Madhara ya kaswende kwa wajawazito na watoto wadogo.
Posti inahusu zaidi madhara ya kaswende kwa mama mjamzito na mtoto, Ni ugonjwa unaopatikana hasa kwa njia ya kujamiiana na utoka kwa mwenye Ugonjwa kwenda kwa mtu ambaye hana ugonjwa, kwa hiyo tunapaswa kujua madhara ya ugonjwa huu kwa mama mjamzito na mt
Madhara ya kaswende kwa wajawazito na watoto
1. Kwanza tuanze kwa Mama, ugonjwa huu usababisha Mimba kutoka kwa sababu Maambukizi uingilia sehemu ambayo imefungwa kwa ajili ya kuzuia kitu chochote kupita na kushambulia sehemu mbalimbali kwa mtoto hatimaye mimba utoka kwa hiyo hali hii inasababisha maumivu makali kwa mama na wote waliomzunguka.
2. Kujifungua mtoto mfu.
Kwa sababu ya Ugonjwa wa kaswende mama anaweza kubeba mimba kwa miezi tisa lakini baadaye akajifungua mtoto mfu, kwa hiyo Mama mjamzito anapaswa kupima kaswende pale anapoanza tu mahudhurio ya kliniki na kuanza kutumia dawa mara moja.
3. Kuzaa mtoto kilema.
Ugonjwa huu wa kaswende usababisha sana kuzaliwa kwa watoto walemavu kwa sababu ya kuwepo kwa Maambukizi ambayo ushambulia sehemu mbalimbali za mwili na kumfanya mtoto kuzaliwa akiwa na ulemavu na pia kuendelea kuwepo kwa ugonjwa huu umpata Mama kuingia kwenye risk ya kupata Maambukizi ya HIV na magonjwa mengine nyemelezi.
4. Pia na kwa mtoto mwenyewe kuna matokeo katika kuwa na ugonjwa huu ambapo ni pamoja na mtoto kuzaliwa akiwa na afya mbaya na kuwa na uzito mdogo ambapo wazazi utumia gharama na mda mwingi katika kumtibu mtoto, kwa hiyo mtoto akizaliwa tu anapaswa kupimwa kaswende kama hali yake sio nzuri kiafya na baba na Mama nao pia wanapaswa kupima ili kupewa madawa.
5. Jamii inapaswa kupewa elimu kuhusu ugonjwa huu, hasa wanawake wajawazito wanapaswa kuelezwa wazi na wahudumu wao au wauguzi kuhusu kupima na kupewa dawa ili kumkinga mtoto na hatari mbalimbali kama vile ulemavu wa viungo, kuzaliwa na kaswende na kuzaliwa mfu.
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 kitabu cha Simulizi 👉2 Kitabu cha Afya 👉3 Madrasa kiganjani 👉4 Dua za Mitume na Manabii 👉5 Bongolite - Game zone - Play free game 👉6 Simulizi za Hadithi Audio
Post zinazofanana:
Dalili na namna ya kujizuia na malaria
Postii hii inshusiana na dalili na ishara za kujikinga au kuzuia malaria kwa Njia mbalimbali.
Soma Zaidi...Kuchelewa kwa hedhi: Sababu 10 zinazoweza kuwa nje ya mimba.
Kuchelewa kwa hedhi ni hali inayowatokea wanawake wengi katika hatua mbalimbali za maisha yao. Ingawa ujauzito ndiyo sababu inayofikiriwa mara ya kwanza, kuna sababu nyingine nyingi za kibiolojia, kisaikolojia, na kiafya zinazoweza kuvuruga mzunguko wa hedhi. Makala hii inaangazia sababu 10 kuu zinazopelekea mzunguko wako kutokwenda kama ulivyozoea.
Soma Zaidi...Matumizi ya dawa za kulevya na athari zake kwenye ubongo.
Dawa za kulevya hazibadili tu tabia ya mtu, bali zinasababisha mabadiliko ya kudumu kwenye muundo na utendaji kazi wa ubongo. Makala haya yanachambua jinsi dawa hizi zinavyoiba mfumo wa furaha wa ubongo (reward system), na jinsi matumizi yake yanavyoweza kusababisha madhara ya kiakili na kimwili ambayo ni vigumu kuyatengua.
Soma Zaidi...Dalili za Ugonjwa wa ini
Posti hii inahusu zaidi dalili za ugonjwa wa inni, hizi ni dalili ambazo ujitokeza kwa mtu Mwenye ugonjwa wa inni, Dalili zenyewe ni kama ifuatavyo.
Soma Zaidi...Fangasi wanaojulikana kama Blastomyces
Fangasi wanaojulikana kama Blastomyces, hawa ni fangasi wanaosababisha maradhi yajulikanayo kama blastomycosis.
Soma Zaidi...