1.
1.2.Kwa Nini Mwanaadamu Hawezi Kuunda Dini Sahihi ?
Au
Haja ya kuhitaji mwongozo kutoka kwa Mwenyezi Mungu (s.w).
Mwanaadamu pamoja na ujuzi na utundu alionao, hana uwezo wa kujiundia dini sahihi (mfumo sahihi wa maisha) utakaomfikisha na kumbakisha kwenye lengo la kuumbwa kwake. Na hii ni kutokana na sababu zifuatazo;
(a)Mwanaadamu anaathiriwa na matashi ya kibinafsi;
Pamoja na ujuzi, utambuzi na vipawa alivyopewa mwanaadamu, bado uamuzi na fikra zake ziaathiriwa na matashi ya nafsi yake katika upendeleo, uonevu na chuki, hivyo hawezi kuunda mfumo utakaosimamia haki na uadilifu.
(b)Nyenzo anazotumia mwanaadamu kujielimisha ni dhaifu;
Mwanaadamu hujielimisha kupitia nyenzo zifuatazo;
i.Milango ya fahamu.
Kama vile pua, masikio, ulimi, macho, ngozi, n.k, ambavyo vyote vina udhaifu na mara nyingine hutoa taarifu zisizo na ukweli.
ii.Akili na fikra.
Uamuzi wa mwanaadamu wa akili na fikra peke yake hauwezi kutoa jibu/mwongozo sahihi wa maisha kwani huathiriwa na wakati, matashi, mazingira, uelewa, upeo wa kufikiri na pia una kikomo.
Rejea Qurβan (10:36,66), (25:43,45), (6:116) na (28:60)
iii.Sayansi na Uchunguzi;
Sayansi na majaribio haviwezi kutumika kama nyenzo kuu ya kuunda muongozo sahihi kwani vyote hivyo vinategemea milango ya fahamu ambayo nayo ina madhaifu mengi na kikomo pia.
iv.Historia;
Kutumia uzoefu wa kihistoria katika kuunda muongozo sahihi wa maisha ni dhaifu kwa sababu mwanaadamu huathiriwa na uzoefu na ujuzi wa awali na hivyo kutokubaliana na mabadiliko yeyote yatakayojitokeza.
Rejea Qurβan (2:170, 257), (5:104) na (6:116).
Je! umeipenda hii post?
Ndio Hapana Save post
Rajabu Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Topic: Main: Post File: Download PDF Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 226
Sponsored links
π1 Kitau cha Fiqh
π2 kitabu cha Simulizi
π3 Simulizi za Hadithi Audio
π4 Kitabu cha Afya
π5 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)
π6 Madrasa kiganjani
KUAMINI MALAIKA
Jifunze tawhid yaani kumpwekesha Allah subhaanah wata'aala Soma Zaidi...
nguzo za uislamu
Soma Zaidi...
Siku ya Taqwiya na kusimama Arafa
5. Soma Zaidi...
Presha ya kupanda (hypertension) dalili zake, na njia za kukabiliana nayo
Soma Zaidi...
ukweli na sifa zake kwenye uislamu na sifa za mtu mkweli
Ukweli ni uhakika wa jambo. Soma Zaidi...
Zijuwe suna (sunnah) za Udhu ama Kutawadha
Soma Zaidi...
Haya ndio matendo ya hija
Soma Zaidi...
2.3.Kuamini Vitabu Vya Mwenyezi Mungu (s.w Quran, tawrat, Zabur na injili
2. Soma Zaidi...
Je mahari inashusha hadhi ya mwanamke?
Je, Mahari inashusha hadhi ya mwanamke? Soma Zaidi...
Hadithi aliyoisimulia Kijakazi kwa sultan
Soma Zaidi...
kusai yaani kukimbia kati ya mlima swafa na marwa mara saba
4. Soma Zaidi...