Karibia fangasi wote hawa wanatibika bila ya ugumu wowote maka mgonjwa atakamilisha dozi. Zipo dawa za kupaka kama losheni, dawa za kunywa za vidonge. Pia zipo dawa za kupewa kwa njia ya sindano. Muone sasa daktari kama una tatizo, kwa hakika utapona kwa msaada wa Mwenyezi Mungu.
Dozi hizi pia zinaweza kuchukuwa muda mpaka miezi mitatu kulingana na ukubwa wa tatizo. Hata ukijihisi umepona hakikisha unamaliza dozi. Hakikisha pia unajiweka katika afya njema muda wowote na usafi wamavazi, malazi na mwili.