Historia ya Mwanadamu

Historia ya Mwanadamu

Download Post hii hapa

Historia ya Mwanadamu

Historia ya Mwanadamu



Historia ya mwanadamu ukiichunguza tangu mwanzo wake utakuta matukio mengi yanayothibitisha kuwepo Allah (s.w) Mmiliki wa kila kitu na mwenye nguvu na uwezo juu ya kila kitu. Mara kwa mara tunatanabahishwa katika Qur-an:“Je! Haikuwabainikia tu kama (kaumu) ngapi tuliziangamiza kabla yao? Na hawa (makafiri wa sasa) wanatembeatembea katika maskani yao, (hawaoni alama za kuangamizwa kwao)? Bila shaka katika hayo zimo ishara kwa wenye akili. ” (20:128 “Je! Haw atembei katika nchi na kuona jinsi ulivyokuw a mwisho wa wale waliokuwa kabla yao? Walikuwa wenye nguvu zaidi kuliko wao na wakilima ardhi na kuistawisha zaidi kuliko wao walivyostawisha. Na mitume wao waliwajia kwa dalili waziwazi, basi hakuwa Mwenyezi Mungu ni mwenye kuwadhulumu, lakini walikuwa wenyewe wakijidhulumu nafsi zao.” (30:9)“Je! Huoni Mola wako alivyo wafanya watu wenye ndovu? Hakujaalia vitimbi vyao kuharibika? Na akawapeleka ndege makundi kwa makundi, wakawapiga kwa mawe ya udongo wa kuchoma, Akaw afanya kam a majani yaliyotafunw a. ” (1 05:1-5)


Tukio hili la watu wenye ndovu lilitokea mwaka 570. A.D. miezi michache kabla ya kuzaliwa Mtume Muhammad (s.a.w).


Mnamo mwaka wa 570 A.D. Abraha, gavana wa Yemen, chini ya himaya ya Kikiristo ya Uhabeshi alikusanya jeshi lenye askari 60,000 na ndovu (tembo) kumi na tatu (13) kwa nia ya kuibomoa na kuisambaratisha Al-Ka’abah, nyumba takatifu ya Allah (s.w) iliyopo Makka.


Walinzi wa Ka’abah, kabila la Quraish waliongozwa na Abdul-Muttalib, Babu yake Mtume (s.a.w), walimfahamisha Abraha kuwa wao hawana uwezo wa kupambana na jeshi lake hilo bali mwenye Ka’abah ndiye atakayeilinda. Abraha alipokaidi na kusisitiza kutekeleza azma yake ya kuivunja Ka’abah, Abdul-Muttalib aliwaamuru wakazi wa Makka wampishe na akaingia ndani ya Ka’abah na kumuomba Allah (s.w) kwa unyenyekevu kama ifuatavyo:“O Allah, mtu hulinda nyumba yake, nawe ilinde nyumba yako.


Usiuachie msalaba na hila zao kesho kushinda hila zako. Kama utaamua kuwaachia waifanye watakavyo Qibla yetu, Basi w ewe ni muweza wa kufanya upendavyo. Wanusuru leo watumishi wako dhidi ya watumishi wa Msalaba na waabudu wake.


Ewe Mola wangu, sina matumaini yoyote toka kwa yeyote dhidi yao isipokuwa kwako. Ewe Mola wangu, ilinde nyumba yako dhidi yao. Adui wa nyumba hii ni adui yako. Wazuie w asiiharibu nyumba yako”.
Kesho yake, Abraha na jeshi lake kabla hawajapiga hatua kutoka kwenye kambi yao, kilometa tano (5) tokea Makka, walizingirwa na jeshi la ndege wadogo wadogo walioitwa “Ababil” waliokuwa na silaha ya vijiwe. Kila ndege alimlenga askari wake na kijiwe hicho kilichomchakaza na kumfanya kama majani yaliyotafunwa na kutemwa.



Tukio hili la “watu wa ndovu” ni kielelezo tosha kutokana na historia ya binaadamu kuwa Allah (s.w) yupo na anauwezo ulio juu ya hila zote za binaadamu na juu ya kila kitu.




                   


Download Post hii hapa

Jiunge nasi WhatsApp
Upate Update zetu

Download App Yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.

Download Now Bongoclass Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Tawhid Main: Dini File: Download PDF Views 1270

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Simulizi za Hadithi Audio    👉2 Kitau cha Fiqh    👉3 Madrasa kiganjani    👉4 Bongolite - Game zone - Play free game    👉5 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉6 kitabu cha Simulizi   

Post zinazofanana:

Maana ya muislamu.
Maana ya muislamu.

Kwenye kipengele hichi tutajifunza ni nani muislamu.

Soma Zaidi...
Maswali kuhusu njia za kumjua mwenyezi Mungu
Maswali kuhusu njia za kumjua mwenyezi Mungu

Nguzo za imani (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu

Soma Zaidi...
Kutowatii Wazazi katika kumuasi Allah (s.w)
Kutowatii Wazazi katika kumuasi Allah (s.w)

"Na (wazazi wako) wakikushurutisha kunishirikisha na (yale) ambayo huna ilimu nayo, usiwatii; lakini kaa nao kwa wema hapa duniani (Maadamu ni wazee wako, ila usiwafuate tu mwenendo wao mbaya); Shika mwenendo wa wale wanaoelekea kwangu, kisha marejeo yenu

Soma Zaidi...
Haki za kielimu za mwanamke katika uislamu
Haki za kielimu za mwanamke katika uislamu

Haki ya ElimuKatika Uislamu kujielimisha ni faradhi inayowahusu Waislamu wote, wanaume na wanawake: "Soma kwa jina ?

Soma Zaidi...
 Kuwa wenye shukurani mbele ya Allah (s.w)
Kuwa wenye shukurani mbele ya Allah (s.w)

Mwanaadamu ametunukiwa neema mbali mbali na Mola wake kuliko viumbe wengine wote kama tuanvyojifunza katika aya mbali mbali za Qur'an.

Soma Zaidi...
 ALAMA YA MUUMINI WA UKWELI KATIKA UISLAMU
ALAMA YA MUUMINI WA UKWELI KATIKA UISLAMU

عَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ رَضِيَ اللهُ عَنْهُ أَنَّ رَسُولَ اللَّهِ صلى الله عليه و سلم قَالَ: "مَنْ كَانَ يُؤْمِنُ بِاَللَّهِ وَالْيَوْمِ...

Soma Zaidi...
Udhaifu wa mtazamo wa makafiri juu ya dini dhidi ya mtazamo wa uislamu
Udhaifu wa mtazamo wa makafiri juu ya dini dhidi ya mtazamo wa uislamu

Somo Hili linaeleza kuhusu mtazamo wa uislamu juu ya dini (EDK form2: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
 zijue Nguzo za uislamu, imani, ihsani pamoja na dalili za qiyama
zijue Nguzo za uislamu, imani, ihsani pamoja na dalili za qiyama

عَنْ عُمَرَ رَضِيَ اللهُ عَنْهُ أَيْضًا قَالَ: " بَيْنَمَا نَحْنُ جُلُوسٌ عِنْدَ رَسُولِ اللَّهِ صلى الله عليه و سلم ذَاتَ يَوْمٍ، إذْ ?...

Soma Zaidi...
Sifa za wanafiki zilizotajwa katika surat at-Tawbah
Sifa za wanafiki zilizotajwa katika surat at-Tawbah

Mwenyezi Mungu amekuwia radhi (amekusamehe).

Soma Zaidi...