Menu



Simulizi za Hadithi EP 6 Part 17: Siri ya wageni yafichuka

Muendelezo........

SIRI YA WAGENI WALE INAFICHUKA

Tambua ewe kijana changu, mimi na baba yako tulikutana zamani sana. Tulikuwa ni marafiki sana tukiwa katika umri wa miaka 7 mapka 18. baba yako alikuwa ni mchamungu toka alipokuwa mdogo. Alipata malezi mema sana. Na mimi nilivutiwa nikawa nirafiki yangu sana. Tulikuwa tukifanya ibada pamoja na karibia mambo yetu yote. Wakati nilipohama Misri kuja Yemeni niliweka ahadi na baba yako kuwa nikipata mtoto wa kike ataolewa na mtoto wake na akiwa wa kiume atauoa wako, na tulimuomba Mungu atutofaitishie watoto wetu, yaani akiwa wangu wakike wake wa kiume ama wake wa kike wangu awe wa kiume.

 

 

 

Miaka mingi ilipita hata tukasahau ahadi zetu. Mimi nilichelewa kupata mtoto na hata yeye. Hata hivi miaka yapata 17 iliyopita nikajiwa na wageni wa ajabu, kisha akataja kisha kama kile kilichomtokea baba. Kisha akaenelea kusema. Wageni wale walikuwa si watu wa kawaida. Ni wajumbe waliotumwa kuja kutukumbusha ahadi zetu na kutupatia habari njema za kaupa watoto. Siku ya mwisho walipoondoka wageni wale walinieleza kuwa mtoto wako atao;ewa na mtoto wa rafiki yako kaam ahadi. Atakuja mwenyewe, na utamjuaje wakaniachia pete hii iliyokufikia. Walinieleza kuwa pete hii ikifika mikononi mwako katu haitaondoka.

 

 

 

Wakanieleza kuwa sifa zako utakuwa ni muuza viatu. Hivyo binti yangu anayemsaidia kazi mke wangu nilimuagiza aje kwako kuuliza viatu kama walivyonieleza wageni wale sifa za viatu. Nikamueleza kama utamuona mtu aliyebadilika utambue huyo ni mtu ninaye mtafuta. Mwambie aje kwangu. Sasa nilikuwa na ugomvi na matajiri wenzangu waliotaka kumuoa binti yangu, niliwakatalia sana, na ndipo wakapanga njama ya mumuua.

 

 

 

Bila ya kutambua wakamuua yule mfanyakazi wangu wakidhani ndiye binti yangu. Baada ya tukio lile kutokea na pete kupotea bikajua kuwa pete imesafika kwa mwenyewe, maana wageni wale walinieleza katu ete isingeweza kuibiwa, ila itamfikia mwenyewe. Baada ya kumaliza kuzungumza akaniambia kuwa nisiendelee tena kuwatafuta wageni wale katu sitawaona. Akamuita binti wake nije nimuone.

 

 

 

Akaja binti mmoja akafunua sura yake. Nilihisi kama nimepigwa shoti kwenye mwili wangu. Ghafla joto likapanda, nilistaajabu kabisha kuona kuwa kumbe duniani kuana mabinti warembo kiasi kile. Nilijisemea kuwa wale waliotaka kumuoa hawakukosea katu. Kwa kweli binti alikuwa ni mzuri sana. Kisha mzee akasema “mwanangu nitakuozesha binti yangu bure ila kwa sharti kuwa uwe ni kama mwanangu”

 

 

 

Nilikubali na ndipo nikaozeshwa. Nilimuoa mke wangu nikiwa sina mkono mmoja. Bada ya harusi niliishi na mke wangu kwa muda wa miaka 5. kumbe kulikuwa na watu wananifanyia uaduni. Na ndipo wakanifanyia uchawi nikapata jini hili lililokuwa likinisumbua. Tulipata sifa zako ndipo tukaja Baghadad kupata matibabu. Ha hii ndio hadithi ya kukatwa mkono wangu.

 

 

 

Baada ya tabibu kusimulia hadithi hii akamuelekea Sulatani na kumuuliza “Je! Sultani hadithi hii haiwezi kuwa nzito kama kifo cha mtoa burudani?” mfalme akajibu angalau ila bado. Kama haitahadithiwa hadithi nyingine iatakayoshinda hii, wote mtapoteza vichwa vyenu. Basi hapo Mshona nguo akaja mbele na kusema “ Mtukufu nitasimulia kisa kilichomtokea huyu marehemu jana,kitakuwa ni cha kushangaza zaidi kuliko hadithi za wenzangu waliotangulia kusimulia. Akaanza kusimulia kama ifuatavyo:-

 

 

 

Download app yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiw ana App yetu. Bofya liln hapo chini kuweza ku download

Download Now Bongoclass

           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Mankaa image Tarehe 2024-09-10 14:17:31 Topic: Simulizi za Hadithi Main: Masomo File: Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Views 154


Sponsored links
👉1 Simulizi za Hadithi Audio     👉2 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)     👉3 Kitau cha Fiqh     👉4 kitabu cha Simulizi     👉5 Madrasa kiganjani     👉6 Kitabu cha Afya    

Post zifazofanana:-

Simulizi za Hadithi EP 9 Part : Taharuki kwa mfalme
Muendelezo..... Soma Zaidi...

Simulizi za Hadithi EP 6 Part 21: Kinyozi mwenyewe
Muendelezo.... Soma Zaidi...

Simulizi za Hadithi EP 7 Part 7: Upendo uliotafsiriwa
Muendelezo.... Soma Zaidi...

Simulizi za Hadithi EP 6 Part 20: Kinyozi maishani mwangu
Muendelezo..... Soma Zaidi...

Simulizi za Hadithi EP 8 Part 2: Siri ya kifo
Simulizi hii pia inapatikana kwenye kitabu cha pili cha hadithi za HALIF LELA U LELA... Soma Zaidi...

Simulizi za Hadithi EP 6 Part 19: Kinyozi
Hii ni simulizi iliyopo ndani ya kitabi cha pili cha hadithi za HALIF LELA U LELA..... Soma Zaidi...

Simulizi za Hadithi EP 3 Part 1: Kisa cha mvuvi na jini
Simulizii hii inapatikana katika kitabu cha kwanza cha HALIF LELA U LELA .... Soma Zaidi...

Simulizi za Hadithi EP 6 Part 14: Wageni
Simulizii hii ni nzuri na ni mojawapo ya hadithi za HALIF LELA U LELA kitabu cha pili...... Soma Zaidi...

Simulizi za Hadithi EP 6 Part 2: Sultani mtoa buradani kufariki
Hadithi za HALIF LELA U LELA kitabu cha pili..... Soma Zaidi...

Simulizi za Hadithi EP 5 Part 5: Bonde la uokozi
Hadithi za HALIF LELA U LELA kitabu cha kwanza....... Soma Zaidi...