CSS - somo la 2: Jinsi ya ku weka code za css kwenye HTML
katika somo hili utajifunza jinsi ya ku install css kwenye ukurasa wa html
Utangulizi
Css ni kifupisho cha maneno cascading style sheet. Hii ni moja katika lugha za kompyuta ambazo hutumika katika kuboresha mtindo kwenye ukurasa wa wavuti. Hutumika kwenye HTML na XML. css ni style sheet angauage, hata hivyo haipo pekee kwenye kundi hili. Lugha nyingine za style ni kama:
- JavaScript Style Sheets (JSSS)
- Formatting Output Specification Instance (FOSI)
- Syntactically Awesome Style Sheets (Sass)
- Less (Less)
- Stylus
- SMIL Timesheets
- Document Style Semantics and Specification Language (DSSSL)
- Extensible Stylesheet Language (XSL)
Css ilianzishwa miaka ya 1990 na kuendelea. Historia a css imeanza punde tu baada ya tovuti ya kwnza kuchapishwa na watu wakaanza kutengeneza tovuti mbalimbali. Hivyo ikaonekana kunahitajika kuwepo na ubireshwaji wa muonekano.
Mwaka 1994 ndipo css ilianzishwa rasmi na Håkon Wium Lie na Bert Bos. Kutokea hapo css iliweza kukuw kwa kasi. Na kuanza kupata u maarufu. Mpaka sasa tupo toleo la 4 la css.
Kama nilivyotangulua kusema kuwa css hutumiaka kwenye HTML na xml katika course hii tutakwenda kujifunza kutumia css kwenye html. Tutajifunza kutumia style sheet kwneye xml kwenye course ya xml.
JINSI YA KU INSTALL CSS
Hakuna uhitaji wa ku install css ili uweze kuitumia kama zilivyo lugha nyingne. Unachotakiwa kufanya ni kuitumia moja kwa moja kwenye ukurasa wako wa wavuti kwenye html. Kuna njia kadhaa ambazo hutumika katika kutumia css kwenye faili la HTML. Njia hizo ni kama:-
- In line css: Hapa tuna andika css ndani ya mstari katika faili la html.
- Internal css Hapa tutatumia css ndani ya faili la html.
- External css Hapa tunaandika css kwenye faili lingine kisha tuna iunganisha moja kwa moja
- Kwa kutumia javascript Katika njia hii tunanaitumia css kenye code za javascript.
Katika course hii tutakwenda kutumia njia hizo tatu za kwanza. Njia ya nne tutatjifunza kwenye course ya javascript level 1 na level 2.
In line css
Njia hii utakuwa na uzoefu nayo kwani tumesha itumia mara kadhaa kwenye course yetu ya html level 1 na level 2. Njia hii ni ile ya kutumia tag za css kwenye fali la html. Tag yenye we ni ile ya <style>. Kwa kutumia tag hii ndani ya html itakuwezesha kuweza kuandika code za css na zikaweza kufanya kazi.
Katika inline css tutaandika css ndani ya tag ya html kw akuanza na neno style likifatiwa na attribute zake. Tutakwenda kutumia code hizi kwenye mfano huu:-
<html>
<head>
<title>Bongoclass</title>
</head>
<body>
<p>Karibu bongoclass</p>
</body>
</html>
Mfano 1:
Tunataka kubadili nano karibu bongoclass kuwa na rangi ya buluu. Tutafanya hivi kwa kutumia in line css. Unachotakiwa kufanya ni kuweka style ndani ya tag ya <p>, ikifuatiwa na alama ya = kisha utaweka hizo attribute za css kwenye alama za kunukuu (“).
Uandishi wa attribute utakuwa hivi, kwanza utaweka jina la property likifuatiliwa na nukta pacha (:) ama colon, Kisha utaandika value. Mfano ikitaka rangi iwe ya buluu utaweka style="color:blue" katika mfano huo hapo neno color ndio property na neno blue ndio value.
Hivyo tag ya html <p>itasomeka hivi <p style ="color:blue">Karibu bongoclass</p>
Pia unaweza kuweka style zaidi ya Moja kwenye inline css. Kufanya hivyo utatenganisha style Moja na nyingine kwa kutumia alama ya semicolon yaani (;).
Mfano 2:
Katika mfano wetu huu tunataka kufanya maadhishi yawe makubwa kwa asilimia 200%. Kufanya hivi tutatumia property ya font-size kwa kuwa tunayo property ya color basi tutatenganisha kwa sem...
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 Tafasiri ya Riyadh Swalihina 👉2 Kitau cha Fiqh 👉3 kitabu cha Simulizi 👉4 Bongolite - Game zone - Play free game 👉5 web hosting 👉6 Dua za Mitume na Manabii
Post zinazofanana:
CSS - somo la 5: Njia tano zinazotumika kuweka rangi kwenye css
Katika somo hili utajifunza aina tano za kuweka rangi kw akutumia css
Soma Zaidi...CSS - SOMO LA 31: CSS Filters (blur, brightness, contrast.)
Katika somo hili tutajifunza kuhusu CSS Filters — mitindo inayotumika kuhariri mwonekano wa picha, video, au elementi nyingine kwa kuongeza athari kama blur, brightness, contrast, grayscale, na nyinginezo. Hii huifanya tovuti kuwa ya kisasa, ya kuvutia, na yenye mwingiliano mzuri.
Soma Zaidi...CSS - SOMO LA 9: Margin na Padding
Katika somo hili utajifunza tofauti kati ya margin na padding, kazi ya kila moja, jinsi ya kuzipima, na jinsi zinavyotumika kudhibiti nafasi ndani na nje ya elementi kwenye ukurasa wa HTML.
Soma Zaidi...CSS - SOMO LA 7: Kutumia Fonti (Fonts) kwenye CSS
Katika somo hili utajifunza jinsi ya kudhibiti mwonekano wa maandishi kwa kutumia fonti kwenye CSS. Utajifunza jinsi ya kubadilisha aina ya fonti, ukubwa, mtindo, unene, na mpangilio wa maandishi ili yaweze kuonekana kwa mvuto na usomaji bora.
Soma Zaidi...CSS - SOMO LA 12: Width, Height, Max/Min Width na Overflow
Katika somo hili, utajifunza jinsi ya kudhibiti upana (width) na urefu (height) wa elementi katika CSS. Pia utaelewa tofauti kati ya max-width, min-width, na jinsi overflow inavyodhibiti tabia ya content inayoizidi element.
Soma Zaidi...CSS - SOMO LA 23: Uelewa Zaidi wa CSS Animation na Transition
Somo hili linakuletea ufahamu wa kina juu ya CSS Transitions na Animations, likifafanua vipengele vyake muhimu, matumizi, na namna ya kutumia properties mbalimbali za animation kwa ufanisi katika kurahisisha muonekano na mtumiaji wa tovuti.
Soma Zaidi...