UHAKIKI WA HADITHI

Uhakiki wa Hadith za Mtume (s.

UHAKIKI WA HADITHI

Uhakiki wa Hadith za Mtume (s.a.w)
Kwa kuwa Hadith hazikuwa na ahadi ya Allah (s.w) ya hifadh kama ilivyo kwa Qur-an - "Hakika sisi ndio tulioteremsha mawaidha haya (Qur-an) na hakika sisi ndio tutakaoyalinda". (15:9) - walitokea watu waovu wakamzulia Mtume (s.a.w) mambo mengi yaliyokinyume kabisa na Uislamu wenyewe.ย  Hili liliwastua wanazuoni wacha-Mungu na kuwafanya wawajibike kuweka utaratibu maalumu wa kuchambua Hadith za Mtume (s.a.w). Katika harakati za uchambuzi wa Hadith, wanazuoni wa Hadith waliigawa Hadith katika sehemu kuu mbili - Isnad na Matin.

Isnad ni sehemu ya Hadith inayoonyesha msururu wa wapokezi wa Hadith hiyo tokea kwa yule aliyemsikia Mtume (s.a.w) akieleza jambo au aliyemuoma Mtume akifanya jambo, au aliyemuona Mtume akiridhia au akithibitisha jambo lililofanyika mbele yake au akieleza tabia ya Mtume (s.a.w) kama alivyoiona.
Mfano wa Isnad:
AmetuHadithia Abdallah bin Yusuf toka kwa Malik toka kwa Abizinadi toka kwa A'araji toka kwa Abu Hurairah ambaye amesema: Hakika ya Mtume wa Allah (s.a.w) amesema: โ€ฆโ€ฆโ€ฆโ€ฆโ€ฆ." (Bukhari) Kwa hiyo msururu wa watu wote hao kuanzia yule aliyemsikia Mtume (s.a.w), Abu Hurairah (r.a) ambaye ni sahaba wa Mtume, hadi kumfikia Bukhari ambaye ni Imamu wa Hadith aliyeipokea na kuiandika ndio Isnad.ย 

Matin ni kauli ya Mtume au matendo yake.
Mfano wa Matin:
Mtume (s.a.w) amesema: โ€œYule ashikaye silaha dhidi yetu si pamoja na sisi." (Muslimu) Maneno aliyosema Mtume (s.a.w) yaliyofungiwa kwenye "โ€ฆโ€ฆโ€ฆโ€ฆโ€ฆโ€ฆโ€ฆโ€ฆ.." ndio matin ya Hadith hii. Riwaya Matin moja ya Hadith inaweza kuripotiwa na msururu wa wapokezi (Isnaad) zaidi ya moja.
Kwa mfano:
Mtume (s.a.w) amesema "Yule ashikaye silaha dhidi yetu si pamoja sisi." (Muslimu) Maneno haya aliyosema Mtume (s.a.w) yamesimuliwa katika riwaya tatu zifuatazo:
1. โ€œAbdullah bin Umar ameeleza kuwa Mtume wa Allah amesema: "Yule ashikaye silaha dhidi yetu si pamoja na sisi." (Muslimu)

2. Ilyas bin Salama ameHadith a kutoka kwa baba yake kuwa Mtume wa Allah amesema: "Yule ashikaye upanga (silaha) dhidi yetu si pamoja na sisi." (Muslimu)

3. Abu Musa Ashiari amesema kuwa Mtume wa Allah amesema: "Yule ashikaye silaha dhidi yetu si pamoja na sisi. (Muslimu)

Uhakiki wa Isnad
Katika harakati za kuchuja Hadith zilizosahihi na zisizo sahihi; wanazuoni wa Hadith walikuwa wakifuatilia kwa undani historia ya wale wote waliomo kwenye msururu wa wapokezi wa Hadith na kumchunguza mtu wa kwanza kuHadith a Hadith hiyo kuwa kweli alikuwa Swahaba balegh na Mkalafi aliyekuwa na uwezo wa kumsikia au kumuona Mtume (s.a.w).ย 

Kwa ujumla, ili Hadith iwe sahihi, kila msimulizi katika Isnad alitakiwa awe Muislamu mwaminifu, mwenye kumbukumbu nzuri, mwenye tabia njema na mcha-Mungu.

Uhakiki wa Matin
Pamoja na kuwa na usahihi katika upokezi wa Hadith, "Matin" ya Hadith inaweza isiwe sahihi. Hivyo Hadith itakuwa shihi iwapo sehemu zote kwa pamoja - Isnad na Matin vitakuwa sahihi. Matin ya Hadith itakuwa sahihi iwapo itatekeleza masharti yafuatayo:
(i) Isipingane na Qur-an.
(ii) Isipingane na Hadith nyingine iliyothibitishwa kuwa ni sahihi.
(iii) Isimzulie Mtume (s.a.w) kufanya jambo ambalo ni kinyume na Uislamu.
(iv) Isipingane na hakika (fact)
(v) Isipingane na ukweli unaothibitishwa na historia.
(vi) Isiwe na maneno ya uongo ndani yake.
(vii) Isiwe inaahidi adhabu kali sana kwa kosa dogo sana na isiwe imeahidi malipo makubwa sana kwa wema mdogo sana.


                   

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Sunnah Main: Dini File: Download PDF Views 1046

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
๐Ÿ‘‰1 Kitabu cha Afya    ๐Ÿ‘‰2 kitabu cha Simulizi    ๐Ÿ‘‰3 Madrasa kiganjani    ๐Ÿ‘‰4 Simulizi za Hadithi Audio    ๐Ÿ‘‰5 Bongolite - Game zone - Play free game    ๐Ÿ‘‰6 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)   

Post zinazofanana:

MUISLAMU ALIYE BORA NI YULE ANAYEWACHA MAMBO YASIYO MUHUSU

ุนูŽู†ู’ ุฃูŽุจููŠ ู‡ูุฑูŽูŠู’ุฑูŽุฉูŽ ุฑูŽุถููŠูŽ ุงู„ู„ู‡ู ุนูŽู†ู’ู‡ู ู‚ูŽุงู„ูŽ: ู‚ูŽุงู„ูŽ ุฑูŽุณููˆู„ู ุงู„ู„ูŽู‘ู‡ู ุตู„ู‰ ุงู„ู„ู‡ ุนู„ูŠู‡ ูˆ ุณู„ู… "ู…ูู†ู’ ุญูุณู’ู†ู ุฅุณู’ู„ูŽุงู…ู ุงู„ู’ู…ูŽุฑู’ุกู ุชูŽุฑู’ูƒูู‡ู ู…ูŽ?...

Soma Zaidi...
MAANA NA FADHILA ZA KUOMBA DUA

DUA Kwa ufupi dua ni kumuomba Allah akuondoshee lililobaya, ama linalo kuudhi ama akupe jambo fulani.

Soma Zaidi...
Dua za kuomba wakati unapokuwa na maumivu kwenye mwili

Posti hii inakwenda kukufundisha dua za kuomba wakati wa kuwa na maumivu kwenye mwili wako.

Soma Zaidi...
Matamshi ambayo ukimwambia Allah kwenye dua yako basi hujibiwa kwa haraka dua hiyo

Post hii inakwenda kukufundisha matamshi ambayo mtu akiyatamka Allah hujibu dua hiyo kwa urahisi.

Soma Zaidi...
Dua za kumuomba Allah wakati wa shida na tabu ama matatizo

Post hii inakwenda kukufundisha dua ambazo ni muhimu kuzisoma wakayi wa shida na taabu.

Soma Zaidi...
Namna ambazo Allah hujibu dua ya mwenye kuomba.

Post hii inakwenda kukufundisha namna ama staili ambazo Allah hujibu dua za watu.

Soma Zaidi...
DUA DHIDI YA WASIWASI, UCHAWI NA MASHETANI

DUA ZA KUONDOA WASIWASI, SIHIRI NA UCHAWI 1.

Soma Zaidi...
Historia ya uandishi wa Hadithi, na ni kwa nini wakati wa Mtunme hakukuwa na uandishibmkubwa wa hadithi

Hapa utakwendabkuijuwabhistoria ya uandishi wa hadithi. Pia utaijuwa sababu iliyopelekea uandishi wa hadithi kuwa mdogo .

Soma Zaidi...