image

tarekh 06

MAISHA YA UTOTONI YA MTUME S.

MAISHA YA UTOTONI YA MTUME S.A.W
Ilikuwa ni tamaduni kwa waarabu waishio mjini kuwapeleka watoto wao wachanga vijijini wakalelewe ili wapate ukakamavu, wajifunze lugha vyema na pia kuwaepusha na magonjwa ya miripuko yanayotokea mijini. Hivyo Mtume s.a.w alichukuliwa na Halima bint Dhuaib kutoka katika kabila la bani Sa’ad bin Bakar. Mume wake aliitwa Al-Harith bin ‘Abdul’Uzza pia alitambulia kwa jina la Abi Kabshah.

Halima anasimulia kuwa ulikuwa ni wakati wa ukame sana hususana sehemu ambay alikuwa akiishi yeye na watu wao. Mvua zilikata, wanyama hawakuweza kutoa maziwa kwa ukame uliopo. Wanyama hawakuweza kushiba. Shakula pia kilikuwa ni taabu, lakini tumaini lao lilikuwa ni kusubiria mvua inyeshe. Wakati huo walitoka watu waende mjini kwenda kutafuta watoto wa kuwalea ili waweze kupata kipato kama ujira wa kulea na kunyonyesha watoti hao kama ilivyokuwa ni kawaida yao. Alikuwepo kwenye msafara huu Halima na mume wake.

Bi Halima akiwa amepata punda wake aliyeonekana ni dhaifu sana na mumewe alikuwa amepanda ngamia ameye hakuwa ni mwenye kutoa maziwa. Walifika Maka na wakaanza kutafuta watoto wa kuwanyonyesha. Anaeleza bi halima kuwa katika msafara ule walotoka watu wote walifika kwa mama yake Mtume na kuelezwa kuwa mtoto huyu ni yatima, basi wote wakakataa kumchukuwa Muhammad kwenda kumlea kwa kuhofia wazazi wake hawataweza kulipa gharama kwani mtoto ni yatima.

Msafara huu uliendelea kuzungua Makkah kutafuta watoto wa kuwalea, halimaye bi Halima hakibahatika kupata mtoto, hivyo akashauriana na mumewe kuwa arudi kule kwa mtoto yatima kwani anaona vibaya kurudi mtupu pila ya kuwa na mtoto. Basi mumewe akakubali, na hapo bi Halia akarudi na kumchukuwa mtoto muhammad (s.a.w). na maajabu ndo yakaanza hapa kama vile bi Halima anavyotueleza, Nitataja kwa ufupi zaidi mambo haya yalotokea.

Anaeleza bi Halima kuwa alipombeba mtoto badi alipofika kwenye hema lao aloshangaa kuona maziwa yamejaa, kwa hakika hii ni ajabu kwake kwani hata mtoto wake alikuwa akikosa usingizi usiku kwa uchache wa maziwa. Lakini leo anakuwa na maziwa na kumtosha mtot muhammad pamoja na mtoto wake. Kwa hakika walinyonya watoto hawa wawili mpaka wakashiba na kulala.

Bi halima anasimulia kuwa mume wake alipotoka kwenda kumuangalia ngamia wake alishangaa kuona ngamia ana maziwa ya kutosha, alikamua maziwa kutoka kwenye ngamia wake wakanywa na kushiba. Hii pia ni ajabu aloishuhudia Bi halima baada ya kumchukuwa kijana Mhammad kwa ni hapo mwanzo ngamia wao hakuweza kutoa hata tone la maziwa ya kuweza kunywa, lakini leo ngamia huyu anatoa maziwa ya kuweza kushiba watu wa familia hii na kuyabakisha. Bi Halima anasimula kuwa asubuhi ya siku ilofata mume wangu aliniambia “ hakikahalima umechukuwa mtoto mwenye kubarikiwa” nikamjibu “nami natarajia iwe hivyo”.

Siku ilofata safari ya kurudi kutoka maka kwenda kwao ilianza. Katika msafara huu walishangaa kumuona punda wa halima amebadilika kwani amekuwa na nguvu na ameongeza uwezo wa kukimbia. Ilifikia wakati wnzie wakawa wanamwmbia nenda kipolepole ewe Halima kwa hakika huyu si yule pinda ulokuja ne. Ukweli ni kuwa punda ni yuleyule lakini Allah ameta miujiza yake hapa.

Walipofika nyumbani walishangaa kuona mifugo yao inarudi kutoka malishoni ikiwa imeshiba sana, wakati kulikuwa na ukame mkubwa sana. Mifugo yao iliweza kutoa maziwa mengi. Ilifikia wakati wamiliki wa mifugo wakawa wanawaambia wachungaji wao kuwa wachunge pale anapochungia mchungaji wa bi Halima. Ukweli ni kuwa majani ni yale yale isipokuwa Allah anaweza miujiza yake kwa bi Halima.

Kwa hakika bi Halima aliona miujiza mingi sana, na maisha yake yalibadilika na kuwa na raha na amani to ka amchukuwe mtoto Muhammad (s.a.w). bi Halima anasimulia kuwa mtoto Muhammad alikuwa anakuwa kwa haraka zaidi tofauti na alivyozoea. Bi Halima alimlea mtoto huyu kwa muda wa miaka miwili hata muda wa kumuachisha ziwa ukawadia. Ilikuwa anatakiwa ampeleke mtoto kwa mama yake.

Basi mtoto alipotimia miaka miwili kwa shingo upande bi Halima alimrudisha mtoto kwa mama yake. Huku akiwa haridhiki kwani ameona neema nyingi toka amchukuwe mtto huyu. Alipofika Makkah alimshawishi mamayake amruhusu aweze kurudi nae aendelee kumlea kwa kuhofia mtoto atpata maradhi ya mjini maradhi ya milipuko. Kwa sababu hii mama yake Mtume bi Amina alikubali hivyo bi Halima akaendelea kumlea mtoto huyu. Hvyo Mtume aliendelea kuishi kule na kuendelea kuimarika kimwili na kuwa na afya njema pamoja na kupata ufasaha katika lugha ya kiarabu.


                   



           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Kama unahitaji kuuliza maswali Bofya hapa

Mwandhishi Tarehe 2018-08-01     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 51


Download our Apps
👉1 Madrasa kiganjani     👉2 Kitabu cha Afya     👉3 Kitau cha Fiqh     👉4 kitabu cha Simulizi    

Post zifazofanana:-

Mapambano ya Dola ya kiislamu dhidi ya maadui wa kikristo (warumi) wakati wa Mtume
Soma Zaidi...

Adam na Hawah Kushushwa Ardhini
Soma Zaidi...

Vitimbi vya Makafiri Dhidi ya Nabii Salih(a.s) na Waumini na kuangamizwa kwao
Makafiri wa Kithamud hawakuishia tu kwenye kuukataa ujumbe wa Nabii Salih(a. Soma Zaidi...

Hatua mbili kuu za kushuka kwa Quran
Quran (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

Kuandaliwa Mtume(s.a.w) maandalizi ya kimafunzo na maandalizi ya ki ilham
Mitume huzaliwa Mitume. Soma Zaidi...

historia na maisha ya Mtume IS-HAQ(A.S.) NA YA‘AQUUB(A.S.)
Is-haq(a. Soma Zaidi...

Kazi na wajibu wa khalifa katika dola ya kiislamu
Kazi na Wajibu wa KhalifaKhalifa katika Serikali ya Kiislamu ndiye mtendaji mkuu wa Serikali kama alivyokuwa Mtume(s. Soma Zaidi...

Bara arabu enzi za jahiliyyah, jiografia ya bara arabu
Bara arabu zama za jahiliyyah (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

Mafunzo Yatokanayo na Historia ya Bani Israil
Soma Zaidi...

Kwanini mwanadamu hawezi kuunda dini sahihi
Dini anayostahiki kufuata mwanadamu (EDK form 2 dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

NI UPI MKATABA WA AL-FUDHUL NA ASILI YAKE, ATHARI ZAKE NA WALOHUSIKA
MKATABA WA AL-FUDHULBaada ya vita hivi viongozi wa pande mbili hizi waliamuwa wakae chini na wakubaliane kuweka kanun i na utaratibu utakaozuia kutotokea uonevu kama huuu tena. Soma Zaidi...

Kusilimu kwa Wachawi wa Firaun
Mawaziri waliokuwa washauri wakuu wa Firauni wakataka wakusanywe magwiji waliobobea katika uchawi nchi nzima, kisha wapambanishwe na Nabii Musa(as). Soma Zaidi...