image

Simulizi za Hadithi EP 4  Part 13: Simulizi ya nyani kibadilika kuwa chongo

Mwendelezo wa hadithi zetu nzuri na za kusisimua kutoka katika kitabu cha kwanza cha hadithi za HALIF LELA U LELA.....

KUTOKA NYANI MPAKA KUWA CHONGO.

 

Katika hali ya unyani nikajiambia “kama nikiishi msituni kwa hakika italiwa na chui bora niende kwa binadamu huenda nikapata muokoaji”. mwazo yangu yakawahivyo nikashuka pale na kuelekea ufukweni. Nikakuta kunajahazi linakaribia kuondoka. Basi niktafuta mti na kuutumia kama mtumbwi na kielekea kwenye jahazi.

 

Watu walishangaa sana kuona nyani anaweza kutumia nyenzo kuweza kuvuka. Wakaanza kukusanyika ili kuona akina ya nyani walioendelea kiasi hiki. Walikuwepo wengine wananipigia makofi na wengine wakawa wananicheka na wengine wananozonea. Mimi sikujali mpaka nikakamata jahazi na kukaa pembeni. Walikuwepo watu walotaka kunirudisha majini na wengune hata wakadiriki kunipiga mawae. Kwa bahati njewa nahodha wa jahazi akawakataza ni kuahidi kunilinda kwa maajabu niloonesha.

 

Haukupita muda ghafla jahazi letu likavamiwa na kundi kubwa la watu walooneka na ni waheshimiwa wenye madaraka ya juu serikalini. Mkubwa wao akajitambulisha “sisi ni watu wa baraza la mtukufu muheshimiwa mfalme. Karani muandishi wa mfalme amefariki mwezi ulopita hivyo tunatafuta mtu mwenye muandiko mzuri ili achukuwe nafasi” basi wakagawa makaratasi kwa kila mtu aandike chochote kwenye karatsi.

 

Basi walipomaliza na mimi nikaashiria nipewe karatasi ya kuandika. Basi nahodha akanipatia karatasi na kaamu na nikakaa mkao wa 4 na kushika kalamu vizuri kisomi. Watu wote walishangaa sana kuona nyani mwenye ujuzi wa hali yajuu hii. Basi niliandika mashairi machache ya kumsifu mfalme na kumjazia sifa kemkem. Kisha nikawapatia karatasi. Kwa hakika walishangaa sana kuona nyani ana ujusi wa namna hii.

 

Basi walichukuwa makaratasi yao na kuondoka, huko mfalme aliziangalia karatasi na kuupenda mwandiko wangu. Palepale aliamuru uletwe usafiri uje kunibeba. Nilibebwa kiheshimiwa zaidi na kuekwa mbele ya mfalme. Nilitowa heshima kinyaninyani na mfalme akaelewa. Alimipa karatasi niandike nikaandika tena mashairi ya kumpamba zaidi ya yale ya mwanzo. Kwakweli alistaajabu na kufurahi pia. Mfalme alikuwa anapenda sana kucheza bao. Hivyo aliashiria liletwe bao.

 

Basi nikacheza mechi na mfalme. Kwa mara ya kwanza nilimfunga nikaona amekasirika. Hivyo nikamwachia kanifunga goli tatu na kulipisha zote. Mwisho mfalme akaamrisha kiletwe chakula asi kikaletwa na sikula kinyaninyani nilinawa mikono na kula kwa kutumia mikono yangu. Yote nilokuwa nikiyafanya yalikuwa yakimstaajabisha mfalme na watu wa baraza lake.

 

Ilipofika jioni mfalme akaagiza aletwe binti yake wa kipekee ili astaajabu uwepo wa nyani mbele ya macho ya mfalme. Kama zilivyo tamaduni za waislamu mtoto wa kike hujifunika mwili wake ila kwa ndugu zake wa karibu na wazazi wake. Kwakuwa aliitwa na baba yake alukuja kawaida hat bila ya kujifunika. Ila maratu alipoingia kwa baba yake alihaza na kurudi nyuma na kwenye kujifunika kisha akarudi. Mfalme alishangaa kilichomsibu hata mwamnae akarudi.

 

Binti akaeleza “baba unaniita mbele ya mwanaume mwingine nikiwa sijajifunika” pale mfalme alishangaa na kumwambia “nipo mimi tu hapa na huyu nyani, ametoka wapi huyo mwanaume mwingie?”. akajibu “baba huyo sionyani ni mtu na amegeuzwa kuwa nyani kiuchawi. Ni aina za uchawi wanaotumia majini” basi mimi kusikia maneno yale nilitingisha kichwa kuashiria kukubaliana na maneno ya binti. Mafalme akamwambia “umeyajuwa vipi haya mwanangu?” binti akajibu “yule bib I aliyekuwa akinilea alinifundisha aina nyingi za uchawi na kuopoa”.

 

Basi mfalme akamtaka binti yake aniopoe na binti akakubali. Siku ilofata asubuhi sisi watatu tulielekea kwenye jumba bovu lililohamwa zamani am,bapo binti amelelewa na huyo bibi. Binti akatuambua mimi na mfalme kukaa pale na tusiondoke kwa loote lile litalotokea. Hivyo binti akaanza kuzungumza maneno yasiyojulukana. Ghafla akatokea nge na binti akageuka kenge akawa anamkimbiza nge amle. Yule nge akageuka tandu na binti akageuka nyoka.

 

Basi ikawa hivyo kila mmoja akigeuka flani mwinzie anageuka kitu kingine. Hali ilikuwa hivyo mpaka yule nge akageuka kunguru basi binti akageuka kipanga wakapaa wakikimbizaa na tusiwaone walipokwenda. Tulikaa pale kwa muda mrefu na tusiwaone. Ghafla tukaona punda aliyefundia kitu anakuja na akatema punje za komamanga. Kisha akageuka kuwa kuku mtembe na uanza kula punje za komamanga. Alizila zote alizoziona akawa anaashiria kama kuna ingine.

 

Kumbe kulikuwa na punje moja imebaki iliyokuwa ikibingiria kulekea kwenye mfereji wa maji. Aliiwahi aikamate lakini akachelewa na ikaangukia kwenye maji, na palepale ikageuka kuwa samaki. Binti akageuka kuwa samaki mkubwa zaidi na wakakimbizana mpaka yule samamki akageuka kuwa dragon na kuanza kumwaga moto. Binti akageuka kuwa dragoni na kutukinga sisi na motoule. Kwa bahati mbaya moto uke ulumchoma binti kwenye miyo na chehe ikajanipata kwenye jicho na kulipasua na hiyo ikawa ndio sababu ya chongo yangu ya jicho la kulia.

 

Baada ya mapamabno makali binti alifanikiwa kulichoma jini lile na kuliuwa. Alianguka chini na kuanza kuhe,a kwa uchovu. Alipopata nguvu akachukuwa majivu ya lieldragoni la kijini na kuchanganya na maji. Akatamka maneno na kunumwagia na palepale nikageuka kuwa mtu kamili. Furaha ilitanda kwa mfalme ila ghafla binti aliikata furaha hii kwa kumwambia “baba nimefanikiwa kumuuwa jini na kumtibu kijana, ila na mimi umri wangu umebakia siku tatau tu. Ule moto uliniunguza kweye moyo”.

 

Siku tatu binti alifariki dunia na majonzi yalienea kwa mfalme kwani alikuwa na mtoto mmoja tu. Baa da ya situ saba mfalme aliniita na kunambia “upo huru kwa sasa maana sio nyani tena. Nimefanikiwa kukuokoa lakini nimepoteza maisha ya binti yangu. Hivyo siwezi kukuangalia. Ninakuomba uondoke nchini hapa na usirudi tena, kwani uwepo wako utaendelea kunikumbusha binti yangu.

 

Basi nikaamua kuondoka nchini pale na nisijuwe pa kwenda. Nikaeekea baghdadi na nikanyoa kichwa cahngu na nyusi zangu. Nilipofika hapa nikakutana na wenzangu hawa na hatukupata kujuwa hadithi ya kila mmoja kati yetu. Hivyo hii ndio hadithi yangu. Zubeidah akamfuata waziri na kumwambia ataje stori yake yeye na wenzie basi akaeleza kuwa wao ni wafanya biashara wameomba hifadha pale baada ya kuingiliwa na usiku.

 

Basi mpaka wanamaliza kusimulia hadithi zao ilikuwa ni majogoo hivyo Zubeydah akwaaruhusu watu wote watoke mule ndani. Bila hata kuomba waruhusiwe kukaa mule mpaka asubuhi walitoka mbiombio. Mfalme aliyejifanya mfanya biashara akamwambia waziri “wachukuwe chongo hawa watatu na ukalale nao nyubani kwako na ifikapo asubuhi niitie wale wanawake watatu wote waje kwenye baraza letu nao wataje hadithi zao. Inaonekana kuna makubwa yamewafika.

 

Basi mambo yakawa kama alivyotaka mfalme, kesho asubuhi wale wadada wakaletwa mbele ya mfalme na mfale akawaambia “hatukuwaita kwa kuwaadhibu kwa mlichotufanyia jana ila tunataka mtueleze na nyinyi haithi zenu hata mkayafanya yale mlikuwa mkiyafanya. Zubeydah aliposikia sauti ile akajua niwale watu wa jana kumbe ni mfalme na watu wake. Basi akapiga magoti na wenzake wakafata na akaanza kuomba msamaha “tusamehe ewe mtukufu mfalme, kwa hakika hatukujuwa kuwa ni wewe mfalme, tumekukosea sana hata tukaweza panga kwenye shingo yako” mfalme akamjibu “nimekwisha samehe tafadhali aeni bila wasi na mueleze hadithi zenu.

 

Mfalme akawa anawashawishi kwa maneno mazuri na kuwaambia “nioneni kama mpo na rafiki zenu hapa na kuwa huru kusema chochote kile”. basi mabinti wakaanza kuangaliana wakitafakari ni nani aanze kusimulia hadithi yake. Kabla hawajaanza na wale machongo watatu wakaletwa ili wapate kusikiliza hadithi za wadada hawa. Basi wakaanza kusimulia hadithi zao kama ifuatavyo;-





           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Mankaa Tarehe 2024-09-10 08:58:20 Topic: Simulizi za Hadithi Main: Masomo File: Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 51


Sponsored links
👉1 Simulizi za Hadithi Audio     👉2 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)     👉3 Madrasa kiganjani     👉4 Kitau cha Fiqh     👉5 Kitabu cha Afya     👉6 kitabu cha Simulizi    

Post zifazofanana:-

Simulizi za Hadithi EP 4 Part 2: Kisa cha kinyozi msiri..
Karibuni tuendelee kusimuliana stori za HALIF LELA U LELA kitabu cha kwanza, stori nzuri sana na za kuvutia zimeandaliwa kwaajili ya kujifunza na kujiburudisha pia..... Soma Zaidi...

Simulizi za Hadithi EP 4 Part 16: Usaliti
Hadithi za HALIF LELA U LELA zipo nyingi sana na zinavutia na zinasomwa na kusikilizwa kwa wakubwa na wadogo na hii simulizi inatoka kwenye kitabu cha kwanza cha hadithi za HALIF LELA U LELA...... Soma Zaidi...

Simulizi za Hadithi EP 4 Part 1: Hadithi ya chongo watatu, watoto wa mfalme na wanawake wa Baghdad.
Skmulizii hii pia imetoka kitabu cha kwanza cha HALIF LELA U LELA kitabu cha kwanza Soma Zaidi...

Simulizi za Hadithi EP 7 Part 7: Upendo uliotafsiriwa
Muendelezo.... Soma Zaidi...

Simulizi za Hadithi EP 6 Part 4: Kilema mtanashati asiye na mkono
Muendelezo wa hadithi za HALIF LELA U LELA kitabu cha pili..... Soma Zaidi...

Simulizi za Hadithi EP 3 Part 6: Simulizi ya samaki wa rangi nne
Simulizi za HALIF LELA U LELA zipo nyingi na zinasisimua.. kisa hiki cha samaku wa rangi nne kipo katika kitabu cha kwanza Soma Zaidi...

Simulizi za Hadithi EP 6 Part 11: Vidole gumba vilikatwa
Kitabu cha pili cha hadithi za HALIF LELA U LELA kina simulizi nyingi nzuri na za kusisimua, muendelezo.... Soma Zaidi...

Simulizi za Hadithi EP 5 Part 2: Sehemu ya safari ya kwanza ya sinbad
Muendelezo wa stori ya safari ya Sinbad ambayo ipo kwenye kitabu cha kwanza cha hadithi za HALIF LELA U LELA.... Soma Zaidi...

Simulizi za Hadithi EP 10 Part 7: Taharuki
Muendelezo..... Soma Zaidi...

Simulizi za Hadithi EP 9 Part : Bostani la kifalme baghadad
Muendelezo..... Soma Zaidi...

Simulizi za Hadithi EP 4 Part 17: Hadithi ya Malipo ya wema ni wema
Mwendelezo wa hadithi za HALIF LELA U LELA kitabu cha kwanza..... Soma Zaidi...

Simulizi za Hadithi EP 3 Part 5: Simulizi ya samaki wa ajabu
Simulizii hii inapatikana kwenye hadhithi za HALIF LELA U LELA katika kitabu cha kwanza.... Soma Zaidi...