picha

Njia za kutibu saratani

Posti hii inahusu zaidi njia mbalimbali za matibabu ya ugonjwa wa saratani,ni ugonjwa ambao unaweza kupona ikiwa umegundulika mapema katika hatua za mwanzo na kama ugonjwa huu umefikia hatua za mwisho Tiba yake huwa ni kupunguza makali ya ugonjwa.

Njia za kutibu ugonjwa wa saratani.

1.Saratani inaweza kutibiwa kwa kutumia njia mojawapo ambayo huitwa Tiba homoni.

Njia hii dawa mbalimbali utumika Ili kuweza  kusimamisha homoni ambazo uzalisha saratani, tukumbuke kuwa Kuna homoni ambazo zikiwa mwilini huwa zinazalisha saratani kwa hiyo hizi homoni kama hazijazuiliwa uendelea kuongezeka na kusababisha madhara kwa mgonjwa , kwa hiyo dawa hizi zimetengenezwa iili kuweza kuzuia kuongezeka kwa homoni hizi ambazo usababisha saratani.

 

2. Aina nyingine ya kutibu saratani ni Tiba mionzi.

Hii ni njia ambayo utumia mionzi yenye nguvu kuua seli za saratani, tukumbuke kuwa saratani usababishwa na kuwepo kwa seli zisizotarajiwa katika mwili wa binadamu ambapo kwa kitaalamu huitwa Abnormal cell, kwa hiyo Ili kuweza kupunguza maambukizi mionzi yenye nguvu utumika Ili kuweza kuua hizi seli ambazo usababisha saratani. Kwa hiyo kiasi kikubwa Cha seli hizi zikifa na Maambukizi upungua.

 

3.Aina nyingine ya tiba ni Tiba kemikali.

Hii ni mojawapo ya tiba ya saratani ambapo  dawa utumika Ili kuweza kuua seli zinazosababisha saratani kwa hiyo dawa hizi zinaweza kuwa kwenye mfumo wa vidonge au wakati mwingine zinakuwa kwenye muuundo wa Maji maji ambayo ni drip, kwa hiyo upewa mgonjwa na hizi dawa huua seli ambazo usababisha saratani.

 

4. Njia nyingine bambayo utumika ni upasuaji.

Ni Aina ya njia ambayo utumika kuondoa seli ambazo usababisha saratani, tukumbuke kuwa saratani inaweza kuwa kwenye sehemu yoyote kwenye mwili kwa hiyo kwa kutumia njia hii ya upasuaji kama sehemu fulani imeshambuliwa sana na saratani hiyo sehemu utolewa Ili kuepuka seli hizi kusambaa kwenye sehemu mbalimbali za mwili wa binadamu.

 

5. Njia nyingine ni kutumia dawa mbadala za miti shamba ambazo utumiwa na watu wengi na wengine wamesshuhudia kupona na pia Kuna kutumia ushauri yaani cancelling kwa wagonjwa wa saratani na watu upunguza mawazo na kuendelea na maisha Yao ya kila siku na wengine wanaotumia masage yaani kunyoosha sehemu iliyoathiriwa na damu inaweza kutembea kwenye sehemu husika na wengine wanaotumia Mazoezi Ili kuweza kutibu sehemu iliyolegea.

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: magonjwa Main: Post File: Download PDF Views 2071

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 Kitabu cha Afya     👉2 kitabu cha Simulizi     👉3 Bongolite - Game zone - Play free game     👉4 Kitau cha Fiqh     👉5 Madrasa kiganjani     👉6 web hosting    

Post zinazofanana:

Dalili za maambukizi ya via vya uzazi (PID) na tiba yake.

Maambukizi ya viungo vya uzazi, kitaalamu kama Pelvic Inflammatory Disease (PID), ni hali ya kuvimba kwa viungo vya uzazi vya ndani ya mwanamke, ikiwemo mji wa mimba, mirija ya uzazi, na ovari. Makala hii inaelezea dalili za ugonjwa huu, sababu zake, na umuhimu wa kupata tiba sahihi na ya haraka ili kulinda uwezo wako wa kuzaa.

Soma Zaidi...
Ishara za Mimba ya Mapema kwa Mara ya Kwanza

​Kugundua ujauzito kwa mara ya kwanza kunaweza kuleta mchanganyiko wa hisia—furaha, msisimko, na wakati mwingine, sintofahamu. Post hii inaangazia ishara za kawaida za ujauzito ambazo mwanamke anaweza kuzihisi katika wiki za kwanza, ikimsaidia msomaji kutambua mabadiliko ya mwili wake kwa usahihi.

Soma Zaidi...
VIRUSI VYA KORONA AU CORONA (CORONAVIRUS)

Virusi vya korona ni katika aina za virusi ambavyo asili yake ni kutoka kwa wanyama na kuja kwa binadamu.

Soma Zaidi...
Vidonda vya tumbo (Peptic Ulcer): Chanzo na vyakula vya kuepuka.

Vidonda vya tumbo ni vidonda wazi vinavyojitokeza kwenye utando wa ndani wa tumbo (gastric ulcers) au sehemu ya juu ya utumbo mdogo (duodenal ulcers). Hali hii hutokea wakati kinga ya utando wa tumbo dhidi ya asidi inapovunjika, na kusababisha maumivu makali, kiungulia, na kichefuchefu. Makala haya yanalenga kukupa uelewa wa chanzo cha vidonda hivi na orodha ya vyakula unavyopaswa kuviepuka ili kusaidia uponyaji wa kidonda na kupunguza maumivu.

Soma Zaidi...
je maambukizi ya virus vya ukimwi yataonekana kwenye kupimo baada ya siku ngap??

Ni muda gani nitaanza kuona dalili za HIV na kilimo kitaonyesha kuwa nimeathirika?

Soma Zaidi...
Fahamu Mambo yanayosababisha Ugonjwa wa kipindupindu

Kipindupindu ni ugonjwa wa bakteria ambao kawaida huenezwa kupitia maji machafu. Kipindupindu husababisha Kuhara na Upungufu wa maji mwilini. Ikiachwa bila kutibiwa, Kipindupindu kinaweza kusababisha kifo kwa muda wa saa chache, hata kwa watu walioku

Soma Zaidi...