Hatima ya kijana mchonganishi

Posti hii inakwenda kukupa muendelezo wa hadithi za alifu lela ulela

HATIMA YA KIJANA MCHONGANISHI

Mansur akaondoka haraka akiwa na majozi sana huku akiwaza nitampata wapi kijana huyu. Mansur alijisemea, Mungu aliyeniokoa na janga la kwanza ataniokoa na hili la pili. Mansuri alipofika kwake aliwaeleza kla kitu, na akabakia kwake kwa siku tatu bila kwenda kokote. Manzur ilipofika siku ya tatu akajiwa na mjumbe kutoka kwa khalifa kuwa anahitajika akiwa na muhalifu ama ajiandae kwa kifo. Mansur akaanza kuagana na famiia yake na kuacha usia.

 

Kabla ya kuondoka mwanae mdogo aliyekuwa akimpenda sana alikuja kumkumbatia baba yake kama ishara ya kuagana. Mansur wakati akimkumbatia mwanaye alihisi ugumu kwenye tumbo la mwanaye. Akamuuliza ameweka nini. Mtoto akajibu kuwa nimeweka tunda epo nimepewa na Manyakazi wetu, alikuwa hataki kunipa eti amemnyang’anya mtoto wa watu ambaye baba yake amekwenda mbali kununua maepo matatu kwa gharama ya vipande 15 vya dhahabu.

 

Mansur aliposikia habari hii alifurahi sana na kusema ssa nimeokoka. Hapo akamchukuwa mfanyakazi wake na kwenda naye kwa khalifa. Kijana akaulizwa na kukirikonsa. Khalifa akaagiza habari hii iandikwe kwa wino wa dhahabu na ihifadhiwe kwenye kumbukumbu ya nyaraka za kushangaza na kutisha. Kisha waziri Mansur akasema ewe khlifa ninakiri kuwa mfanyakazi wangu amepatwa na hatia. Ila ninakuomba kuwa nitakusimulia kisa cha kushangaza zaidi ya hiki, na endapo utakirikuwa kimeshangaza zaidi naomba iwe fidia umuache huru mfanyakazi wangu.

 

Khalifa alikubaliana na maneno haya na hapo Mansur akaanza kusimulia hadithi ya Nurdini.

 

Tukutane kitabu cha tatu hadithi ya Nurdin

 

Huu ndio mwisho wa kitabu cha pili hadithi za Alif lela u lela. Usiwache kuwa nasi tukutane kitabu cha tatu. Kama unahitajikitabu cha kwanza na pili wasiliana nasi.

Download App Yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.

Download Now Bongoclass

Nyuma Endelea


Je umeipenda post hii ?

Ndio            Hapana            Save post
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Aliflela2 Main: Burudani File: Download PDF Views 1066

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Madrasa kiganjani    👉2 Kitau cha Fiqh    👉3 Simulizi za Hadithi Audio    👉4 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉5 kitabu cha Simulizi    👉6 Kitabu cha Afya   

Post zinazofanana:

Aladini na binti wa mfalme

Posti hii inakwenda kukupa muendelezo wa hadithi ya aladini na taa ya mshumaa wa ajabu

Soma Zaidi...
Ugeni wa dhati

Posti hii inakwenda kukupa muendelezo wa hadithi ya aladini na taa ya ajabu

Soma Zaidi...
Hadithi iliyosimuliwq na mlevi mbele ya sultani

Posti hii inakwenda kukusimulia hadithi iliyosimuliwa na mlevi mbele ya sultan

Soma Zaidi...
Hadithi ya aliyekatwa vidole gumba

Posti hii inakwenda kukupa muendelezo kuhusu kifo cha mtoa burudani wa sultani

Soma Zaidi...
Siri ya kifo yafichuka

Posti hii inakwenda kukupa muendelezo wa hadithi za alifu lela ulela

Soma Zaidi...
Ndoa ya siri

NDOA YA SIRI YAFANYIKA Hatimaye siku ya ijumaa ikafika na mimi nikaoga nyema na kuchukuwa kanzu iliyo nadhifu zaidi.

Soma Zaidi...
Kwanini dirisha moja?

Posti hii inakwenda kukupa muendelezo wa hadithi ya aladini na taa ya ajabu

Soma Zaidi...