CSS - somo la 3: syntax za css yaani sheria za uandishi wa css
Katika somo hili utakwenda kujifunza sheria za uandish wa css yaani syntax za css
Sheria za uandishi wa css yaani syntax za css.
Css ni moja katika lugha za ki kompyuta (computer language) ambayo ina sheria zilizo rahisi sana na ni chache. Ukishazijuwa hizo basi mabo yote yatakuwa sawa.
Sheria za kuandka css zimezama kwenye mambo makuu mawili tu ambayo ni selector na declaration. Yaani code zote za css unaweza kuzigawa kwenye sehemu kuu hizi mbili ambazo ni selector na declaration.
Selectors: hii ni sehemu ambayo yenyewe inahusisha element za html. Yaani hapa ndipo tunakwenda kujuwa je hizo code za css zinahud element gani. Mfano ukisema
haloo
katika code hizi selector ni
ambapo inaonesha kuwa tuna target paragraph.
Declaration: hii ni sehemu ambayo inakwenda kuweka code za css. Declaration yenyewe imegawanyika katika sehemu kuu mbili ambazo ni property na value. Kwa mfano katika mfano niliotoa hapo juu declaration ni color:yellow ambapo tunapata color ni property na yellow ni value.
Kwa ufupi selector ina kuwa na tag husika ya html na declaration inakuwa na protery pamoja na value. Declaration inakuwa kwenye mabano ya {} kama utatumia internal css ama external css.

Selector inaweza kuwa zaidi ya moja na declaration pia inawezakuwa zaidi ya moja. Jambo la kuzingatia nikiwa unapotumia selector zaidi ya Moja utatakiwa kuzitenganisha kwa alama ya koma (,). Na unapotumia declation zaidi ya Moja utatenganisha kwa kutumia semicolon (;). Angalia mfano hapo chini
p, h1, u, i, b{
color:blue;
font-size:200%;
background: red;
}
Katika code hizi selectors ni p, h1, u, i na b hizi zinatarget tag za html. Tag hizo ni <p>, <h1>, <u>, <i> na <b>. Kwa pamoja element hizo zote zitafuata style hiyo popote zitakapotumiwa.
Pia hapo kuna declaration tatu ambazo ni color:blue yenye property color na value blue, font-size:100% yenye property font-size na value 100%, na ya mwisho ni background-color:red yenye property background-color na value red.
Baada ya kutambuwa...
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 ai web app 👉2 Kitau cha Fiqh 👉3 Tafasiri ya Riyadh Swalihina 👉4 Dua za Mitume na Manabii 👉5 Madrasa kiganjani 👉6 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)
Post zinazofanana:
CSS - SOMO LA 16: Flexbox Basics
Katika somo hili, utajifunza msingi wa mfumo wa Flexbox unaotumika kupanga elementi kwa usahihi ndani ya kontena. Utajifunza kuhusu display: flex;, pamoja na properties muhimu kama justify-content, align-items, flex-direction, na gap.
Soma Zaidi...CSS - somo la 4: Aina za css selecto
Katika somo hili uatkwenda kujifunza aina za css selectors
Soma Zaidi...CSS - SOMO LA 17: Flexbox Advanced
Katika somo hili, utajifunza vipengele vya juu zaidi vya Flexbox: flex-wrap, flex-grow, flex-shrink, na flex-basis. Pia tutajifunza jinsi ya kujenga muundo wa safu (rows) na nguzo (columns) kwa kutumia Flexbox layout.
Soma Zaidi...CSS - SOMO LA 18: Grid Layout
Katika somo hili, utajifunza misingi ya CSS Grid Layout, mfumo wenye nguvu wa kupanga vipengele katika safu (rows) na nguzo (columns). Tutachambua display: grid, pamoja na grid-template-columns, grid-template-rows, gap, grid-column, na grid-row.
Soma Zaidi...CSS - SOMO LA 28: CSS Timing Functions
Katika somo hili tutajifunza kuhusu CSS Timing Functions, ambazo hutumika kudhibiti kasi na mtiririko wa transition na animation. Utaelewa tofauti kati ya ease, linear, ease-in, ease-out, ease-in-out, pamoja na jinsi ya kutumia cubic-bezier() kwa kudhibiti mwendo wa mabadiliko kwenye elementi.
Soma Zaidi...CSS - SOMO LA 22: CSS Transition na Animation
Katika somo hili, tutajifunza jinsi ya kuleta miondoko na harakati kwenye tovuti kwa kutumia CSS Transitions na Animations. Hii itasaidia kuboresha muonekano na matumizi ya tovuti.
Soma Zaidi...