Koo langu limekauka yaweza kuwa ni muadhirika?

Koo langu limekauka yaweza kuwa ni muadhirika?

kuwashwa na koo ni katika dalili za kuwa na maambukizi mwilini. Kuwa na maambukizi haimaanishi ni HIV ama UKIMWI laa hili ni neno pana. Hapa nitakujuza kwa ufupi kuhusu swali hilo la muulizaji kuwa anawashwa na koo.

SWALI

Koo langu limekauka yaweza kuwa ni muadhirika?

 

JIBU:

Kuwa shwa na koo ni dalili ya maradhi na huweza pia aikawa sio maradhi. Watu wengi wamekuwa wakidhani kuwa katika dalili za mwanzo za HIV ama UKIMWI ni kuwashwa na koo. Wengine wamekuwa wakiogopa sana pindi akiwashwa na koo baada ya kushiriki ngono zembe. Ha[pana hii sio sahihi. Kuwashwa na koo kunaweza kuwa hata sio jambo la kuhitaji uangalizi zaidi wa Daktari.

 

Sababu za kuwashwa na koo:-

1. Hali ya hewa kama kupata mavumbi

2. Mazingira kama kuwa katika mazingira ya mosho

3. Baridi kwa mfano aliyekula mbarafu ama juisi ya baridi sana anaweza kuwashwa na koo

4. maambukizi ya bakteria kwenye mfumo wa hewa

5. maambukizi ya Virusi kwenye mfumo wa hewa kama virusi vya Corona

6. Maambukizi ya virusi vinginevyo. 

 

Je kuwashwa na koo ni dalili ya HIV na UKIMW?

Yes huweza ikawa i dalili ya maambukizi ya virusi vya HIV lendapo mtu alishiriki ngono zembe hivi karibuni na mtu aliyeathirika. Ama huwenda amepata virusi kwa njia nginginezo. Lakini itambulike kuwa katika daliki za mwanzo za HIV kuwashw akwa koo si sana kutokea. Hata hivyo hizi ni dalili tu zinaweza kuwa ni kitu kingine. Kinachotakiw ani kupata vipimo kwanza.

 

DALILI ZAMWANZO ZA HIV

1.kuvimba kwa tezi za kwenye makwapa, mapaja na shingo
2.Homa
3.Uchovu
4.Kuharisha
5.Kupungua uzito
6.Kikohozi
7.Pumzi kutoka kidogodogo
8.Mafua

 

DALILI ZA UKIMWI

1.kutokwa na jasho jingi wakati wa usiku
2.Kupata homa za mara kwa mara na kuhisi baridi
3.Kikohozi
4.Kushinwa kupumua vyema
5.Madoa madoa kwenye ulimi na mdomoni
6.Maumivu ya kichwa
7.Uchovu usiokuwa na sababu na usioisha
8.Kutokuona vyema
9.Kupungua uzito
10.Mapele na ukurutu kwenye ngozi

 

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu Rajabu
Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: magonjwa Main: Post File: Download PDF Views: 4312

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 web hosting     👉2 Madrasa kiganjani     👉3 ai web app     👉4 Bongolite - Game zone - Play free game     👉5 Kitabu cha Afya     👉6 Kitau cha Fiqh    

Post zinazofanana:

Sababu za miguu kufa ganzi.

Posti hii inahusu zaidi sababu mbalimbali,za miguu kufa ganzi,ni tatizo ambalo uwakumba watu wengi na walio wengi hawafahamu kabisa ni sababu zipi ambazo uleta tatizo hili.

Soma Zaidi...
Dalili za Saratani ya figo.

Saratani ya Figo ni Saratani ambayo huanzia kwenye figo. Figo zako ni viungo viwili vyenye umbo la maharagwe, kila kimoja kikiwa na ukubwa wa ngumi yako. Ziko nyuma ya viungo vyako vya tumbo, na figo moja kila upande wa mgongo wako.

Soma Zaidi...
Maumivu ya mgongo (Sciatica): Dalili na mazoezi ya kupunguza.

Sciatica ni hali ya maumivu yanayotokana na shinikizo au kuwasha kwa neva ya sciatic, ambayo ndiyo neva ndefu na kubwa zaidi mwilini mwako. Makala haya yanatoa mwongozo wa kitaalamu kuhusu jinsi ya kutambua dalili za sciatica, sababu za msingi zinazoleta maumivu haya, na mfululizo wa mazoezi yaliyothibitishwa kitabibu kusaidia kupunguza maumivu na kurejesha utendaji wa mwili.

Soma Zaidi...
HPV (Human Papillomavirus): Chanjo na saratani ya shingo ya kizazi.

​Virusi vya Human Papillomavirus (HPV) ni kundi la virusi vinavyoambukiza ngozi na utando wa ndani wa mwili. Ingawa maambukizi mengi ya HPV hupona yenyewe, aina fulani za virusi hivi zinaweza kusababisha mabadiliko ya seli yanayoendelea na kuwa saratani, hasa saratani ya shingo ya kizazi. Makala hii inachambua uhusiano kati ya HPV na saratani, umuhimu wa chanjo, na hatua za kinga ambazo kila jamii inapaswa kuzichukua.

Soma Zaidi...
Jinsi ya kujikinga na magonjwa ya zinaa (STIs).

Magonjwa ya zinaa, yanayojulikana pia kama STIs (Sexually Transmitted Infections), ni miongoni mwa changamoto kubwa za afya ya umma duniani. Kila mwaka, mamilioni ya watu hupata maambukizi mapya ya magonjwa haya, huku wengi wakikosa kutambua kuwa wameambukizwa kutokana na kutokuwa na dalili katika hatua za awali. Habari njema ni kwamba sehemu kubwa ya maambukizi ya magonjwa ya zinaa inaweza kuzuilika kwa kufuata mbinu sahihi za kinga na kufanya maamuzi salama kuhusu afya ya uzazi. Katika makala hii utajifunza maana ya magonjwa ya zinaa, namna yanavyoenea, sababu zinazoongeza hatari ya maambukizi, njia bora za kujikinga, umuhimu wa kupima afya mara kwa mara, pamoja na ukweli muhimu ambao kila mtu anapaswa kuufahamu kuhusu STIs.

Soma Zaidi...
Je unazijuwa dalili za Ukimwi na HIV?

Huwenda ukawa ni moja kati ya watu wanaotaka kujuwa juu ya dalili za ukimwi. Kama wewe ni katika watu hawa tambuwa kuwa kuna dalili za VVU (hiv) na dalili za ukimwi. Makala hii itakwenda kukuletea dalili kuu za mwanzo za VVU na HIV kuanzia wiki tatu za mw

Soma Zaidi...