image

Hadithi Ya 29: Muabudu Allaah Na Usimshirikishe Na Chochote

Hadithi Ya 29: Muabudu Allaah Na Usimshirikishe Na Chochote

Hadithi Ya 29: Muabudu Allaah Na Usimshirikishe Na Chochote

الحديث التاسع والعشرون

"تعبد الله لا تشرك به شيئا"

عن معاذِ بن جبلٍ رضي الله عنه قال: قلت: يا رسول الله، أخْبِرني بِعَمَلٍ يُدْخِلُني الجنَةَ ويُبَاعِدُني عَنِ النارِ. قال: ((لَقَدْ سألْتَ عَنْ عَظيمٍ، وإنَهُ لَيَسيرٌ عَلى من يَسَّرَهُ اللهُ تعالى عَلَيْهِ : تَعْبُدُ اللهَ لا تُشْرِكُ بِهِ شَيئاً، وتُقيمُ الصَّلاةَ  ،وتُؤتي الزكاةَ، وتصومُ رمضانَ، وتَحُجُّ البيتَ)) .ثم قال:  (( ألا أَدُلُّكَ على أبْوَابِ الخيرِ؟: الصَّومُ جُنَّةٌ، والصَّدقةُ تُطْفِىءُ الخَطِيئةَ كما يُطْفىءُ الماءُ النارَ، وصَلاةَ الرَّجُلِ في جَوْفِ الَّليْلِ، ثم تلا: {تَتَجَافَى جُنُوبُهُمْ عَنْ الْمَضَاجِعِ} - حتى بلغ - {يَعْمَلُونَ}   السجدة: 16-17 .

ثم قال:  ((ألا أُخْبِرُكَ بِرَأسِ الأمْرِ وَعَمودِهِ وَذِرْوَةِ سَنَامِهِ؟)) قلتُ: بَلىَ يا رسول الله. قال:  (( رَأْسُ الأمْرِ الإسلامُ، وعَمُودُهُ الصَّلاةُ، وَذِرْوَةُ سَنَامِهِ الجِهادُ )).

ثم قال: (( ألا أخْبِرُكَ بِمِلاكَ ذَلِكَ  كلِّهِ ؟)) فَقُلْتُ بَلَى يا رَسول الله، فأخَذَ بِلِسانِهِ وقال:   ((كُفَّ عَلَيْكَ هذا)) . قلت : يا نبيَّ الله، وإنَّا لمؤاخَذُونَ بِما نَتَكَلَّمُ بِه ؟)) فقال: (( ثَكِلَتْكَ أمُّكَ يَا مُعَاذُ,  وَهَلْ يَكُبُّ الناسَ في النارِ على وُجُوهِهِمْ ))   أو قال: ((على مناخِرِهِم - إلاَّ حَصَائدُ  ألسِنَتهم))

 

رَوَاهُ التِّرْمِذِيُّ   وَقَالَ: حَدِيثٌ حَسَنٌ صَحِيحٌ. 

 


HADITHI YA  29 MUABUDU ALLAAH  NA USIMSHIRIKISHE NA CHOCHOTE

 

Kutoka kwa  Mu'aadh Ibn Jabal رضي الله عنه  amesema:

Nilisema: Ewe Mtume صلى الله عليه وسلم  , niambie kitendo ambacho kitanipeleka peponi na kitaniokoa na moto.  Akasema : Umeniuliza jambo kubwa lakini ni rahisi kwa yule ambae Mola anaemsahilishia.   Muabudu Allaah wala usimshirikishe na chochote, Swali, toa Zaka, funga             Ramadhani, nenda kuhiji (Makka).  Kisha akasema:  Je? Nikuonyeshe  milango ya kheri?  Saumu ni ngao, sadaka inazima dhambi kama vile maji yanavyozima moto, na kuswali katikati ya usiku: Kisha akasoma  {Mbavu zao zinaachana na vitanda kwa kumwomba Mola wao Mlezi kwa khofu na kutumaini, na hutoa kutokana na tulivyo waruzuku. Nafsi yoyote haijui waliyo fichiwa katika hayo yanayo furahisha macho - ni malipo ya yale waliyo kuwa wakiyatenda}

 Sura As-Sajda  32: 16 na 17

Tena akasema:  Je, nikwambie kilele cha hilo jambo; nguzo yake na sehemu yake ya juu kabisa?  Nikasema : Ndio ewe Mjumbe wa Mwenyeezi Mungu.  Akasema:  kilele chake ni Uislamu, nguzo yake ni Swala na sehemu yake ya juu kabisa ni Jihaad.   Kisha akasema : Je, nikwambie muhimili wa yote haya?  Nikasema:  Ndio ewe Mjumbe  wa Mwenyeezi Mungu.   Akaukamata ulimi wake na akasema;  Uzuie huu.  Nilisema: Ewe Mjumbe wa Mwenyeezi Mungu; yale tunayoyasema tutahukumiwa  kwayo? Akasema:  mama yako akuhurumie ewe Mu'aadh!  Kuna kitu zaidi kinachowaangusha watu kifudifudi motoni kama si mavuno ya ndimi zao?

Imesimuliwa na At-Tirmidhi na ni hadithi Hasan.



                   





           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Topic: Sunnah Main: Post File: Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 497


Sponsored links
👉1 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)     👉2 kitabu cha Simulizi     👉3 Kitau cha Fiqh     👉4 Madrasa kiganjani     👉5 Kitabu cha Afya     👉6 Simulizi za Hadithi Audio    

Post zifazofanana:-

Dua za kuwaombea wazazi
Kwenye Quran kuna duaambazo Allah ametufundisha tuziombe kwa ajili ya wazazi, familia na kwa ajili yetu wenyewe. Soma Zaidi...

KUKUSANYIKA KATIKA DUA
KUKUSANYIKA KATIKA DUA. Soma Zaidi...

Hadithi ya pili: sifa za muumini wa kweli
Sunnah na hadithi (EDK form 3: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

HALI AMBAZO MTU AKIOMBA DUA HUJIBIWA
HALI AMBAZO MTU AKIOMBA DUA ITAJIBIWA. Soma Zaidi...

DUA 120
Soma Zaidi...

Hadithi Ya 30: Allaah Amefaridhisha Mambo Ya Dini Tusiyapuuze
Soma Zaidi...

MAANA YA HADITHI SUNNAH
Maana ya SunnahKilugha: Neno sunnah katika lugha ya Kiarabu lina maana ya mwenendo au mila. Soma Zaidi...

darasa la dua
Soma Zaidi...

Hadithi Ya 31: Upe Ulimwengu Kisogo Allaah Atakupenda
Soma Zaidi...

Hadithi Ya 29: Muabudu Allaah Na Usimshirikishe Na Chochote
Soma Zaidi...

DUA YA 1 - 10
1. Soma Zaidi...

DUA 61 - 84
61. Soma Zaidi...