Hadithi iliyosimuliwa na mshona nguo

Posti hii inakwenda kukupa muendelezo kuhusu kifo cha mtoa burudani wa sultani

HADITHI ILIYOSIMULIWA NA MSHONA NGUO (FUNDI SHERAHANI)

Jana tulikuwepo kwenye sherehe moja ya wafanyabiashra. Mmoja kati ya wafanyabiashara alikuwa na sherehe yake, nayo ni nadhiri aliyoiweka pindi mambo yakiwa safi atalisha watu bure kwa masaa machache ya siku. Katika sherehe hiyo ilipofanyika chakula kizuri kiliandaliwa. Niliwaza hata kuchukuwa chakula niende nikampatia mkewangu naye apate kuonja vitamu, vilivyoandaliwa na mfanyabiashara.

 

Sikuwa na mtoto hivyo chakula kidogo kingemtosha mke wangu kipenzi kutuliza hamu yake. Kama ilivyo ni kawaida hatukupewa viti vya kukalia bali mazulia mazurimazuri yaliyopambwa vyema yalitandikwa. Waungwana na watumwa tukajiweka vyema na kuandaa matumbo yetu kwa kinacholetwa. Mazulia yalitandikwa kwa mpango wa duara na katikati ndipo kulikuwa na meza kuu.

 

Zulia lililopo kati lilikuwa ni bora, zuri na lenye thamani kubwa. Kimoyoni nilijisemea “kweli itifaki imezingatiwa”. zulia hilo la meza kuu liliandikwa maneno ya kiarabu yaliyonyooka vyema kama mapambo ya mauwa. Rangi ya manjano ilikolea mithili ya dhahabu ya Moroko. Lilipata kubonyea zulia hili midhili ya godoro, hata nikastaajabu uzito ulioje wa zulia hili. Nilitamani niengeliona wakati linatandikwa. Ila nikajiridhisha badala ya kuliona lipo kwenye vipande vilivyoungwa vyema.

 

Muda haukukawia sana mnawishaji akapita na kutoa maelekezo kuwa wawiliwawili ndio mpango wa kula. Nilikuwa na mwenzangu ambaye alikuwa akijishughulisha na shughuli za unyoaji yaani kinyozi. Alikuwa amevaa vyema na mavazi yamemkaa sawiya. Muda wote hakuwacha kutabasamu utadhani amebebeshwa gunia la furaha. Nilitamani sana kuwa kama yeye hasa ilipoona uso wake ulio mkunjufu usio na mikunyo kama anayekula ndimu.

 

Nilitamani niwenaye karibu, nipate kujuwa ni manukato gani anatumia, lakini sikufanya hivyo. Wakati haya yote yakiendelea nikathubutu kuchungulia kwa ndani kwa furaha niliona sahani zinaletwa. Sahani za vyakula ziliongozana na waheshimiwa waliopaswa kukaa kwenye zulia la wageni maalumu. Katia msafara huo ilionyesha kweli ni msafara wa wafanya bishara. Kwa mavazi, walipendeza vyema. Wakina ni vijana watatu na mzee wa makamo mwenye ndevu nyeupe na nyeusi..

 

Walipofika mlangoni wakasimama kuangalia hadhara, wakati huo wanaongea na mwenyeji wa shughuli. Wakiwa wao wanazungumza huku tayari vyakula vilianzwa kugawiwa. Sinia kubwa liliwekwa mbele yetu. Ndani ya sinia hili kulikuwa na vyakula pamoja na vinywaji. Nyama za kuoka na kupikwa vyema, vyakula vipendwavyo pamoja na michuzi mizito. Mikate iliyopikwa vyema na mchuzi wa kutowea. Juisi ya matunda yaliyochujwa vyema, uzitowake utadhani ni asali mbichi iliyokaa siku 10 ndani ya mtungi. Kwa ukarimu walio nao maji ya kuywa yalikuwa ni maji kutoka Miji mitakatifu.

 

Wale wageni badala ya kuzungumza kidogo wakaanza kuelekea kwenye kikalio chao. Sasa kijana mmoja kati ya wale wageni akakunja sura kwa ghafla, kanakwamba amechanganyikiwa badala ya kuona kitu cha ajabu sana. Haya yote yalitokea badala ya yeye kuangalia upande ambao mimi na wenzangu tuliuwa tumekaa. Watu walipatwa na shauku ya kutaka kujuwa nini kimemtokea mbele za watu pale. Yule kijana ikaonekana anataka kuondoka kwenye shughuli ile. Mwenyeji alionekana kumsihi sana asiondoke lakini wapi.

 

Kumbe sikuwa mimi tu bali tulikuwa wengi ambao tulikuwa tukifatilia kwa ukaribu tukio lile. Watu walio karibu wakatika kujuwa hasa kwa nini mgeni wetu anataka kuondoka. Hapo mwenyeji wa shuguli akamuomba aeleze kitu ambacho hakukifurahia. Kijana yule akasema kuwa hapa nimeoa mtu ambaye niliapa katika maisha yangi kuwa sitakaa naye sehemu moja, mji mmoja wala nchi mmoja. Kisha akamuonyesha yule kinyozi. Watu wakataka kujuwa hasa ni kitu gani kilitokea kati yao. Kijana akasema kuwa huyo kinyozi ndio sababu ya yeye maisha yake kuwa vululu, kuvunjiaka mguu na mabaya makubwa mengi yalimpata kwa sabbu ya kinyozi. Kisha kijana akaanza kusimulia hasa kilichotokea kati yao:-



Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Kama unahitaji kuuliza maswali Bofya hapa

Mwandhishi Tarehe 2021-11-07     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 941


Download our Apps
👉1 Kitabu cha Afya     👉2 kitabu cha Simulizi     👉3 Kitau cha Fiqh     👉4 Madrasa kiganjani    

Post zifazofanana:-

USALITI (sehemu ya kwanza)
Post hii inahusu zaidi vijana wawili ambao ni msichana na mvulana walioingia kwenye mahusiano wakiwa sekondari na wakahaidiana kuoana ila kwa sababu mbalimbali walizokutana nazo kwenye safari yao ya mahusiano mmoja akamsaliti mwingine na kusababisha kupo Soma Zaidi...

Aladini katika pango la utajiri
Posti hii inakwenda kukupa muendelezo wa hadithi ya aladini na taa ya ajabu Soma Zaidi...

Malipo ya wema ni wema
Posti hii inakwenda kukuletea hadithi za alifu lela ulela Soma Zaidi...

NIMLAUM NANI? (Sehemu ya pili)
Post hii ni mwendelezo wa hadithi iliyopita ambapo Frank aliwakuta Amina ambaye ni mpenzi wake ameumbatiana na James ambaye ni rafiki yake ,kwa hiyo tuendelee kusikia yaliyotokea baada ya Amina na James kukutwa na Franki. Soma Zaidi...

Hadithi iliyosimuliwa na tabibu
Posti hii inakwenda kukupa muendelezo kuhusu kifo cha mtoa burudani wa sultani Soma Zaidi...

Dalili za vidonda vya tumbo
Vidonda vya tumbo no tatizo linalotokea baada ya kuta za tumbo au utumbo mdogo kuwa na vidonda,hutokea baada ya ukuta wenye ute unaozuia kemikali za kuyeyusha chakula unaitwa mucus kuharibika. Vidonda vya tumbo (peptic ulcers) imegawanyika katika ma Soma Zaidi...

Fikra potofu kuhusu vidonda vya tumbo
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu baadhi ya fikra potofu kuhusu vidonda vya tumbo Soma Zaidi...

Hadithi ya tunda la tufaha (epo)
Posti hii inakwenda kukupa muendelezo wa hadithi za alifu lela ulela Soma Zaidi...

Hadithi ya binti mwenye kufichwa mtoto wa mfalme
Posti hii inakwenda kukuletea hadithi za alifu lela ulela Soma Zaidi...

Kuelekea bonde la uokozi
Posti hii inakwenda kukupa muendelezo wa safari saba za Sinbad Soma Zaidi...

Safari ya tano ya Sinbad
Posti hii inakwenda kukupa muendelezo wa safari saba za Sinbad Soma Zaidi...

Dalili ya mimba ya wiki moja(1)
Mwanaume na mwanamke wanapo kutana na kujamiina kama mwanamke yupo kwenye ferlile process ni rahisi kupata mbimba. Sparm Zaid ya million moja huingia kwenye mfuko wa lakin sparm moja ndio huweza kuingia kwenye ovum(yai)lakin nyingine hubaki kwenye follopi Soma Zaidi...