Download kitabu Hiki Bofya hapa HADITHI YA MVUVI NA JINI Hapao zamani kulikuwepo na mvuvi aliyekuwa masikini wenye watoto watatu na mke mmoja.
Download kitabu Hiki Bofya hapa
HADITHI YA MVUVI NA JINI
Hapao zamani kulikuwepo na mvuvi aliyekuwa masikini wenye watoto watatu na mke mmoja. Alikuwa anavuwa kwa kutumia nyavu ya kutupa. Alijiwekea sheria ya kutupa nyavu mara nne kwa siku.
Alitoka sikumoja asubuhi, akatupa nyavu yake mara ya kwanza na asiambulie kitu. Akarudi nyumbani na kurudi baada ya muda, akatupa nyavu yake na akaambulia mauchavu. Akatupa mara ya tatau akaambulia mauchafu bila ya samaki. Na hapo nyavu yake alikuwa imeharibiwa hivyo akaishona na kuiweka tayari kutupa mara ya mwisho. Mara hii alipotupa aliambukia kuvua lichiupa la shaba lenye mfuniko wa silva.
Kwa kutaka kujuwa kilichomo mule akaamua kuofunguwa chupa ile. Akaanza kuitowa kifuniko. Ghafta akaona moshi mkubwa unatoka kwenye ile chupa. Moshi ukajikusanya angani kama kiwingu na punde tu kukatokea jini kubwa sana. “chaguwa mwenyewe kifo cha kukuuwa” ni sauti ya kushangaza ya jini lile. Mvuvi akashngaa kusikia anaambiwa achaguwe kifo.
“nimefanya nini mkuu? Na wewe ni nani? Na umetoka wapi?”. Ni fgurushi la maswali ya mvuvi kuliuliza lile jini.
“Mimi ni jini nilikuwa nimefungiwa kwenye chupa hii na mkuu wangu, na wewe ndo umenifungulia”. Ni maneno ya jini
Mkuvu akamuuliza “sasa kama nimekufungulia ulipokuwa umefungu ina maana nimekutendea wema , haya mbona unataka kuniuwa”?
“nilifanya kosa na mkuu wangu akanifungia humu, miaka mia moja kwa kwanza niliahidi atakaye nifungulia nitampa utajiri mkubwa. Mika ile ikapita na sikupata wa kunifungulia. Miaka nia ya pili nikaahidi atakaye nifungulia nitampa thamani kubwa ya duniani, pia hakutokea wa kunifungulia. Miaka mia ta tatun nikaahidi atakaye nifungulia nitamfanya mfalme na nimpa anachotaka kwa kila siku. Pia miaka hii ikapita bila ya kufunguliwa. Baada ya hapo nikaahidi kuwa atakaye nifungulia nitamuuwa ila nitampa nafasi ya kuchagywa kifo atakachotaka. Hivyo wewe ndo umekuja kunifungulia, chaguwa kifo gani unataka ufe”.
Mvuvi akamwambia hule jini, “mimi siamini kama umetoka humu kwe nye chupa. Umeingiaje humu wewe mkubwa hivyo kwenye kichupa kidogo hiki?. Hebu ingia nikuone ndo nitaamini”.
Yule jini akajirudisha kwenye jhali ya moshi na akaingia kwenye ile chupa. “umeona sasa nilivyoingia?, nipo kwenye chupa sasa, umeamini?” ni maneno ya jini kumwambia mvuvi. Mvuvi baada ya pale kwa haraka zaidi akachukuwa kifuniko na akaifunga chupa. “sasa nitakurudisha kulekule baharini ulikokuwa.” ni maneno ya mvuvi akimwambia jini.
Jini akajitahidi atoke lakini akashindwa ikabidi amwambie mvuvi “ naomba nifungulie, nitakupa utajiri ukunifungulia” mvuvi kwa sauti kubwa akamjibu “hapana siwezi kukutowa usije ukawa umenidanganya. Nitakutupa baharini na nitaweka tangazo hapa ili atakaye ivua chupa ajuwe kuna jini airudishe”.
Jini likaanza kujitetea kwa saiti ya kinyonge “nakuomba, nakuahidi pia unifungulie, nitakupa utajiri”. Mvuvi kwa sauti ya busara akamjibu “naogopa yasije yakanikuta yaliyompata tabibu wa mfalme.” “ni yapi hayo yaliyompata tabibu?” ni swali la jini kumuuliza mvuvu. Mvuvi akaanza kusimulia hadithi ya tabibu kama ifuatavyo;-
Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.
Download NowPosti hii inakwenda kukupa muendelezo wa safari saba za Sinbad
Soma Zaidi...Download kitabu Hiki Bofya hapa SAFARI YA NNE YA SINBAD Basi ikafikia siku ya kuanza safari yangu ya nne ya kibiashara.
Soma Zaidi...Posti hii inakwenda kukuletea hadithi za alifu lela ulela
Soma Zaidi...Posti hii inakwenda kukuletea hadithi za alifu lela ulela
Soma Zaidi...Download kitabu Hiki Bofya hapa HADITHI YAKISIWA CHA MAWE YANAYOLIA.
Soma Zaidi...Download kitabu Hiki Bofya hapa KUTOKA NYANI MPAKA KUWA CHONGO.
Soma Zaidi...Posti hii inakwenda kukuletea hadithi za alifu lela ulela
Soma Zaidi...