HADITHI YA KINYOZI
Baba yangu alikuwa ni mfanyabiashara mkubwa nchini Misri. Hakujaaliwa kuwa na watoto wengi, ni mimi tu ndiye niliyekuwa mtoto wa pekee katika jumba la Tajiri. Baba yangu alifariki na kuniwachia mali zake zote. Nilikuwa naishi na bibi pamoja na watumwa wa baba waliokuwa ni wafanyakazi wangu. Pia nilikuwa naishi na mama yangu. Sikuwa na mke hivyo nilikuwa nikila nyumbani. Sikuwa na hamu na mwanamke, yaani ni kama mtu aliyerogwa. Nilikuwa nikichukia sana mwanamke, niliamini kuwa nikiwa karibu na wanawake nitaweza kufilisika. Wanawake pekee niliokuwa nikiwaheshimu na kufurahia uwepo wao ni ndugu zangu na watu wengine wa karibu na familia yangu.
Hali hii ilinifanya niwaze sana kuendeleza biashara kuliko kucheza na wanawake hasa wale wa mitaani. Umri wangu ulizidi kwenda na hatimaye wakati wa kuoa ulifika. Nilitamani sasa kutafuta mchumba lakini moyo ulikuwa ukinisuta maana wale nilokuwa nawachukia sasa natakiwa nitafute nitakaeishi naye milele. Chuki yangu haikuisha hivyo ikawa vigumu kwangu kumpata mchumba kutoka mabinti waliyopo mtaani. Niliamini njia pekee ni kutoka nje ya mji n kwendatafuta mke vijijini ama mji mwingine.
Sikumoja katika pirika zangu za utafutaji , wakati wa jioni ulinikuta pembeni ya jumba moja la kitajiri. Niliwa pembeni nimekaa napiga mahesabu yangu ghafla dirisha kubwa likafunguliwa na nikaona ukumbi mkubwa sana kwenye jumba la tajiri. Bostani zuri sana lilionekana kwenye kumbi hilo kubwa. Nilipoangalia vyema kumbi lile halikuwa lenye kufunikwa juu, mwangaza mzuri ulikuwa ukipenya kwa juu. Niliamini itakuwa wemefunika kwa turubai la mpira.
Mauwa mazuri yalijibanga vyema, harufu mwanana ilikuwa ukipenya puani mwangu. Mauwa yalichanua vyema na kufanya ji ukimbi lingare na kuvutia mtazamaji. Ilitulia kidogo huku nikithaminisha uzuri ulioje wa bustani lile. Wakati nikiangalia zaidi ghafla sura nzuri ikatokea nyuma ya uwa moja kubwa. Loo! Ni mwanamke mmoja mzuri sana alikuwa nakuja huku akiwa amebeba keni la kumwagilia mauwa.
Nikatafuta sehemu nzuri ya kukaa nipate kumuona vyema. Nilianza kuvutiwa na urefu alio nao, kwani hakuwa mfupi mno na si mrefu mmo. Nilipata kuiona vyema sura iliyo na ngozi nyeupe, pua iliyo tokeza vyema, macho makubwa kama mwanamwari wa pakistani. Nikiwa mbali kidogo nilitamani kusogea jirani ili nillihofu kumshitua, nilipata mwanya wa kujibanza sehemu nikaanza kumuona vyema. Nikaanza kutazama kwenye maeneo kadha na kugundua makubwa mabayo wengi katika wanawake wa mtaani hawakuwa nayo.
Kirundo cha nywele kilionekana ndani ya hijabu, kirundo kilishuka mpaka mgongoni, nilianza kuhisi mapigo ya moyo kama yanabadilika. Wakati alipokuwa akinyanyua keni na kuanza kumwagilia mauwa nilipata kuona bangili kwenye mgono wake. Zilikuwa zikimeremeta sana. Niliamini kuwa bila shaka ni babguli za dhahabu. Ziliweza kugongana na kutoa mlio mzuri. Nilianza kunogewa na uwepo wa mwanamwari. Nilibahatika kuona nyusi zilizotiwa wanja na kunyooka kama mbalamwezi ya mwezi mwandamo.
Akiwa anaendelea kumwagilia mauwa ghafla nyuki akamuingia kwenye hijabu yake. Akiwa katika harakati za kumtowa nyuki alimuuma na kutoa miguno ya maumivu. Sauti ile ilikuwa ni kama moto uliomwagiwa petroli kwenye moyo wangu. Binti aliendelea kumtoa nyuki, hatimaye akapunguza baadhi ya mafazi yake kwa haraka. Nilianza kukodoa mimacho nipate kuona vya ndani. Ghafla dirisha likafungwa, na nisijuwe nini kimeendelea zaidi. Kwa unyonge na upole nilirudi nymbani na kujitupa kitandani.
Sikuthubutu kula wala kunywa, hamu ya kula, kuzungumza na kunywa ilitoweka yote. Ghafla nilionyesha dalili za kuumwa na nikaanza kuchemshiwa dawa. Bibi yangu akaja ndani na aliponiangalia tu akagunduwa kuwa kuna jambo linaendelea. Bibi akaendelea kunidodosa ili apatekujuwa undani ndipo nikamuhadithia vyete vilivyonikuta. Bibi akanieleza “usipatetabu mjukuu wangu, mimi binti yule ninamjuwa na hata kwao ninakwenda sana, nitaongea naye kisha nitakuja kupa jibu ni lini ukutane naye”. baada ya kusikia maneno yale nilifurahi sana na hapohapo nikapona.
Siku mbili zikapita bila ya bibi kunieleza chochote, hatimaye nikaanza kuumwa tena. Siku ya tano bibi akaja chumbani kwangu na kuanza kunipa habari za furaha. Bibi akanieleza kuwa “Nilikwenda kumfata yule binti, na nikamueleza kuhusu ugonjwa wako baada ya kukuona. Alichonijibu kuwa hata yeye alikuona na hakutaka ufahamu, alianza kukupenda tuka alipokuona. Naye toka mlipoonana hakuamka kitandani kwa kukuwaza na asijuwe wewe ni nani na atakupata wapi. Hakuweza kuamini kama wewee ni mjukuu wangu. Hivyo ameniomba mkutane kesho kabla ya kutoka watu msikitini, maana geti lao litafunguliwa kwa ajili yako lakini ukichelewa baba yake atarudi na hutopata nafasi tena”
Maneno ya bibi yakuwa kama mkuki wa furaha uliokita katikati ya moyo wangu. Kwa furaha nilimkumbatia bibi na kumbusu. Ilikuwa ni siku ya Al-hamisi, nilitamani iwe ijumaa. Siku ya ijumaa hatimaye ikifika na asubuhi baada ya kupata kifungua kinywa bibi akaja na kunieleza kuwa nishevu nywele zangu vizuri nipendeze. Nikaagiza kijana aende akaniletee kinyozi anayesifika. Basi ndipo nikaletewa kinyozi huyu mnayemona hapa. Na hapo ndipo mambo yalipoanza kuharibika.
Je! umeipenda hii post?
Ndio Hapana Save post
Rajabu
Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Topic: Aliflela2
Main: Post
File: Download PDF
Share On
Facebook
or
Whatsapp
Imesomwa mara 906
Sponsored links
👉1 Kitau cha Fiqh
👉2 Kitabu cha Afya
👉3 Madrasa kiganjani
👉4 kitabu cha Simulizi
👉5 Simulizi za Hadithi Audio
👉6 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)
Siri ya wageni wale
SIRI YA WAGENI WALE INAFICHUKA Tambua ewe kijana changu, mimi na baba yako tulikutana zamani sana. Soma Zaidi...
Familia mpya baada ya harusi
Posti hii inakwenda kukupa muendelezo wa hadithi ya aladini na taa ya ajabu Soma Zaidi...
KIFO CHA MTOA BURUDANI WA MFALME
Hapo zamani katika mi wa Baghadani wakati wa utawala wa Sultani Harun Rashid alikuwepo kijana mmoja aliyekuwa karibu sana na Sultani kwa kuwa alikuwa akimpa burudani. Soma Zaidi...
MSHENGA WA ALADINI MBELE YA MFALME KWA MARA YA PILI
Soma Zaidi...
HADITHI YA KILEMA WA VIUNGO
HADITHI YA KILEMA, MTANASHATI ASIYE NA MKONO Basi tambu kuwa mimi ni Mtu wa Baghadad na ni mtoto wa aliyekuwa mfanyabishara mkubwa sana. Soma Zaidi...
Mrembo mtoto wa tajiri
Posti hii inakwenda kukupa muendelezo kuhusu kifo cha mtoa burudani wa sultani Soma Zaidi...
HADITHI YA CHONGO WATATU WATOTO WA WAFALME
Soma Zaidi...
Hadithi ya tabibu
HADITHI ILIYOSIMULIWA NA TABIBU: Tambua ewe Sultani mwadilifu kuwa mimi nimezaliwa katika familia ya wachamungu waabuduji wanaofata mila za kiyahudi. Soma Zaidi...
Ujumbe wa Siri kwenye kitabu cha ajabu
Posti hii inakwenda kukupa muendelezo wa hadithi ya aladini na taa ya ajabu Soma Zaidi...
Hadithi ya Kaka wa tatu wa kinyozi
Posti hii inakwenda kukupa muendelezo kuhusu kifo cha mtoa burudani wa sultani Soma Zaidi...
HADITHI YA TUNDA EPO
Soma Zaidi...
Deni la mapenzi
Posti hii inakwenda kukupa muendelezo kuhusu kifo cha mtoa burudani wa sultani Soma Zaidi...