Uhakiki wa Hadith za Mtume (s.
Uhakiki wa Hadith za Mtume (s.a.w)
Kwa kuwa Hadith hazikuwa na ahadi ya Allah (s.w) ya hifadh kama ilivyo kwa Qur-an - "Hakika sisi ndio tulioteremsha mawaidha haya (Qur-an) na hakika sisi ndio tutakaoyalinda". (15:9) - walitokea watu waovu wakamzulia Mtume (s.a.w) mambo mengi yaliyokinyume kabisa na Uislamu wenyewe.
Hili liliwastua wanazuoni wacha-Mungu na kuwafanya wawajibike kuweka utaratibu maalumu wa kuchambua Hadith za Mtume (s.a.w). Katika harakati za uchambuzi wa Hadith, wanazuoni wa Hadith waliigawa Hadith katika sehemu kuu mbili - Isnad na Matin.
Isnad ni sehemu ya Hadith inayoonyesha msururu wa wapokezi wa Hadith hiyo tokea kwa yule aliyemsikia Mtume (s.a.w) akieleza jambo au aliyemuoma Mtume akifanya jambo, au aliyemuona Mtume akiridhia au akithibitisha jambo lililofanyika mbele yake au akieleza tabia ya Mtume (s.a.w) kama alivyoiona.
Mfano wa Isnad:
AmetuHadithia Abdallah bin Yusuf toka kwa Malik toka kwa Abizinadi toka kwa A'araji toka kwa Abu Hurairah ambaye amesema: Hakika ya Mtume wa Allah (s.a.w) amesema: ……………." (Bukhari)
Kwa hiyo msururu wa watu wote hao kuanzia yule aliyemsikia Mtume (s.a.w), Abu Hurairah (r.a) ambaye ni sahaba wa Mtume, hadi kumfikia Bukhari ambaye ni Imamu wa Hadith aliyeipokea na kuiandika ndio Isnad.
Matin ni kauli ya Mtume au matendo yake.
Mfano wa Matin:
Mtume (s.a.w) amesema: “Yule ashikaye silaha dhidi yetu si pamoja na sisi." (Muslimu) Maneno aliyosema Mtume (s.a.w) yaliyofungiwa kwenye "…………………….." ndio matin ya Hadith hii. Riwaya
Matin moja ya Hadith inaweza kuripotiwa na msururu wa wapokezi (Isnaad) zaidi ya moja.
Kwa mfano:
Mtume (s.a.w) amesema "Yule ashikaye silaha dhidi yetu si pamoja sisi." (Muslimu) Maneno haya aliyosema Mtume (s.a.w) yamesimuliwa katika riwaya tatu zifuatazo:
1. “Abdullah bin Umar ameeleza kuwa Mtume wa Allah amesema: "Yule ashikaye silaha dhidi yetu si pamoja na sisi." (Muslimu)
2. Ilyas bin Salama ameHadith a kutoka kwa baba yake kuwa Mtume wa Allah amesema: "Yule ashikaye upanga (silaha) dhidi yetu si pamoja na sisi." (Muslimu)
3. Abu Musa Ashiari amesema kuwa Mtume wa Allah amesema: "Yule ashikaye silaha dhidi yetu si pamoja na sisi. (Muslimu)
Uhakiki wa Isnad
Katika harakati za kuchuja Hadith zilizosahihi na zisizo sahihi; wanazuoni wa Hadith walikuwa wakifuatilia kwa undani historia ya wale wote waliomo kwenye msururu wa wapokezi wa Hadith na kumchunguza mtu wa kwanza kuHadith a Hadith hiyo kuwa kweli alikuwa Swahaba balegh na Mkalafi aliyekuwa na uwezo wa kumsikia au kumuona Mtume (s.a.w).
Kwa ujumla, ili Hadith iwe sahihi, kila msimulizi katika Isnad alitakiwa awe Muislamu mwaminifu, mwenye kumbukumbu nzuri, mwenye tabia njema na mcha-Mungu.
Uhakiki wa Matin
Pamoja na kuwa na usahihi katika upokezi wa Hadith, "Matin" ya Hadith inaweza isiwe sahihi. Hivyo Hadith itakuwa shihi iwapo sehemu zote kwa pamoja - Isnad na Matin vitakuwa sahihi. Matin ya Hadith itakuwa sahihi iwapo itatekeleza masharti yafuatayo:
(i) Isipingane na Qur-an.
(ii) Isipingane na Hadith nyingine iliyothibitishwa kuwa ni sahihi.
(iii) Isimzulie Mtume (s.a.w) kufanya jambo ambalo ni kinyume na Uislamu.
(iv) Isipingane na hakika (fact)
(v) Isipingane na ukweli unaothibitishwa na historia.
(vi) Isiwe na maneno ya uongo ndani yake.
(vii) Isiwe inaahidi adhabu kali sana kwa kosa dogo sana na isiwe imeahidi malipo makubwa sana kwa wema mdogo sana.
Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiw ana App yetu. Bofya liln hapo chini kuweza ku download
Download NowJe! umeipenda hii post?
Ndio Hapana Save post
Rajabu Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Topic: Sunnah Main: Post File: Download PDF Share On Facebook or Whatsapp Views 643
Sponsored links
👉1
Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)
👉2
Simulizi za Hadithi Audio
👉3
Kitau cha Fiqh
👉4
Madrasa kiganjani
👉5
kitabu cha Simulizi
👉6
Kitabu cha Afya
MAANA NA FADHILA ZA KUOMBA DUA
DUA Kwa ufupi dua ni kumuomba Allah akuondoshee lililobaya, ama linalo kuudhi ama akupe jambo fulani. Soma Zaidi...
Sura za kujikinga na Uchawi na mashetani
Post hii itakwenda kukufundisha sura katika Quran ambazo ni kinga dhidi ya Wachawi, uchawi na Masheitwani. Soma Zaidi...
hadithi ya 8
عَنْ ابْنِ عُمَرَ رَضِيَ اللَّهُ عَنْهُمَا، أَنَّ رَسُولَ اللَّهِ صلى الله عليه و سلم قَالَ: "أُمِرْتُ أَنْ أُقَاتِلَ النَّاسَ حَتَّى ?... Soma Zaidi...
ADABU ZA KUOMBA DUA
ADABU ZA KUOMBA DUA. Soma Zaidi...
DUA ZENYE MANENO HAYA HUJIBIWA
SIFA ZA (MANENO NA MATAMSHI YA) DUA YENYE KUJIBIWA. Soma Zaidi...
Hadithi Ya 25: Wenye Mali Wameondoka Na Fungu (jaza) Kubwa
Soma Zaidi...
JINSI YA KUOMBA DUA ILI IKUBALIWE NA ALLAH
Kukubaliwa kwa dua kunategemea mahusiano yako na Allah. hata hivyo kuna baadhi ya mabo ukiyafanya dua yako inaweza kukubaliwa kwa haraka zaidi. Post hii inakwenda kukufundisha kuhusu jinsi ya kuomba dua ikubaliwe. Soma Zaidi...
DUA YA MUUMINI NA DUA YA KAFIRI
DUA YA KAFIRI NA DUA YA MUUMINI. Soma Zaidi...