MAGONJWA
Kama tulivyoona huko juu kuwa kuumwa ni hali ya kutokuwa sawa kimwili na kiakili. Sasa katika kurasa hii tutaangalia zaidi kuhusu magonjwa, na namna ambavyo yanaambukizwa na kusababishwa. Pia tutaangalia zaidi namna ambavyo mwili hupambana na magonjwa hayo. Ukurasa huu utakuwa ni mwangaza kwako msomaji wetu juu ya maradhi na yanayohusiana na maradhi hyo. Pia tutaangalia namna ambavyo maradhi huambukizwa katika mazingira na kutoka mtu na mtu mwingine. Tutaangalia kwa undani mawakala wa kueneza maradhi.
Kabla ya kuendelea mbele zaidi ningependa kuwajulisha wasomaji kuwa hapa tutatumia pia maneno ya kitaalamu. Maneno haya nitaanza kuyatolea ufafanuzi wake kabla ya kuendelea mbele. Maneno hayo ni kama haya;-
1.Maradhi ya kuambukiza (infection diseases) haya ni magonjwa ambayo yana sababishwa na mawakala wa maradhi waliovamia mwilini.
2.Pathogen ni mawakala wa maradhi ambao husababisha maradhi mwilini
3.Virusi nivijidudu vidogo sana ambavyo ni wakala wa kusababisha maradhi
4.Fungus ni vijidudu vidogo ambavyo huula miili ya vitu milivyokufa
5.Antibiotic resistance ni hali ambapo mwili unashindwa kabisa kuuwa virusi