picha

Koo langu limekauka yaweza kuwa ni muadhirika?

kuwashwa na koo ni katika dalili za kuwa na maambukizi mwilini. Kuwa na maambukizi haimaanishi ni HIV ama UKIMWI laa hili ni neno pana. Hapa nitakujuza kwa ufupi kuhusu swali hilo la muulizaji kuwa anawashwa na koo.

SWALI

Koo langu limekauka yaweza kuwa ni muadhirika?

 

JIBU:

Kuwa shwa na koo ni dalili ya maradhi na huweza pia aikawa sio maradhi. Watu wengi wamekuwa wakidhani kuwa katika dalili za mwanzo za HIV ama UKIMWI ni kuwashwa na koo. Wengine wamekuwa wakiogopa sana pindi akiwashwa na koo baada ya kushiriki ngono zembe. Ha[pana hii sio sahihi. Kuwashwa na koo kunaweza kuwa hata sio jambo la kuhitaji uangalizi zaidi wa Daktari.

 

Sababu za kuwashwa na koo:-

1. Hali ya hewa kama kupata mavumbi

2. Mazingira kama kuwa katika mazingira ya mosho

3. Baridi kwa mfano aliyekula mbarafu ama juisi ya baridi sana anaweza kuwashwa na koo

4. maambukizi ya bakteria kwenye mfumo wa hewa

5. maambukizi ya Virusi kwenye mfumo wa hewa kama virusi vya Corona

6. Maambukizi ya virusi vinginevyo. 

 

Je kuwashwa na koo ni dalili ya HIV na UKIMW?

Yes huweza ikawa i dalili ya maambukizi ya virusi vya HIV lendapo mtu alishiriki ngono zembe hivi karibuni na mtu aliyeathirika. Ama huwenda amepata virusi kwa njia nginginezo. Lakini itambulike kuwa katika daliki za mwanzo za HIV kuwashw akwa koo si sana kutokea. Hata hivyo hizi ni dalili tu zinaweza kuwa ni kitu kingine. Kinachotakiw ani kupata vipimo kwanza.

 

DALILI ZAMWANZO ZA HIV

1.kuvimba kwa tezi za kwenye makwapa, mapaja na shingo
2.Homa
3.Uchovu
4.Kuharisha
5.Kupungua uzito
6.Kikohozi
7.Pumzi kutoka kidogodogo
8.Mafua

 

DALILI ZA UKIMWI

1.kutokwa na jasho jingi wakati wa usiku
2.Kupata homa za mara kwa mara na kuhisi baridi
3.Kikohozi
4.Kushinwa kupumua vyema
5.Madoa madoa kwenye ulimi na mdomoni
6.Maumivu ya kichwa
7.Uchovu usiokuwa na sababu na usioisha
8.Kutokuona vyema
9.Kupungua uzito
10.Mapele na ukurutu kwenye ngozi

 

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu
Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: magonjwa Main: Post File: Download PDF Views 3307

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 kitabu cha Simulizi     👉2 Dua za Mitume na Manabii     👉3 Kitau cha Fiqh     👉4 Kitabu cha Afya     👉5 Bongolite - Game zone - Play free game     👉6 Simulizi za Hadithi Audio    

Post zinazofanana:

Mambo yanayosababisha kiuno au mgongo kuwa na maumivu

Posti hii inazungumzia kuhusiana na Mambo yanayoweza kusababishwa mgongo wAko au kiuno kwa na maumivu, Mgongo ukiwa na maumivu makali Sana yanaweza kusababishwa shida kubwa ata utakapokaa au ukilala au ukitumia bado maumivu yanakuwepo.

Soma Zaidi...
Nini sababu ya kuchubuka midomo na kuwa myeupe

Kama una tatizo la midomo kuchubuka na kuwa myeupe ama kuwa na vidonda. Post hii inakwenda kuangalia swala hili.

Soma Zaidi...
Zijue sababu za moyo kutanuka.

Posti hii inahusu zaidi sababu za moyo kutanuka, Kuna kipindi ambapo moyo utoka kwenye hali yake ya kawaida na kutanuka hali ambayo usababisha madhara kwa mwenye tatizo hilo, ila Kuna sababu ambazo usababisha moyo kutanuka kama tutakavyoona.

Soma Zaidi...
KUJIANDAA KWA AJILI YA KUMUONA DAKTARI

KUJIANDAA KWA AJILI YA KUMUONA DAKTARI Fanya miadi na daktari wako wa kawaida ikiwa una ishara au dalili zinazokupa wasiwasi.

Soma Zaidi...
Nini hasa chanzo cha pumu, na je inarithiwa?

Ugonjwa wa pumu ni moja katika magonjwa hatari yanayoweza kutokea kwa ghafla, na endapo itacheleweshwa kudhibitiwa inaweza sababisha athari mbaya zaidi

Soma Zaidi...
Saratani ya Matiti ya wanaume.

Posti hii inazungumzia kuhusiana na Saratani ya matiti ya Mwanaume ni Saratani nadra ambayo hutokea katika tishu za matiti za wanaume. Ingawa saratani ya matiti hufikiriwa zaidi kuwa ugonjwa wa wanawake, saratani ya matiti ya mwanaume hutokea. Saratani y

Soma Zaidi...