Upendo uliotafsiriwa kwa michoro

Posti hii inakwenda kukupa muendelezo wa hadithi ya aladini na taa ya ajabu

UPENDO ULIOTAFASIRIWA KWA MICHORO

Bint mfalme akamwambia mama akae kwenye kiti kilichopo pembeni kidogo na kitanda. Kilikuwa ni kiti kikubwa, kizuri kilichotandikwa magotoro yaliyotengenezwa kwa hariri. Kiti kilikuwa na minguu minne yote imetengenezwa kwa madini ya shaba nyekundu. Viigemeo vya kiti kwa kichwani vilitengenezwa kwa dhahabu na kutengeneza umbo zuri mithili ya uwa liliochanua. Vipande vilaini vya hariri vilifunika viegemeo hivyo. Kwa upande wa pembeni viegemeo vya kiti vilitengenezwa kwa vibao vilivyo kunywa vyema ka kuwekewa virungu vilivyotengenezwa kwa lulu. Kwa uzuri wa kiti hiki mama aladini alijisemea kuwa hata kiti cha mfalme hakifikii uzuri huu. Mama aladini aliendelea kufikiri uzuri wa chumba hiki wapi aladini atamuweka mtoto huwu aendane na hadhi yake.

 

Mama alikaa kwenye kiti na binti mfalme akakaa wenye kitanda. Ijapokuwa ndani kulikuwa na kajikiti kengine kadogo lakini binti huyu hakutaka kukaa kwenye kiti hiko. Hapo mama akapata muda wa kuanza kumthaminsha vyema mkwe wake mtarajiwa. Hakika binti sultani alikuwa ni mzuri. Hakuwa na kichogo, kichwa kilijawa a nywele zilizo shuka mpaka katikati ya mgongo. Wakiwa kwenye mazungumzo mama Aladini aligunduwa kuwa midomo ya binti mfalme imenona vyema, kama ametoka nywa subu ya kongoro. Mama Aladini aliendelea kumthaminisha zadi na kujiridhisha kuwa anafaha zaidi. Binti mfalme hakuwa na macho makubwa ila yalikuwa ni meupe yaliyoonekana vyema, nyusi zilizojipanga na kuchora umbo la mwezi mwandamo. Weusi wa nyusi ulizidi weusi wa nywele zake.

 

Zilisimama vyema kope zake, na kutengeneza sura iliyoonekana na umbo la duara kama yai la mbuni. Hakuwa na chunusi wala kipele. Binti sultani aligunduwa kuwa mkwe wake anamthaminisha, hapo akatabasamu kidogo. Binti sultani alikuwa anajikubali kuwa na yeye ni katika warembo, ukweli ni kuwa hakujuwa tu ila yeye ni namba moja. Tabasamu la binti mfalme lilimfanya mama aladini afurahi zaidi. Ukimmya ulitawala kwa kuda kidogo kisha binti mfalme akavuja ukimya na kumwambia mama Aladini “karibu sana mam, kuwa huru, nimekuwa nikiisubiri sana siku kama hii” mama aladini aliridhishwa zaidi na sauti ya mkwe wake. Hakuwa na mikwaruzo, wala ukakasi, ilitoka vyema na kutengeneza mawimbi mazuuri ya sauti yanayoweza kupennya kwene masikio na kuingia ndani yana ya sikio la ndani na kutengeneza maana ya kilichozungumzwa. “ahsante sana mwanangu, yaani nimefurahi sana, kukuona ukarimu wako, ila uzuri wa chumba hiki umenistaajabisha sana” ni maneno ya mama Aladini kuonyesha mshangao wake.

 

“ahasante sana mama, chumba hiki nilikipamba hivi huku nikiwa ninamkumbuka mwanao, kwani tulianza kukutana bwawani akiwa amevaa nguo iliy na rangi ya kijivu. Nilivutiwa na nguo yake lakini ndege wa ajabu alitoea mwenye rangi za kupendeza, ndege huyu alinituwa kichwani na kuelekea juu ya mti alipokuwa mwanao, niliamini kuwa ndege huyu hakuwa ni wa kawaida, ni ndege aliyetumwa kutuunganisha. Toka siku hiyo niliamini kuwa mume wangu si mwingine ila ni kijana yule. Sikuwa nimetambuwa jina lake wala wapi anaishi. Ila kwa uwezo wa mungu nikatambuwa baada ya yale yaliyotokea kati ya mimi na mtoto wa waziri. “

 

Binti mfalme akaendelea kusema “toka siku ile niliyokutana na mwanao nilianza kukibadili chumba hiki, na kukiweka katika hadthi inayofanana na thamani ya mwanao kwenye moyo wangu. Hata hivyo nahisi hata robo yake sikiweza kuifikia, ndipo nikaamuwa kutengeneza mdori kwa wenye sura ya mwanao nipate kumuona kila siku, kila saa kila wakati. Nilidiriki kutuma mashishushu waje kumchora mwanao bila yeye kugundua. Kama unavyoona mapazia, kitanda na kila unachokiona ni ishara ya upendo wangu kwa Aladini.” binti mfalme alizungumza maeno haya mpaka machozi yakaanza kumtoka. hakika nguvu ya mapenzi haina mfano, mama aladini alikuwa akizidi kushangaa kwa kila anachokion, sikia na shuhudia hapa ndani.

 

Bunti mfalme akaendelea kusema “baadaye nikagunduwa kuwa waziri ana njama ya kuniozesha mtoto wake, nililia sana ila machozi yangu hayakuweza kubadili maamuzi ya baba. Nikaamuwa kukipamba chumba hiki na kuweka picha ya ndege yule aliyetukutanisha ili iwe kumbukumbu ya moyo wangu. Amini ninachokwambia kuwa chumba hiki sikupata kumuingiza mtu yeyote ila ni wewe tu. Na huwa nikilala pindi ninapomkumbuka Aladini. Hata baba yangu hatambui uwepo wa chumba hiki katika ikulu hii” mama Aladini alithibitisha uwepo wa nguzu za giza la mapenzi kwa mtoto huyu. “sikui Aladini amemroga binti wa watu” ni aneno aliyojisemea mama Aladini huku akimkumbatia mkwewe na kumfuta machozi.

 

Wawili hawa waliendelea kuzungumza hata ukafika muda wa kuondoka. Mama Aladini aliondoka kwenye chumba na kurudi kwa mfalme ili kupata maelekezo nini kitafuata. Mfalme akamueleza kuwa mwambie mwanao ajinadae ijumaa ya wiki ijayo ndi harusi yao. Mama Aladini aliondoka kwa furaha, lakini kwa upande wa waziri hakukuwa hata na tone la furaha, ila majuto, hasira na ukatili ndio vilitawala zaidi. Mama Aladini lifika kwa mwanaye kipenzi na kumpatia habari za furaha. Aladini alifurahi sana. Pia mama Alimueleza kila alichokiona na kugundua yaliyokuwemo kwenye moyo wa binti mfalme. Aladini laifurahi zaidi. Aladini alimuahidi mama yake nitajenga ikulu nzui kuliko ikulu zote duniani, chumba kizuri kuliko nyumba vyote duniani.

Mama aladini alimuangalia mwanaye kwa macho ya ukali na mshangao. Aladini hujatembea popote, hiko chumba kizuri utakijuaje, ukweli ni kuwa Aladini alikusudia baadhi ya aliyoyaona kule kwenye pango yawepo kwenye ikulu yake na mengineyo. Hivyo mambp yakawa kama hivyo na Aladini akaanza kujenga ikulu lake kwa ajili ya mrembo binti mfalme.

Kama unahitaji kuuliza maswali Bofya hapa

Mwandhishi Tarehe 2021-11-08     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 1141

Post zifazofanana:-

Mambo yanayochangia Ili dawa kuingia kwenye damu vizuri
Post hii inahusu zaidi mambo yanayochangia Ili dawa iingie vizuri kwenye damu, na mambo yanayoweza kusababisha dawa kuingia au kutoingia vizuri kwenye damu. Soma Zaidi...

Faida za kula karoti
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu faida za kula karoti Soma Zaidi...

Faida kula fenesi
Somo hili linakwenda kukuletea faida za kiafya za kula fenesi Soma Zaidi...

Changamoto za kwenye ndoa kwa waliotoa mimba mara Kwa mara
Posti hii inahusu zaidi changamoto za kwenye ndoa kwa wale waliotoa mimba mara Kwa mara,hizi ni changamoto za wakati wa kufanya tendo na mme wake au mtu mwingine kwa ajili ya kupata mtoto. Soma Zaidi...

Maumivu ya uume baada ya tendo la ndoa
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu maumivu ya uume baada ya tendo la ndoa Soma Zaidi...

Sababu za kshuka surat al Asr
Sura hii ni katika sura za kitawhidi sana. Maulamaa wanasema inatosha sura hii kuwa ni mawaidha. Imamu sharifu anasema kuwa sura hii inatosha kuwa muongozo… Soma Zaidi...

Njia za jumla za kujikinga na magonjwa mbalimbali
Posti hii inahusu zaidi njia mbalimbali za kujikinga na magonjwa, kwa kawaida tunajua wazi kuwa magonjwa yapo na yanasambaa kutoka kwa mtu mmoja kwenda kwa mwingine na mengine hayasambai yanaweza kumpata mtu mmoja akapona au magonjwa mengine si ya kupona Soma Zaidi...

Vyakula vya vitamin K
Some Hili linakwenda kukueleza kuhusu faida za vyakula vya vitamin K Soma Zaidi...

Mwanaune anapataje fangasi kwenye uume
Post hii itakujulishs kwa namna gani mwanaune anaweza kupata fangasi kwenye uume wake Soma Zaidi...

Matibabu ya vidonda vya tumbo
Makala hii inakwenda kukufundisha kuhusu matibabu ya vidonda vyatumbo. Pia utajifunza kwa nini kunakuwa na vidonda vya tumbo sugu. Soma Zaidi...

Mambo muhimu anayofanyiwa muislamu kabla ya kufa
Dhana ya faradh kwa muislamu (EDK form 2:dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

Dua za wakati wa shida na taabu
Hizi ni Dua ambazo unatakiwa uziombe wakati wa shida na taabu Soma Zaidi...