1.
1.2.Kwa Nini Mwanaadamu Hawezi Kuunda Dini Sahihi ?
Au
Haja ya kuhitaji mwongozo kutoka kwa Mwenyezi Mungu (s.w).
Mwanaadamu pamoja na ujuzi na utundu alionao, hana uwezo wa kujiundia dini sahihi (mfumo sahihi wa maisha) utakaomfikisha na kumbakisha kwenye lengo la kuumbwa kwake. Na hii ni kutokana na sababu zifuatazo;
(a)Mwanaadamu anaathiriwa na matashi ya kibinafsi;
Pamoja na ujuzi, utambuzi na vipawa alivyopewa mwanaadamu, bado uamuzi na fikra zake ziaathiriwa na matashi ya nafsi yake katika upendeleo, uonevu na chuki, hivyo hawezi kuunda mfumo utakaosimamia haki na uadilifu.
(b)Nyenzo anazotumia mwanaadamu kujielimisha ni dhaifu;
Mwanaadamu hujielimisha kupitia nyenzo zifuatazo;
i.Milango ya fahamu.
Kama vile pua, masikio, ulimi, macho, ngozi, n.k, ambavyo vyote vina udhaifu na mara nyingine hutoa taarifu zisizo na ukweli.
ii.Akili na fikra.
Uamuzi wa mwanaadamu wa akili na fikra peke yake hauwezi kutoa jibu/mwongozo sahihi wa maisha kwani huathiriwa na wakati, matashi, mazingira, uelewa, upeo wa kufikiri na pia una kikomo.
Rejea Qurโan (10:36,66), (25:43,45), (6:116) na (28:60)
iii.Sayansi na Uchunguzi;
Sayansi na majaribio haviwezi kutumika kama nyenzo kuu ya kuunda muongozo sahihi kwani vyote hivyo vinategemea milango ya fahamu ambayo nayo ina madhaifu mengi na kikomo pia.
iv.Historia;
Kutumia uzoefu wa kihistoria katika kuunda muongozo sahihi wa maisha ni dhaifu kwa sababu mwanaadamu huathiriwa na uzoefu na ujuzi wa awali na hivyo kutokubaliana na mabadiliko yeyote yatakayojitokeza.
Rejea Qurโan (2:170, 257), (5:104) na (6:116).
Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiw ana App yetu. Bofya liln hapo chini kuweza ku download
Download NowJe! umeipenda hii post?
Ndio Hapana Save post
Rajabu Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Topic: Main: Post File: Download PDF Share On Facebook or Whatsapp Views 431
Sponsored links
๐1
Kitabu cha Afya
๐2
Madrasa kiganjani
๐3
Simulizi za Hadithi Audio
๐4
Kitau cha Fiqh
๐5
Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)
๐6
kitabu cha Simulizi
swala za tahiyatu al masjid, qabliya na baadiya
Muislamu anapoingia Msikitini kabla hajakaa anatakiwa aswali rakaa mbili za maamkizi ya msikiti, Tahiyyatul-Masjid. Soma Zaidi...
Uthibitisho Kuwa Qurโan ni Neno la Mwenyezi Mungu (s.w)
Soma Zaidi...
Ni nini maana ya ndoa?
Soma Zaidi...
Hukumu ya zakat Al-Fitir na namna ya kuitoa zaka ya fitir
Soma Zaidi...
DARSA ZA TAWHID
Jifunze tawhid yaani kumpwekesha Allah subhaanah wata'aala Soma Zaidi...
UANDISHI WA HADITHI WAKATI WA TABI'I TABI'IIN
Wakati wa Wafuasi wa Masahaba (Tabi'i Tabi'ina)201-300 A. Soma Zaidi...
swala ya kuomba mvua na namna ya kuiswali
12. Soma Zaidi...
Sababu Ya Uislamu Kuwa Ndiyo Dini Sahihi Pekee
1. Soma Zaidi...
Kuamini Mwenyezi Mungu sio suala la Kibubusa au Kufuata Mkumbo
Kuamini Mwenyezi Mungu sio suala la Kibubusa au Kufuata Mkumbo. Soma Zaidi...