picha

Historia ya Mtume Muhammad ﷺ somo la 69: Kikao cha kumuuwa Mtume Muhammad s.a.w kinakaliwa

Katika somo hili utajifunza mambo yaliojiri katika kikao kilicho andaliwa kwa ajili ya kumuuwa Mtue Muhammad s.a.w. Katika kikao hiki mpaka Iblis alihudhuria

Katika Nyumba ya An-Nadwah: Bunge la Kuraish

Washirikina wa Makkah walikuwa wameshikwa na hofu kubwa kutokana na mpango wa haraka na uliojaa weledi wa wafuasi wa Mtume (Rehema na Amani ziwe juu yake) kuhamia Madinah, makao mapya ya Uislamu. Walikumbwa na wasiwasi mkubwa kuhusu hatima ya jamii yao ya kipagani na mfumo wao wa kiuchumi. Tayari walikuwa wamemshuhudia Muhammad (Rehema na Amani ziwe juu yake) kama kiongozi mwenye ushawishi, huku wafuasi wake wakiwa ni watu waaminifu, wanyofu, na walio tayari kujitolea mali zao zote kwa ajili ya Mtume wa Allah.

 

Makabila ya Al-Aws na Al-Khazraj, waliotarajiwa kuwa wenyeji wa Waislamu wa Makkah, walijulikana kote Arabia kwa uwezo wao wa kijeshi na busara zao katika masuala ya amani. Walikuwa wamechoka vita vya kikabila na walikuwa wapinzani wa chuki na uhasama. Madinah, yenyewe, iliyoonekana kuwa makao makuu ya mwito wa Kiislamu uliokuwa ukikua kwa kasi, ilikuwa na umuhimu mkubwa wa kistratejia. Mji huo ulidhibiti njia muhimu za biashara zinazoelekea Makkah, ambapo watu wake walihusika na biashara yenye thamani ya takribani dinari za dhahabu robo milioni kila mwaka. Usalama wa njia hizi za misafara ulikuwa muhimu kwa ustawi wa maisha ya kiuchumi.

 

Kwa kuzingatia mambo haya yote, washirikina walihisi kuwa walikuwa katika hatari kubwa. Hivyo basi, walianza kutafuta mbinu bora zaidi za kuzuia hatari hiyo iliyokuwa inakuja kwa kasi. Mnamo Alhamisi, tarehe 26 Safar, mwaka wa 14 wa Utume (12 Septemba 622 BK), yaani miezi miwili na nusu baada ya Ahadi Kubwa ya ‘Aqabah, walikusanyika kwa mkutano wa dharura katika Nyumba ya An-Nadwah, “Bunge la Makkah.” Huu ulikuwa mkutano wa kihistoria, ukiwa na ajenda moja: kutafuta suluhisho la kuzuia wimbi hili kubwa la Uislamu.

Wajumbe waliwakilisha makabila yote ya Kuraish, miongoni mwao wakiwa:

Wakiwa njiani kuelekea Nyumba ya An-Nadwah, Ibilisi (Shetani), katika sura ya mzee mwenye haiba kutoka Najd, alisimama mlangoni na kuwakatiza. Alijitambulisha kama mtu anayevutiwa na mkutano huo, akitaka kusikiliza mjadala na kutoa baraka zake kwa maamuzi ya busara. Alipewa ruhusa ya kuingia.

 

Ukweli wa mambo ni kuwa mzee huyu hakuwa ni mtu wa Najid bali alikuwa ni iblisi na alikuja ili kuhakikisha inapatikana rai itakayokuwa ni mujarabu katika kummaliza Muhammad. Basi punde baada ya watu kuingia ndani mkutano ukaanza. Rai mbalimbali zikaanza kutolewa na huku mzee wa Najd (Iblis) akawa anapangua rai hizo kwa hoja zilizo madhubuti. Miongoni mwa rai hizo ni kama zifuatazo:-

 

A. Basi mtu mmoja aliyetambulika kwa jina la Abuu Aswad akazungumza kuwa “tumtoeni (tumfukuzeni) Muhammad kwenye mji wetu (Makkah) na aende kokote atakakotaka na katu tusijali popote atakapokwenda, tukifanya hivyo kwa hakika tutakuwa tumesalimika na mambo yatarudi kama yalivyokuwa.


B. Basi hapo mzee wa Najd (Iblis) akasema kuwa: kwa hakika jambo hili sio salama kabisa kwenu. Akasema “hivi hamjaona jinsi yalivyo matamu maneno yake?, na utamu na ufasaha wa matamko yake, kama mkimtoa atakwenda kupata wafuasi wengine wasiokuwa nyinyi, na atakuwa na nguvu kisha atakuvamieni na kukutoeni kwenye miji yenu, na afanye atakachokitaka. Kwa hakika rai hii sio salama toeni rai nyingine isiyokuwa hii.


C. Mtu mwingine aliyefahamika kwa jina la Abuu Al-Bakhtar akasema “mfungieni kwenye chumba chenye milango madhubuti, na kisha abakie humo na yampate yele yalowapata waliotangulia kabla yenu (baada ya kupewa adhabu kama hii) mpaka mauti yamkute”


D. Baada ya kutolewa rai hii mzee wa Nadj (Iblis) akaipinga tena rai hii kwa kusema hapana hili pia si jema, kwa hakika naapa kwa Allah kuwa kama mtafanya hivyo wafuasi wake watakuja kumtoa. Watu walionekana pia kukubali wazo hilo kuwa rai hii pia sio salama. Kwani hata nduguzake wangemtoa wasingeweza kumuacha, kwani walisha mfungia kabla hapo yeye na familia yake.


E. Basi baada ya muda mkuu wa makafiri wa Makkah Abuu Jahal akazungumza “kwa hikika naapa kwa Allah kuwa nina rai ambayo hamjaitoa” watu wakasema ni ipi rai hiyo? Akasema “na tuchukuwe kutoka katika kabila mtukijana mmoja mwenye nguvu na afya njema, kisha tumpatie upanga ulio safi na mkali kisha kila mmoja katia vijana hawa akampige (Muhammad) upanga mmoja na wamuue na wakifanya hivi atakuwa ameuliwa na kabila zote za watu wa Makkah hivyo hata familia yake haitaweza kulipiza kisasi.


F.Watu walionekana kuikubali rai hii na hata mzee wa Najd (Iblis) hakuweza kuipinga rai hii hata kidogo. Na kisha akasema mzee wa Najd “hii ndio rai ambayo hakuna rai nyingine (bora zaidi) kuliko hii".

 

Baada ya kumaliza kikao kwa kukubaliana kutekeleza hoja ya kumuua Muhammad, watu wote walitawanyika. Vijana kutoka katika kila kabila walichukuliwa tayari kwa kwenda kummaliza Muhammad

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2025-01-25 08:43:51 Topic: Historia ya Mtume Muhammad (s.a.w) Main: Masomo File: Download PDF Views 1186

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 Simulizi za Hadithi Audio     👉2 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)     👉3 Madrasa kiganjani     👉4 Kitabu cha Afya     👉5 Kitau cha Fiqh     👉6 Tafasiri ya Riyadh Swalihina    

Post zinazofanana:

Historia ya Mtume Muhammad ﷺ somo la 55: Mazungumzo ya Utbah bin Rabi'a na Mtume Muhammad (SAW)

Baada ya Quraish kufeli mbinu zao za mateso, sasa wanaanza mbinu za diplomasi, wanajaribu kumshawishi Mtume kwa kumpa mali nauongozi

Soma Zaidi...
Historia ya Mtume Muhammad ﷺ somo la 9: Kupasuliwa kwa Kifua Mtume Wakati Akiwa Mtoto

Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu tukio la Kupasuliwa kwa Kifua Mtume Wakati Akiwa Mtoto

Soma Zaidi...
Historia ya Mtume Muhammad ﷺ somo la 41: Mbinu za kukomesha kuenea kwa uislamu

Katika somo hili utakwenda kujifunza mambo yaliyofanyika katika harakati za kukomesha kuenea kwa uislamu.

Soma Zaidi...
Historia ya Mtume Muhammad ﷺ somo la 29: Amri za kwanza alizopewa Mtume Muhammad ﷺ

Katika somo hili utajifunza amri ambazo alipewa Mtume Muhammad ﷺ mwanzoni kabisa mwa kazi yake ya Kulingania dini

Soma Zaidi...
Historia ya Mtume Muhammad ﷺ somo la 47: Nyumba ya Arqam Ibn Abi Al Arqam na kazi zake

Katika somo hili utakwenda kujifunza mchango mkubwa wa nyumba ya Arqam Ibn Abi AL Arqam katika historia nzima ya Uislamu

Soma Zaidi...
Historia ya Mtume Muhammad ﷺ somo la 37: Amri ya kulingania watu wote kwenye Mlima As-Safa

Katika somo hili utakwend akujifunza kuhusu amri ya kulingania wtu wote, yale yaliyojiri katika mkutano wa kwanza na laana ya Abu Lhab. TUkio hili lilianyika katika mlima As-safa

Soma Zaidi...