Maandalizi ya hijrah ya mtume na waislamu kuhamia madinah


image


Bara arabu zama za jahiliyyah (EDK form 2 dhana ya elimu ya uislamu)


  • Maandalizi ya Hijra ya Mtume (s.a.w) na Waislamu kuhamia Madinah.
  • Mtume (s.a.w) hakuhama mpaka alipoletewa amri ya kuhama, na aliindaa safari yake kistretejia akiwa sahibu wake Abubakar (r.a).

 

  • Mikakati na Maandalizi ya Kistretejia aliyofanya Mtume (s.a.w) na Abubakar (r.a) kabla ya kuanza safari ya kuhama kwenda Yathrib (Madina); 

 

  1. Walipanga kuwa watajificha katika pango Thaur kwa siku tatu kabla ya kuanza safari ya kuelekea Yathrib (Madinah).

 

  1. Walipanga kutumia njia ya uficho isijulikana na mtu ya kuelekea kusini badala ya njia ya kawaida ya kuelekea kaskazini.

 

  1. Walimkodi bedui mweledi wa njia ile atakayewaongoza mpaka Yathrib kwa dinari 300.

 

  1. Abubakar (r.a) alinunua ngamia wawili kwa ajili ya safari yake na Mtume (s.a.w).

 

  1. Abubakar (r.a) alimchukua bint yake Asma kwa siri ili kumuonyesha pango lilipo na awe anawaletea chakula muda watakapo kuwa pangoni.

 

  1. Pia Abubakar (r.a) alimwagiza mchunga mbuzi wake awe anachungia karibu na pango ili awapatie maziwa.

 

  1. Abubakar (r.a) pia alimpa jukumu kijana wake Abdullah kuwaletea taarifa za mjini kwa yatakayojitokeza baada ya wao kuondoka. 

 

  • Maquraish baada ya kubaini kuwa waislamu wameshahamia Yathrib, na Mtume (s.a.w) anajiandaa naye ahame, walipanga njama ya kumuua kabla hajahama.

 

  • Maquraish walichagua vijana shupavu kutoka kila ukoo wa kiquraish na kuwapa mapanga makali ili wajewamvamie kwake akiwa amelala usiku kwa pamoja ili lawama ya kumuua isiangukie ukoo mmoja.

 

  • Kabla ya kuondoka, Mtume (s.a.w) alimkabidhi Ali (r.a) amana zote za watu ili kuwarejeshea na akamwamuru alale katika kitanda chake.

 

  •  Allah (s.w) alimnusu na kabla ya Alfajir, Mtume (s.a.w) aliondoka pamoja na Abubakar (r.a) kuelekea pangoni akawaacha ‘wauaji’ nje ya nyumba yake wamelala fofofo.

 

  • Kufeli kwa zoezi la kumuua Mtume (s.a.w), Maquraish walitangaza zawadi ya ngamia 100 kwa atakaye mleta Muhammad au Abubakar yuko hai au amekufa.

 

  • Maquraish kwa kumkodi bedui mjuzi wa kufuatilia nyayo, akiwaongoza mpaka pangoni lakini Allah (s.w) aliwanusu. Rejea Qur’an (9:40).

 

  •  Mwishowe baada ya siku tatu, Mtume (s.a.w) na sahibu wake, Abubakar (r.a) waliondoka kuelekea Madinah na walifika salama kabisa.

 

  • Kwa heshima ya Mtume (s.a.w), mji wa Madinah ukawa unaitwa ‘Madinatul-Munwwarah’ (mji ung’aao).


Baada ya kufariki (kutawafu) Mtume (s.a.w), Waislamu walikubaliana kuanzisha Kalenda ya mwaka wa Kiislamu ‘Al-Hijrah’ (A.H) ianzie siku ile aliyohama (hijra ya) Mtume (s.a.w) kwenda Madinah



Sponsored Posts


  ðŸ‘‰    1 Jifunze Fiqh       ðŸ‘‰    2 Download App zetu hapa ujifunze zaidi       ðŸ‘‰    3 Madrasa kiganjani offline       ðŸ‘‰    4 Tunakukaribisha kwenye Maktaba yetu    


Je una maswali, maoni ama ushauri, tutumie sms ✉ bofya hapa hapa, ama wasiliana nasi kwa WhatsApp bofya hapa



Post Nyingine


image Uhakiki wa hadithi za mtume
Sunnah na hadithi (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

image Mtazamo wa uislamh juu ya ibada
Katika kipengele hich tutajifunza dhana ya ibada katika uislamu,maana ua ibada Soma Zaidi...

image Haki za viumbe na mazingira
Haki na uadilifu katika uislamu (EDK form 3: Dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

image Sifa au vigezo vya dini sahihi
Dini sahihi anayostahiki kufuata mwanadamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

image Kuwapa wanaostahiki
Nguzo za uislamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

image Tofauti kati ya Quran na vitabu vingine vya mwenyezi Mungu
Nguzo za imani (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

image Zoezi la 6 kusimamisha swala
Zoezi hili linamaswali mbalimbali kuhusiana na swala na masharti ya swala. Soma Zaidi...

image Umuhimu na msisitizowa zakat na sadaqat katika uislamu
Nguzo za uislamu,umuhimu na msisitizowa zakat na sadaqat katika uislamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

image Aina za hijjah
Nguzo za uislamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

image Tofauti kati ya zakat na sadaqat
Nguzo za Imani, tofauti kati ya sadaqat na zakat (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...