CSS - somo la 3: syntax za css yaani sheria za uandishi wa css
Katika somo hili utakwenda kujifunza sheria za uandish wa css yaani syntax za css
Sheria za uandishi wa css yaani syntax za css.
Css ni moja katika lugha za ki kompyuta (computer language) ambayo ina sheria zilizo rahisi sana na ni chache. Ukishazijuwa hizo basi mabo yote yatakuwa sawa.
Sheria za kuandka css zimezama kwenye mambo makuu mawili tu ambayo ni selector na declaration. Yaani code zote za css unaweza kuzigawa kwenye sehemu kuu hizi mbili ambazo ni selector na declaration.
Selectors: hii ni sehemu ambayo yenyewe inahusisha element za html. Yaani hapa ndipo tunakwenda kujuwa je hizo code za css zinahud element gani. Mfano ukisema
haloo
katika code hizi selector ni
ambapo inaonesha kuwa tuna target paragraph.
Declaration: hii ni sehemu ambayo inakwenda kuweka code za css. Declaration yenyewe imegawanyika katika sehemu kuu mbili ambazo ni property na value. Kwa mfano katika mfano niliotoa hapo juu declaration ni color:yellow ambapo tunapata color ni property na yellow ni value.
Kwa ufupi selector ina kuwa na tag husika ya html na declaration inakuwa na protery pamoja na value. Declaration inakuwa kwenye mabano ya {} kama utatumia internal css ama external css.

Selector inaweza kuwa zaidi ya moja na declaration pia inawezakuwa zaidi ya moja. Jambo la kuzingatia nikiwa unapotumia selector zaidi ya Moja utatakiwa kuzitenganisha kwa alama ya koma (,). Na unapotumia declation zaidi ya Moja utatenganisha kwa kutumia semicolon (;). Angalia mfano hapo chini
p, h1, u, i, b{
color:blue;
font-size:200%;
background: red;
}
Katika code hizi selectors ni p, h1, u, i na b hizi zinatarget tag za html. Tag hizo ni <p>, <h1>, <u>, <i> na <b>. Kwa pamoja element hizo zote zitafuata style hiyo popote zitakapotumiwa.
Pia hapo kuna declaration tatu ambazo ni color:blue yenye property color na value blue, font-size:100% yenye property font-size na value 100%, na ya mwisho ni background-color:red yenye property background-color na value red.
Baada ya kutambuwa...
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w) 👉2 ai web app 👉3 Simulizi za Hadithi Audio 👉4 Madrasa kiganjani 👉5 Kitau cha Fiqh 👉6 web hosting
Post zinazofanana:
Drone: Nyuki Dume na Majukumu Yake
Simulizi hii inaelezea maisha ya nyuki dume, zinazojulikana kama drone. Inafafanua majukumu yao, maisha yao ya kila siku ndani ya kiwanda cha nyuki, na hatima yao baada ya kufanikisha kuzaliana na kifalme cha nyuki. Simulizi pia inaangazia tofauti zao na nyuki wa kike, na umuhimu wao katika uzazi wa kifalme.
Soma Zaidi...CSS - SOMO LA 24: CSS Variables (Custom Properties)
Katika somo hili, tutajifunza kuhusu CSS Variables, au Custom Properties. Utajifunza jinsi ya kuunda, kuitumia, na faida za kutumia variables katika CSS ili kuweka msimamizi mzuri wa rangi, ukubwa, na mitindo mingine ya kurudia-rudia.
Soma Zaidi...CSS - SOMO LA 13: Display Property
Katika somo hili utajifunza kuhusu property muhimu ya CSS inayoitwa display, ambayo huamua jinsi element inavyoonyeshwa kwenye ukurasa. Tutachambua aina kuu za display: block, inline, inline-block, na none.
Soma Zaidi...CSS - SOMO LA 20: Media Queries na Responsive Design
Katika somo hili, utajifunza jinsi ya kutumia media queries kwa ajili ya kutengeneza tovuti zinazojibadilisha kulingana na ukubwa wa skrini. Tutazungumzia @media rules, breakpoints, na dhana ya mobile-first design.
Soma Zaidi...Jinsi ya kumsaidia Mtoto mdogo aliyekabwa na kitu kooni
Mfano wa kitu kinachoweza kumaba mtoto kooni ni kama chagula kigumu, pesa ya sarafu, kijiwe na mengineyo. Endapo hili litataokea msaada wa haraka unahitajika kwa ulazima.
Soma Zaidi...CSS - SOMO LA 15: Float na Clear katika CSS
Katika somo hili utajifunza jinsi ya kutumia float ili kupanga elementi upande wa kushoto (left) au kulia (right). Pia utajifunza jinsi ya kutumia clear kuondoa athari za float na kuhakikisha layout yako inabaki thabiti.
Soma Zaidi...