Menu



Ni nini maana ya Tajwid, na ni ipi nafasi yake kwenye uislamu

Hapa utajifunza maana ya Tajwid kilugha na kisheria. Pia nitakujuza jukumu ya kusoma tajwid.

Neno ‘Tajwiyd ’
linatoka na neno جَ و د (jawwada) kilugha ina maana ‘ufundi’, yaani kufanya kitu kwa uhodari au ustadi.
Maana yake Kishariy’ah: Kuitamka kila herufi kama inavyotakiwa kutamkwa, kwa kuipa haki yake na swiffah zake huku ukifuata hukmu zote za Tajwiyd.



Katika qurani na sunnah imehimizwa sana kusoma qurani kwa tajwid au tartila. Elimu hii ya tajwid imeanza zamani toka enzi za masahaba na toka mtume yupo hai. Pia alikuwa Mtume akiwaelekeza masahaba kwa watu maalumu ili wapate kujifunza qurani kiufasaha. Imepokewa kuwa Mtume (s.a.w) amesema: ((Mwenye kupenda kuisoma Qur-aan kama vile ilivyoteremshwa basi na asome kwa Qiraa-ah [kisomo] cha ibn Ummi ‘Abd)) (amepokea Ibn Majah na ahmad)



Pia Allah amesema :وَرَتِّلِ ٱلْقُرْءَانَ تَرْتِيلً “na soma Qur-aan kwa tartiylaa (kisomo cha utaratibu upasao” Katika kuonesha maana ya neno tartiyla ‘Aly Ibn Abi Talib ambaye ni khalifa wa nne baada ya kufariki mtume amesema: التَّتيلُ هُوَ تَجيد الحْوفَ ومَ عْ رِفةِ الوقوفِ “Ni kuisoma Qur-aan kwa ujuzi wa kutamka herufi ipasavyo na kuwa na ujuzi wa hukmu za kusimama”
Hukumu ya kujifunza tajwid:


Kusoma qurani bila ya tajwid yaani kuchunga herufi ni katika makosa mbele ya maulamaa wa tajwid. Maulamaa wa elimu hii wanazungumza kuwa kujifunza tajwid ni faradh al-kifaya kwa kauli za walio wengi. Pia wapo wanaosema ni faradh ‘ayn yaani ni faradhi ya lazima kwa kila muislamu.



Hawa waliosema ni faradhi kifaya yaani sio faradhi ya lazima kwa wote ila inatosha kwa wachache wakiwa na elimu hii, kundi hili pia linazungumza kuwa inapasa kwa msomaji asisome kwa kukosea ijapokuwa hajui hukumu za tajwiid. Yaani achunge matamchi kama yalivyoandikwa asije akatamka vinginevyo na kubadilisha maana.
 

Download app yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiw ana App yetu. Bofya liln hapo chini kuweza ku download

Download Now Bongoclass

           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu image Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Topic: Quran Main: Post File: Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Views 1804


Sponsored links
👉1 Kitabu cha Afya     👉2 Simulizi za Hadithi Audio     👉3 Madrasa kiganjani     👉4 kitabu cha Simulizi     👉5 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)     👉6 Kitau cha Fiqh    

Post zifazofanana:-

HUKUMU ZA IDGHAM
Jifunze namna ya kusoma quran, pata mafunzo ya tajwid hapa Soma Zaidi...

Sababu za kushuka kwa surat Dhuha
Sura hii imetermka Makkah na ina aya 11. Sura hii ni moja ya sura ambazo zimeshuka mwanzoni wakati ambapo Mtume ameanza kazi ya utume. Soma Zaidi...

Kukusanywa na kuhifadhiwa kwa quran
Quran (EDK form 3: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

quran na sayansi
YALIYOMONENO LA AWALI1. Soma Zaidi...

Wanaadamu kushindwa Kuandika Kitabu Mithili ya Qur-an:
Soma Zaidi...

Nini maana ya Quran
Post hii inakwenda kukuambia maana ya Quran Soma Zaidi...

Sababu za kushuka kwa Surat Al-Asr
Surat Al-Asri imeteremshwa Makka, na hapa utazujuwa sababu za kushuka kwa sura hii Soma Zaidi...

Maana ya Quran na Majina ya quran n amaana zao
Soma Zaidi...

Hukumu ya tafkhim na tarqiq katika usomaji wa Quran tajwid
Tarqiq ni kuisoma herufi kwa kuipa wepesi na tqfkhim ni kuisoma herufi kwa kuipa uzito. Soma Zaidi...

quran na tajwid
TAJWID Utangulizi wa elimu ya Tajwid YALIYOMO SURA YA 01 . Soma Zaidi...