Kwa Nini Mwanaadamu Hawezi Kuunda Dini Sahihi ?
1.
1.2.Kwa Nini Mwanaadamu Hawezi Kuunda Dini Sahihi ?
Au
Haja ya kuhitaji mwongozo kutoka kwa Mwenyezi Mungu (s.w).
Mwanaadamu pamoja na ujuzi na utundu alionao, hana uwezo wa kujiundia dini sahihi (mfumo sahihi wa maisha) utakaomfikisha na kumbakisha kwenye lengo la kuumbwa kwake. Na hii ni kutokana na sababu zifuatazo;
(a)Mwanaadamu anaathiriwa na matashi ya kibinafsi;
Pamoja na ujuzi, utambuzi na vipawa alivyopewa mwanaadamu, bado uamuzi na fikra zake ziaathiriwa na matashi ya nafsi yake katika upendeleo, uonevu na chuki, hivyo hawezi kuunda mfumo utakaosimamia haki na uadilifu.
(b)Nyenzo anazotumia mwanaadamu kujielimisha ni dhaifu;
Mwanaadamu hujielimisha kupitia nyenzo zifuatazo;
i.Milango ya fahamu.
Kama vile pua, masikio, ulimi, macho, ngozi, n.k, ambavyo vyote vina udhaifu na mara nyingine hutoa taarifu zisizo na ukweli.
ii.Akili na fikra.
Uamuzi wa mwanaadamu wa akili na fikra peke yake hauwezi kutoa jibu/mwongozo sahihi wa maisha kwani huathiriwa na wakati, matashi, mazingira, uelewa, upeo wa kufikiri na pia una kikomo.
Rejea Qurβan (10:36,66), (25:43,45), (6:116) na (28:60)
iii.Sayansi na Uchunguzi;
Sayansi na majaribio haviwezi kutumika kama nyenzo kuu ya kuunda muongozo sahihi kwani vyote hivyo vinategemea milango ya fahamu ambayo nayo ina madhaifu mengi na kikomo pia.
iv.Historia;
Kutumia uzoefu wa kihistoria katika kuunda muongozo sahihi wa maisha ni dhaifu kwa sababu mwanaadamu huathiriwa na uzoefu na ujuzi wa awali na hivyo kutokubaliana na mabadiliko yeyote yatakayojitokeza.
Rejea Qurβan (2:170, 257), (5:104) na (6:116).
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
π1 web hosting π2 Simulizi za Hadithi Audio π3 Bongolite - Game zone - Play free game π4 Kitabu cha Afya π5 Kitau cha Fiqh π6 Tafasiri ya Riyadh Swalihina
Post zinazofanana:
swala za tahiyatu al masjid, qabliya na baadiya
Muislamu anapoingia Msikitini kabla hajakaa anatakiwa aswali rakaa mbili za maamkizi ya msikiti, Tahiyyatul-Masjid.
Soma Zaidi...ushahidi juu ya Dalili Za Kuwepo Mwenyezi Mungu (S.W)
Dalili Za Kuwepo Mwenyezi Mungu (S.
Soma Zaidi...