JARIBIO LA TATU LA A LADINI
Baada ya yule mchawi na waziri kushindwa kufanikisha wazo lao, sasa mchawi aliamua kuanza kutafuta mbinu mbadala. Mcawi alitambua kuwa endapo ataweza kumiliki kitu chochote kutoka kwenye lile pango ataweza kufanikisha mpango wake wa kulipiza kisasi cha kaka yake. Mchawi yule akaenda mjini kwa bibi mmoja aliyefahamika kwa jina la Hawiya. Hawiya alikuwa ni bibi mchamungu sana ambaye alikuwa akiwaombea watu dua na kukubaliwa maombi yake. Watu wa mjini waliamini kuwa Hawiya ni mwanamke aliye karibu na mungu sana. Kwa maana hiyo mchawi akaenda kwa hawiya na mumuuwa, kisha akachukuwa sura yake.
Kwa sura ya Hawiya Mchawi aliweza kufika nyumbani kwa Aladini. Alivizia wakati ambao Aladini hakuwepo nyumbani. Alipofika akajifanya anaombea watu dua na hatimaye akataka kuombea nyumba ya Aladini na familia yake. Mke wa Aladini alifurahi sana kumuona bi Hawiya na alipenda aiombee nymba na ndoa yao iwe na upendo endelevu. Bila ya kufahamu kinachoendlea kuwa yule sio hawiya. Mchawi akiwa katika sura ya hawiya akaanza kuomba dua. Aliweza kutumia nguvu za kichawi kuwashawishi watu kuwa kweli yeye ni Hawiya Mchamungu. Aliweza kutumia viini macho na kuonyesha miujiza mikubwa.
Wakati anamuombea Binti Mfalme mchawi alitumia mazingaombwe na kumfanya binti mfalme aone mambo ya baadaye. Akiwa katika hali hiyo binti Mfalme alimuona Aladini akiwa katika mavazi meume sana, huku ameongozana na kundi la watu. Alipochunguza kwa umakini aligunduwa kuwa Aladini anakwenda kuoa mke wa pili. Moyo wa binti Mfalme uliruka kwa wivu na hasira. Alipokuja kushituka kumbe alikuwa anaota. Uchawi uliweza kufanya kazi vyema na sasa binti mfalme alianza kupata wasiwasi kuwa ipo siku Aladini ataoa.
Mchawi akaanza kuingiza maneno hapo hapo, “inaonekana huna amani na ndoa yako, kuwa mumeo ataoa kke wapili, nitakusaidia kitu kumsahaulisha hizo fikra kabisa” nitashukuru sana jamani mamaangu” “usijali mwanangu nitakusaidia, ila sharti ni moja tu” ni lipi hilo mama kipenzi” “upate mafuta ya mshumaa wa kale, mafuta hayo yamehifadhiwa kwenye pango la ajabu kwenye yai la ajabu pia ni lazima ayalete mumeo mafuta hayo” mama yakipatikana nitafanikiwa kweli maana nampenda sana mumewangu Aladini” “ndio nakuhakikkishia utafanikiwa kabisa”. haya yalikuwa ni mazungumzo ya Hawiya na binti Mfalme.
Basi binti Mfalme akampatia chumba bi Hawiya awezekukaa pale kwa muda wa siku tatu mpaka mafuta yatakapopatikana. Aladini siku hiyo alirudi jioni na hakuwa na muda wa kukagua ndani. Usiku alipata chakula na kupumzika. Bint Mfalme akaanza kuzungumza maneno matamu kwa mumewe. Lengo lake ni kumvutavuta ili aweze kumletea mafuta ya ajabu. Katika mazungumzo ndipo akayataja afuta ya ajabu na akahitaji aletewe na yeye ayajuwe. Aladini aliposikia hivyo alitambua kuwa hapa kuna kitu. Hakutaka kumchafulia fikra mkewe, hivyoa akamuahidi kumtekelezea haja yake. Binti mfalme siku iyo alilala na furaha sana.
Ilipofika asubuhi Aladini alianza kufanya uchunguzi wake. Na akagunduwa kuwa kuna mwanamke mgeni amelala hapa ndani. Kwa kutumia mshumaa wake Aladini aliweza kutambuwa kuwa huyu ni yule mchawi. Aladini alicukuwa upanga wake na kwenda kumkata kichwa chake mchawi. Na hapo hadithi ya mchawi ikaisha. Waziri alipozipata habari hizi alirudi kwa Aladini kuomba msamaha. Aladini aliakubali kumsamehe waziri kwani hakuna ubaya wowote aliyomfanyia zaidi ya kushirikiana na mchawi.
Baad ya matukio haya Aladini alitambuwa kuwa ipo siku atatokea mchawi mwingine ama jini aliye mkubwa kuliko yule wa mshumaa. Na ataweza kumnyang’anya mali ama kuzipeleka kwenye mikono mibaya. Aladini aliamini njia pekee ni kuzudisha mali alizo nazo kwa wenyewe koo za majini. Aladini alimuita jini wa mshumaa na kumueleza wazo hiyo naye akakubaliana. Aladin alitumia mshumaa kwa mara ya mwiho kuwa na stoo ya madini mengi yenye thamani, dhahabu, ilijaa chumba kizima, Almasi na madini mengine mazuri. Kisha alilima shamba kubwa na kuweka wafanyakazi. Aladini alifanya mambo kadhaa kama vitega uchumi vyake. Kwani alianza kuiandaa kuishi maisha ya amani bila ya kuwa na pete wala mshumaa.
Aladini alipojirishisha kila kitu akamakabidhi jini wa mshumaa pete na mshumaa. Ijapokuwa jini wa mshumaa hakutaka kutengana na Aladini ila hakuwa na budi, na aliahidi kumsaidia Aladini muda wowote atakapokuwa na shida. Alipata kumueleza naman ya kukutana naye.baada ya makabidhiano hayo Aladini alilala kwa Amani siku hiyo. Ilipofika asubuhi alikwenda pangoni kushuhudia kilichoendela. Loo hakukuta kitu zaidi ya msitu. Hapo Aladini alihisi amani maana anakwenda kuishi maisha a kujitegemea.
Aladini aliweza kuishi vyema na familia yake. Baadaye akamhamisha mama yake wakae pamoja. Urafiki wa mama Aladini na Mfalme uliongezeka wakawa kama kaka na dada. Baada ya miaka kadhaa mfalme alifarika baada ya kushuhudia wajukuu wawili watoto wa Aladini mmoja wa kike na wa kiume. Wakike aliitwa Hawila na wa kiume aliitwa Mustapha. Alipofariki mfalme Aladini alichukuwa nafasi kama mtoto wa kiume wa Mfalme. Hakika nchi ilipata kiongozi bora mwenye upendo. Aliweza kutuma mali yake mwenyewe kwa ajili ya maisha ya watu wa nchi yake. Hakika historia haitamsahau Aladini.
Mpaka kufika hapa Dinarzade akamaliza Hadithi ya Aladini. Kweli mfalme Shaharia aliyekuwa akisikiliza masimulizi haya kati ya Dinarzade na Shahrazade aliweza kufarujika sana. Ni mwaka sasa umefika bila hadithi kukoma. Mfamle amesahau kabisa kama alikuwa akiwauwa mabinti. Kisha Dinarzade akaanza kusimulia hadithi ya tunda tufaha (epo)
Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiw ana App yetu. Bofya liln hapo chini kuweza ku download
Download NowJe! umeipenda hii post?
Ndio Hapana Save post
Rajabu Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Topic: Aliflela2 Main: Post File: Download PDF Share On Facebook or Whatsapp Views 537
Sponsored links
👉1
kitabu cha Simulizi
👉2
Kitau cha Fiqh
👉3
Kitabu cha Afya
👉4
Madrasa kiganjani
👉5
Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)
👉6
Simulizi za Hadithi Audio
Alif lela ulela
Posti hii inakwenda kukusimulia hadithi za alifu lela ulela Soma Zaidi...
Ugeni wa dhati
Posti hii inakwenda kukupa muendelezo wa hadithi ya aladini na taa ya ajabu Soma Zaidi...
Ndoa ya Siri yafanyika
Posti hii inakwenda kukuendelezea hadithi kuhusu kifo cha mtoa burudani wa sultan Soma Zaidi...
Ujumbe wa Siri kwenye kitabu cha ajabu
Posti hii inakwenda kukupa muendelezo wa hadithi ya aladini na taa ya ajabu Soma Zaidi...
ALIF LELA U LELA KITABU CHA PILI
Download kitabu Hiki Bofya hapa KITABU CHA PILI HADITHI ZA ALIF LELA U LELA UFUPISHO WA ALIF LELA U LELA KITABU CHA KWANZA. Soma Zaidi...
Kukatwa mkono na kuurithi utajiri
Posti hii inakwenda kukupa muendelezo kuhusu kifo cha mtoa burudani wa sultani Soma Zaidi...
ALADINI NA BINTI WA MFALME.
ALADINI NA BINTI WA MFALME. Soma Zaidi...
Nje ya jumba la kifahari la aladini
Posti hii inakwenda kukupa muendelezo wa hadithi ya aladini na taa ya ajabu Soma Zaidi...
Ndani ya jumba la aladini
Posti hii inakwenda kukupa muendelezo wa hadithi ya aladini na taa ya ajabu Soma Zaidi...
Hadithi ya tabibu
HADITHI ILIYOSIMULIWA NA TABIBU: Tambua ewe Sultani mwadilifu kuwa mimi nimezaliwa katika familia ya wachamungu waabuduji wanaofata mila za kiyahudi. Soma Zaidi...