Dua sehemu 03

Zijuwe njia ambazo Allah hujibu Dua yako. Tambua kama umejibiwa dua yako au bodo, soma darsa za dua hapa.

Dua sehemu 03

KUKUSANYIKA KATIKA DUA.
Ni jambo la kupendeza kuomba dua mkiwa kwenye kundi. Zipo dua ambazo siku zote zinaombwa watu wakikusanyika kama dua ya kuomba mvua. Kukusanyika kwenye dua ni sunnah katika sunnah zingine. Ijulikane kuwa pindi mtu akiomba dua kisha wengine wakaitikia aamiin huenda katika waloitikia akawepo walii wa Allah ambae ikawa sababu ya dua kujibiwa. Pia watu waliokuwepo kwenye kundi aombe mmoja na wengine waitikie aamiin na wanyanyue mikono yao.

Maswahaba Allah awaridhie walikiwa wakiombeana dua na walikuwa pia wakikusanyika kayika kuomba dua. Mtume ุตู„ู‘ูŠ ุงู„ู„ู‡ ุนู„ูŠู‡ ูˆุณู„ู‘ู… alikuwa pia akiwahimiza maswahaba wake kuwa katika kundi wanapoomba dua na wengine waitikie aamiin. Amesimulia Habiib Ibn Salamah ุฑุถู‰ุงู„ู„ู‡ ุนู†ู‡ kuwa mtume ุตู„ู‘ูŠ ุงู„ู„ู‡ ุนู„ูŠู‡ ูˆุณู„ู‘ู… amesema โ€œhalikusanyiki kundi la watu na wakaomba dua wengine na wengine wakaitikia โ€˜aamiinโ€™ isipokuwa Allah ataijibu dua hiyoโ€. (amepokea tbrany, Bayhaqy na Alhaakim).

NAMNA AMBAYO ALLAH HUJIBU DUA.
Itambulike kuwa dua ambayo imefata vigezo na masharti ya dua itajibiwa tu. Ila pia itambulike kuwa dua hujibiwa katika njia kuu tatu ambazo ni kupewa alichoomba, kufutiwa madhambi au kulipwa siku ya qiama kwa kuingizwa peponi. Hivyo itambuluke kuwa mtu anaweza kuomba dua kisha asijibiwe huenda Allah anataka kumpa kheri zaidi au huenda ameshamjibu kwa kumfutia madhambi yake. Allah ndiye anaejua lile ambalo ni bora kwa wajawake katika wakati wowote ule.

Amesimulia Abuuhurairah ุฑุถู‰ุงู„ู„ู‡ ุนู†ู‡ kuwa Mtume ุตู„ู‘ูŠ ุงู„ู„ู‡ ุนู„ูŠู‡ ูˆุณู„ู‘ู… amesema ู…ูŽุง ู…ูู†ู’ ุฃูŽุญูŽุฏู ูŠูŽุฏู’ุนููˆ ุจูุฏูุนูŽุงุกู ุฅูู„ุงู‘ูŽ ุขุชูŽุงู‡ู ุงู„ู„ู‘ูŽู‡ู ู…ูŽุง ุณูŽุฃูŽู„ูŽ ุฃูŽูˆู’ ูƒูŽูู‘ูŽ ุนูŽู†ู’ู‡ู ู…ูู†ูŽ ุงู„ุณู‘ููˆุกู ู…ูุซู’ู„ูŽู‡ู ู…ูŽุง ู„ูŽู…ู’ ูŠูŽุฏู’ุนู ุจูุฅูุซู’ู…ู ุฃูŽูˆู’ ู‚ูŽุทููŠุนูŽุฉู ุฑูŽุญูู…ู โ€"โ€ โ€œ โ€œmtu yeyote anaeomba dua ila atajibiwa ima awahishiwe kujibiwa haphapa duniani, au acheleweshewe (kujibiwa hapa duniani na badala yake ) ajibiwe akhera au asamehewe madhambi yake kwa kiasi kile alichoomba, maadam hajaomba (jambo la) madhambi au kukata udugu aua hajafanya haraka ya kutaka kujibiwa hata akawa anasema โ€˜nimemuomba Mola wangu na hakunijibuโ€™โ€. (amepokea tirmidh).

DUA YA KAFIRI NA DUA YA MUUMINI.
Itambulike pia kuwa Allah huenda akacheewa kujibu dua ya mja wake si kwa sababu hataki ni kwa sababu anapenda kusikia sauti na maneno ya mja wake pindi anapoomba. Na hii ni kwa sababu Allah anapenda kuombwa. Pia wakati mwingine mtu anaweza kuomba dua na akajibiwa hapohapo au kwa haraka bila ya kujali awe muislamu ama sio muislamu. Hutokea kuwa Allah akawa hapendi sauti na maombi ya kafiri hivyo akaijibu dua ile ili amnyamazize mdomo wake. Jambo la msingi ni kuwa Allah anapompenda mja anapenda pia kumsikiliza anayoyasema na anachokiomba. Na anapomchukia mja huwa hapendi hata kumuona akiomba hivyo humjibu ili anyamaze.

Amesimulia Jabir ุฑุถู‰ุงู„ู„ู‡ ุนู†ู‡ kuwa mtume ุตู„ู‘ูŠ ุงู„ู„ู‡ ุนู„ูŠู‡ ูˆุณู„ู‘ู… amesema โ€œhakika (Malaika) Jibril ndiye aliyepewa kazi ya kutekeleza haja za wanaadamu, basi pindi mja kafiri anapoomba dua Allah husema kumwambia Jibril โ€˜ewe Jibril mpe haja yake kwani mimi sipendi kusikia dua yake. Na pindi anapoomba dua Mja muumini Allah humwambia Jibril โ€˜ewe Jibril izuie haja yake (usimjibu dua yake) kwani mimi napenda kusikia dua yakeโ€™โ€. )amepokea Ibn Najar).



        

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Sunnah Main: Dini File: Download PDF Views 1242

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
๐Ÿ‘‰1 kitabu cha Simulizi    ๐Ÿ‘‰2 Bongolite - Game zone - Play free game    ๐Ÿ‘‰3 Madrasa kiganjani    ๐Ÿ‘‰4 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    ๐Ÿ‘‰5 Kitabu cha Afya    ๐Ÿ‘‰6 Simulizi za Hadithi Audio   

Post zinazofanana:

DUA 85 - 93

SWALA YA MTUME 85.

Soma Zaidi...
Al-Arbauwn An-Nawawiyyah hadithi ya 6: ubainifu wa halali na haramu

Post hii inakwenda kukupa tahadhari juu ya mambo ya halali na mambo ya haramu.

Soma Zaidi...
DUA na Adhkar kutoka kwenye quran

hii ni orodha ya dua mbalimbali kutoka kwenye quran. Unaweza kuzitumia dua hizi kujipendekeza kwa Allah na kupata msamaha, neema na mengineyo.

Soma Zaidi...
MAANA NA FADHILA ZA DUA

DUA Kwa ufupi dua ni kumuomba Allah akuondoshee lililobaya, ama linalo kuudhi ama akupe jambo fulani.

Soma Zaidi...
Maana ya Hadith al Quds na Hadith an-Nabawiy

Katika somo hili utakwenda kujifunza maana ya hadithi al Quds na Hadith an-Nabawiy

Soma Zaidi...
DUA ZA WAKATI WA SHIDA

DUA ZA WAKATI WA SHIDA 1.

Soma Zaidi...
Wajbu wa wazazi kwa watoto wao

Wajibu wa Wazazi kwa Watoto Wazazi wanawajibu kwa watoto wao.

Soma Zaidi...
Uislamu ni Nasaha (kunasihiana) kwa Mwenyezi Mungu, Kitabu chake Mtume wake , Viongozi na waislamu wote

ุนูŽู†ู’ ุฃูŽุจููŠ ุฑูู‚ูŽูŠูŽู‘ุฉูŽ ุชูŽู…ููŠู…ู ุจู’ู†ู ุฃูŽูˆู’ุณู ุงู„ุฏูŽู‘ุงุฑููŠูู‘ ุฑูŽุถููŠูŽ ุงู„ู„ู‡ู ุนูŽู†ู’ู‡ู ุฃูŽู†ูŽู‘ ุงู„ู†ูŽู‘ุจููŠูŽู‘ ุตู„ู‰ ุงู„ู„ู‡ ุนู„ูŠู‡ ูˆุณู„ู… ู‚ูŽุงู„ูŽ: "ุงู„ุฏูู‘ูŠู†ู ุงู„ู†ูŽู‘ุตู?...

Soma Zaidi...