Sababu ya kukatwa vidole gumba

Sababu ya kukatwa vidole gumba

KWA NINI VIDOLE GUMBA VILIKATWA?

Sababu ya kukatwa vidole gumba

KWA NINI VIDOLE GUMBA VILIKATWA?
Baada ya harusi niliendelea kukaa pale kwa muda wa miezi mitatu hata bila ya kurudi kwangu au kuwasiliana na ndugu zangu. Siku moja mkewangu akanieleza kuwa ana ujauzito. Nilifurahi sana, nilimkumbatia kwa furaha. Habari njema zikamfikia mke wa Sltani, basi akaandaa tafrija ndogo ya pale ndani kama kusherekea furaha ya mdogo wake kuata ujauzito. Katika tafrija hiyo muda wa kula ulipofika vyakula mbalimbali vikaletwa.



Nikanawa mikono na kuanza kula. Mkewangu hakuwepo alitokakidogo. Nilitamani hata awepo nipate kumlisha. Nilianza kula na kunywa kisha kikala Zerbajeh, nilipogusa tu chakula kile badhi ya wajakazi walikunja sura, Mke wa Sultani akanieleza kuwa mke wako anachukia sana harufu ya chakula hiko, na ndo umeshaanz akula, hivyo itakubidi uvumilie kwa lolote litakalo tokea. Sisi katu hatuta ingilia ugomvi wenu. Basi nilijitahidi kunawa vyema kwa sabuni. Baada ya tafrija kwisha nikarudi kujipumzisha.



Ghafla nikaona mkewangu amebadilika sura, na kuniambia “yaani mtu kama wewe unakula zerbajeh bila hata ya kunawa”? nikamueleza mkewangu kipenzi mbona nimenawa” kama umenawa na hii harufu ninayoipata ni ya nini” “ nimejitahidi kunawa ila hii harufu haikati kwa urahisi” haya ni maneno tuliokuwa tukijibizana.



Looo!!! Looo!!!! huwezi amini kumbe kubishana ndipo nikawa nauchochea moto wa kifuu. “nilikuona mstaarabu, nikakupenda, na nakupenda sana kipenzi, lakini kwa hili katu siwezi kuvumilia….,” mtu mstaarabu kama wewe unakula bila kunawa jamani, hapana …!! hapana…!!! kwa hili lazima nikupe adhabu, itabidi ukatwe vidole vyako. Ulivyokulia bila ya kunawa.



Aliagiza wajakazi wanifunge wanipeleke kwa hakinu ili nikakatwe vidole. Wakanifunga kamba na kunifungia kwenye chumba. Nilikaa kwa siku 10 kwenye kachumba hako huku nikawa ninakula mlo mmoja tu kwa siku. Siku ya kumi akawaambia wajakazi wanitoe, akaninusa mikono yangu na kujiridhisha kuwa harufu imekoka. Hapo akaagiza dawa ziletwe na mkasi, bendeji na vitu vingine. Akawaambia wajakazi wanikamate madhubuti, na hapo akanikata vidole gumba vyangu vyote



“nakukata hivi vidole vilivyokuacha ukala zerbajeh bila ya kunawa. Nataka ukumbuke kuwa chakula hiki, utakapokula unawe mara 40 kwa alita, mara 40 kwa sabuni na mara 50 kwa maji. Vinginevyo nitamaliza na vingine. Nilijiwazia mambo mengi hata nikasema huwenda ni huu ujauzit ndio unamsumbuwa. Lakini ujauzto ndi anikate vidole. Baada ya hapo alilia sana na akachukuwa dawa akanipaka na kuendelea kuniuguza.



Niligunduwa kuwa ananipenda sana, japo sikupatapo kujuwa hasa kilichomtokea hata akachukia sana chakula hiki. Milipanga siki moja nije nimuulize. Baada ya wiki kama 3 vidonda vyangu vilipona na hapo akaja mke wa sultani na aliponikuta akapiga tema makofi na kuniambia kuwa “umefaulu mtihani wa nne” sasampohuru kuondoka. Sikuwa naelewa maneno ya mke waSultani kuhusu mitihani ile lakini pia nilifurahi.



Jioni mke wangua akanipatia pesa nyingi na vipande vya dhahabu na kunieleza kuwa nikanunue nyumba nzuri ya ssi kuishi. Nilifanya hivyo, nilitafuta nyumba nzuri sana nje kidogo ya mji na sasa nina watoto wawili. Nimeamua leo kuja kufurahi na watu wa mjini ndipo nikakutana na shuhuli hii.



Baada ya huyu bwana kusimulia habari yake, basi mjakazi wa Sultani akamwambia Sultani, Je! Hadithi hii si yenye kushangaza kuliko hadithi ya mtoa burudani? Hapo sultani akasema “ni nzuri ila bado haijashinda hadithi ya mtoa burudani” kufikia hapo tabibu akapiga magoti na kusema “mtukufu Sultani, nitasimulia hadithi ya kushangaza zaidi kuliko mazungumzo yaliyo tangulia, kama utaikubali zaidi iwe kafara la tukio la leo. Hapo tatibu akaanza kusimulia hadithi yake





Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Kama unahitaji kuuliza maswali Bofya hapa

Mwandhishi Tarehe 2018-08-01     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 218


Download our Apps
👉1 Madrasa kiganjani     👉2 kitabu cha Simulizi     👉3 Kitau cha Fiqh     👉4 Kitabu cha Afya    

Post zifazofanana:-

Penzi la Mitihani
MTIHANI PENZINI Sikuwa na wasiwasi maana niliamini kuwa nitafanikiwa tu. Soma Zaidi...

Hadithi ya tabibu
HADITHI ILIYOSIMULIWA NA TABIBU: Tambua ewe Sultani mwadilifu kuwa mimi nimezaliwa katika familia ya wachamungu waabuduji wanaofata mila za kiyahudi. Soma Zaidi...

Siri ya kifo yafichuka
Posti hii inakwenda kukupa muendelezo wa hadithi za alifu lela ulela Soma Zaidi...

KIFO CHA AJABU
Download kitabu Hiki Bofya hapa KIFO CHA MTOA BURUDANI WA SULTAN. Soma Zaidi...

MUENDELEZO WA HADITHI YA MSHONA NGUO
Soma Zaidi...

Utajiri wa Baba na kifo chake
UTAJIRI WA BABA NA KIFO CHAKE. Soma Zaidi...

FAMILIA MPYA BAADA YA HARUSI
Soma Zaidi...

KIFO CHA MTOA BURUDANI WA MFALME
Hapo zamani katika mi wa Baghadani wakati wa utawala wa Sultani Harun Rashid alikuwepo kijana mmoja aliyekuwa karibu sana na Sultani kwa kuwa alikuwa akimpa burudani. Soma Zaidi...

Muendelezo wa hadithi ya mshona nguo
Posti hii inakwenda kukupa muendelezo kuhusu kifo cha mtoa burudani wa sultani Soma Zaidi...

HADITHI YA KAKA WA SITA WA KINYOZI
Soma Zaidi...

HARUSI YA ALADINI NA BINTI SULTANI
Soma Zaidi...

Ujio wa wageni wa baraka
Posti hii inakwenda kukupa muendelezo kuhusu kifo cha mtoa burudani wa sultani Soma Zaidi...