image

UHAKIKI WA HADITHI

Uhakiki wa Hadith za Mtume (s.

UHAKIKI WA HADITHI

Uhakiki wa Hadith za Mtume (s.a.w)
Kwa kuwa Hadith hazikuwa na ahadi ya Allah (s.w) ya hifadh kama ilivyo kwa Qur-an - "Hakika sisi ndio tulioteremsha mawaidha haya (Qur-an) na hakika sisi ndio tutakaoyalinda". (15:9) - walitokea watu waovu wakamzulia Mtume (s.a.w) mambo mengi yaliyokinyume kabisa na Uislamu wenyewe.  Hili liliwastua wanazuoni wacha-Mungu na kuwafanya wawajibike kuweka utaratibu maalumu wa kuchambua Hadith za Mtume (s.a.w). Katika harakati za uchambuzi wa Hadith, wanazuoni wa Hadith waliigawa Hadith katika sehemu kuu mbili - Isnad na Matin.

Isnad ni sehemu ya Hadith inayoonyesha msururu wa wapokezi wa Hadith hiyo tokea kwa yule aliyemsikia Mtume (s.a.w) akieleza jambo au aliyemuoma Mtume akifanya jambo, au aliyemuona Mtume akiridhia au akithibitisha jambo lililofanyika mbele yake au akieleza tabia ya Mtume (s.a.w) kama alivyoiona.
Mfano wa Isnad:
AmetuHadithia Abdallah bin Yusuf toka kwa Malik toka kwa Abizinadi toka kwa A'araji toka kwa Abu Hurairah ambaye amesema: Hakika ya Mtume wa Allah (s.a.w) amesema: ……………." (Bukhari) Kwa hiyo msururu wa watu wote hao kuanzia yule aliyemsikia Mtume (s.a.w), Abu Hurairah (r.a) ambaye ni sahaba wa Mtume, hadi kumfikia Bukhari ambaye ni Imamu wa Hadith aliyeipokea na kuiandika ndio Isnad. 

Matin ni kauli ya Mtume au matendo yake.
Mfano wa Matin:
Mtume (s.a.w) amesema: “Yule ashikaye silaha dhidi yetu si pamoja na sisi." (Muslimu) Maneno aliyosema Mtume (s.a.w) yaliyofungiwa kwenye "…………………….." ndio matin ya Hadith hii. Riwaya Matin moja ya Hadith inaweza kuripotiwa na msururu wa wapokezi (Isnaad) zaidi ya moja.
Kwa mfano:
Mtume (s.a.w) amesema "Yule ashikaye silaha dhidi yetu si pamoja sisi." (Muslimu) Maneno haya aliyosema Mtume (s.a.w) yamesimuliwa katika riwaya tatu zifuatazo:
1. “Abdullah bin Umar ameeleza kuwa Mtume wa Allah amesema: "Yule ashikaye silaha dhidi yetu si pamoja na sisi." (Muslimu)

2. Ilyas bin Salama ameHadith a kutoka kwa baba yake kuwa Mtume wa Allah amesema: "Yule ashikaye upanga (silaha) dhidi yetu si pamoja na sisi." (Muslimu)

3. Abu Musa Ashiari amesema kuwa Mtume wa Allah amesema: "Yule ashikaye silaha dhidi yetu si pamoja na sisi. (Muslimu)

Uhakiki wa Isnad
Katika harakati za kuchuja Hadith zilizosahihi na zisizo sahihi; wanazuoni wa Hadith walikuwa wakifuatilia kwa undani historia ya wale wote waliomo kwenye msururu wa wapokezi wa Hadith na kumchunguza mtu wa kwanza kuHadith a Hadith hiyo kuwa kweli alikuwa Swahaba balegh na Mkalafi aliyekuwa na uwezo wa kumsikia au kumuona Mtume (s.a.w). 

Kwa ujumla, ili Hadith iwe sahihi, kila msimulizi katika Isnad alitakiwa awe Muislamu mwaminifu, mwenye kumbukumbu nzuri, mwenye tabia njema na mcha-Mungu.

Uhakiki wa Matin
Pamoja na kuwa na usahihi katika upokezi wa Hadith, "Matin" ya Hadith inaweza isiwe sahihi. Hivyo Hadith itakuwa shihi iwapo sehemu zote kwa pamoja - Isnad na Matin vitakuwa sahihi. Matin ya Hadith itakuwa sahihi iwapo itatekeleza masharti yafuatayo:
(i) Isipingane na Qur-an.
(ii) Isipingane na Hadith nyingine iliyothibitishwa kuwa ni sahihi.
(iii) Isimzulie Mtume (s.a.w) kufanya jambo ambalo ni kinyume na Uislamu.
(iv) Isipingane na hakika (fact)
(v) Isipingane na ukweli unaothibitishwa na historia.
(vi) Isiwe na maneno ya uongo ndani yake.
(vii) Isiwe inaahidi adhabu kali sana kwa kosa dogo sana na isiwe imeahidi malipo makubwa sana kwa wema mdogo sana.


                   





           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 251


Sponsored links
👉1 kitabu cha Simulizi     👉2 Madrasa kiganjani     👉3 Kitabu cha Afya     👉4 Kitau cha Fiqh    

Post zifazofanana:-

DUA ZA KUONDOA WASIWASI
DUA ZA KUONDOA MAUMIVU MWILINI Katika uislamu Allah amejaalia dawa katika kufuata sunnah. Soma Zaidi...

HADITHI YA 34 YEYOTE ATAKAYEONA KITENDO KIOVU AKIONDOE KWA MKONO WAKE
Soma Zaidi...

Faida za swala ya Mtume
Hapa utajifunza fadhila za kumswalia Mtume (s.a.w) Soma Zaidi...

JINSI YA KUOMBA DUA ILI IKUBALIWE NA ALLAH
Kukubaliwa kwa dua kunategemea mahusiano yako na Allah. hata hivyo kuna baadhi ya mabo ukiyafanya dua yako inaweza kukubaliwa kwa haraka zaidi. Post hii inakwenda kukufundisha kuhusu jinsi ya kuomba dua ikubaliwe. Soma Zaidi...

WACHA KILE ULICHO NA SHAKA NACHO NA FANYA USICHO NA SHAKA NACHO
عَنْ أَبِي مُحَمَّدٍ الْحَسَنِ بْنِ عَلِيِّ بْنِ أَبِي طَالِبٍ سِبْطِ رَسُولِ اللَّهِ صلى الله عليه و سلم وَرَيْحَانَتِهِ رَضِيَ اللَ... Soma Zaidi...

DUA na Adhkar kutoka kwenye quran
hii ni orodha ya dua mbalimbali kutoka kwenye quran. Unaweza kuzitumia dua hizi kujipendekeza kwa Allah na kupata msamaha, neema na mengineyo. Soma Zaidi...

Hadithi inayokataza bidaa (bid's) uzushi katika dini
عَنْ أُمِّ الْمُؤْمِنِينَ أُمِّ عَبْدِ اللَّهِ عَائِشَةَ رَضِيَ اللَّهُ عَنْهَا، قَالَتْ: قَالَ: رَسُولُ اللَّهِ صلى الله عليه و سلم "... Soma Zaidi...

KAMA HUNA HAYA BASI FAJA UNACHOTAKA
عَنْ أَبِي مَسْعُودٍ عُقْبَةَ بْنِ عَمْرٍو الْأَنْصَارِيِّ الْبَدْرِيِّ رَضِيَ اللهُ عَنْهُ قَالَ: قَالَ رَسُولُ اللَّهِ صلى الله عل?... Soma Zaidi...

DUA ZENYE MANENO HAYA HUJIBIWA
SIFA ZA (MANENO NA MATAMSHI YA) DUA YENYE KUJIBIWA. Soma Zaidi...

UHAKIKI WA HADITHI
Uhakiki wa Hadith za Mtume (s. Soma Zaidi...

Uislamu ni Nasaha (kunasihiana) kwa Mwenyezi Mungu, Kitabu chake Mtume wake , Viongozi na waislamu wote
عَنْ أَبِي رُقَيَّةَ تَمِيمِ بْنِ أَوْسٍ الدَّارِيِّ رَضِيَ اللهُ عَنْهُ أَنَّ النَّبِيَّ صلى الله عليه وسلم قَالَ: "الدِّينُ النَّصِ?... Soma Zaidi...

DUA 85 - 93
SWALA YA MTUME 85. Soma Zaidi...