Madhara ya kaswende kwa wajawazito na watoto wadogo.
Posti inahusu zaidi madhara ya kaswende kwa mama mjamzito na mtoto, Ni ugonjwa unaopatikana hasa kwa njia ya kujamiiana na utoka kwa mwenye Ugonjwa kwenda kwa mtu ambaye hana ugonjwa, kwa hiyo tunapaswa kujua madhara ya ugonjwa huu kwa mama mjamzito na mt
Madhara ya kaswende kwa wajawazito na watoto
1. Kwanza tuanze kwa Mama, ugonjwa huu usababisha Mimba kutoka kwa sababu Maambukizi uingilia sehemu ambayo imefungwa kwa ajili ya kuzuia kitu chochote kupita na kushambulia sehemu mbalimbali kwa mtoto hatimaye mimba utoka kwa hiyo hali hii inasababisha maumivu makali kwa mama na wote waliomzunguka.
2. Kujifungua mtoto mfu.
Kwa sababu ya Ugonjwa wa kaswende mama anaweza kubeba mimba kwa miezi tisa lakini baadaye akajifungua mtoto mfu, kwa hiyo Mama mjamzito anapaswa kupima kaswende pale anapoanza tu mahudhurio ya kliniki na kuanza kutumia dawa mara moja.
3. Kuzaa mtoto kilema.
Ugonjwa huu wa kaswende usababisha sana kuzaliwa kwa watoto walemavu kwa sababu ya kuwepo kwa Maambukizi ambayo ushambulia sehemu mbalimbali za mwili na kumfanya mtoto kuzaliwa akiwa na ulemavu na pia kuendelea kuwepo kwa ugonjwa huu umpata Mama kuingia kwenye risk ya kupata Maambukizi ya HIV na magonjwa mengine nyemelezi.
4. Pia na kwa mtoto mwenyewe kuna matokeo katika kuwa na ugonjwa huu ambapo ni pamoja na mtoto kuzaliwa akiwa na afya mbaya na kuwa na uzito mdogo ambapo wazazi utumia gharama na mda mwingi katika kumtibu mtoto, kwa hiyo mtoto akizaliwa tu anapaswa kupimwa kaswende kama hali yake sio nzuri kiafya na baba na Mama nao pia wanapaswa kupima ili kupewa madawa.
5. Jamii inapaswa kupewa elimu kuhusu ugonjwa huu, hasa wanawake wajawazito wanapaswa kuelezwa wazi na wahudumu wao au wauguzi kuhusu kupima na kupewa dawa ili kumkinga mtoto na hatari mbalimbali kama vile ulemavu wa viungo, kuzaliwa na kaswende na kuzaliwa mfu.
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
π1 Simulizi za Hadithi Audio π2 Kitau cha Fiqh π3 web hosting π4 ai web app π5 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w) π6 Tafasiri ya Riyadh Swalihina
Post zinazofanana:
Bawasili usababishwa na nini?
Posti hii inahusu zaidi visababishi vya ugonjwa wa Bawasili,kuna watu wengi wanapenda kujua kabisa chanzo cha kuwepo kwa ugonjwa wa Bawasili kwenye jamii na kuna maswali mengi yanayoulizwa kuhusu visababishi vya Bawasili.
Soma Zaidi...Kupunguzwa kwa kiwosi cha lehemu (Cholesterol) mwilini.
Lehemu (cholesterol) ni kiambato muhimu katika mwili wa binadamu, lakini kiwango chake kinapozidi kiasi kinachohitajika, huwa hatari kubwa kwa mfumo wa moyo na mishipa ya damu. Makala hii inatoa uchambuzi wa kitaalamu kuhusu taratibu za kupunguza lehemu mbaya (LDL), umuhimu wa uwiano wa lehemu nzuri (HDL), na mikakati ya kisayansi ya kudhibiti lehemu kupitia lishe, mazoezi, na dawa.
Soma Zaidi...Kuhara na kutapika (Cholera): Kinga na tiba ya haraka.
Kipindupindu ni ugonjwa hatari wa mfumo wa mmengβenyo wa chakula unaosababishwa na bakteria Vibrio cholerae. Ugonjwa huu husababisha kuhara sana na kutapika, hali inayosababisha upungufu mkali wa maji mwilini (dehydration) ambao unaweza kuua ndani ya saa chache ikiwa hautatibiwa. Makala hii inasisitiza umuhimu wa utambuzi wa haraka na uingizaji wa maji mwilini kama tiba kuu.
Soma Zaidi...Je maumivu juu ya kitovu ni miongoni mwa dalili za mimba?
Dalili za mimba zinaweza kuanzia kuonekana mapema ndani ya wiki ya kwanza, japo sio rahisi nabhakuna uthibitishobwa uhakika juu ya kauli hii. Makala hii itakwebda kujibubswali la msingi la muuulizaji kama maumivu ya tumbo ni dalili ya ujauzito.
Soma Zaidi...Dalili na Ishara za mawe kwenye figo
Mawe kwenye figo yana sababu nyingi na yanaweza kuathiri sehemu yoyote ya njia yako ya mkojo kutoka kwa figo hadi kibofu chako.
Soma Zaidi...Ugonjwa wa macho mekundu (Conjunctivitis): Jinsi ya kujikinga.
Ugonjwa wa macho mekundu, kitaalamu Conjunctivitis (au Pink eye), ni uvimbe wa utando mwororo unaofunika sehemu nyeupe ya jicho na ndani ya kope. Ugonjwa huu unaweza kusababishwa na virusi, bakteria, au mzio (allergy). Kwa kuwa ni rahisi sana kuambukiza, elimu kuhusu usafi wa kibinafsi na mbinu za kuzuia usambazaji ndizo nguzo kuu ya kudhibiti mlipuko wa ugonjwa huu ndani ya jamii.
Soma Zaidi...