Mafunzo yatokanayo na vita vya uhudi
Dola ya uislamu madinah (EDK form 3: dhana ya elimu ya uislamu)
Mafunzo yatokanayo na Vita vya Uhudi.
- Lengo la maadui wa Uislamu na waislamu kupigana ni kuwaangamiza wao, kuharibu miji yao na mali zao pia. Hivyo ni wajibu waislamu kuwa na tahadhari muda wote kupambana na maadui wao.
- Kushauriana katika kupanga mambo ni jambo la busara sana, kama alivyoshauriana Mtume (s.a.w) juu ya sehemu ya kupiganwa vita vya Uhudi.
Rejea Qur’an (3:159) na (3:166-167).
- Tunajifunza pia ni wajibu waislamu kutumia mbinu, ujuzi, uzoefu, na jitihada za kivita pamoja na kuwa wanapata msaada wa Mwenyezi Mungu (s.w).
Rejea Qur’an (8:60).
- Msaada wa Mwenyezi Mungu (s.w) kwa waislamu unapatikana pale tu waislamu watakapotii amri zake na wakapigania dini vilivyo.
Rejea Qur’an (3:151-152).
- Kuvunja na kutotii amri ya Mwenyezi Mungu na Mtume wake hupelekea kutofikia mafanikio hata kama watajizatiti na kufanya jitihada ipasavyo.
Rejea Qur’an (3:152), (3:165) na (33:36).
- Tunajifunza pia, makosa ya watu wachache yasipuuzwe na kufumbiwa macho bali yarekebishwe kwani athari yake itasibu jamii nzima.
Rejea Qur’an (8:25).
- Mwenyezi Mungu (s.w) anatukumbusha kuwa pepo haipatikani kwa kutamani, lele mama na ushabiki bali, kufanya jitihada ya kweli.
Rejea Qur’an (3:142-150), (3:156-160) na (3:169-171).
- Msamaha na nusura ya Mwenyezi Mungu (s.w) upo karibu kwa waislamu pindi watakapotubia na kurejea kwake na kupambana na maadui ipasavyo.
Rejea Qur’an (3:152-154), (3:166-167) na (3:139-141).
- Ushindi wa waislamu katika vita unatoka kwa Mwenyezi Mungu (s.w) na sio kutokana na ubora wa silaha na wingi wa askari.
Rejea Qur’an (3:123-124), (8:42-45).
- Choko choko na mbinu za maadui dhidi ya Uislamu na waislamu ni zenye kuendelea na hazitaisha kamwe hadi siku ya Qiyama.
Download App Yetu
Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.
Download Now
Nyuma
Endelea
Umeionaje Makala hii.. ?
Nzuri Mbaya Save
Author:
Rajabu 
Tarehe:
1970-01-01 03:33:44
Topic:
Sira
Main:
Dini
File:
Download PDF
Views
1765
Post zinazofanana:
KULELEWA NA MAMA YAKE ALIPOFIKA MIAKA MINNEMtume (s.
Soma Zaidi...
Bara arabu zama za jahiliyyah (EDK form 2 dhana ya elimu ya uislamu)
Soma Zaidi...
Luqman ni katika watu wema kabisa waliopita zama za nyuma.
Soma Zaidi...
Dini anayostahiki kufuata mwanadamu (EDK form 2 dhana ya elimu ya uislamu)
Soma Zaidi...