Kazi alizokuwa akizifanya Mtume Muhammad s.a.w kabla ya utume.
Historia na sifa ya Mtume Muhammad s.a.w , sehemu ya 14. Hapa utajifunza kuhusu kazi alizozifanya Mtume s.a.w Enzo za ujana wake kabla ya utume.
KAZI ALIZOKUWA AKIFANYA MUHAMMAD (S.A.W) ZA KUMPATIA RIZKI
Muhammad (s.a.w) hakuwaga na shughuli maalumu ya kuweza kumpatika kazi. Kama ilivyokuwa ni desturi ya mitume kuchunga mifugo kama mbuzi na kondoo hivyo hivyo kijana Muhammad (s.a.s) alikuwa akifanya kazi hii. Muhammad (s.a.s) alikuwa akichunga mifugo ya bani Sa’ad kwa malipo maalum.
Pia kijana Muhammad (s.a.s) alikuwa ni mfanya biashara. Aliweza kupata uzoefu wa biashara kutoka kwa Baba yake mdogo Abu Tallib ambaye pia alikuwa ni mfanya biashara.
Alipokuwa na umri wa miaka 25 alisafiri kuwenda Sham (Syria) kwa ajili ya kufanya biashara. Na itambulike kuwa wakazi wa Makwa wakati huo walikuwa ni wafanya biashara wakubwa sana. Matajiri wengi wa Makkah walikuwa wakitegemea biasha. Kutokana na uadilifu, uaminifu na ukweli alokuwa nao kijana Muhammad (s.a.s) Bi Khadija alimtaka akamuuzie biashara zake Syria.
Bi khadija alikuwa ni katika wanawake wafanyabiashara wakubwa Mjini Mkkah. Alikuwa akiajiri wanaume kwa ajili yakufanyiwa biashara zake. Aliposikia sifa za Muhammad (s.a.s) alivutiwa kufanyabiashara nae.
Hivyo akazungumza nae na awalikubaliana kuwa atamlipa zaidi kuliko wenzie. Akamtuma Muhammad (s.a.s) akiwa na mfanyakazi wa bi Khadija aitwaye Maisarah, aliwatuma waende kufanya biashara Syria. Basi Muhammad (s.a.s) alikubali ombi aba safari akaelekea kwenda Sham. Na katika safari hii Bi Khadija aliona miujiza mikubwa sana kwa Muhammad (s.a.s).
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
π1 Kitau cha Fiqh π2 Bongolite - Game zone - Play free game π3 Simulizi za Hadithi Audio π4 Dua za Mitume na Manabii π5 web hosting π6 Tafasiri ya Riyadh Swalihina
Post zinazofanana:
MJADALA JUU YA NDOA YA MTUME S.A.W NA BI KHADIJA (HADIJA)
LAKINI UMRI WANGU MKUBWABaada ya kuwaza na kufikiri muda mrefu, bibi Khadija (Radhiya Llahu anha) akafikia uamuzi wa kutaka kuolewa na Muhammad (Swalla Laahu alayhi wa sallam).
Soma Zaidi...Mafunzo Yatokanayo na Historia ya Nabii Nuhu(a.s)
(i) Tuanze kulingania kwa Tawhiid β kumjua Allah(s.
Soma Zaidi...Historia ya Dhulqarnain
Dhulqarnain sio jina la mtu bali cheo, maana yake ikiwa: βMwenye Pembe Mbiliβ.
Soma Zaidi...Mafunzo Yatokanayo na mambo Aliyofanya Mtume (s.a.w) Katika Kuanzisha Dola ya Kiislamu
Kwanza, ili tuweze kusimamisha Uislamu katika jamii hatunabudi kuanzisha na kuendeleza vituo vya harakati, misikiti ikiwa ndio vitovu.
Soma Zaidi...Mafunzo yatokanayo na vita vya uhudi
Dola ya uislamu madinah (EDK form 3: dhana ya elimu ya uislamu)
Soma Zaidi...