Katika somo hili utakwenda kujifunza sheria za uandish wa css yaani syntax za css
Sheria za uandishi wa css yaani syntax za css.
Css ni moja katika lugha za ki kompyuta (computer language) ambayo ina sheria zilizo rahisi sana na ni chache. Ukishazijuwa hizo basi mabo yote yatakuwa sawa.
Sheria za kuandka css zimezama kwenye mambo makuu mawili tu ambayo ni selector na declaration. Yaani code zote za css unaweza kuzigawa kwenye sehemu kuu hizi mbili ambazo ni selector na declaration.
Selectors: hii ni sehemu ambayo yenyewe inahusisha element za html. Yaani hapa ndipo tunakwenda kujuwa je hizo code za css zinahud element gani. Mfano ukisema
haloo
katika code hizi selector ni
ambapo inaonesha kuwa tuna target paragraph.
Declaration: hii ni sehemu ambayo inakwenda kuweka code za css. Declaration yenyewe imegawanyika katika sehemu kuu mbili ambazo ni property na value. Kwa mfano katika mfano niliotoa hapo juu declaration ni color:yellow ambapo tunapata color ni property na yellow ni value.
Kwa ufupi selector ina kuwa na tag husika ya html na declaration inakuwa na protery pamoja na value. Declaration inakuwa kwenye mabano ya {} kama utatumia internal css ama external css.
Selector inaweza kuwa zaidi ya moja na declaration pia inawezakuwa zaidi ya moja. Jambo la kuzingatia nikiwa unapotumia selector zaidi ya Moja utatakiwa kuzitenganisha kwa alama ya koma (,). Na unapotumia declation zaidi ya Moja utatenganisha kwa kutumia semicolon (;). Angalia mfano hapo chini
p, h1, u, i, b{
color:blue;
font-size:200%;
background: red;
}
Katika code hizi selectors ni p, h1, u, i na b hizi zinatarget tag za html. Tag hizo ni <p>, <h1>, <u>, <i> na <b>. Kwa pamoja element hizo zote zitafuata style hiyo popote zitakapotumiwa.<">...
Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu
Umeionaje Makala hii.. ?
Katika somo hili, utajifunza kuhusu pseudo-classes kama :hover, :first-child, na :last-child, pamoja na pseudo-elements kama ::before, ::after, na ::selection. Hizi husaidia kubadili au kuongeza mitindo maalum kulingana na hali ya elementi au sehemu maalum ya elementi.
Soma Zaidi...Katika somo hili utajifunza kuhusu property muhimu ya CSS inayoitwa display, ambayo huamua jinsi element inavyoonyeshwa kwenye ukurasa. Tutachambua aina kuu za display: block, inline, inline-block, na none.
Soma Zaidi...Katika somo hili utakwenda kujifunza maana ya CSS, pia nitakujulisha kazi zake. Mwisho utatambuwa historia ya CSS toka kuanzishwa.
Soma Zaidi...Katika somo hili tutajifunza kuhusu z-index, ambayo hutumika kudhibiti ni elementi ipi ionekane juu au chini wakati kuna elementi nyingi zinazofunika sehemu moja. Pia tutajifunza kuhusu stacking context, yaani jinsi vivinjari vinavyopanga
Soma Zaidi...Katika somo hili tutajifunza kuhusu CSS frameworks mbalimbali zinazosaidia kuharakisha uundaji wa mitindo kwenye tovuti. Tutazungumzia frameworks maarufu kama W3.CSS, Bootstrap, Google Fonts, na nyinginezo, faida, matumizi, na tofauti zao.
Soma Zaidi...Katika somo hili utajifunza aina tano za kuweka rangi kw akutumia css
Soma Zaidi...Somo hili linakuletea ufahamu wa kina juu ya CSS Transitions na Animations, likifafanua vipengele vyake muhimu, matumizi, na namna ya kutumia properties mbalimbali za animation kwa ufanisi katika kurahisisha muonekano na mtumiaji wa tovuti.
Soma Zaidi...Katika somo hili utajifunza jinsi ya kudhibiti mwonekano wa maandishi kwa kutumia fonti kwenye CSS. Utajifunza jinsi ya kubadilisha aina ya fonti, ukubwa, mtindo, unene, na mpangilio wa maandishi ili yaweze kuonekana kwa mvuto na usomaji bora.
Soma Zaidi...Katika somo hili, utajifunza vipengele vya juu zaidi vya Flexbox: flex-wrap, flex-grow, flex-shrink, na flex-basis. Pia tutajifunza jinsi ya kujenga muundo wa safu (rows) na nguzo (columns) kwa kutumia Flexbox layout.
Soma Zaidi...Katika somo hili, utajifunza jinsi ya kudhibiti muonekano wa sehemu ya nyuma (background) ya HTML element kwa kutumia CSS. Utaweza kuongeza rangi, picha, kuweka picha zisirudiwarudiwe, na hata kusogeza picha kwenye maeneo tofauti ya ukurasa.
Soma Zaidi...