Mafunzo Yatokanayo na Historia ya Adam(a.s)

Mafunzo Yatokanayo na Historia ya Adam(a.s)

(i) Utukufu wa mtu katika Uislamu hautokani na nasaba, rangi,kabila,utajiri ila uwajibikaji kwa Allah(s.

Jiunge nasi WhatsApp
Upate Update zetu

Mafunzo Yatokanayo na Historia ya Adam(a.s)

Mafunzo Yatokanayo na Historia ya Adam(a.s)

(i) Utukufu wa mtu katika Uislamu hautokani na nasaba, rangi,kabila,utajiri ila uwajibikaji kwa Allah(s.w)unaolandana na Elimu sahihi.

(ii) Tujiepushe na tabia ya kiiblis ya kumtukuza au kumdharau mtu kutokana na nasaba, rangi, sura, hali yake kiuchumi, n.k.

(iii) Tujiepushe na tabia ya Kiiblis ya kuwa na chuki binafsi dhidi ya watu wasio na hatia yeyote.

(iv) Tujiepushe na tabia ya Kiiblis ya kibri na majivuno.

(v) Tuwe na msimamo katika kutekeleza amri za Allah(s.w) na Mtume wake na tusiwe tayari kuyumbishwa na hadaa za shaitwani.

(vi) Tunapofikwa na tashwishi za kishetani tujikinge kwa Allah(s.w).



“Na kama shetani akikushawishi kwa tashwishi (zake), wewe jikinge kwa Mwenyezi Mungu (kwa kusema: A’uudhubillah Minash-shaytwanir-Rajiim). Yeye ni mwenye kusikia mwenye kujua.” (41:36)

Au ujikinge kwa kusema:




Sema: najikinga kwa Bwana mlezi wa watu. Mfalme wa watu. Muabudiwa wa watu. Na shari ya mwenye kutia wasiwasi mwenye kurejea nyuma. Atiaye wasiwasi nyoyoni mwa watu. Ambaye ni katika majini na watu. (114:1-6)

Au kuleta Dua ifuatayo:




“...... Mola wangu! Najikinga kwako uniepushe na wasiwasi wa mashetani. Na najikinga kwako, Mola wangu, ili wasinihudhurie”. (23:97-98)


(vii) Muda wote Waislamu hawana budi kuchukua tahadhari kwani kiasili (tangu mwanzo wake) Uislamu ni dini yenye maadui miongoni mwa mashetani wa kijini na watu.



................

“Na namna hii tumemfanyia kila Nabii maadui, (nao ni) mashetani katika watu na majini. Baadhi yao wanawafunulia wenziwao maneno ya kupamba pamba ili kuwadanganya…..........” (6:112)


(viii)Mwanaadamu tangu mwanzo wa kuumbwa kwake amekusudiwa kuwa Khalifa katika ardhi na nyenzo kuu ya kumuwezesha kuwa Khalifa ni elimu ya mazingira na ya mwongozo.

(ix) Tujiepushe na kuwahusudu watu juu ya meema walizotunukiwa na Allah(s.w) bali tumuelekeeAllah(s.w) kwa unyenyekevu na
k umuomba atuneemeshe kama wale aliowaneemesha.

Wala msitamani vile ambvyo MwenyeziMungu amewafadhilisha badhi yenu (kwa vitu hivyo) kuliko wengine. wanaume wanayo sehemu (kamili) ya vile walivyovichuma; na wanawake nao wanayo sehemu(kamili) ya vile walivyovichuma na mwombeni Mwenyezi Mungu fadhila zake. Hakika Mwenyezi Mungu ni mjuzi wa kila kitu.(4:32)

(x) Allah(s.w) huwaongoza na kupokea maombi ya wale wajitakasao:
........

“...... Hakika Mwenyezi Mungu huwapenda wanaotubu na kuwapenda wanaojitakasa” (2:222)

(xi) Muislamu muumini anatakiwa ajihidi kuondosha ubaya au alipize ubaya aliofanyiwa kwa wema,yaani kumsamehe aliyemkosea kumpa aliyemnyima na kumchangamkia aliye mkasirikia. Tunahimizwa katika Qur’an:



“Mambo mazuri na mabaya hayawi sawa. Ondosha (ubaya uliofanyiwa kwa wema), tahamaki yule ambaye baina yako na baina yake kuna uadui atakuwa kama ni jamaa (yako) mwenye kukufia uchungu. Lakini (jambo hili) hawatapewa ila wale wanaosubiri wala hawatapewa ila wenye hadhi kubwa (mbele ya Mwenyezi Mungu)”(41:34-35)

(xii) Tunapoteleza na kumkosea Allah(s.w),tumuelekee kwa unyenyekevu kwa kuleta toba ya kweli kama alivyofanya Adam(a.s) na mkewe.

(xiii) Kumkosea Allah(s.w) kwa kibri kama alivyofanya Iblis ni jambo baya mno la hatari kwani humpelekea mtu kupigwa muhuri moyoni mwake kiasi cha kumfanya asione haja yoyote ya kuleta toba. Tunakumbushwa hili katika Qur’an.



“Hakika wale waliokufuru (kwa ukaidi tu na inadi) ni sawa kwao ukiwaonya au usiwaonye hawataamini. Kama kwamba Mwenyezi Mungu amepiga muhuri juu ya ya nyoyo zao na juu ya masikio yao; na juu ya macho yao pana kifuniko; basi watakuwa na adhabu kubwa.”(2:6-7)



                   

Download Post hii hapa

Download App Yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.

Download Now Bongoclass Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Sira Main: Dini File: Download PDF Views 2385

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Kitau cha Fiqh    👉2 kitabu cha Simulizi    👉3 Simulizi za Hadithi Audio    👉4 Kitabu cha Afya    👉5 Madrasa kiganjani    👉6 Bongolite - Game zone - Play free game   

Post zinazofanana:

tarekh 07
tarekh 07

KUPASULIWA KWA KIFUA MTUMEWAKATI AKIWA MTOTO.

Soma Zaidi...
Malezi ya mtume
Malezi ya mtume

Bara arabu zama za jahiliyyah (EDK form 2 dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Kulingania Uislamu kwa Jamii Nzima
Kulingania Uislamu kwa Jamii Nzima

Baada ya miaka mitatu ya Utume, Muhammad(s.

Soma Zaidi...
Kulelewa kwa Mtume,  maisha yake ya Utotoni na kunyonya kwake.
Kulelewa kwa Mtume, maisha yake ya Utotoni na kunyonya kwake.

Historia na sura ya Mtume Muhammad S.A.W sehemu ya 06. Hapa utajifunza kuhusu historia ya Mtume akiwa mtoto.

Soma Zaidi...
Hatua mbili kuu za kushuka kwa Quran
Hatua mbili kuu za kushuka kwa Quran

Quran (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
KUCHIMBWA UPYA KWA KISIMA CHA ZAMZAMA NA KUNYWA MAJI YA ZAMZAMA KISIMA KILICHO BARIKIWA
KUCHIMBWA UPYA KWA KISIMA CHA ZAMZAMA NA KUNYWA MAJI YA ZAMZAMA KISIMA KILICHO BARIKIWA

KUCHIMBWA UPYA KISIMA CHA ZAMZAMKwa kifupi ni kuwa Abdul-Muttalib alipata agizo kutoka ndotoni kuwa achimbe kisima cha zamzam, na akaelekezwa sehemu ya kupachimba.

Soma Zaidi...
Chokochoko na Upinzani wakati wa khalifa uthman khalifa wa Tatu
Chokochoko na Upinzani wakati wa khalifa uthman khalifa wa Tatu

KUPOROMOKA KWA DOLA YA KIISLAMU ALIYOICHA MTUME(S.

Soma Zaidi...
Kazi na wajibu wa khalifa katika dola ya kiislamu
Kazi na wajibu wa khalifa katika dola ya kiislamu

Kazi na Wajibu wa KhalifaKhalifa katika Serikali ya Kiislamu ndiye mtendaji mkuu wa Serikali kama alivyokuwa Mtume(s.

Soma Zaidi...