UHAKIKI WA HADITHI

Uhakiki wa Hadith za Mtume (s.

UHAKIKI WA HADITHI

Uhakiki wa Hadith za Mtume (s.a.w)
Kwa kuwa Hadith hazikuwa na ahadi ya Allah (s.w) ya hifadh kama ilivyo kwa Qur-an - "Hakika sisi ndio tulioteremsha mawaidha haya (Qur-an) na hakika sisi ndio tutakaoyalinda". (15:9) - walitokea watu waovu wakamzulia Mtume (s.a.w) mambo mengi yaliyokinyume kabisa na Uislamu wenyewe.  Hili liliwastua wanazuoni wacha-Mungu na kuwafanya wawajibike kuweka utaratibu maalumu wa kuchambua Hadith za Mtume (s.a.w). Katika harakati za uchambuzi wa Hadith, wanazuoni wa Hadith waliigawa Hadith katika sehemu kuu mbili - Isnad na Matin.

Isnad ni sehemu ya Hadith inayoonyesha msururu wa wapokezi wa Hadith hiyo tokea kwa yule aliyemsikia Mtume (s.a.w) akieleza jambo au aliyemuoma Mtume akifanya jambo, au aliyemuona Mtume akiridhia au akithibitisha jambo lililofanyika mbele yake au akieleza tabia ya Mtume (s.a.w) kama alivyoiona.
Mfano wa Isnad:
AmetuHadithia Abdallah bin Yusuf toka kwa Malik toka kwa Abizinadi toka kwa A'araji toka kwa Abu Hurairah ambaye amesema: Hakika ya Mtume wa Allah (s.a.w) amesema: ……………." (Bukhari) Kwa hiyo msururu wa watu wote hao kuanzia yule aliyemsikia Mtume (s.a.w), Abu Hurairah (r.a) ambaye ni sahaba wa Mtume, hadi kumfikia Bukhari ambaye ni Imamu wa Hadith aliyeipokea na kuiandika ndio Isnad. 

Matin ni kauli ya Mtume au matendo yake.
Mfano wa Matin:
Mtume (s.a.w) amesema: “Yule ashikaye silaha dhidi yetu si pamoja na sisi." (Muslimu) Maneno aliyosema Mtume (s.a.w) yaliyofungiwa kwenye "…………………….." ndio matin ya Hadith hii. Riwaya Matin moja ya Hadith inaweza kuripotiwa na msururu wa wapokezi (Isnaad) zaidi ya moja.
Kwa mfano:
Mtume (s.a.w) amesema "Yule ashikaye silaha dhidi yetu si pamoja sisi." (Muslimu) Maneno haya aliyosema Mtume (s.a.w) yamesimuliwa katika riwaya tatu zifuatazo:
1. “Abdullah bin Umar ameeleza kuwa Mtume wa Allah amesema: "Yule ashikaye silaha dhidi yetu si pamoja na sisi." (Muslimu)

2. Ilyas bin Salama ameHadith a kutoka kwa baba yake kuwa Mtume wa Allah amesema: "Yule ashikaye upanga (silaha) dhidi yetu si pamoja na sisi." (Muslimu)

3. Abu Musa Ashiari amesema kuwa Mtume wa Allah amesema: "Yule ashikaye silaha dhidi yetu si pamoja na sisi. (Muslimu)

Uhakiki wa Isnad
Katika harakati za kuchuja Hadith zilizosahihi na zisizo sahihi; wanazuoni wa Hadith walikuwa wakifuatilia kwa undani historia ya wale wote waliomo kwenye msururu wa wapokezi wa Hadith na kumchunguza mtu wa kwanza kuHadith a Hadith hiyo kuwa kweli alikuwa Swahaba balegh na Mkalafi aliyekuwa na uwezo wa kumsikia au kumuona Mtume (s.a.w). 

Kwa ujumla, ili Hadith iwe sahihi, kila msimulizi katika Isnad alitakiwa awe Muislamu mwaminifu, mwenye kumbukumbu nzuri, mwenye tabia njema na mcha-Mungu.

Uhakiki wa Matin
Pamoja na kuwa na usahihi katika upokezi wa Hadith, "Matin" ya Hadith inaweza isiwe sahihi. Hivyo Hadith itakuwa shihi iwapo sehemu zote kwa pamoja - Isnad na Matin vitakuwa sahihi. Matin ya Hadith itakuwa sahihi iwapo itatekeleza masharti yafuatayo:
(i) Isipingane na Qur-an.
(ii) Isipingane na Hadith nyingine iliyothibitishwa kuwa ni sahihi.
(iii) Isimzulie Mtume (s.a.w) kufanya jambo ambalo ni kinyume na Uislamu.
(iv) Isipingane na hakika (fact)
(v) Isipingane na ukweli unaothibitishwa na historia.
(vi) Isiwe na maneno ya uongo ndani yake.
(vii) Isiwe inaahidi adhabu kali sana kwa kosa dogo sana na isiwe imeahidi malipo makubwa sana kwa wema mdogo sana.


                   

Download App Yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.

Download Now Bongoclass

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Sunnah Main: Dini File: Download PDF Views 825

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Kitabu cha Afya    👉2 Bongolite - Game zone - Play free game    👉3 Madrasa kiganjani    👉4 Kitau cha Fiqh    👉5 Simulizi za Hadithi Audio    👉6 kitabu cha Simulizi   

Post zinazofanana:

Dua za kumuomba Allah wakati wa shida na tabu ama matatizo

Post hii inakwenda kukufundisha dua ambazo ni muhimu kuzisoma wakayi wa shida na taabu.

Soma Zaidi...
Nafasi ya Sunnah (suna) katika Uislamu.

Hapa utajifunza nafasi ya kufuata suna katika Uislamu

Soma Zaidi...
DUA 94 - 114

DUA ZA KUONDOA WASIWASI, SIHIRI NA UCHAWI 94.

Soma Zaidi...
Al-Arba'uwn An-Nawawiyyah hadithi ya 1: Nia

huu ni mwanzo wa kitabu hiki cha Matn arbaina Naway

Soma Zaidi...
WACHA KILE ULICHO NA SHAKA NACHO NA FANYA USICHO NA SHAKA NACHO

عَنْ أَبِي مُحَمَّدٍ الْحَسَنِ بْنِ عَلِيِّ بْنِ أَبِي طَالِبٍ سِبْطِ رَسُولِ اللَّهِ صلى الله عليه و سلم وَرَيْحَانَتِهِ رَضِيَ اللَ...

Soma Zaidi...
DUA ZA KUONDOA WASIWASI

DUA ZA KUONDOA MAUMIVU MWILINI Katika uislamu Allah amejaalia dawa katika kufuata sunnah.

Soma Zaidi...