Mtume amezaliwa mwaka gani?

Mtume amezaliwa mwaka gani?

Na tumemuusia mwanaadamu afanye wema kwa wazazi wake.

Jiunge nasi WhatsApp
Upate Update zetu

v

Maadili katika surat Al-Ahqaf


Na tumemuusia mwanaadamu afanye wema kwa wazazi wake. Mama yake amechukua mimba yake kwa taabu na akamza kwa taabu. Na kubeba mimba yake hata kumwachisha ziwa; (uchache wake) ni miezi thelathini. Hata anapofikia baleghe yake na akawa mwenye umri wa miaka arubaini, (mtoto mwema) husema: "Ee Mola wangu! Niwezeshe nishukuru neema zako ulizonineemesha mimi na wazazi wangu, na niwezeshe nifanye vitendo vizuri unavyovipenda, na unitengenezee watoto wangu; kwa yakini ninatubu kwako; na hakika mimi ni miongoni mwa waliosilimu (walionyenyekea)." (46:15).


Hao ndio tunaowakubalia vitendo vyao vyema walivyovifanya, na tunayapita kando makosa yao, (tunayasamehe); (watakuwa) miongoni mwa watu wa Peponi: miadi ya kweli waliyoahidiwa. (4 6:16).



Na ambaye anawaambia wazazi wake: "Kefule nyi! Oh! Mnanitishia kuwa nitafufuliwa; na hali karne nyingi, (watu wengi) zimekwisha pita kabla yangu (wala hazikufufuliwa)?" Na hao (wazee wake) wawili huomba msaada wa Mwenyezi Mungu; (na humwambia mtoto wao:) "Ole wako! Amin (haya unayoambiwa). Hakika ahadi ya Mwenyezi Mungu ni kweli." Lakini yeye husema: "Hayakuwa haya (mnayoyasema) ila ni visa vya watu wa kale (tu si maneno ya kweli)."



Hao ndio ambao imelazimika hukumu juu yao (ya kutiwa Motoni, pamoja na mataifa yaliyopita kabla yao ya majini na watu, hakika hao ndio waliojitia khasarani. (46:17-18)
Kutokana na aya hizi tunajifunza kuwa:



(a)Hatunabudi kuwafanyia wema wazazi wawili na hasa mama ambaye anapata dhiki kubwa katika kutuzaa na kutunyonyesha mpaka kufikia umri wa miaka miwili.



(b)Hatunabudi kumshukuru Allah (s.w) kwa kutuneemesha kwa neema mbali mbali ikiwa ni pamoja na kuwapa wazazi wetu moyo wa huruma na mapenzi ya kutulea mpaka kufikia utu uzima.



(c)Pamoja na kumshukuru Allah (s.w), hatubabudi kuwashukuru wazazi wetu kwa kutulea kwa huruma na mapenzi. Shukrani zetu kwao tutazidhihirisha kwa kuwatii, kuwafanyia ihsani na kuwaombea dua na maghfira kwa Allah (s.w).


(d)Hatuna budi kujiepusha mbali na kuwafanyia wazazi wetu ufedhuli na jeuri. Tusisubutu hata kuwagunia.



(e)Hatunabudi kuomba kizazi chema na kumuomba Allah (s.w) atuwezeshe kukilea vyema kizazi chetu.



(f)Hatunabudi kufuatilia kwa makini usia mwema wanaotupa wazazi wetu.



(g)Hatunabudi kuleta toba na kuomba maghfira mara kwa mara (angalau kila siku mara mia moja).




                   


Download Post hii hapa

Download App Yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.

Download Now Bongoclass Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Sira Main: Dini File: Download PDF Views 953

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Kitau cha Fiqh    👉2 Kitabu cha Afya    👉3 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉4 kitabu cha Simulizi    👉5 Simulizi za Hadithi Audio    👉6 Madrasa kiganjani   

Post zinazofanana:

Kujengwa upya al Kabah baada ya kuwa na mipasuko.
Kujengwa upya al Kabah baada ya kuwa na mipasuko.

Sira na historia ya Mtume Muhammad s.a.w sehemu ya 18. Hapa utajifunza kuhusu tukio la kujengwa upya kwa al kaaba 🕋

Soma Zaidi...
Si Yesu Aliyesulubiwa (yesu hakufa msalabani wala hakusulubiwa
Si Yesu Aliyesulubiwa (yesu hakufa msalabani wala hakusulubiwa

Katika Qur,an tukufu, Mwenyezi Mungu aliye muweza na mjuzi wa mambo anathibitisha kuwa aliyesulubiwa si Nabii Isa(a.

Soma Zaidi...
Vitimbi vya Wapinzani Dhidi ya Ujumbe wa Nabii Shu’ayb(a.s)
Vitimbi vya Wapinzani Dhidi ya Ujumbe wa Nabii Shu’ayb(a.s)

Kama ilivyokuwa katika kaumu zilizotangulia, waliomuamini Shu’ayb(a.

Soma Zaidi...
Historia ya Watoto Wawili wa Nabii Adam
Historia ya Watoto Wawili wa Nabii Adam

“Na wasomee khabari za watoto wawili wa Adam kwa kweli, walipotoa sadaka, ikakubaliwa ya mmoja wao na ya mwingine haikukubaliwa Akasema (yule asiyekubaliwa sadaka yake): “Nitakuua”.

Soma Zaidi...
Ibrahiim(a.s) Aomba Kupata Kizazi Chema
Ibrahiim(a.s) Aomba Kupata Kizazi Chema

Nabii Ibrahiim na mkewe Sarah walikaa mpaka wakawa wazee bila ya kupata mtoto.

Soma Zaidi...