(ii) Wanyama wafugwao kwa ajili ya chakula Wanyama wafugwao wanaotolewa Zakat ni ngamia, ngo’ombe, mbuzi na kondoo.
(ii) Wanyama wafugwao kwa ajili ya chakula
Wanyama wafugwao wanaotolewa Zakat ni ngamia, ngo’ombe, mbuzi na kondoo. Farasi na Punda hawatolewi Zakat. Hadith zifuatazo zinatufahamisha juu ya Zakat ya wanyama:
Ali bin Abii Talib (r.a) amesimulia kuwa Mtume wa Allah amesema: “Hapana Zakat kutoka kwa Farasi na Punda...” (Tirmidh, Abu Daud)
Sayydina Ali (r. a) vile vile am eeleza: “Nina eleza kutoka kw a Mtum e (s.a.w) aliyesema: “Lete moja ya nne ya ushuru, ikimaanisha kuwa kuna Dirham moja kwa kila Dirham arubaini na mtu haijuzu kwake Zakat mpaka awe na Dirham mia mbili (200). Kwa hiyo zinapokuwa Dirham 200 kuna Dirham tano za Zakat kinachozidi kitatolewa kulingana na hisabu hiyo (ya 1/40). Na kwa mbuzi kuna mbuzi mmoja katika kila arobaini mpaka ifikie idadi ya mbuzi 120, kama wakizidi kwa mmoja mpaka 200
watatolewa mbuzi majike wawili wa mwaka mmoja. Kama wakiwa zaidi ya hapo mpaka kufikia 300 mbuzi 3 wa mwaka mmoja; kama hakuna zaidi ya mbuzi 39 haina Zakat juu yake kutokana na mbuzi hao. Na kuhusu ng’ombe, kwa kila ng’ombe ng’ombe 30 kuna ndama mmoja wa mwaka mmoja na katika kila ng’ombe 40, kuna ndama mmoja wa miaka miwili, na hapana Zakat inayojuzu kutokana na ng’ombe waliotiwa kwenye kazi” (Abu Daud).
Nisaab na kiasi cha kila aina ya mnyama
Wanyama waliotajwa watastahiki kutolewa Zakat baada yakuwa katika malisho na katika milki ya mfugaji kwa kipindi cha mwaka mmoja. Kwa hiyo kila mwaka wafugaji wanatakiwa wahesabu mifugo yao iliyopindukia mwaka na kutoa Zakat kama ilivyoeleza hadithi iliyotajwa hapo juu. Wanyama watolewao Zakat wawe wazima na wachanga wasio na kilema chochote. Watolewe wanyama walio wazuri zaidi tukikumbuka msisitizo wa Qur-an:
Enyi mlioamini! Toeni katika vizuri mlivyovichuma, na katika vile tulivyokutoleeni katika ardhi. Wala msikusudie kutoa vilivyo vibaya, hali nyinyi wenyew e msingevipokea isipokuw a kw a kuviangalia. Basi jueni ya kwamba Mwenyezi Mungu ni Mkwasi na Asifiwaye. (2:267).
Hivyo, japo majike katika ng’ombe na mbuzi hayaku sisitizwa katika Hadithi mbali mbali kama ilivyosisitizwa kwa upande wa ngamia, ni bora kutoa mbuzi jike au kondoo jike wa mwaka mmoja. Majike ni bora zaidi kuliko madume kwa kuwa yatazaa na kuongeza idadi ya mifugo. Kama katika kuthaminisha na fedha taslimu dume litakuwa na thamani zaidi kuliko jike na ikiwa mtoaji ametoa fedha taslimu badala ya wanyama, basi atoe thamani ya dume. Pia mifugo ya Zakat inaweza kuthamanishwa zitakapotolewa fedha taslim badala ya mifugo yenyewe. Lakini katika kufanya hivyo ni lazima liangaliwe lile litakalokuwa na maslahi bora kwa mpokeaji Zakat. Kama itakuwa ni bora kwa mpokeaji apokee mifugo badala ya kutoa thamani yake itakuwa sawa. Jambo muhimu linalosisitizwa hapa ni kwamba vinavyotolewa Zakat viwe vizuri vinavyopendeka kwa mtoaji na mpokeaji.
Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiw ana App yetu. Bofya liln hapo chini kuweza ku download
Download NowJe! umeipenda hii post?
Ndio Hapana Save post
Rajabu Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Topic: Aliflela1 Main: Post File: Download PDF Share On Facebook or Whatsapp Views 696
Sponsored links
👉1
Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)
👉2
Simulizi za Hadithi Audio
👉3
Madrasa kiganjani
👉4
kitabu cha Simulizi
👉5
Kitau cha Fiqh
👉6
Kitabu cha Afya
alif lela u lela
Soma Zaidi...
SAFARI YA SABA YA SINBAD
Download kitabu Hiki Bofya hapa SAFARI YA SABA YA SINBAD Walipokusanyika siku ilofata Sinbad akawaambia kuwa kilichofanya nikavunja ahadi yangu ya kutosafiri tena ni kauli ya Sultani Nilipopunzika kwa muda wa miezi miwili nilipata habari kuwa Sultani Soma Zaidi...
alif lela u lela
Download kitabu Hiki Bofya hapa Kupata mwendelezo wa hadithi hii Download App yetu. Soma Zaidi...
SAFARI YA MAJIBU JUU YA MASWALI MAWILI
Download kitabu Hiki Bofya hapa SAFARI YA MAJIBU JUU YA MASWALI MAWILI. Soma Zaidi...
Ndani ya pango la makaburi
Posti hii inakwenda kukupa muendelezo wa safari saba za Sinbad Soma Zaidi...
Kitabu Cha Hadithi ya kifo cha Damu
Kupata kitabu hiki download faili la PDF hapo chini na usome bila ya internet. Soma Zaidi...
HADITHI ZA ALIF LELA U LELA: HADITHI YA WANAWAKE WATATU NA CHONGO WATATU
Soma Zaidi...
Usaliti unaanza hapa
Posti hii inakwenda kukuletea hadithi za alifu lela ulela Soma Zaidi...
Kuelekea bonde la uokozi
Posti hii inakwenda kukupa muendelezo wa safari saba za Sinbad Soma Zaidi...
HADITHI YA SAMAKI WA RANGI NNE
Download kitabu Hiki Bofya hapa HADITHI YA SAMAKI WA RANGI NNE. Soma Zaidi...