Katika somo hili, utajifunza kuhusu pseudo-classes kama :hover, :first-child, na :last-child, pamoja na pseudo-elements kama ::before, ::after, na ::selection. Hizi husaidia kubadili au kuongeza mitindo maalum kulingana na hali ya elementi au sehemu maalum ya elementi.
Pseudo-classes na pseudo-elements ni sehemu muhimu ya CSS ambazo hukuwezesha kubadilisha mwonekano wa elementi kulingana na hali fulani au kuongeza content ya ziada bila kubadilisha HTML. Ni zana muhimu sana kwenye ubunifu wa kipekee na mwingiliano bora wa mtumiaji.
:hoverInatumika kubadilisha style ya element unapoelekezewa pointer ya mouse.
button:hover {
background-color: green;
color: white;
}
💡 Inafaa sana kwa vitufe (buttons), links, na menyu.
:first-childHuchagua elementi ya kwanza ndani ya mzazi wake.
p:first-child {
font-weight: bold;
}
:last-childHuchagua elementi ya mwisho ndani ya mzazi wake.
li:last-child {
color: red;
}
::beforeHuchomeka content kabla ya element kuonekana.
p::before {
content: "👉 ";
}
::afterHuchomeka content baada ya element.
p::after {
content: " ✅";
}
💡 Zinafaa sana kwa kuongeza icons au alama bila kubadilisha HTML.
::selectionHubadilisha mwonekano wa maandishi yanapochaguliwa (highlighted).
::selection {
background: yellow;
color: black;
}
<p>Hii ni paragraph ya mfano.</p>
p:hover {
color: blue;
}
p:first-child {
text-transform: uppercase;
}
p::before {
content: "💡 ";
}
p::after {
content: " 📘";
}
Pseudo-classes na pseudo-elements huongeza nguvu ya CSS bila kuingilia HTML. Zinaruhusu kufanya mabadiliko ya hali (state), kuchagua elementi maalum, na kuongeza content ya ziada kwa ubunifu. Ni nyenzo muhimu sana kwenye urembo na usability ya tovuti.
Tutajifunza jinsi ya kuleta miondoko (motion) kwa kutumia transition, transform, na animation kwenye CSS.
:hover hutumika lini?
a) Wakati wa kubonyeza tu
b) Wakati element inaonekana tu
c) Wakati pointer ya mouse iko juu ya element
d) Wakati element iko mwisho wa HTML
::before hufanya nini?
a) Kubadilisha background ya element
b) Kuongeza content kabla ya element
c) Kuficha element
d) Kuweka margin mpya
Ili kuchagua element ya mwisho ndani ya mzazi, utatumia:
a) :hover
b) :nth-child(1)
c) :last-child
d) ::after
::selection hutumika wapi?
a) Kwenye picha pekee
b) Kubadilisha style ya content inayo-highlightiwa
c) Kubadilisha background tu
d) Kuweka icon
Kipi kati ya vifuatavyo ni pseudo-class?
a) ::after
b) :hover
c) ::selection
d) ::before
Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu
Umeionaje Makala hii.. ?
Katika somo hili, tutajifunza kipengele kipya kinachoitwa if() function ndani ya CSS, kilichoanza kupatikana kwenye toleo la Chrome 137. Kipengele hiki kinaturuhusu kuandika mantiki ya masharti moja kwa moja kwenye property ya CSS, bila kutumia JavaScript wala media query zilizotawanyika. Tutajifunza pia aina za queries: media(), supports(), na style() pamoja na matumizi yao ya kivitendo kwenye tovuti. Mwisho, tutaeleza kwa kina kuhusu pointer na any-pointer.
Soma Zaidi...Katika somo hili utajifunza kuhusu property muhimu ya CSS inayoitwa display, ambayo huamua jinsi element inavyoonyeshwa kwenye ukurasa. Tutachambua aina kuu za display: block, inline, inline-block, na none.
Soma Zaidi...Katika somo hili, tutajifunza kuhusu CSS Specificity — yaani mfumo wa kipaumbele unaotumiwa na kivinjari kuchagua ni mtindo (style) upi utumike iwapo kuna migongano kati ya selectors mbalimbali. Utaelewa jinsi ya kupanga selectors zako vizuri ili kuzuia matatizo ya mitindo kutofanya kazi kama ulivyotarajia.
Soma Zaidi...Katika somo hili tutajifunza kuhusu z-index, ambayo hutumika kudhibiti ni elementi ipi ionekane juu au chini wakati kuna elementi nyingi zinazofunika sehemu moja. Pia tutajifunza kuhusu stacking context, yaani jinsi vivinjari vinavyopanga
Soma Zaidi...Katika somo hili tutajifunza kwa kina kuhusu CSS Shorthand Properties — ni nini, jinsi zinavyofanya kazi, faida zake, na mifano mbalimbali ya kutumia shorthand kuandika CSS kwa njia fupi na bora zaidi.
Soma Zaidi...Katika somo hili, utajifunza jinsi ya kutumia media queries kwa ajili ya kutengeneza tovuti zinazojibadilisha kulingana na ukubwa wa skrini. Tutazungumzia @media rules, breakpoints, na dhana ya mobile-first design.
Soma Zaidi...Katika somo hili, tutajifunza kuhusu CSS functions muhimu zinazotumika kufanya mahesabu, kuweka vipimo vya kisasa vinavyobadilika kulingana na hali ya kifaa, na kutumia variables. Tutazingatia functions kama: calc(), clamp(), var(), min(), max(), na mwishoni tutajifunza jinsi ya kutengeneza custom function kwa kutumia variables.
Soma Zaidi...Katika somo hili, tutajifunza kuhusu @import — amri inayotumika kuingiza faili moja la CSS ndani ya jingine. Tutaona namna ya kuitumia, faida zake, hasara zake, na tofauti kati yake na njia mbadala ya <link> ndani ya HTML.
Soma Zaidi...Katika somo hili utakwenda kujifunza maana ya CSS, pia nitakujulisha kazi zake. Mwisho utatambuwa historia ya CSS toka kuanzishwa.
Soma Zaidi...Katika somo hili, tutajifunza kuhusu CSS Variables, au Custom Properties. Utajifunza jinsi ya kuunda, kuitumia, na faida za kutumia variables katika CSS ili kuweka msimamizi mzuri wa rangi, ukubwa, na mitindo mingine ya kurudia-rudia.
Soma Zaidi...