Madhara ya kaswende kwa wajawazito na watoto wadogo.

Madhara ya kaswende kwa wajawazito na watoto wadogo.

Posti inahusu zaidi madhara ya kaswende kwa mama mjamzito na mtoto, Ni ugonjwa unaopatikana hasa kwa njia ya kujamiiana na utoka kwa mwenye Ugonjwa kwenda kwa mtu ambaye hana ugonjwa, kwa hiyo tunapaswa kujua madhara ya ugonjwa huu kwa mama mjamzito na mt

Madhara ya kaswende kwa wajawazito na watoto

1. Kwanza tuanze kwa Mama, ugonjwa huu usababisha Mimba kutoka kwa sababu Maambukizi uingilia sehemu ambayo imefungwa kwa ajili ya kuzuia kitu chochote kupita na kushambulia sehemu mbalimbali kwa mtoto hatimaye mimba utoka kwa hiyo hali hii inasababisha maumivu makali kwa mama na wote waliomzunguka.

 

2. Kujifungua mtoto mfu.

Kwa sababu ya Ugonjwa wa kaswende mama anaweza kubeba mimba kwa miezi tisa lakini baadaye akajifungua mtoto mfu, kwa hiyo Mama mjamzito anapaswa kupima kaswende pale anapoanza tu mahudhurio ya kliniki na kuanza kutumia dawa mara moja.

 

3. Kuzaa mtoto kilema.

Ugonjwa huu wa kaswende usababisha sana kuzaliwa kwa watoto walemavu kwa sababu ya kuwepo kwa Maambukizi ambayo ushambulia sehemu mbalimbali za mwili na kumfanya mtoto kuzaliwa akiwa na ulemavu na pia kuendelea kuwepo kwa ugonjwa huu umpata Mama kuingia kwenye risk ya kupata Maambukizi ya HIV na magonjwa mengine nyemelezi.

 

4. Pia na kwa mtoto mwenyewe kuna matokeo katika kuwa na ugonjwa huu ambapo ni pamoja na mtoto kuzaliwa akiwa na afya mbaya na kuwa na uzito mdogo ambapo wazazi utumia gharama na mda mwingi katika kumtibu mtoto, kwa hiyo mtoto akizaliwa tu anapaswa kupimwa kaswende kama hali yake sio nzuri kiafya na baba na Mama nao pia wanapaswa kupima ili kupewa madawa.

 

5. Jamii inapaswa kupewa elimu kuhusu ugonjwa huu, hasa wanawake wajawazito wanapaswa kuelezwa wazi na wahudumu wao au wauguzi kuhusu kupima na kupewa dawa ili kumkinga mtoto na hatari mbalimbali kama vile ulemavu wa viungo, kuzaliwa na kaswende na kuzaliwa mfu.

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu Rajabu
Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: magonjwa Main: Post File: Download PDF Views: 4219

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 ai web app     👉2 Kitau cha Fiqh     👉3 Bongolite - Game zone - Play free game     👉4 kitabu cha Simulizi     👉5 Kitabu cha Afya     👉6 Madrasa kiganjani    

Post zinazofanana:

Vidonda vya tumbo (Peptic Ulcer): Chanzo na vyakula vya kuepuka.

Vidonda vya tumbo ni vidonda wazi vinavyojitokeza kwenye utando wa ndani wa tumbo (gastric ulcers) au sehemu ya juu ya utumbo mdogo (duodenal ulcers). Hali hii hutokea wakati kinga ya utando wa tumbo dhidi ya asidi inapovunjika, na kusababisha maumivu makali, kiungulia, na kichefuchefu. Makala haya yanalenga kukupa uelewa wa chanzo cha vidonda hivi na orodha ya vyakula unavyopaswa kuviepuka ili kusaidia uponyaji wa kidonda na kupunguza maumivu.

Soma Zaidi...
Maambukizi kwenye Tumbo na utumbo mdogo.

Posti hii inahusu Maambukizi kwenye tumbo na kwenye utumbo mdogo,ni Maambukizi ambayo uwa kwenye tumbo na utumbo mdogo.

Soma Zaidi...
Yajue mashambulizi ya bacteria kwenye Ngozi (cellulitis)

Mashambulizi ya bacteria kwenye Ngozi hujitokeza sehemu yenye jeraha pia huonyesha wekundu wenye upele,Uvimbe na malengelenge.

Soma Zaidi...
Ugonjwa wa kisukari

Ugonjwa wa kisukari hurejelea kundi la magonjwa yanayoathiri jinsi mwili wako unavyotumia sukari kwenye damu (glucose). Glucose ni muhimu kwa afya yako kwa sababu ni chanzo muhimu cha nishati kwa seli zinazounda misuli na tishu zako. Pia ndio chanzo ki

Soma Zaidi...
Namna ya kuzuia maambukizi kwenye nephroni

Post hii inahusu zaidi namna ya kuzuia maambukizi kwenye nephroni, ni njia zinazotumika kuzuia maambukizi kwenye nephroni

Soma Zaidi...
Kuumwa na mgongo: Matatizo ya disc na jinsi ya kuepuka upasuaji.

​Maumivu ya mgongo ni mojawapo ya changamoto kubwa za kiafya zinazomkabili binadamu wa karne ya 21. Kati ya visababishi vikuu, matatizo ya diski za mgongo (spinal disc issues) yanashika nafasi ya juu. Makala hii inatoa mwongozo wa kina kuhusu namna diski zinavyofanya kazi, nini kinatokea zinapoharibika, na muhimu zaidi, mikakati ya kitabibu na mazoezi yanayoweza kukusaidia kuepuka njia ya upasuaji na kurejesha ubora wa maisha yako.

Soma Zaidi...