Binti wa ndotoni


image


Posti hii inakwenda kukupa muendelezo wa safari saba za Sinbad


BINTI WA NDOTONI.

Baada ya kufikiri kwa kina na kumuomba mungu nilipitiwa na usingizi. Niliwa usingizini nikaota ndoto ya ajabu sana. Nilipokuja kuamka niliona watu ndo wanaanza kujaa msikitini lakini mfalme bado hajafika. Nikaanza kujiuliza maana na tafasiri ya ndoto ile ya ajabu. Nikiwa katika hali ya mawazo nilikuwa nikikumbuka machache kuhusu tafasiri za ndoto. Nikaanza kuichambua ndoto yangu nilioora. Nikiwa kwenye mawazo hayo nikaona kama kuna mtu amekuja na kuniuliza kuhusu ndoto yangu ili anitafasirie.

 

Nimeota nipo safarini na binti mfalme akiwa kwenye safari ile. Tukiwa tupo kwenye jahazi kwa ghafla tulipatwa na ajali. Mule kwenye jahazi lile hakuna mtu ninayemjua asipokuwa ni binti mfalme tu. Katika ajali ile jino lanhu moja liling’oka na nikatumbukia ndani ya maji. Binti mfalme akaja na kamba na kunirushia nikaikamata kamba ile na kufika kwenye mbao kubwa ambayo binti mfalme alikuwemo. Kwa bahati mbaya bint mfalme aliteleza kwenye mbao ile na kuingia kwenye maji, niliwa sijui uogelea nilijitahidi kumuokoa bila mafanikio na akaniashiria kuwa niondoke niendezangu. Baada ya hapo nikashituka

 

Katika hali kama hiyo yule mtu akanieleza kuwa ndoto ile ni ya ukweli na kunajambo ninaelezwa kwenye ndoto ile. Yule mtu akaanza kunieleza maana ya ndoto ile. “kuhusu kuwa safarini wewe na bint mfalme ni ishara ya kushirikiana. Na kuhusu kupata ajali inamaanisha kuwa katika kushirikiana kwenu mtapatwa na matatizo lakini yeye ndiye atakayekuokoa.

 

Na kwakuwa kwenye ndoto ni wewe ndiye uliyeokolewa inamaana wewe katika matatizo yako utapata njia kupitia kushirikiana nae. Na kuhusu yeye kushindwa kuokolewa na wewe na hatimaye akaishia majini inaonesha atapatwa na matatizo na atafariki bila ya wewe kufanikiwa kumuokoa. Ama jino linamaanisha kituchako cha karibi kama mke na ndugu. Hivyo jino lako lile linaonesha ni bint mfale atakuwa mkeo na kung’oka kwa jino ni ishara ya kufariki kwa mkeo. Hii ndiyo tafariri ya ndoto yako”

 

Baada ya hpo yule mtu akatoweka, nilipokuja kupaa fahamu kutoka kwenye mawazo yale sikumuona yeyote. Nikutaka kutafuta zaidi nikaweka imani kuwa huenda ni malaika ametumwa kunisaidia kufasiri ndoto yangu. Basi nikaamuwa kumuoa bint mfalme kutokana na ndoto ile inaonesha yeye ataanza kufa na mimi nitaokoka. Hivyo nikaamini hii ni mipango ya mungu. Basi baada ya swala nikaende kwa mfalme na kumueleza kuwa nimekubai ombi lake.

 

Nilipokuwa nazungumza na mfalme kumbe yele binti alikuwa akisikiliza mazungumzo yale na aliposikia nimekubali alipata furaha kubwa iliyopelekea akazimia. Tulishangaa kusikia kishindo nyuma ya mlango na kuenda kuangalia alikuwa ni binti mfalme aliyezimia pale chini. Moyowangu uliruka sana nikawa najiuliza ndo qadar zimeanza yaani atakufa kweli hapahapa na kuniacha mimi. Aliitwa muuguzi na kuanza kumpa tiba. Nilirudi nyumbani nikiwa nasikilizia kama atakufa au atapona maana akifa nitazikwa hatakama shererhe ya ndoa haijafanyika.

 

Nikiwa na wasiwasi siku ilofata nilielekea kwa mfalme kwenda kujulia hali ya binti yake. Nilishangaa kuona mfalme akiwa na bashasha punde tu aliponiona “mwanangu, mwenzio amepata fahamu tayari na mama yenu anaandaa maandalizi ili wiki ijayo iwe ni sherehe ya ndoa yenu. Nilifurahi sana kuona kuwa binti yupo hai maana alikuwa amebeba dhamana ya uhai wangu. Nikawa najiambia moyoni kuwa wiki ijayo naingia maisha mapya na nitakuwa mfalme mtarajiwa. Sinbad mimi ndo utakuwa mwisho wa kuiona familia yangu.



Sponsored Posts


  ðŸ‘‰    1 Tunakukaribisha kwenye Maktaba yetu       ðŸ‘‰    2 Download App zetu hapa ujifunze zaidi       ðŸ‘‰    3 Jifunze Fiqh       ðŸ‘‰    4 Madrasa kiganjani offline    


Je una maswali, maoni ama ushauri, tutumie sms ✉ bofya hapa hapa, ama wasiliana nasi kwa WhatsApp bofya hapa



Post Nyingine


image Hasara za wivu na kutokuwa wazi (sehemu ya 4)
Posti hii inaendelea kuelezea hasara za kuwepo kwa wivu na kutokuwa wazi katika, jamii inafikia wakati baba anapifahamu ukweli anawaita wazazi wawili na kuwaombeza kwa kuwa kimya baada ya kuona matatizo yaliyokuwa yanampata mtoto Lisa. Soma Zaidi...

image Mwendelezo wa hadithi ya Binti mfalme sehemu ya sita
Post hii inahusu zaidi mwendelezo wa hadithi ya Binti mfalme sehemu ya sehemu ya sita.sehemu hii inaonyesha jinsi bibi alivyo ndumila kuwili na hapendi kuonekana mbaya. Soma Zaidi...

image UFUPISHO WA ALIFU LELA ULELA KITABU CHA KWANZA
Posti hii inakwenda kukisimulia kuhusu hadithi za alifu lela ulela KITABU CHA KWANZA Soma Zaidi...

image Binti huyu Ni Nani?
Posti hii inakwenda kukuendelezea hadithi kuhusu kifo cha mtoa burudani wa sultan Soma Zaidi...

image Hadithi ya chongo watatu wa mfalme na wanawake wa Baghdad
Posti hii inakwenda kukuletea hadithi za alifu lela ulela Soma Zaidi...

image Hadithi ya chongo wa pili mtoto wa mfalme
Posti hii inakwenda kukuletea hadithi za alifu lela ulela Soma Zaidi...

image Kisa Cha mfugaji na mkewe
Posti hii inakwenda kukuletea hadithi za alifu lela ulela Soma Zaidi...

image Hadithi ya mzee wa tatu na mbwa wake mwekundu
Posti hii inakwenda kukuletea hadithi za alifu lela ulela Soma Zaidi...

image Hasara za wivu na kutokuwa wazi ( sehemu ya 2)
Posti hii inahusu zaidi hasara za wivu na kutokuwa wazi sehemu ya pili, sehemu hii inahusu mama Lisa anaenda kwa mama lina ili kuuliza kinachoendelea kwa mtoto wake , kwa hiyo tuona atapata jibu gani. Soma Zaidi...

image Hadithi ya mzee wa kwanza na mbuzi wake
Posti hii inakwenda kukuletea hadithi za alifu lela ulela Soma Zaidi...