa baada ya kujifungua

Posti hii inahusu zaidi mda ambao mama anapaswa kukaa bila kufanya tendo la ndoa mara tu baada ya kujifungua.

Soma Zaidi...
Magonjwa ya kwenye ovari na Dalili zake.

Post hii inahusu zaidi Magonjwa yanayoshambulia sana ovari na Dalili zake, haya ni magonjwa ambayo yanashambulia sana ovari ni kama ifuatavyo.

Soma Zaidi...
Sababu za kuharibika kwa ujauzito na dalili zake

Dalili za kuharibika kwa ujauzito na dalili za kuharibika kwa ujauzo

Soma Zaidi...
Madhara ya fangasi ukeni

Maambukizi ya fangasi katika sehemu za Siri za mwanamke husababishwa na fangasi wanaoitwa CANDIDA ALBICANS pia maambukizi haya hujulikana kama YEAST INFECTION. Pia hupatikana katika midomo, mpira wa kupitisha chakula,kibofu Cha mkojo ,uume na uke.

Soma Zaidi...
Wajibu wa mjamzito katika utaratibu wa uleaji wa mimba

Posti hii inahusu zaidi wajibu wa Mama mjamzito katika kileo mimba sio yeye tu Bali na wote waliomzunguka wanapaswa kuhakikisha kuwa mama mjamzito anapaswa kufanyiwa huduma zote Ili kuweza kujifungua salama na bila shida yoyote.

Soma Zaidi...
Sababu za maumivu ya tumbo wakatu wa tendo la ndoa

Jifunze sababu kuu zinazosababisha kuhisi maumivu makali ya tumbo wakati wa kushiriki tendo la ndoa

Soma Zaidi...