VYAKULA VYA WANGA NA MADINI

VYAKULA VYA WANGA NA MADINI

Kuna aina nyingi za vyakula kama mafuta, wanga, fati, protini na vitamini. Je! unajuwa faida zake na hasara zake?

Download Post hii hapa

VYAKULA VYA WANGA NA MADINI

3.VYAKULA VYA WANGA
Vyakula vya wanga ndio vyanzo vikuu vya nguvu ndani ya mwili. Vyakula hivi hupatikana kwenye starch. Mwili unatumia vyakula vya wanga katika hali ya glucose. Ambayo huenda maeneo mengine ya mwili kwa ajili ya kuzalisha energy.

Unawza kupata wanga kwa kula nafaka kama maharage, matama, mihogo. Pia asali, miwa na viazi ni vyanzo vizuri vya wanga. inashauriwa kwa watu wanaofanya kazi ngumu zinazohitaji nguvu kubwa wale vyakula hivi.

4.VYAKULA VYA MADINI
Mwili unahitaji vyakula hivi ili uwezesj\he matumizi ya vyakula vingine yawe mazuri tunahitaji viyamini kwa kuulinda mwili dhidi ya magonkwa. Vitamin c hujulikana kwa kusaidia ugonjwa wa scuvy ugonjwa huu humfanya mtu atoke samu mwenue mafinzi. Vitamin A husaidia kurekebisha afya ya macho. Vitamin K husaidia kuganda kwa damu unapopata jeraha.

Mwili unahitaji madini pia ili uweze kujikinga na hatari zingine. Madini ya chuma ni muhimu katika kujenga seli nyekundu za damu.madini ya calcium ni muhimu kwa afya ya mifupa na meno

Madini na vitamin hpatikana zaidi kwenye mboga za majani, na matunda. Matunda yenye uchachu kama limao, chungwa husaidia kwa vitamin C na mapapai pi hujulukana kwa kuwa na vitamin C. spinachi ni muhimu kwa vitamin A. samaki husaidia kwa madini menhine.

5.VYAKULA VYA VITAMINI
Vitamin ni muhimu katika kuhakikisha kuwa mwili unatumia virutubisho vingine kufanya kazi zake. Kuna vitamin A,B,C,D,E na K. vitamin B vimegawanyika katika makundi kama vitamin B1,B2,B6, na B12. Ukosefu wa vitamin vyovyote kati ya hivi unaweza ukapelekea matatizo makubwa kwa afya ya mtu.

Vitamin A,D,E na K, vinaitwa fat soluble vitamin. Hivi nhuweza kuhifadhiwa ndani ya mwili. Hivyo hatuhitaji kula vyakula kuvipata kwa kila siku. Kwa upande mwengingine vitamin B na C huitwa water soluble vitamin, hivi havihifadhiwi ndani ya mwili, hivyo tunahitaji kula vyakula vyenye vitamin hivi kwa kila siku.

Vitamin A hupatikana kwenye maziwa, maini, karoti,machungwa, na mboga za rangi nya njano.. vitamin hivi ni muhimu kwa kusaidia afya ya macho na mfumo wa upumuaji (respiratory track). Ukosefu wa vitamin hivi unapelekea mtu kushindwa kuona wakati wa usiku. Mwili unakuwa ni rahisi kupata mashambulio pindi mtu akiwa na vitamin A kwa uchache.

Vitamin B1 hivi hupatikana kwenye nyama, maini, mayai,hamira na mchele. Husaidia katika kuhakikisha michakato ya kikemikali ndani ya seli inafanyika vizuri (metabolism). Pia husaidia katika kuunganisha taarifa za misuli. Ukosefu wa vitamin hivi unapelekea ugonjwa wa beriberi ambopo mtu anakosa hamu ya kula. Misuli kukaza pia ni dalili ya upungufu wa vitamin hivi. Wakati mwingine moyo kushindwa kufanya kazi ni kutokana na upungufu wa vitamin hivi.

Vitamin B2 hivi hupatikana kwenye nyama, maini, nafaka na hamira. Husaidia katika ufanyikaji wa michakato ya kikemia ndani ya seli (metabolism). Kupasuka kwa midomo ni dalili ya ukosefu wa vitamin hivi

Vitamin B3 hupatikana kwenye samaki, karanga,nyama, mchele usio kobolewa na hamira.. huhitajika kwa ajili ya kuwasaidia enzymes kubadilimchakula kuwa energy. Pellagra ni ugonjwa unaotokana na upungufu wa vitamin hivi. Mgonjwa anakosa hamu ya kula, misuli kukosa nguvu na kuharibika kwa ngozi.

Vitamin B12 hivi hupatikana kwenye samaki,nyama, mayai,maziwa na maini. Husaidia katika utengezaji wa damu, na utengezaji wa genetic meterials. Ugonjwa wa anaemia, upungufu wa uzito na nerve damage hutokana na upungufu wa vitamin hivi.

Vitamin C hivi hupatikana kwenye matunda yenye uchachu kama limao na machungwa. Mboga za kijani,na nyanya. Husaidia mwili kufyonza madini ya chuma. Kukosa nguvu za misuli,na maumivu ya viungio(joints)kutokwa na damu kwenye mafinzi kuchelewa kupona kwa vidonda na kuumwa mara kwa mara ni dalili ya upungufu wa vitamin hivi.

Vitamin D hupatikana kwenye mayai, maziwa, samaki na maini. Husaidia katika kukuwa na kuimarisha meno na mifupa. Ugonjwa wa matege kwa watoto na osteoporosis yaani mifupa kuwa milaini husababishwa na upungufu wa vitamin D.

Mitamini E hupatikana kwenye alizeti, butter, mchele na peanuts. Husaidi akatika kulinda utando uliopo ndani ya mwili. Mfumo wa fahamu kutokuwa katika hali ya kawaida ni dalili ya upungufu wa vitamin E

Vitamin K hupatikana kwnye maini na mboga za majani. Husaidia katika kuganda kwa damu baada ya kupata jeraha. Damu kutoka kwa wingi baada ya jeraha ni upungufu wa vitamin K.
vMtu atapata matatizo pia kama hata kunywa maji ya kutosha kwa siku. Maumivu ya kishwa huweza kusababishwa na kutokunywa maji ya kutosha. Choo kuwa kigumu huweza kusababishwa na uchache wa kunywa maji.


                   

Download Post hii hapa

Jiunge nasi WhatsApp
Upate Update zetu

Download App Yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.

Download Now Bongoclass Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Vyakula Main: Afya File: Download PDF Views 1637

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉2 Madrasa kiganjani    👉3 Kitabu cha Afya    👉4 kitabu cha Simulizi    👉5 Kitau cha Fiqh    👉6 Bongolite - Game zone - Play free game   

Post zinazofanana:

FAIDA ZA KIAFYA ZA KULA TUNDA PERA
FAIDA ZA KIAFYA ZA KULA TUNDA PERA

Pera ni tunda bora lakini pia ni dawa, tambua umuhimu wa tunda hili kiafya

Soma Zaidi...
Faida za kiafya za viazi vitamu
Faida za kiafya za viazi vitamu

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu faida za kiafya za kula viazi vitamin

Soma Zaidi...
Madhara ya mafuta mengi mwilimi
Madhara ya mafuta mengi mwilimi

Post hii itakufundisha madhara ya kuwa na mafuta mengi mwilimi

Soma Zaidi...
Parachichi (avocado)
Parachichi (avocado)

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu faida za parachichi

Soma Zaidi...
Faida za kula kunde, maharage, njegere, mbaazi na njugu mawe
Faida za kula kunde, maharage, njegere, mbaazi na njugu mawe

Somo hili linakwenda kukuletea faida za kiafya za kula kunde, maharage, njegere, mbaazi na njugu mawe

Soma Zaidi...
FAIDA ZA MATUNDA
FAIDA ZA MATUNDA

Somo hili linakwenda kukuletea faida za MATUNDA mbalimbali na mboga, upatikanaji wake na faida zake kiafya. Pia utakwenda kuona MATUNDA na mboga ambayo Ni kinga dhidi ya maradhi hatari Kama kisukari, saratani, maradhi ya moyo na mfumo wa fahamu pamoja na

Soma Zaidi...
Mabadiliko ya matiti yanayopaswa kutolewa taarifa mara moja
Mabadiliko ya matiti yanayopaswa kutolewa taarifa mara moja

Posti hii inahusu zaidi mabadiliko ya matiti yanayopaswa kutolewa taarifa mapema, kwa sababu ya kuwepo kwa saratani ya matiti, kuna dalili ambazo zikijitokeza zinapaswa kutolewa taarifa mara moja bila kuchelewa kama ifuatavyo.

Soma Zaidi...
Faida za kiafya za kula tunda pera
Faida za kiafya za kula tunda pera

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu faida za kiafya za kula tunda pera

Soma Zaidi...
Ukosefu wa madini ya Shaba mwilini
Ukosefu wa madini ya Shaba mwilini

Posti hii inahusu zaidi Ukosefu wa madini ya Shaba mwilini, ni Ukosefu wa madini ya Shaba mwilini ambao usababisha madhara kama ifuatavyo.

Soma Zaidi...
VYAKULA VYA MADINI
VYAKULA VYA MADINI

Pata elimu juu ya afya hapa ukiwa na vitabu vyetu bila ya malipo yoyote

Soma Zaidi...