HADITHI YA MLEVI

HADITHI YA MLEVI

HADITHI ILIYOSIMULIWA NA MLEVI
Tambua ewe Sultani muadilifu wa Baghdad mwa na wa Rashidi utambulikae kwa Harun, tambua kuwa mimi ni mzaliwa wa Misri na huku nimefika tu kwa sababu za utafutaji wa riziki. Baba yangu alikuwa ni mfanyabishara mzkubwa sana huko misri. Alijulikana sana katika miji na hata viji na nchi za majirani ya misri. Nilikuwa nikishiriki biashara na baba yangu toka nilipokuwa mdogo.



Hatimaye Mwenyezi Mungu akamchukuwa baba yangu na hapo mimi nikarithi kazi ya baba. Katika familia nipo peke yangu na mama yangu alishafariki zamani sana nikiwa mdogo. Nilifanyabiashara misri. Biashara yangu kuu ilikuwa ni kuuza kanzu. Nilikuwa nikizipaka manukato mazuri hata zikawa zikinukia sana na kumvutia mpita njia.



Watu walipenda sana biashara yangu na jina langu lilikuwa hata kumzidi baba yangu. Ila katu sikuweza kusafiri kibiashara kama alivyokuwa akifanya baba yangu. Niliweza kutengeneza chaneli za kibiashara wakawa wafanyabiashara wadogowadogo wanachukuwa mzugo kutoka kwangu. Kwa hakika biashara ya kanzu ilikuwa ikinilipa vyema. Kipindi chote hiki sikuwa mwenye kuoa.



Ilitokea siku moja akaja mtu mmoja na kuulizia bei ya kanzu. Badala ya kumtajia akanipatia kiasi kikubwa cha fedha na kunieleza nimpelekee mzigo wake sehemu ambayo alinitajia. Haikuwa ni kazi nzito kwani ni katika majukumu ya kazi yangu. Nilipomaliza maandalizi nikampelekea mzigo wake. Alipouona akanieleza kuwa nimuuzie mzigo ule pale kwake na faida yeyote nitakayoipata tutagawana.



Kwa uchu wangu wa pesa nikakubali. Yule bwana akaniaga safari ila akanieleza nimtunzie pesa yake mpaka atakapo rejea. Mambo yakawa hivyo nilimaliza kuuza mzigo na nilipata faida kubwa sana. Yule bwana baada ya mwezi akaja na kuniulizia pesa yake. Nikamueleza kuwa ipo salama. Basi akanieleza nimtunzie hadi atakaporudi tena.



Baada ya mwezi akarejea, na kuniambia kuwa ana shughuli nyingi, baada ya kumaliza atakuja kuchuuwa pesa yake. Alipoondoka akakaa kiasi cha mwezi. Hata aliporudi alikuwa mapendeza sana. Alifaa nguo nadhifu na za kupendeza.. alipokuja akanieleza ataondoka tena ila akirudi atachukuwa pesa yake. Mimi nikajiapiza kuwa pindi akija nitamkirimu kama mgeni wa heshma.



Safari hii alikaa kama mwaka hivi na aliporudi akaulizia pesa yake nikamueleza kuwa ipo salama. Basi nikamuomba awe mgeni wangu kwa siku ile na akakubali kwa sharti kuwa matumizi nitakayotumia yasiwe katika ile pesa yake. Nikakubali, baada ya muda kikaletwa chakula safi sana. Nikamnawisha kisha akanawa mgono wa kushoto. Nilistaajabu sana. Apilpoanza kula akala kwa mkono wa kushoto.



Nilistaajabu sana kwa mtu mtanashati na msafi kama huyu alafua anakula kwa shoto. Tulipomaliza kula akanywa maji kw ashoto. Basi baada ya chakula tukaanza kuzimulia za hapa na pale. Ndipo nikamuulza anitoe mashaka kuhusu kula kwake kwa shoto. Huenda ana ugonjwa ama ameumia ama anafanya masifa. Ndipo akatoa mkono wake. Looo! Mkoni wake ni kugupu aani ni kiwete ana mkono lakini kiganja kimekatwa.



Baada ya hapo akanieleza kuwa si kama ametaka kula na kushoto ila kuna sababu ilopelekea hali hiyo. Basi kwa udadisi niauiza kuhusu chanzo bila kusita ndipo akaanza kuzimulia hadithi yake na kukatwa kwa mkono wae:-




Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Kama unahitaji kuuliza maswali Bofya hapa

Mwandhishi Tarehe 2018-08-01     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 216


Download our Apps
👉1 Kitabu cha Afya     👉2 Madrasa kiganjani     👉3 kitabu cha Simulizi     👉4 Kitau cha Fiqh    

Post zifazofanana:-

Chemsha bongo namba 16
9. Soma Zaidi...

Chemsha bongo namba 18
21. Soma Zaidi...

HADITHI YA KILEMA WA VIUNGO
HADITHI YA KILEMA, MTANASHATI ASIYE NA MKONO Basi tambu kuwa mimi ni Mtu wa Baghadad na ni mtoto wa aliyekuwa mfanyabishara mkubwa sana. Soma Zaidi...

HADITHI ZA ALIF LELA U LELA: HADITHI YA SAFARI SABA ZA BAHARIA SINBAD
SAFARI SABA ZA SINBADKatika nchi ya Baghdad kulikuwepo na kijana aliyejulikana kama Sinbad mbeba mizigo. Soma Zaidi...

kamaralzamani
HADITHI YA CAMARALZAMANI PRINCE PEKEE Inapata mwendo wa safari ya siku 4 kwa farasi kutokea nchi ya Peshia alikuwepo mfalme maarufu sana aliyefahamika kwa jina la Shahzaman. Soma Zaidi...

HADITHI YA KAKA WA TANO WA KINYOZI
Soma Zaidi...

Alif lela u lela: utangulizi
Katika nchi za China, Hindi, Uarabuni na Uajemi alikuwepo mfalme aliyefahamika na kuheshimika sana kwa uhodari wake na utawala wake mzuru. Soma Zaidi...

HISTORIA YA NABII AYYUUB(A.S)
Ayyuub(a. Soma Zaidi...

Kitabu Cha hadithi ya Chongo
Kupata kitabu hiki download faili la PDF hapo chini na usome bila ya internet. Soma Zaidi...

SHAIRI -CHUKI
Soma Zaidi...

KISIWA CHA UOKOZE CHA PILI
Download kitabu Hiki Bofya hapa KISIWA CHA UOKOZI Nilikwenda mpaka nikakuta misitu minene na nisijuwe pa kuenda. Soma Zaidi...

Chemsha bongo namba 26
19. Soma Zaidi...