HATMA YA NURDINI NA NCHI YAKE

HATMA YA NURDINI NA NCHI YAKE

Hadithi za alif lela u lela kitabu cha tatu sehemu ya 9

HATMA YA NURDINI NA NCHI YAKE

HATMA YA NURDINI NCHINI KWAKE.
Baada ya mfalme kuondoka pale ndani zilipita siku tatu bila hata kuongea na mte yeyote yule. Jambo hili lilileta taharuki kubwa sana. Hatimaye siku ya nne na mapema mfalme akaonekana kwenye baraza la asubuhi. Akiwana barua yake mkononi alionekana kuhoji baadhi ya walinzi. Alikuwa akihoji ni kitu gani kilitokea kwa Nurdini na wapi alipo. Majibu aliyopatiwa huwenda hayakumfurahisha kwa sababu uso wake haukuonekana kufurahia kabisa. Moja kwa moja alikwenda kuketi kwenye kiti chake cha kifalme. Kilikuwa ni kiti kirefu chenye vishikizo vya dhahabu, vilalio vya hariri iliyo laini vyema. Ijapokuwa kiti kilikuwa ni kizuri na lakini mfamle hakuwa na raha kabisa.



"nimepokea barua kutoka kwa Haru Rashid wa Baghadad ananitaka nijivuwe madaraka kwa amani ili nimkabidhi Nurdini kijana wa hayati waziri wangu mzee Farid". Yalikuwa ni maneno ya mfalme yaliyoonekana kumstaajabisha kila mtu aliyekuwepo pale ndani ya ukumbi ule. Hapo zamani mfalme wa nchi hii hupata uthibitisho wa kuendelea na madaraka ama kuyawacha kutoka Baghadad.



Ni kuwa wakati fulani nchi hii ilivamiwa na majeshi kutoka meneo ya India. Hivyo mfalme wa Baghadadi akiwa anatokea Maka kuhiji aliweza kuokoa nchi hii dhidi ya jeshi la wahindi. Tokea hapo wakaweka mkataba kuwa mchi hii mfalme hatakuwa halali mfapa athibitishwe na mfalme Harun Rashid wa Baghdad. Mkataba huu utaendelea kuwa hai mpaka pale ambapo Mfalme Harun Rashid atakapofariki.



Sasa kabla ya mfalme huyu walisha pita wafalme watatu nyuma. Mzee Farid pia alikuwa katika orodha ya kuwa Mfalme lakini alikatwa kutokana na upole wake. Hivyo kwa mkataba walioweka mfalme wa Baghadad ataweza kumuachisha madaraka mfalme wa nchi hiyo endapo hataridhishwa na utendaji wake kama kunyanyasa wananchi ama kupuuza majukumu yake. Hivyo basi kwa barua aliyoleta Nurdini inamaana mfalme huyu anatakiwa ajivue na Nurdini awe mfalme mpya.



Baada ya majadiliano marefu sana mawaziri walionekana kutokukubaliana na maamuzi hayo. Nusu walikuwa wanataka mfalme wao aendelee, kiongozi wa kundi hili alikuwa ni Masoud. Na nusu nyingine ilitaka mfalme akubali kuachia madaraka na kiongozi wa kudni hili walikuwa na rafiki na jamaa wa mzee Farid. Mwisho Masoud alitowa hitimisho kwa kusema "kwanza barua yenyewe haipo sahihi, ilipaswa iletwe na waziri ama kiongozi yeyote kutoka serikalini kwake, sasa haiwezekani Nurdini alete barua hii, mimi naona nurdini ni muongo, ameghushi barua hii hivyo akamatwe kisha auliwe"



Yalikuwa ni maamuzi magumu lakini mfalme alikubaliana nayo. Mfalnme akaruhusu Nurdini akamatwe atiwe kwenye gereza lililo madhubuti sana . swala la kumuuwa hakutaka lifanyike mpaka ainarishe ulinzi kwanza maana kunaweza kukatokea vita kutokana kupuuza barua ile endapo itakuwa ni ya kweli. Masoud ijapokuwa alisisitiza nurdini auliwe lakini hakuwa na pingamizi kwa maamuzi ya mfalme wake.



Siku arobaini sasa zimepita toka Nurdini aondoke baghadad. Siku hiyo mfalme alipita kwenye nyumba ambapo mke wa Nurdjini yupo. Alimkuta anaimba mashairi ambayo yalikuwa ni kuilaumu nafsi yake kwa kumuachia mune wake kipenzi kuondoka peke yake. Mfalme alisikitishwa sana pia akaijona yupo makosani. Ikabidi aitishe mkutano kidogo kuhusu barua yake aliyoituma. Katika mkutano wakakubaliana liondoke jeshi la watu 3000 kajini lisiibgie nchini likae nje ya mji ama mipakani, kisha waziri wawili akiwepo Jafari waingie kwa mfalme wa nchi ile ili kufuatilia barua ya mfalme Harun rashid. Endapo mfalme ataipinga jeshi linatakiwa limtoe kwa nguvu.



Katika msafara huu mke wa Nurdini pia likuwepo. Wakatoka kuelekea huko. Siku ya tatu wanaingin, kumbe na kule mfalme aliitaka kumuuwa Nurdini. Taarifa za jeshi la wa tu 3000 zikamfikia mfalme na wakati huo mawaziri wa mfalme harun rashid wanaingia. Mfalme Muhammad ibn Suleiman hakuwa na njia nyingine ya kuema barua ni feki. Hivyo ikabidi akabidhi madaraka kwa amani kabisa kwa Nurdini.



Kutoka hapo Nurdini akawa ndio mfalme mpya wa nchi hii. Mahusiano mazuri ya nchi mbili hizi yalitanuka na kuchanua vyema. Wananchi waliweza kusafiri na kushirikiana kibiashara kati ya nchi mbili hizi. Uongozi wa Nurdini ulipenda sana kwani hakuweza kuwabaguwa wanyonge. Kwa masaada wa mke wake aliyekuwa na akili na busara kubwa Nurdini alibadilika sana na kutoka Nurdini mzembe kuwa Nurdini bora sana.
Huu ndio mwisho wa hadithi hii. Ahsante sana kwa kuwa mvumilivu tukutane hadithi ya Badrudini, bila sjaka utaipenda zaidi kuiko hii.



Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Kama unahitaji kuuliza maswali Bofya hapa

Mwandhishi Tarehe 2018-08-01     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 284


Download our Apps
👉1 Kitau cha Fiqh     👉2 Kitabu cha Afya     👉3 kitabu cha Simulizi     👉4 Madrasa kiganjani    

Post zifazofanana:-

HADITHI YA NURDINI 04: Mtihani wa Nurdini
Mama aliendelea kugomba sana kisha akamfungia binti ndani na kuweka walinznwa kiume, kisha akawaambia 'haruhusiwi kuingia wala kutoka yeyote humu ndnai, hata mbwa Nurdini' neno mbwa lilimtoka tu mama Nurdini kisha akajilaumu kwa kumfana nisha ... Soma Zaidi...

Taharuki na mwisho wa Kmaralzaman Feki
TAHARUKI Siku hiyo kamaralzamani Feki alikuwa ufukweni kukaguwa mendeleo, alikuwa yeye na mke mwenzie. Soma Zaidi...

kamaralzamani
HADITHI YA CAMARALZAMANI PRINCE PEKEE Inapata mwendo wa safari ya siku 4 kwa farasi kutokea nchi ya Peshia alikuwepo mfalme maarufu sana aliyefahamika kwa jina la Shahzaman. Soma Zaidi...

ASUBUHI YA VARANGATI NA KAMARALZAMAN
VARANGATI ASUBUHI; Baada ya kugunduwa kuwa haikuwa ndoto kamaralzamani aliamini kuwa yule ndio mke ambaye baba yake alimchagulia. Soma Zaidi...

HADITHI YA NURDINI 03: Mtumwa wa Gharama
Kama wasemavyo waliokula chumvi nyingi kuwa muomba mungu hachoki, basi waziri Faridi aliendelea kuomba Mungu hata siku moja akapata taarifa kuwa kuna watumwa wametokea nchi za Uajemi. Soma Zaidi...

Ndoa ya kwanza ya kamaralzamani
NDOA YA HAMU Basi hali ikawa kama hivyo wawili hawa binamu na Kamaralzamani wakaanza kupanga njama ya kuweza kuondoka eneo lile kuelekea nchi za mbali kwa ajili ya kukutana na binti mfalme. Soma Zaidi...

Kamaralzaman akiwa katika ndoto ya kweli
NDOTO AMA KWELI? Soma Zaidi...

TAHARUKI YA MFALME WA BAGHADANI
Soma Zaidi...

HADITHI YA NURDINI 05: Rafiki wa Kweli
Mungu ashukuriwe sana, hatimaye miezi kadhaa ikapita bila ya waziri Masoud kugundua siri nzito. Soma Zaidi...

HADITHI ZA ALIF LELA U LELA KITABU CHA TATU: HADITHI YA NURDINI
Soma Zaidi...

HADITHI YA NURDINI 02: mawaziri wa Mfalme
Alikuwepo mfalme aliyetambulika kwa jina la Muhammad Suleiman Azeyn. Soma Zaidi...

KWENYE BOSTANI LA MFALME WA
KATIKA BOSTANI LA KIFALME BAGHADADBasi Nurdini na mke wake bila hata ya kujuwa wapi watafikia waliingia kwenye mashua na kuwasili Baghada wakati wa jioni. Soma Zaidi...