Zaka ni nini? Nini maana ya zaka katika uislamu

Zaka ni nini? Nini maana ya zaka katika uislamu

Zaka, kilugha ni kukua; kubariki na kuzidi kheri.

Download Post hii hapa

Zaka ni nini? Nini maana ya zaka katika uislamu

Nini Zaka?

Zaka, kilugha ni kukua; kubariki na kuzidi kheri. Husemwa imekua konde yake, na husemwa imeongezeka mali yake, na husemwa umezidi uchamngu na kutenda kheri kwake, na husemwa kwa ku'tahirika (takasika): "Hakika amefanikiwa alieitakasa". (Ash-shamsu : 9).

Na hutumika kwa kusifu: "............ Basi msijisifu usafi. ............". (Annajm : 32).

Na Zaka, kisharia ni jina lililowekwa kwa kukusudiwa kiwango makhsusi cha mali chenye kutolewa kwa kadiri makhsusi na kupewa watu wa aina makhsusi kwa shuruti makhsusi. Zaka imepewa jina hili - kwa vile mali inayotolewa Zaka hukua na kubariki kwa du'a za wale wenye kupewa hio Zaka. Amesema Mwenyezi Mungu Mtukufu:

……Lakini mnacho kitoa kwa Zaka kwa kutaka radhi ya Mwenyezi Mungu, basi hao ndio watao zidishiwa". (Ar-rum : 39).

Hukumu ya Zaka

Kuwajibika Zaka kumekuja kwa Qauli ya Mwenyezi Munguna Hadithi za Mtume s.a.w. na itifaqi ya wanazuoni.

Amesema Mwenyezi Mungu Mtukufu: . "……na toeni Zaka; ………". (Al Baqara : 110).

Na amesema Mwenyezi Mungu Mtukufu: "Chukua sadaka katika mali zao, ...........". (Tawba : 103).

Na amesema Mtume s.a.w.: . Maana ya Hadithi hii ni kama hivi:

"Umejengwa Uislam juu ya (Nguzo) tano". Miongoni mwa nguzo tano hizo za Uislam ni Zaka. Basi mwenye kukanya kulazimika kutoa Zaka huwa amekufuru, ila akiwa ni aliesilim karibuni hajapata kuufaham vyema Uislam, au amekulia mbali na elimu ya Kiislam. Mwenye kukataa kutoa Zaka, huchukuliwa (na Dola) Zaka yake kwa nguvu; hivi ndivyo alivyofanya Sayyidna Abu Bakar r.a. kwa wale waliokataa kutoa Zaka na akasema r.a.:

Maana ya maneno haya ya Sayyidna Abu Bakar r.a. ni kama hivi: "Wallahi, lau kama wangalinizuilia (wangalikataa kutowa) pingu za ngamia walikuwa wakizitekeleza (wakizitowa) kwa Mtume wa Mwenyezi Mungus.a.w.; basi ningaliwapiga vita kwa ajili ya hizo".


Download Post hii hapa

Jiunge nasi WhatsApp
Upate Update zetu

Download App Yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.

Download Now Bongoclass Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Fiqh Main: Dini File: Download PDF Views 1648

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Simulizi za Hadithi Audio    👉2 Kitau cha Fiqh    👉3 Kitabu cha Afya    👉4 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉5 Madrasa kiganjani    👉6 kitabu cha Simulizi   

Post zinazofanana:

Madhara ya riba kwenye jamii
Madhara ya riba kwenye jamii

Haya ni madhara ya riba katika jamii. Ni kwa namna gani jamii inadhurika kutokana na riba?

Soma Zaidi...
sunnah za swala
sunnah za swala

Sunnah za SwalaSunnah za Swala Vipengele vya sunnah katika swala ni vile ambavyo mwenye kuswali akivitenda husaidia sana kukuza daraja ya swala yake na kuipa nguvu na msukumo mkubwa wa kuiwezesha kufikia lengo lililokusudiwa kwa urahisi zaidi.

Soma Zaidi...
Taratibu za kuchaguwa mchumba katika uislamu
Taratibu za kuchaguwa mchumba katika uislamu

Hapa utajifunza hatuwa kwa hatuwa za kuchaguwa mchumba kulingana na sheria za kiislamu.

Soma Zaidi...
Saumu (funga)
Saumu (funga)

Nguzo za uislamu (EDK form 3:dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Jinsi ya kuswali swala ya kuoatwa kwa juwa ama swala ya kuoatwa kwa mwezi.
Jinsi ya kuswali swala ya kuoatwa kwa juwa ama swala ya kuoatwa kwa mwezi.

Post hii itakufundisha kuhusu swala ya kupatwa yaani kupatwa kwa juwa na kupatwa kwa mwezi swalat kusuf na swalat khusuf

Soma Zaidi...
MTAZAMO WA UISLAMU JUU YA ELIMU
MTAZAMO WA UISLAMU JUU YA ELIMU

Maana ya elimuElimu ni ujuzi ulioambatanishwa na utendaji.

Soma Zaidi...