Katika somo hili utakwenda kujifunza sheria za uandish wa css yaani syntax za css
Sheria za uandishi wa css yaani syntax za css.
Css ni moja katika lugha za ki kompyuta (computer language) ambayo ina sheria zilizo rahisi sana na ni chache. Ukishazijuwa hizo basi mabo yote yatakuwa sawa.
Sheria za kuandka css zimezama kwenye mambo makuu mawili tu ambayo ni selector na declaration. Yaani code zote za css unaweza kuzigawa kwenye sehemu kuu hizi mbili ambazo ni selector na declaration.
Selectors: hii ni sehemu ambayo yenyewe inahusisha element za html. Yaani hapa ndipo tunakwenda kujuwa je hizo code za css zinahud element gani. Mfano ukisema
haloo
katika code hizi selector ni
ambapo inaonesha kuwa tuna target paragraph.
Declaration: hii ni sehemu ambayo inakwenda kuweka code za css. Declaration yenyewe imegawanyika katika sehemu kuu mbili ambazo ni property na value. Kwa mfano katika mfano niliotoa hapo juu declaration ni color:yellow ambapo tunapata color ni property na yellow ni value.
Kwa ufupi selector ina kuwa na tag husika ya html na declaration inakuwa na protery pamoja na value. Declaration inakuwa kwenye mabano ya {} kama utatumia internal css ama external css.
Selector inaweza kuwa zaidi ya moja na declaration pia inawezakuwa zaidi ya moja. Jambo la kuzingatia nikiwa unapotumia selector zaidi ya Moja utatakiwa kuzitenganisha kwa alama ya koma (,). Na unapotumia declation zaidi ya Moja utatenganisha kwa kutumia semicolon (;). Angalia mfano hapo chini
p, h1, u, i, b{
color:blue;
font-size:200%;
background: red;
}
Katika code hizi selectors ni p, h1, u, i na b hizi zinatarget tag za html. Tag hizo ni <p>, <h1>, <u>, <i> na <b>. Kwa pamoja element hizo zote zitafuata style hiyo popote zitakapotumiwa.<">...
Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu
Umeionaje Makala hii.. ?
Katika somo hili, tutajifunza kuhusu CSS functions muhimu zinazotumika kufanya mahesabu, kuweka vipimo vya kisasa vinavyobadilika kulingana na hali ya kifaa, na kutumia variables. Tutazingatia functions kama: calc(), clamp(), var(), min(), max(), na mwishoni tutajifunza jinsi ya kutengeneza custom function kwa kutumia variables.
Soma Zaidi...Katika somo hili utajifunza kuhusu property ya position katika CSS, ambayo hutumika kuamua jinsi element inavyowekwa ndani ya ukurasa. Tutajifunza aina tano kuu za position: static, relative, absolute, fixed, na sticky.
Soma Zaidi...Katika somo hili tutajifunza kuhusu z-index, ambayo hutumika kudhibiti ni elementi ipi ionekane juu au chini wakati kuna elementi nyingi zinazofunika sehemu moja. Pia tutajifunza kuhusu stacking context, yaani jinsi vivinjari vinavyopanga
Soma Zaidi...Katika somo hili tutajifunza kuhusu CSS frameworks mbalimbali zinazosaidia kuharakisha uundaji wa mitindo kwenye tovuti. Tutazungumzia frameworks maarufu kama W3.CSS, Bootstrap, Google Fonts, na nyinginezo, faida, matumizi, na tofauti zao.
Soma Zaidi...Katika somo hili, utajifunza jinsi ya kudhibiti upana (width) na urefu (height) wa elementi katika CSS. Pia utaelewa tofauti kati ya max-width, min-width, na jinsi overflow inavyodhibiti tabia ya content inayoizidi element.
Soma Zaidi...Katika somo hili utakwenda kujifunza maana ya CSS, pia nitakujulisha kazi zake. Mwisho utatambuwa historia ya CSS toka kuanzishwa.
Soma Zaidi...Katika somo hili, tutajifunza kuhusu @import — amri inayotumika kuingiza faili moja la CSS ndani ya jingine. Tutaona namna ya kuitumia, faida zake, hasara zake, na tofauti kati yake na njia mbadala ya <link> ndani ya HTML.
Soma Zaidi...Katika somo hili utajifunza tofauti kati ya margin na padding, kazi ya kila moja, jinsi ya kuzipima, na jinsi zinavyotumika kudhibiti nafasi ndani na nje ya elementi kwenye ukurasa wa HTML.
Soma Zaidi...Katika somo hili uatkwenda kujifunza aina za css selectors
Soma Zaidi...Katika somo hili, utajifunza jinsi ya kudhibiti mipaka (borders) ya vipengele kwa kutumia CSS. Tutajifunza namna ya kuweka unene wa border, rangi, aina ya mstari, na pia jinsi ya kutumia border kwa upande mmoja tu.
Soma Zaidi...