Madhara ya kaswende kwa wajawazito na watoto wadogo.
Posti inahusu zaidi madhara ya kaswende kwa mama mjamzito na mtoto, Ni ugonjwa unaopatikana hasa kwa njia ya kujamiiana na utoka kwa mwenye Ugonjwa kwenda kwa mtu ambaye hana ugonjwa, kwa hiyo tunapaswa kujua madhara ya ugonjwa huu kwa mama mjamzito na mt
Madhara ya kaswende kwa wajawazito na watoto
1. Kwanza tuanze kwa Mama, ugonjwa huu usababisha Mimba kutoka kwa sababu Maambukizi uingilia sehemu ambayo imefungwa kwa ajili ya kuzuia kitu chochote kupita na kushambulia sehemu mbalimbali kwa mtoto hatimaye mimba utoka kwa hiyo hali hii inasababisha maumivu makali kwa mama na wote waliomzunguka.
2. Kujifungua mtoto mfu.
Kwa sababu ya Ugonjwa wa kaswende mama anaweza kubeba mimba kwa miezi tisa lakini baadaye akajifungua mtoto mfu, kwa hiyo Mama mjamzito anapaswa kupima kaswende pale anapoanza tu mahudhurio ya kliniki na kuanza kutumia dawa mara moja.
3. Kuzaa mtoto kilema.
Ugonjwa huu wa kaswende usababisha sana kuzaliwa kwa watoto walemavu kwa sababu ya kuwepo kwa Maambukizi ambayo ushambulia sehemu mbalimbali za mwili na kumfanya mtoto kuzaliwa akiwa na ulemavu na pia kuendelea kuwepo kwa ugonjwa huu umpata Mama kuingia kwenye risk ya kupata Maambukizi ya HIV na magonjwa mengine nyemelezi.
4. Pia na kwa mtoto mwenyewe kuna matokeo katika kuwa na ugonjwa huu ambapo ni pamoja na mtoto kuzaliwa akiwa na afya mbaya na kuwa na uzito mdogo ambapo wazazi utumia gharama na mda mwingi katika kumtibu mtoto, kwa hiyo mtoto akizaliwa tu anapaswa kupimwa kaswende kama hali yake sio nzuri kiafya na baba na Mama nao pia wanapaswa kupima ili kupewa madawa.
5. Jamii inapaswa kupewa elimu kuhusu ugonjwa huu, hasa wanawake wajawazito wanapaswa kuelezwa wazi na wahudumu wao au wauguzi kuhusu kupima na kupewa dawa ili kumkinga mtoto na hatari mbalimbali kama vile ulemavu wa viungo, kuzaliwa na kaswende na kuzaliwa mfu.
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 kitabu cha Simulizi 👉2 Kitabu cha Afya 👉3 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w) 👉4 Kitau cha Fiqh 👉5 Bongolite - Game zone - Play free game 👉6 Dua za Mitume na Manabii
Post zinazofanana:
Dalili kuu 7 za malaria na dawa ya kutibu malaria
Makala hii itazungumzia dalili za Malaria, athari za kuchelewa kutibu malaria, na matibabu ya malaria
Soma Zaidi...Dalili za Kuvimbiwa kwa watoto
Posti hii inazungumzia kuhusiana Kuvimbiwa kwa watoto ni tatizo la kawaida.Kuvimbiwa kwa watoto mara nyingi kuna sifa ya kupata haja kubwa mara kwa mara au kinyesi kigumu, kikavu. Sababu mbalimbali zinaweza kusababisha kuvimbiwa kwa watoto.Sababu za kawa
Soma Zaidi...Maambukizi ya tishu ya Matiti.
Posti hii inazungumzia kuhusiana na maambukizi ya tishu ya matiti ambayo husababisha maumivu ya matiti, uvimbe, joto na uwekundu. Pia unaweza kuwa na Homa na baridi. Ugonjwa huu huwapata zaidi wanawake wanaonyonyesha ingawa wakati mwingine hali hi
Soma Zaidi...Mzio (aleji) na Dalili zake
Posti hii inahusu zaidi mzio na Dalili zake ni Dalili ambazo ujitokeza kwa mtu mwenye mzio, kuna wakati watu wengine ushindwa kutambua kuwa ni mzio au la, lakini leo tunaenda kujua Dalili za mzio kama ifuatavyo.
Soma Zaidi...Shida ya kifua kubana inaweza kuwa dalili ya maambukizi ya ukimwi
Kubana kwa kifuwa ni katika hali ambazo si naweza kuhatarisha maisha. Huwenda kuwa ni miongoni mwa dalili za magonjwa mengi. Je unadhani na HIv na UKIMWI ni moja ya magonjwa hayo?
Soma Zaidi...Dalili za Saratani ya utumbo mdogo.
Posti hii inaonyesha ishara na dalili za Saratani ya utumbo mdogo
Soma Zaidi...