Home Afya Shule ICT Burudani Dini Maktaba Maswali Madrasa Apps Blog Legacy Login

MAANDALIZI YA HIJRAH YA MTUME NA WAISLAMU KUHAMIA MADINAH


image


Bara arabu zama za jahiliyyah (EDK form 2 dhana ya elimu ya uislamu)


  • Maandalizi ya Hijra ya Mtume (s.a.w) na Waislamu kuhamia Madinah.
  • Mtume (s.a.w) hakuhama mpaka alipoletewa amri ya kuhama, na aliindaa safari yake kistretejia akiwa sahibu wake Abubakar (r.a).

 

  • Mikakati na Maandalizi ya Kistretejia aliyofanya Mtume (s.a.w) na Abubakar (r.a) kabla ya kuanza safari ya kuhama kwenda Yathrib (Madina); 

 

  1. Walipanga kuwa watajificha katika pango Thaur kwa siku tatu kabla ya kuanza safari ya kuelekea Yathrib (Madinah).

 

  1. Walipanga kutumia njia ya uficho isijulikana na mtu ya kuelekea kusini badala ya njia ya kawaida ya kuelekea kaskazini.

 

  1. Walimkodi bedui mweledi wa njia ile atakayewaongoza mpaka Yathrib kwa dinari 300.

 

  1. Abubakar (r.a) alinunua ngamia wawili kwa ajili ya safari yake na Mtume (s.a.w).

 

  1. Abubakar (r.a) alimchukua bint yake Asma kwa siri ili kumuonyesha pango lilipo na awe anawaletea chakula muda watakapo kuwa pangoni.

 

  1. Pia Abubakar (r.a) alimwagiza mchunga mbuzi wake awe anachungia karibu na pango ili awapatie maziwa.

 

  1. Abubakar (r.a) pia alimpa jukumu kijana wake Abdullah kuwaletea taarifa za mjini kwa yatakayojitokeza baada ya wao kuondoka. 

 

  • Maquraish baada ya kubaini kuwa waislamu wameshahamia Yathrib, na Mtume (s.a.w) anajiandaa naye ahame, walipanga njama ya kumuua kabla hajahama.

 

  • Maquraish walichagua vijana shupavu kutoka kila ukoo wa kiquraish na kuwapa mapanga makali ili wajewamvamie kwake akiwa amelala usiku kwa pamoja ili lawama ya kumuua isiangukie ukoo mmoja.

 

  • Kabla ya kuondoka, Mtume (s.a.w) alimkabidhi Ali (r.a) amana zote za watu ili kuwarejeshea na akamwamuru alale katika kitanda chake.

 

  •  Allah (s.w) alimnusu na kabla ya Alfajir, Mtume (s.a.w) aliondoka pamoja na Abubakar (r.a) kuelekea pangoni akawaacha ‘wauaji’ nje ya nyumba yake wamelala fofofo.

 

  • Kufeli kwa zoezi la kumuua Mtume (s.a.w), Maquraish walitangaza zawadi ya ngamia 100 kwa atakaye mleta Muhammad au Abubakar yuko hai au amekufa.

 

  • Maquraish kwa kumkodi bedui mjuzi wa kufuatilia nyayo, akiwaongoza mpaka pangoni lakini Allah (s.w) aliwanusu. Rejea Qur’an (9:40).

 

  •  Mwishowe baada ya siku tatu, Mtume (s.a.w) na sahibu wake, Abubakar (r.a) waliondoka kuelekea Madinah na walifika salama kabisa.

 

  • Kwa heshima ya Mtume (s.a.w), mji wa Madinah ukawa unaitwa ‘Madinatul-Munwwarah’ (mji ung’aao).


Baada ya kufariki (kutawafu) Mtume (s.a.w), Waislamu walikubaliana kuanzisha Kalenda ya mwaka wa Kiislamu ‘Al-Hijrah’ (A.H) ianzie siku ile aliyohama (hijra ya) Mtume (s.a.w) kwenda Madinah



Sponsored Posts


  ðŸ‘‰    1 Magonjwa na afya       ðŸ‘‰    2 Jifunze fiqh       ðŸ‘‰    3 Hadiythi za alif lela u lela       ðŸ‘‰    4 Maktaba ya vitabu       ðŸ‘‰    5 Madrasa kiganjani       ðŸ‘‰    6 Mafunzo ya html kwa kiswahili    


Je! una maswali, mapendekezo ama maoni? tuma ujumbe wa meseji SMS hapo chini ili kuunganishwa na muhusika au bofya hapa

SMS SMS

Imeandikwa na Tags Dini , DARSA , ALL , Tarehe 2022/01/08/Saturday - 01:59:36 am     Share On facebook or WhatsApp Topic school Zaidi Dini AFYA ICT Burudani Tags Uzazi maswali Afya mengineyo dini HIV Sira vyakula Matunda HTML php Alif Lela 1 Alif Lela 2 FANGASI Dawa SQL Tips Quran Sunnah fiqh DARSA Magonjwa Tajwid tawhid simulizi Dua Academy Wahenga chemshabongo WAJUWA Michezo ICT Imesomwa mara 1003



Post Nyingine


image Kwa nini Elimu imepewa nafasi ya kwanza katika Uislamu?
Kwa nini katika uislamu elimu imepewa nafasi ya kwanza ( EDK form 1 Dahana ya elimu) Soma Zaidi...

image Waislamu wanaolazimika kufunga
Nguzo za uislamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

image Kuandaliwa kwa Muhammad kabla ya kupewa utume
Bara arabu zama za jahiliyyah (EDK form 2 dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

image Uandishi wa hadithi wakati wa maswahaba wa mtume (s.a.w)
Sunnah na hadithi (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

image Mafunzo ya hadithi zilizochaguliwa
Sunnah na hadithi (EDK form 3: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

image Mgawanyo sahihi wa elimu kwa mtazamo wa uislamu
Ni upi mgawanyo sahihi wa elimu kwa mtazamo wa uislamu (EDK form 1: mgawanyo sahihi wa elimu kwa mtazamo wa uislamu Soma Zaidi...

image Kumuamini mwenyezi Mungu (S.W)
Nguzo za imani (EDK form 2: elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

image Kuandaliwa kwa Muhammad wakati na baada ya kupewa utume
Bara arabu zama za jahiliyyah (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

image Tofauti kati ya sura za makkah na madinah
Quran (EDK form 3:dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

image Misingi ya fiqh
Kwenye kipengele hichi tutajifinza vyanzo mbalimbali vya sheria ua kiislamu. Soma Zaidi...