darasa la lishe

Jifunze mengi kuhusu afya na lishe, ujuwe utaratibu wa lishe

darasa la lishe

1.VYAKULA VYA KUPAMBANA NA SARATANI

Kansa ni katika magonjwa yanayosumbuwa kwa kiasi kikubwa leo duniani. Kansa huweza kusababishwa na vitu mbalimbali ikiwemo uvutaji wa sigara kwa 31%, vyakula kwa 37%, pombe kwa 3% na nyingine nyingi. Katika sababu hizi vyakula huchukuwa nafasi kubwa katika kusababisha kansa.

Mwaka 2015 watu milioni 90.5 waligungulika kuwa na kansa. Inakadiriwa kuwa kila mwaka takribani watu milioni 14.1 wanaupata kansa kila mwaka. Watu milioni 15.7 walikufa na kansa ambayo ni sawa na asilimia 15.7% ya vifo vyote mwaka huo.

1. VITUNGUU SAUMU ( GARLIC) Hivi vina kiasi kikubwa cha madini ya salfa (sulphur compounds) ambayo husaidia kuimarisha mfumo wa afya mwilini (immune system) Pia wanasayansi wanafahamu kuwa kitunguu thaumu kinasaidia katika kupunguza uwezekano wa kupata kansa ya tumbo.

2. Samaki Tafiti za kisayansi zilizofanyika Australia zimegunduwa kuwa ulaji wa samaki mara 4 au zaidi humuepusha mtu na kansa ya damu ( blood cancers leukemia, myekoma, and non- Hodgkin's lymphoma). Samaki wanaoshauriwa zaidi ni wale wenye mafuta kwa wingi kama salmon.

Kama ilivyoosheshwa kuwa mpangilio mbovu wa vyakula na uvutaji wa sigara huchangia kwa kiasi kikubwa kupata kansa, leo tutakuletea baadhi ya vykula ambavyo vinasadikika kupambana na kansa. Vyakila hivi huweza kuzuia seli za kansa kutengenezwa ndani ya mwili na kutowa msaada wa kupambana na zo . Vipo vyakula vingi tuu lakini kwa uchache tunakuletea hivi kwa leo;-

3. Apple (maepo) Matunda haya yanafahamika kwa uwezo wake mkubwa wa kuuwa seli za kansa. Tafiti za kisayansi zilizofanywa nchini Ujerumani zinathibitisha uwepo wa procyanidins ambayo hufahamika kudhibiti seli za kansa kutengenezwa ndani ya mwili.

4. Avocado (palachichi) Matunda haya pia husaidia kwa kiwango kikubwa kupambana na seli za kansa. Fat iliyoko kwenye matunda haya huweza kusaidia kwa iwango kikubwa kupambana na kansa.

5. Kabichi ( cabbage) Kabichi hujulikana kwa kuwa na bioflavonoids kemikali ambazo hupambana na seli za kansa. Kabichi kusaidia kupambana na kansa ya tumbo kansa ya matiti na aina zingine za kansa.

6. Karoti ( carrots) Karoti zina alpha-carotene na bioflavonoids ambazo husaidia katika kupambana na seli za kansa. Karoti huweza kupambana hasa na kansa ya ini. Wanasayansi pia wanatahadharisha matumizi ya karoti kwa kiasi kikubwa kwa mtu anayevuta sigara.

7.Tende Tende hujulikana kuwa na polyphenols ambazo husaidia kupambana na kansa kwa kiwango kikubwa. Vitamin B12 na fiber katika tende husaidi kwa kuiwango kupambana na aina mbalimbali za kansa.

8. Mayai yana vitamin D kwa kiwango kukubwa. Vitamin hivi pia hufahamika kwa uwezo wake wa kupambana na seli za kansa.

9. Tangawizi

10. Komamanga

11. njegere MWISHO Tungependa kutoa ushauri kwa dada na ndugu hao ambao huvuta na kunywa pombe kwamba haya yote yana kemikali ambazo zinajulikana kwa kuwa na uwezo wa kusababisha kansa. Kwa hivyo wanapaswa kuchukua maandalizi kabla hali inakuwa mbaya zaidi katika afya yao.


                   

Kama unahitaji kuuliza maswali Bofya hapa

Mwandhishi Tarehe 2018-08-01     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 996

Post zifazofanana:-

TAMBUA NAMNA YA KUTOA HUDUMA YA KWANZA WAKATI WA DHARURA, AJALI NA HATARI
Soma Zaidi...

MADHARA YA KIAFYA YANAYOHUSIANA NA MINYOO: kuliwa kwa tishu, damu, ini na nyama, kuisha damu, kutapika,
MADHARA YA KIAFYA YANAYOHUSIANA NA MINYOO Tofauti na madhara ambayo tumeyaona huko juu kwenye dalili kama maumivu ya kicha, tumbo na miwasho, kichefuchefu na kutapika. Soma Zaidi...

What is Chemisty?
The meaning of a word chemistry by difinition Soma Zaidi...

MAAJABU YA MBU
7. Soma Zaidi...

SHIRK
Jifunze tawhid yaani kumpwekesha Allah subhaanah wata'aala Soma Zaidi...

Darsa za Sira historia ya Mtume (s.a.w) Jaribio la 04
Soma Zaidi...

Mafunzo Yatokanayo na Historia ya Nabii Isa(a.s)
Kutokana na Historia ya Nabii Isa(a. Soma Zaidi...

Mtume(s.a.w) Kulingania Uislamu Katika Mji wa Taif
Baada tu ya Mtume(s. Soma Zaidi...

Umuhimu wa swala
Umuhimu wa KusimamishaSwala Kwa mujibu wa Hadith ya Ibn Umar (r. Soma Zaidi...

Namna ya kutambuwa kibla na umuhimu wa kuelekea kibla wakati wa kuswali
4. Soma Zaidi...

NINI MAANA YA SWALA (SALA AU KUSWALI), KILUGHA NA KISHERIA KATIKA UISLAMU
Maana ya Swala Maana ya Swala kilugha(a) Kilugha Katika lugha ya Kiarabu neno 'Swalaat' lina maana ya 'ombi au 'dua. Soma Zaidi...

hadithi ya 8
' ' ' ' ' ' ' ' ' ' ' ' ' ' ': "' ' ' ' ' ?... Soma Zaidi...