Home Afya Shule ICT Burudani Dini Maktaba Maswali Madrasa Apps Blog Legacy Login

UPENDO ULIOTAFSIRIWA KWA MICHORO


image


Posti hii inakwenda kukupa muendelezo wa hadithi ya aladini na taa ya ajabu


UPENDO ULIOTAFASIRIWA KWA MICHORO

Bint mfalme akamwambia mama akae kwenye kiti kilichopo pembeni kidogo na kitanda. Kilikuwa ni kiti kikubwa, kizuri kilichotandikwa magotoro yaliyotengenezwa kwa hariri. Kiti kilikuwa na minguu minne yote imetengenezwa kwa madini ya shaba nyekundu. Viigemeo vya kiti kwa kichwani vilitengenezwa kwa dhahabu na kutengeneza umbo zuri mithili ya uwa liliochanua. Vipande vilaini vya hariri vilifunika viegemeo hivyo. Kwa upande wa pembeni viegemeo vya kiti vilitengenezwa kwa vibao vilivyo kunywa vyema ka kuwekewa virungu vilivyotengenezwa kwa lulu. Kwa uzuri wa kiti hiki mama aladini alijisemea kuwa hata kiti cha mfalme hakifikii uzuri huu. Mama aladini aliendelea kufikiri uzuri wa chumba hiki wapi aladini atamuweka mtoto huwu aendane na hadhi yake.

 

Mama alikaa kwenye kiti na binti mfalme akakaa wenye kitanda. Ijapokuwa ndani kulikuwa na kajikiti kengine kadogo lakini binti huyu hakutaka kukaa kwenye kiti hiko. Hapo mama akapata muda wa kuanza kumthaminsha vyema mkwe wake mtarajiwa. Hakika binti sultani alikuwa ni mzuri. Hakuwa na kichogo, kichwa kilijawa a nywele zilizo shuka mpaka katikati ya mgongo. Wakiwa kwenye mazungumzo mama Aladini aligunduwa kuwa midomo ya binti mfalme imenona vyema, kama ametoka nywa subu ya kongoro. Mama Aladini aliendelea kumthaminisha zadi na kujiridhisha kuwa anafaha zaidi. Binti mfalme hakuwa na macho makubwa ila yalikuwa ni meupe yaliyoonekana vyema, nyusi zilizojipanga na kuchora umbo la mwezi mwandamo. Weusi wa nyusi ulizidi weusi wa nywele zake.

 

Zilisimama vyema kope zake, na kutengeneza sura iliyoonekana na umbo la duara kama yai la mbuni. Hakuwa na chunusi wala kipele. Binti sultani aligunduwa kuwa mkwe wake anamthaminisha, hapo akatabasamu kidogo. Binti sultani alikuwa anajikubali kuwa na yeye ni katika warembo, ukweli ni kuwa hakujuwa tu ila yeye ni namba moja. Tabasamu la binti mfalme lilimfanya mama aladini afurahi zaidi. Ukimmya ulitawala kwa kuda kidogo kisha binti mfalme akavuja ukimya na kumwambia mama Aladini “karibu sana mam, kuwa huru, nimekuwa nikiisubiri sana siku kama hii” mama aladini aliridhishwa zaidi na sauti ya mkwe wake. Hakuwa na mikwaruzo, wala ukakasi, ilitoka vyema na kutengeneza mawimbi mazuuri ya sauti yanayoweza kupennya kwene masikio na kuingia ndani yana ya sikio la ndani na kutengeneza maana ya kilichozungumzwa. “ahsante sana mwanangu, yaani nimefurahi sana, kukuona ukarimu wako, ila uzuri wa chumba hiki umenistaajabisha sana” ni maneno ya mama Aladini kuonyesha mshangao wake.

 

“ahasante sana mama, chumba hiki nilikipamba hivi huku nikiwa ninamkumbuka mwanao, kwani tulianza kukutana bwawani akiwa amevaa nguo iliy na rangi ya kijivu. Nilivutiwa na nguo yake lakini ndege wa ajabu alitoea mwenye rangi za kupendeza, ndege huyu alinituwa kichwani na kuelekea juu ya mti alipokuwa mwanao, niliamini kuwa ndege huyu hakuwa ni wa kawaida, ni ndege aliyetumwa kutuunganisha. Toka siku hiyo niliamini kuwa mume wangu si mwingine ila ni kijana yule. Sikuwa nimetambuwa jina lake wala wapi anaishi. Ila kwa uwezo wa mungu nikatambuwa baada ya yale yaliyotokea kati ya mimi na mtoto wa waziri. “

 

Binti mfalme akaendelea kusema “toka siku ile niliyokutana na mwanao nilianza kukibadili chumba hiki, na kukiweka katika hadthi inayofanana na thamani ya mwanao kwenye moyo wangu. Hata hivyo nahisi hata robo yake sikiweza kuifikia, ndipo nikaamuwa kutengeneza mdori kwa wenye sura ya mwanao nipate kumuona kila siku, kila saa kila wakati. Nilidiriki kutuma mashishushu waje kumchora mwanao bila yeye kugundua. Kama unavyoona mapazia, kitanda na kila unachokiona ni ishara ya upendo wangu kwa Aladini.” binti mfalme alizungumza maeno haya mpaka machozi yakaanza kumtoka. hakika nguvu ya mapenzi haina mfano, mama aladini alikuwa akizidi kushangaa kwa kila anachokion, sikia na shuhudia hapa ndani.

 

Bunti mfalme akaendelea kusema “baadaye nikagunduwa kuwa waziri ana njama ya kuniozesha mtoto wake, nililia sana ila machozi yangu hayakuweza kubadili maamuzi ya baba. Nikaamuwa kukipamba chumba hiki na kuweka picha ya ndege yule aliyetukutanisha ili iwe kumbukumbu ya moyo wangu. Amini ninachokwambia kuwa chumba hiki sikupata kumuingiza mtu yeyote ila ni wewe tu. Na huwa nikilala pindi ninapomkumbuka Aladini. Hata baba yangu hatambui uwepo wa chumba hiki katika ikulu hii” mama Aladini alithibitisha uwepo wa nguzu za giza la mapenzi kwa mtoto huyu. “sikui Aladini amemroga binti wa watu” ni aneno aliyojisemea mama Aladini huku akimkumbatia mkwewe na kumfuta machozi.

 

Wawili hawa waliendelea kuzungumza hata ukafika muda wa kuondoka. Mama Aladini aliondoka kwenye chumba na kurudi kwa mfalme ili kupata maelekezo nini kitafuata. Mfalme akamueleza kuwa mwambie mwanao ajinadae ijumaa ya wiki ijayo ndi harusi yao. Mama Aladini aliondoka kwa furaha, lakini kwa upande wa waziri hakukuwa hata na tone la furaha, ila majuto, hasira na ukatili ndio vilitawala zaidi. Mama Aladini lifika kwa mwanaye kipenzi na kumpatia habari za furaha. Aladini alifurahi sana. Pia mama Alimueleza kila alichokiona na kugundua yaliyokuwemo kwenye moyo wa binti mfalme. Aladini laifurahi zaidi. Aladini alimuahidi mama yake nitajenga ikulu nzui kuliko ikulu zote duniani, chumba kizuri kuliko nyumba vyote duniani.

Mama aladini alimuangalia mwanaye kwa macho ya ukali na mshangao. Aladini hujatembea popote, hiko chumba kizuri utakijuaje, ukweli ni kuwa Aladini alikusudia baadhi ya aliyoyaona kule kwenye pango yawepo kwenye ikulu yake na mengineyo. Hivyo mambp yakawa kama hivyo na Aladini akaanza kujenga ikulu lake kwa ajili ya mrembo binti mfalme.



Sponsored Posts


  ðŸ‘‰    1 Mafunzo ya html kwa kiswahili       ðŸ‘‰    2 Jifunze fiqh       ðŸ‘‰    3 Magonjwa na afya       ðŸ‘‰    4 Madrasa kiganjani       ðŸ‘‰    5 Maktaba ya vitabu       ðŸ‘‰    6 ICT    


Je! una maswali, mapendekezo ama maoni? tuma ujumbe wa meseji SMS hapo chini ili kuunganishwa na muhusika au bofya hapa

SMS SMS

Imeandikwa na Drsky Tags Burudani , simulizi , ALL , Tarehe 2021-11-08     Share On facebook or WhatsApp Topic school Zaidi Dini AFYA ICT Burudani Tags Uzazi maswali Afya mengineyo dini HIV Sira vyakula Matunda HTML php Alif Lela 1 Alif Lela 2 FANGASI Dawa SQL Tips Quran Sunnah fiqh DARSA Magonjwa Tajwid tawhid simulizi Dua Academy Wahenga chemshabongo WAJUWA Michezo ICT Imesomwa mara 1041



Post Nyingine


image Ujio wa wageni wa baraka
Posti hii inakwenda kukupa muendelezo kuhusu kifo cha mtoa burudani wa sultani Soma Zaidi...

image Kisiwa cha uokozi
Posti hii inakwenda kukupa muendelezo wa safari saba za Sinbad Soma Zaidi...

image Mafundisho kutokana na hadithi ya Binti mfalme
Posti hii inahusu zaidi mafundisho ambayo tunayapata kutoka kwa binti mfalme, tunapotoa hadithi sio kusoma na kufurahia tu ila kuna mafundisho muhimu katika maisha yetu. Soma Zaidi...

image Kwisha kwa chakula
Posti hii inakwenda kukuletea muendelezo wa safari za Sinbad Soma Zaidi...

image Utajiri wa baba na kifo chake
Posti hii inakwenda kukupa muendelezo kuhusu kifo cha mtoa burudani wa sultani Soma Zaidi...

image Mahusiano ya vijana wawili
Posti hii inahusu zaidi mahusiano yaliyotokea kati ya vijana wawili ila yanafika baadae mmoja akamsaliti mwenzake. Soma Zaidi...

image Mwendelezo wa hadithi ya vijana wawili
Posti hii inahusu zaidi hadithi ya vijana wawili ambapo mtihani unafika ila Jackie hakujiandaa alishutuliwa na marafiki zake baada ya kuona mwenendo wake haueleweki. Soma Zaidi...

image Hadithi iliyosimuliwa na tabibu
Posti hii inakwenda kukupa muendelezo kuhusu kifo cha mtoa burudani wa sultani Soma Zaidi...

image Malipo ya wema ni wema
Posti hii inakwenda kukuletea hadithi za alifu lela ulela Soma Zaidi...

image Hadithi ya binti mwenye kufichwa mtoto wa mfalme
Posti hii inakwenda kukuletea hadithi za alifu lela ulela Soma Zaidi...