Historia ya Mtume Muhammad ﷺ somo la 69: Kikao cha kumuuwa Mtume Muhammad s.a.w kinakaliwa

Katika somo hili utajifunza mambo yaliojiri katika kikao kilicho andaliwa kwa ajili ya kumuuwa Mtue Muhammad s.a.w. Katika kikao hiki mpaka Iblis alihudhuria

Katika Nyumba ya An-Nadwah: Bunge la Kuraish

Washirikina wa Makkah walikuwa wameshikwa na hofu kubwa kutokana na mpango wa haraka na uliojaa weledi wa wafuasi wa Mtume (Rehema na Amani ziwe juu yake) kuhamia Madinah, makao mapya ya Uislamu. Walikumbwa na wasiwasi mkubwa kuhusu hatima ya jamii yao ya kipagani na mfumo wao wa kiuchumi. Tayari walikuwa wamemshuhudia Muhammad (Rehema na Amani ziwe juu yake) kama kiongozi mwenye ushawishi, huku wafuasi wake wakiwa ni watu waaminifu, wanyofu, na walio tayari kujitolea mali zao zote kwa ajili ya Mtume wa Allah.

 

Makabila ya Al-Aws na Al-Khazraj, waliotarajiwa kuwa wenyeji wa Waislamu wa Makkah, walijulikana kote Arabia kwa uwezo wao wa kijeshi na busara zao katika masuala ya amani. Walikuwa wamechoka vita vya kikabila na walikuwa wapinzani wa chuki na uhasama. Madinah, yenyewe, iliyoonekana kuwa makao makuu ya mwito wa Kiislamu uliokuwa ukikua kwa kasi, ilikuwa na umuhimu mkubwa wa kistratejia. Mji huo ulidhibiti njia muhimu za biashara zinazoelekea Makkah, ambapo watu wake walihusika na biashara yenye thamani ya takribani dinari za dhahabu robo milioni kila mwaka. Usalama wa njia hizi za misafara ulikuwa muhimu kwa ustawi wa maisha ya kiuchumi.

 

Kwa kuzingatia mambo haya yote, washirikina walihisi kuwa walikuwa katika hatari kubwa. Hivyo basi, walianza kutafuta mbinu bora zaidi za kuzuia hatari hiyo iliyokuwa inakuja kwa kasi. Mnamo Alhamisi, tarehe 26 Safar, mwaka wa 14 wa Utume (12 Septemba 622 BK), yaani miezi miwili na nusu baada ya Ahadi Kubwa ya ‘Aqabah, walikusanyika kwa mkutano wa dharura katika Nyumba ya An-Nadwah, “Bunge la Makkah.” Huu ulikuwa mkutano wa kihistoria, ukiwa na ajenda moja: kutafuta suluhisho la kuzuia wimbi hili kubwa la Uislamu.

Wajumbe waliwakilisha makabila yote ya Kuraish, miongoni mwao wakiwa:

Wakiwa njiani kuelekea Nyumba ya An-Nadwah, Ibilisi (Shetani), katika sura ya mzee mwenye haiba kutoka Najd, alisimama mlangoni na kuwakatiza. Alijitambulisha kama mtu anayevutiwa na mkutano huo, akitaka kusikiliza mjadala na kutoa baraka zake kwa maamuzi ya busara. Alipewa ruhusa ya kuingia.

 

Ukweli wa mambo ni kuwa mzee huyu hakuwa ni mtu wa Najid bali alikuwa ni iblisi na alikuja ili kuhakikisha inapatikana rai itakayokuwa ni mujarabu katika kummaliza Muhammad. Basi punde baada ya watu kuingia ndani mkutano ukaanza. Rai mbalimbali zikaanza kutolewa na huku mzee wa Najd (Iblis) akawa anapangua rai hizo kwa hoja zilizo madhubuti. Miongoni mwa rai hizo ni kama zifuatazo:-

 

A. Basi mtu mmoja aliyetambulika kwa jina la Abuu Aswad akazungumza kuwa “tumtoeni (tumfukuzeni) Muhammad kwenye mji wetu (Makkah) na aende kokote atakakotaka na katu tusijali popote atakapokwenda, tukifanya hivyo kwa hakika tutakuwa tumesalimika na mambo yatarudi kama yalivyokuwa.


B. Basi hapo mzee wa Najd (Iblis) akasema kuwa: kwa hakika jambo hili sio salama kabisa kwenu. Akasema “hivi hamjaona jinsi yalivyo matamu maneno yake?, na utamu na ufasaha wa matamko yake, kama mkimtoa atakwenda kupata wafuasi wengine wasiokuwa nyinyi, na atakuwa na nguvu kisha atakuvamieni na kukutoeni kwenye miji yenu, na afanye atakachokitaka. Kwa hakika rai hii sio salama toeni rai nyingine isiyokuwa hii.


C. Mtu mwingine aliyefahamika kwa jina la Abuu Al-Bakhtar akasema “mfungieni kwenye chumba chenye milango madhubuti, na kisha abakie humo na yampate yele yalowapata waliotangulia kabla yenu (baada ya kupewa adhabu kama hii) mpaka mauti yamkute”


D. Baada ya kutolewa rai hii mzee wa Nadj (Iblis) akaipinga tena rai hii kwa kusema hapana hili pia si jema, kwa hakika naapa kwa Allah kuwa kama mtafanya hivyo wafuasi wake watakuja kumtoa. Watu walionekana pia kukubali wazo hilo kuwa rai hii pia sio salama. Kwani hata nduguzake wangemtoa wasingeweza kumuacha, kwani walisha mfungia kabla hapo yeye na familia yake.


E. Basi baada ya muda mkuu wa makafiri wa Makkah Abuu Jahal akazungumza “kwa hikika naapa kwa Allah kuwa nina rai ambayo hamjaitoa” watu wakasema ni ipi rai hiyo? Akasema “na tuchukuwe kutoka katika kabila mtukijana mmoja mwenye nguvu na afya njema, kisha tumpatie upanga ulio safi na mkali kisha kila mmoja katia vijana hawa akampige (Muhammad) upanga mmoja na wamuue na wakifanya hivi atakuwa ameuliwa na kabila zote za watu wa Makkah hivyo hata familia yake haitaweza kulipiza kisasi.


F.Watu walionekana kuikubali rai hii na hata mzee wa Najd (Iblis) hakuweza kuipinga rai hii hata kidogo. Na kisha akasema mzee wa Najd “hii ndio rai ambayo hakuna rai nyingine (bora zaidi) kuliko hii".

 

Baada ya kumaliza kikao kwa kukubaliana kutekeleza hoja ya kumuua Muhammad, watu wote walitawanyika. Vijana kutoka katika kila kabila walichukuliwa tayari kwa kwenda kummaliza Muhammad

Download App Yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.

Download Now Bongoclass

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:45 Topic: Historia ya Mtume Muhammad (s.a.w) Main: Dini File: Download PDF Views 172

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Kitabu cha Afya    👉2 Bongolite - Game zone - Play free game    👉3 Kitau cha Fiqh    👉4 Madrasa kiganjani    👉5 Simulizi za Hadithi Audio    👉6 kitabu cha Simulizi   

Post zinazofanana:

Historia ya Mtume Muhammad ﷺ somo la 70: Kuhama kwa Mtume Muhammad s.a.w kuelekea Madina

Katika somo hili utakwend akujifunz akuhusu safari ya Mtume Muhammad s.a.w kuelekea Madina. Utajifunza changamoto za safari alizokutana nazo.

Soma Zaidi...
Historia ya Mtume Muhammad ﷺ somo la 25 Jibril analeta Wahyi kwa Mtume Muhammad ﷺ

Katika somo hili utakwend akujifunz akuhusu historia ya Mwanzoni mwa Wahyi aliouleta Jibril kwa Mtume Muhammad ﷺ

Soma Zaidi...
Historia ya Mtume Muhammad ﷺ somo la 3: Kufukuliwa upya wa kisima cha Zamzamm

Katika somo hili utakwend akujfunza historia ya kufukuliwa upya kwa kisima cha zamzam baada ya kutoweka kwa muda mrefu

Soma Zaidi...
Historia ya Mtume Muhammad ﷺ somo la 43: Mateso walyoyapata waslamu

Katka somo hili utakwenda kujifunza kuhusu mateso ambayo wamepewa Waislamu ili kuachana na uislamu wao

Soma Zaidi...
Historia ya Mtume Muhammad ﷺ somo la 40: Historia fupi ya Walib Ibn Al-Mughira

Katika somo hili utajifunza kuhusu mmoja katika maadui wakubwa wa Mtume Muhammad wakati akilingania watu.

Soma Zaidi...
Historia ya Mtume Muhammad ﷺ somo la 13: Historia fupi ya Abd al-Muttalib

Katika somo hili utakwenda kujifunza historia ya mzee Abdul al MUttalib. Historia hii inaweza kutofautiana kidogo na ambayo umeshajifunza. na hii ni kutokana kutofautiana kwa mapokeo.

Soma Zaidi...
Historia ya Mtume Muhammad ﷺ somo la 53: Kuslimu kwa Hamza bin Abdul-Muttalib

Hapa utajifunza historia ya kuslimu kwa Hamzah bin Abdul-Muttalib.

Soma Zaidi...
Historia ya Mtume Muhammad ﷺ somo la 11: Kufarki kwa babu yake na kulelewa na baba yake mkubwa

Katika somo hili utajifunza kuhusu Mtume MUhammad ﷺ kulelewa na Kufarki kwa babu yake na kulelewa na baba yake mkubwa:

Soma Zaidi...
Historia ya Mtume Muhammad ﷺ somo la 26: Kusimama kwa Wahy

Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu kusimama kwa Wahyi kuja kwa Mtume Muhammad ﷺ

Soma Zaidi...
Historia ya Mtume Muhammad ﷺ somo la 38: Taharuki yaingia Mjini Mkkah

Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu yaliyotokea baada ya watu wa Mkkah kulinganiwa kwenye dini kwa mara ya kwanza

Soma Zaidi...