picha

Njia za kutibu saratani

Posti hii inahusu zaidi njia mbalimbali za matibabu ya ugonjwa wa saratani,ni ugonjwa ambao unaweza kupona ikiwa umegundulika mapema katika hatua za mwanzo na kama ugonjwa huu umefikia hatua za mwisho Tiba yake huwa ni kupunguza makali ya ugonjwa.

Njia za kutibu ugonjwa wa saratani.

1.Saratani inaweza kutibiwa kwa kutumia njia mojawapo ambayo huitwa Tiba homoni.

Njia hii dawa mbalimbali utumika Ili kuweza  kusimamisha homoni ambazo uzalisha saratani, tukumbuke kuwa Kuna homoni ambazo zikiwa mwilini huwa zinazalisha saratani kwa hiyo hizi homoni kama hazijazuiliwa uendelea kuongezeka na kusababisha madhara kwa mgonjwa , kwa hiyo dawa hizi zimetengenezwa iili kuweza kuzuia kuongezeka kwa homoni hizi ambazo usababisha saratani.

 

2. Aina nyingine ya kutibu saratani ni Tiba mionzi.

Hii ni njia ambayo utumia mionzi yenye nguvu kuua seli za saratani, tukumbuke kuwa saratani usababishwa na kuwepo kwa seli zisizotarajiwa katika mwili wa binadamu ambapo kwa kitaalamu huitwa Abnormal cell, kwa hiyo Ili kuweza kupunguza maambukizi mionzi yenye nguvu utumika Ili kuweza kuua hizi seli ambazo usababisha saratani. Kwa hiyo kiasi kikubwa Cha seli hizi zikifa na Maambukizi upungua.

 

3.Aina nyingine ya tiba ni Tiba kemikali.

Hii ni mojawapo ya tiba ya saratani ambapo  dawa utumika Ili kuweza kuua seli zinazosababisha saratani kwa hiyo dawa hizi zinaweza kuwa kwenye mfumo wa vidonge au wakati mwingine zinakuwa kwenye muuundo wa Maji maji ambayo ni drip, kwa hiyo upewa mgonjwa na hizi dawa huua seli ambazo usababisha saratani.

 

4. Njia nyingine bambayo utumika ni upasuaji.

Ni Aina ya njia ambayo utumika kuondoa seli ambazo usababisha saratani, tukumbuke kuwa saratani inaweza kuwa kwenye sehemu yoyote kwenye mwili kwa hiyo kwa kutumia njia hii ya upasuaji kama sehemu fulani imeshambuliwa sana na saratani hiyo sehemu utolewa Ili kuepuka seli hizi kusambaa kwenye sehemu mbalimbali za mwili wa binadamu.

 

5. Njia nyingine ni kutumia dawa mbadala za miti shamba ambazo utumiwa na watu wengi na wengine wamesshuhudia kupona na pia Kuna kutumia ushauri yaani cancelling kwa wagonjwa wa saratani na watu upunguza mawazo na kuendelea na maisha Yao ya kila siku na wengine wanaotumia masage yaani kunyoosha sehemu iliyoathiriwa na damu inaweza kutembea kwenye sehemu husika na wengine wanaotumia Mazoezi Ili kuweza kutibu sehemu iliyolegea.

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: magonjwa Main: Post File: Download PDF Views 2136

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
πŸ‘‰1 ai web app     πŸ‘‰2 Kitabu cha Afya     πŸ‘‰3 Dua za Mitume na Manabii     πŸ‘‰4 Simulizi za Hadithi Audio     πŸ‘‰5 Tafasiri ya Riyadh Swalihina     πŸ‘‰6 kitabu cha Simulizi    

Post zinazofanana:

Namna ya kutoa huduma kwa mgonjwa wa Dengue.

Posti hii inahusu zaidi huduma anayopaswa kupata mgonjwa wa ndengue, kwa sababu tunafahamu wazi Ugonjwa huu hauna dawa ila kuna huduma muhimu ambayo anaweza kupata na akaendelea vizuri.

Soma Zaidi...
Virusi vinavyopelekea Kuharisha Sana na Kutapika Sana(norovirus)

Maambukizi ya Norovirus yanaweza kusababisha kutapika sana na Kuhara. Virusi huambukiza sana na kwa kawaida huenea kupitia chakula au maji ambayo yamechafuliwa na kinyesi wakati wa kutayarisha. Unaweza pia kuambukizwa kwa kuwasiliana kwa karibu na mtu

Soma Zaidi...
Zijue dalili za maambukizi ndani ya sikio na madhara yake

Sikio ni mojawapo ya milango ya fahamu inayotumiwa kwa ajili ya kusikia, Kuna wakati mwingine hushambulia na bakteria na virusi

Soma Zaidi...
Namna ya kuzuia Ugonjwa wa ini

Posti hii inaelezea namna na jinsi ya kujikinga au kuzuia Ugonjwa wa ini.

Soma Zaidi...
Dalilili za saratani ya utumbo

Saratani ya Utumbo ni Saratani ya utumbo mpana (koloni), sehemu ya chini ya mfumo wako wa usagaji chakula. Kwa pamoja, mara nyingi hujulikana kama Saratani ya utumbo mpana. Visa vingi vya Saratani ya utumbo mpana huanza

Soma Zaidi...
Sasa UKIMWI unatokeaje?

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu njia ambazo UKIMWI hutokea

Soma Zaidi...