Madhara ya kaswende kwa wajawazito na watoto wadogo.
Posti inahusu zaidi madhara ya kaswende kwa mama mjamzito na mtoto, Ni ugonjwa unaopatikana hasa kwa njia ya kujamiiana na utoka kwa mwenye Ugonjwa kwenda kwa mtu ambaye hana ugonjwa, kwa hiyo tunapaswa kujua madhara ya ugonjwa huu kwa mama mjamzito na mt
Madhara ya kaswende kwa wajawazito na watoto
1. Kwanza tuanze kwa Mama, ugonjwa huu usababisha Mimba kutoka kwa sababu Maambukizi uingilia sehemu ambayo imefungwa kwa ajili ya kuzuia kitu chochote kupita na kushambulia sehemu mbalimbali kwa mtoto hatimaye mimba utoka kwa hiyo hali hii inasababisha maumivu makali kwa mama na wote waliomzunguka.
2. Kujifungua mtoto mfu.
Kwa sababu ya Ugonjwa wa kaswende mama anaweza kubeba mimba kwa miezi tisa lakini baadaye akajifungua mtoto mfu, kwa hiyo Mama mjamzito anapaswa kupima kaswende pale anapoanza tu mahudhurio ya kliniki na kuanza kutumia dawa mara moja.
3. Kuzaa mtoto kilema.
Ugonjwa huu wa kaswende usababisha sana kuzaliwa kwa watoto walemavu kwa sababu ya kuwepo kwa Maambukizi ambayo ushambulia sehemu mbalimbali za mwili na kumfanya mtoto kuzaliwa akiwa na ulemavu na pia kuendelea kuwepo kwa ugonjwa huu umpata Mama kuingia kwenye risk ya kupata Maambukizi ya HIV na magonjwa mengine nyemelezi.
4. Pia na kwa mtoto mwenyewe kuna matokeo katika kuwa na ugonjwa huu ambapo ni pamoja na mtoto kuzaliwa akiwa na afya mbaya na kuwa na uzito mdogo ambapo wazazi utumia gharama na mda mwingi katika kumtibu mtoto, kwa hiyo mtoto akizaliwa tu anapaswa kupimwa kaswende kama hali yake sio nzuri kiafya na baba na Mama nao pia wanapaswa kupima ili kupewa madawa.
5. Jamii inapaswa kupewa elimu kuhusu ugonjwa huu, hasa wanawake wajawazito wanapaswa kuelezwa wazi na wahudumu wao au wauguzi kuhusu kupima na kupewa dawa ili kumkinga mtoto na hatari mbalimbali kama vile ulemavu wa viungo, kuzaliwa na kaswende na kuzaliwa mfu.
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
π1 Bongolite - Game zone - Play free game π2 Kitabu cha Afya π3 Dua za Mitume na Manabii π4 Tafasiri ya Riyadh Swalihina π5 ai web app π6 web hosting
Post zinazofanana:
Dalili za ugonjwa sugu wa Figo.
Ugonjwa sugu wa figo, pia huitwa kushindwa kwa figo sugu, huelezea upotevu wa taratibu wa utendakazi wa figo. Figo zako huchuja taka na Majimaji kupita kiasi kutoka kwa damu yako, ambayo hutolewa kwenye mkojo wako. Ugonjwa sugu wa figo unapofikia hatua
Soma Zaidi...Njia za kuzuia kiungulia
Somo hili linakwenda kukueleza baadhi ya njia za kuzuia kiungulia
Soma Zaidi...Kukosa hamu ya kufanya chochote: Nini cha kufanya?
βKatika ulimwengu wa sasa wenye kasi kubwa, kukumbwa na hali ya kukosa hamu ya kufanya chochote (ambayo kitaalamu hujulikana kama avolition au apathy) ni changamoto inayowakabili watu wengi. Makala hii inachunguza visababishi vya hali hii, athari zake katika maisha ya kila siku, na kutoa mikakati madhubuti ya kurejesha ari, nguvu, na motisha ya kufanya kazi na kufurahia maisha.
Soma Zaidi...Tetekuwanga kwa watu wazima: Ni hatari zaidi?
Tetekuwanga (Varicella) kwa kawaida huchukuliwa kama ugonjwa wa utotoni, na watoto wengi huupata na kupona bila matatizo makubwa. Hata hivyo, unapoupata ukiwa mtu mzima, hali inabadilika. Tetekuwanga kwa watu wazima huchukuliwa kuwa na hatari zaidi, ikiwa na uwezekano mkubwa wa kusababisha dalili kali na maambukizi ya viungo muhimu kama mapafu. Makala haya yanafafanua kwa nini hali hii ni hatari na nini unapaswa kufanya.
Soma Zaidi...Maumivu ya miguu na ganzi nyakati za usiku.
Maumivu ya miguu na ganzi nyakati za usiku ni malalamiko ya kawaida yanayoathiri ubora wa maisha na usingizi. Makala haya yanachunguza visababishi mbalimbali vya kiafya kama vile matatizo ya neva (neuropathy), mzunguko wa damu hafifu, na upungufu wa virutubisho, huku yakitoa mikakati ya kitaalamu ya kupunguza usumbufu huu na kuboresha afya ya mfumo wa neva.
Soma Zaidi...Dawa za kuua wadudu (Antibiotics): Matumizi sahihi na hatari zake.
βDawa za kuua vimelea, maarufu kama antibiotics, ni moja ya uvumbuzi muhimu zaidi katika historia ya tiba ya kisasa. Zimeokoa mamilioni ya maisha kwa kutibu maambukizi ya bakteria. Hata hivyo, matumizi yasiyo sahihi, yasiyo ya lazima, na yasiyokamilika yamesababisha ongezeko la hatari ya "usugu wa dawa" (Antimicrobial Resistance - AMR). Makala haya yanachunguza kwa kina jinsi ya kutumia dawa hizi kwa usahihi, madhara yake, na hatua za kuchukua ili kulinda ufanisi wa dawa hizi kwa vizazi vijavyo.
Soma Zaidi...