Madhara ya kaswende kwa wajawazito na watoto wadogo.
Posti inahusu zaidi madhara ya kaswende kwa mama mjamzito na mtoto, Ni ugonjwa unaopatikana hasa kwa njia ya kujamiiana na utoka kwa mwenye Ugonjwa kwenda kwa mtu ambaye hana ugonjwa, kwa hiyo tunapaswa kujua madhara ya ugonjwa huu kwa mama mjamzito na mt
Madhara ya kaswende kwa wajawazito na watoto
1. Kwanza tuanze kwa Mama, ugonjwa huu usababisha Mimba kutoka kwa sababu Maambukizi uingilia sehemu ambayo imefungwa kwa ajili ya kuzuia kitu chochote kupita na kushambulia sehemu mbalimbali kwa mtoto hatimaye mimba utoka kwa hiyo hali hii inasababisha maumivu makali kwa mama na wote waliomzunguka.
2. Kujifungua mtoto mfu.
Kwa sababu ya Ugonjwa wa kaswende mama anaweza kubeba mimba kwa miezi tisa lakini baadaye akajifungua mtoto mfu, kwa hiyo Mama mjamzito anapaswa kupima kaswende pale anapoanza tu mahudhurio ya kliniki na kuanza kutumia dawa mara moja.
3. Kuzaa mtoto kilema.
Ugonjwa huu wa kaswende usababisha sana kuzaliwa kwa watoto walemavu kwa sababu ya kuwepo kwa Maambukizi ambayo ushambulia sehemu mbalimbali za mwili na kumfanya mtoto kuzaliwa akiwa na ulemavu na pia kuendelea kuwepo kwa ugonjwa huu umpata Mama kuingia kwenye risk ya kupata Maambukizi ya HIV na magonjwa mengine nyemelezi.
4. Pia na kwa mtoto mwenyewe kuna matokeo katika kuwa na ugonjwa huu ambapo ni pamoja na mtoto kuzaliwa akiwa na afya mbaya na kuwa na uzito mdogo ambapo wazazi utumia gharama na mda mwingi katika kumtibu mtoto, kwa hiyo mtoto akizaliwa tu anapaswa kupimwa kaswende kama hali yake sio nzuri kiafya na baba na Mama nao pia wanapaswa kupima ili kupewa madawa.
5. Jamii inapaswa kupewa elimu kuhusu ugonjwa huu, hasa wanawake wajawazito wanapaswa kuelezwa wazi na wahudumu wao au wauguzi kuhusu kupima na kupewa dawa ili kumkinga mtoto na hatari mbalimbali kama vile ulemavu wa viungo, kuzaliwa na kaswende na kuzaliwa mfu.
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 Tafasiri ya Riyadh Swalihina 👉2 Kitau cha Fiqh 👉3 Simulizi za Hadithi Audio 👉4 Kitabu cha Afya 👉5 Madrasa kiganjani 👉6 Dua za Mitume na Manabii
Post zinazofanana:
Maumivu ya mgongo.
Post yetu Leo inaenda kuzungumzia Maumivu ya nyuma ni malalamiko ya kawaida. Kwa upande mkali, unaweza kuchukua hatua za kuzuia au kupunguza matukio mengi ya maumivu ya mgongo. Ikiwa kinga itashindikana, matibabu rahisi ya nyumbani na mbinu sahihi za m
Soma Zaidi...Maumivu ya koo na uhusiano wake na tonsils.
Maumivu ya koo ni malalamiko ya kawaida ambayo mara nyingi husababishwa na maambukizi ya virusi au bakteria. Hata hivyo, mara nyingi maumivu haya yanahusishwa moja kwa moja na uvimbe wa tonsils—viungo viwili vidogo vilivyopo nyuma ya koo vyenye jukumu la kusaidia kinga ya mwili dhidi ya vimelea. Makala haya yanafafanua uhusiano kati ya maumivu ya koo na tonsillitis (kuvimba kwa tonsils) na jinsi ya kutofautisha kati ya maambukizi ya kawaida na yale yanayohitaji msaada wa daktari.
Soma Zaidi...Tofauti kati ya homa ya mapafu (Nimonia) na mafua makali.
Mara nyingi watu huchanganya Nimonia (Pneumonia) na mafua makali kwa sababu yote huathiri mfumo wa upumuaji. Hata hivyo, haya ni magonjwa tofauti kimsingi: mafua husababishwa na virusi na huathiri njia ya juu ya hewa (pua, koo), wakati Nimonia ni maambukizi ya viini (bakteria, virusi, au fangasi) yanayoshambulia mifuko ya hewa ndani ya mapafu (alveoli). Makala hii inaelezea tofauti za kifizikia na umuhimu wa kupata matibabu sahihi.
Soma Zaidi...Dalili za HIV kwa Mwanamke Mjamzito
Makala haya yanalenga kutoa uelewa muhimu kuhusu virusi vya UKIMWI (HIV) na ujauzito. Tutachunguza dalili zinazoweza kujitokeza, umuhimu wa upimaji wa mapema kwa afya ya mama na mtoto, na jinsi ya kuzuia maambukizi kutoka kwa mama kwenda kwa mtoto (PMTCT).
Soma Zaidi...Makundi yaliyo katika hatari ya kupata Ugonjwa wa ngiri.
Posti hii inahusu zaidi makundi ambayo yapo katika hatari ya kupata ugonjwa wa ngiri, ni hatari kwa sababu tunajua kuwa ngiri utokea kwa sababu ya kuta au tishu zinazoshikilia viungo fulani mwilini kupoteza uimara wake au kuwepo kwa uwazi na kufanya viun
Soma Zaidi...