image

Safari saba za sinbad

Posti hii inakwenda kukuletea hadithi za safari saba za Sinbad

SAFARI SABA ZA SINBAD

Katika nchi ya Baghdad kulikuwepo na kijana aliyejulikana kama Sinbad mbeba mizigo. Kijana huyu alijaaliwa kuwa na uwezo mkubwa wa nguvu za kuweza kubeba mizgo. Pia alikuwa na uwezo mzuri wa kiakili. Sinbad aliipenda sana kazi yake pia watu walimpenda kwa kuwa alikuwa akifanya kazi zake kwa umakini.

 

Ilitokea sikumoja alipokuwa katika kituo chake cha kufanyia kazi alikuwa mtu mmoja asiyemfahamu kabisa na kumpa kazi ya kupeleka mzigo wake sehemu husika. Mtu yule alitoweka baada ya kutoa maelekezo na kumpatia pesa yake. Sinbad baada ya kupewa maelekezo aliuchukuwa ule mzigo na kuanza kuukokota kwenye mkokoteni wake kuupeleka alikoelekezwa.

 

Njiani Sinbad alikutana na geti liliozungukwa na mauwa mazuri yenye kuvutia ndege, wadudu na wanyama kwa harufu na utamu wake. Sinbad alisimama kidogo eneo hili ili apate kushangaa uzuri ulioje wa eneo hili. Akilini alijiambia kuwa bila shaka ndani ya eneo hili kuna nyumba kubwa yenye bosi mkubwa.

 

Sinbad akiwa katika hali hiyo alituwa mzigo wake chini na kuanza kufuta jasho lake. Alisogea kidogo kwenye geti lile na kuona ndani kuna mambo ya kuvutia. Sinbad alikuwa ni kijana mwenye adabu na heshima lakini leo alisahau mambo yote hayo na akaanza kuchungulia ndani kwa watu. Alipokuwa hatoshelezi macho yake aliamua kuingia kwenye geti lile ili aone zaidi.

 

Sinbad hakuamini macho yake kama yanamuonesha sahihi, aliona nyumba kubwa yenye kila akijuacho kuwa kinahitajika, na aliona pia ambavyo havijui. Aliona nyumba iliyozungushiwa malumalu na lulu zikiwa zinaningi’inia kama mauwa mazuri yaliyopambwa. Rangi za nyumba utadhani ni dhahabu iliyochovywa. Kawahakika Sinbad alistaajabu sana. Kisha akaanza kuzungumza maneno yaloonesha kumalaumu mwenyezi Mungu kwa kuwapa watu wengine mali nyingi kama anazoziona pale. Pa aliendelea kumlaumu mwenyezi mungu kwa kumfanya yeye apate rizki kwa jasho jingi lakini watu wengine wapo wamekaa na bila jasho wanapata rizk.

 

Sinbad alilalamika sana hata akasikiwa na mwenye nyumba. Basi akaamrisha aletwe, akiwa natetemeka kwa woga Sinbad alipelekwa mbelel za Mkuu wa nyumba. Kisha akamwambia akae. Sinbad hakuamini kama meambiwa akae maana alifikiri atapewa adhabu kali. Basi mkuu wa nyumba akamuuliza “unaitwa nani kijana” “naitwa Sinbad “ au Sinbad mbeba mizigo. Yule mzee akamwambia jina zuri sana na inaonekana wewe ni wajina wangu. Mimi naitwa Sinbad au ukipenda niite Sinbad wa baharini.

 

Baada ya kutambulishana majina Sinbad wa baharini akaanza kumwambia Sinbad mbeba mizigo. “kijana nimekusikia maneno yako, ila sio kosa lako kusema maneno yale na wewe pia si wa kwanza. Kwani wapo wengi wamesema kama wewe. Sasa leo nataka nikueleze kuwa mimi sikupata mali zote hizi kwa kukaa hapa bila ya jasho. Kabla sijapata mali hizi nilipata tabu kubwa sana na pengine hakuna anayeweza kunifikia jasho na taabu nilizopata wakati natafuta malihizi”

 

Huu ni wakatii sasa wa mimi kula na kuulia kwani mchumia juani hula kivulini. Kabla ya hapo mimi nilikuwa ni mfanya biashara wa majini yaani nasafiri visiwa mbalimbali. Utajiri wote kuu umettoka na na taabu na mashaka yalonikuta. Nilisafiri safari SABA ambazo hizo nilipata taabu kubwa sana na sito sahau. Leo nitakueleza wewe na walokuwepo hapa yalonikuta kwenye safari hizo.”

 

Basi kabla hajaanza kusimulia Sinbad mbeba mizigo akamwambia Mkuu mimi nina mzigo wangu natakiwa niupeleke sehemu hivyo niruhusu niondoke. Palepale Sinbad wa baharini akamwambia nitakupa mtu umuelekeze apeleke yeye hiyo mizigo na nitakulipa pato la siku yako yote ila ukae na mimi leo upate kusikia hadithi saba za safari zangu saba. Basi palepale akamuagiza mtu apeleke mzigo ule na vinywaji na vyakula vialetwa. Watu wakakusanyika na kukaa tayari kusikiliza hadithi za safari saba za sinbad. Badi bila ya kuchelewa akaanza kusimulia hadithi ya safari zake kama ifuatavyo:-





           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 1316


Sponsored links
👉1 Madrasa kiganjani     👉2 Kitau cha Fiqh     👉3 Kitabu cha Afya     👉4 kitabu cha Simulizi    

Post zifazofanana:-

Hadithi ya binti wa kwanza na mbwa
Posti hii inakwenda kukuletea hadithi za alifu lela ulela Soma Zaidi...

Kitabu Cha Hadithi ya jini
Kupata kitabu hiki download faili la PDF hapo chini na usome bila ya internet. Soma Zaidi...

SAMAKI WA AJABU
Download kitabu Hiki Bofya hapa SAMAKI WA AJABU Walikwenda upane wa magharibu na mji wakauacha upande wa kusini. Soma Zaidi...

HADITHI ZA ALIF LELA U LELA: KIFO CHA DAMU
Soma Zaidi...

Kiapo cha sultani
Posti hii inakwenda kukusimulia hadithi za alifu lela ulela Soma Zaidi...

HADITHI YA MZEE WA TATU NA MBWA
Download kitabu Hiki Bofya hapa HADITHI YA MZEE WA TATU NA MBWA WAKE MWEKUNDU Kama nilivyotangulia kusema , huyu ni mkewangu wa ndoa tulioishi pamoja kwa muda wa miaka zaidi ya kuni na tano sasa. Soma Zaidi...

HADITHI ZA ALIF LELA U LELA (sehemu ya kwanza): KIAPO CHA SULTAN
Soma Zaidi...

UFUPISHO WA ALIFU LELA ULELA KITABU CHA KWANZA
Posti hii inakwenda kukisimulia kuhusu hadithi za alifu lela ulela KITABU CHA KWANZA Soma Zaidi...

HADITHI YA CHONGO WATATU NA WANAWAKE WA BAGHADAD
Download kitabu Hiki Bofya hapa HATITHI YA CHONGO WATATU WATOTO WA WAFALME NA WANAWAKE WA BAGHDAD Hapo zamani katika nchi ya Baghdad kulikuwepo na mbeba mizigo maarufu sana. Soma Zaidi...

Hadithi ya samaki wa Rangi nne
Posti hii inakwenda kukuletea hadithi za alifu lela ulela Soma Zaidi...

Hadithi ya tabibu wa mfalme
Posti hii inakwenda kukuletea hadithi za alifu lela ulela Soma Zaidi...

HADITHI YA TABIBU NA MFALME
Download kitabu Hiki Bofya hapa HADITHI YA TABIBU WA MFALME Katika nchi ya Zouman iliyopo maeneo ya uajemi alikuwepo mfalme mkubwa sana. Soma Zaidi...